Nilivyoingiza 17.6M ndani ya mwaka mmoja na nusu, kwa biashara ya Mgahawa kwa mtaji wa kawaida kabisa

Nilivyoingiza 17.6M ndani ya mwaka mmoja na nusu, kwa biashara ya Mgahawa kwa mtaji wa kawaida kabisa

Ni mawazo yako potofu. JF bwana nini unataka kuleta imani potofu za kishikina hapa. Eti chuma ulete! Hili utawadanganya wajinga tu!
Hata hiyo yako inaweza kuwa imani potofu kwa wengine, hatuwezi kulazimishana maswala ya imani na ndiomaana hata mimi sijalazimisha mtu.

Sina muda wa kubishana, nikutakie mchana mwema.
 
Habari zenu humu ndani? Mimi si muandishi mzuri sana wa nyuzi humu jf ila leo nimejisikia kushare kitu kidogo na nyinyi juu ya biashara, nikiamini kwamba naweza kubadili fikira za baadhi ya vijana na wazee humu juu ya biashara.

Kwa taaluma mimi ni Civil Engineer na huwa napata vikazikazi ambavyo husukuma maisha yangu kwa kipato cha kawaida tu ila mwaka 2021 nilienda na jamaa yangu mmoja kama msindikizaji (kupoteza muda na kujifunza kitu kuhusu biashara ya dhahabu) sehemu moja inaitwa Dutwa ambako machimbo ya dhahabu yalizuka, kwa watu wa dhahabu watakuwa wanapajua vizuri. Sasa ile kufika kule nikakuta pilika za watu wengi balaa na huduma za jamii zinatolewa kwa bei ya juu kabisa, kwamfano watu walikuwa wanalala kwenye tugest tudogo twa mabati kwa 10K pre day so ukikuta mtu anavyumba 20 anakunja 200K yake kwa siku vizuri kabisa tena kwa kugombaniwa.

Nilivyorudi nyumbani Mwanza nikaa na kujiuliza sana mwisho wa siku nikaamua kuja na wazo la kwenda kuuza chakula kule, nilipojaribu kukusanya mawazo kutoka kwa watu nilikatishwa sana tamaa maana wengi walisema biashara kwenye migodi ya kulipuka huwa sio za kudumu kwana watu huhama mara kwa mara. Nilifikiria sana baadae nikaamua kujitoa mhanga, nikaandaa 2M kwaajili ya kujenga guesthouse za mabati na mgawaha na vyote nilivipa jina la CALFONIA HOLEL & CALFONIA GUEST (kwa wale waliowahi kufika dutwa namba moja watakuwa wanazijua), hazikuwa za kisasa sana ila kwa kiasi fulani niliset standards ukilinganisha na vimigahawa vingine vidogovidogo na guest za pale kihuduma.

MWANZO WA BIASHARA:
Nilinunua kila kitu kinachotakiwa kuanzisha mgahawa na ilinigharimu kama 1M nyingine, nilidhamiria kuuza kila kitu tofauti na wengine ambao walikariri chapati na chai, wali maharage nyama. Mimi nilitafuta mpishi mzuri kwaajili ya bites tu(chapati, Af cakes, na vitumbua na chai) ambae nilimlipa 10K siku, kisha nikatafuta pishi wa ugali na wengine wawili kwajili ya vitu vingine (Nyama, Samaki, wali, kuku, mbogamboga, maharage, maini...nk). Wahudumu nilitafuta wanne ambao niliwashonea sare kabisa.

Nilivyoanza sikutaka kucheka na nyani kwakua vitu vilikuwa standard nilikuja na bei ambazo hazikuwako kabisa. Kwamfano:-

Chapati 500Tsh (wao 300)
Andazi 500Tsh (wao 200)
Kitumbua 250Tsh (wao 200)
Wali nyama 3500Tsh (wao 2000)
Wali roast 4000Tsh (wao 3000)
Supu 2000Tsh (wao 1000)
Kipande kimoja cha nyama ya kuku ilikuwa ni 6000.
Samaki mzima nilikuwa nauza 10K hadi 12 wakati mimi nilikuwa nawachukulia 5k hadi 7K pale Ramadi, yani ni kwamba nilinunua vitu kwa bei ndogo na kuuza mara mbili yake. Nilizingatia usafi wa eneo langu na wahudumu wangu muda wote.

Siku ya kwanza hadi ya nne mauzo hayakuwa mazuri sana ila yalienda yanaongezeka,nadhani walikuwa wanapeana habari. Wiki ya pili nilianza kuuza hadi nilishangaa maana watu wa kule wakikaa kula hakuna kujibana, kwenye mgahawa wangu watu walipishana wengi sana ambao kwa mjini ili uwapate unahitaji uwe na mtaji mkubwa sana, nilipata tenda hadi kwenye ofisi za shamba ambako walikaa wale makota wa dhahabu. Mauzo ya chai na supu(7Kg) yalifika hadi 120K-140K kutokana na siku, mchana hadi usiku kwa pamoja nilikuwa nakusanya mauzo si chini ya 350K-400K (watu mtashangaa ila uhalisia ulinishangaza hata mimi)

Baada ya hesabu na kuwalipa wafanyakazi kukunja 60k-70k kama faida ilikuwa ni swala la kawaida kabisa. Nikikaa pale kama cashier kwa wiki tatu kisha baada nikaleta ndugu asimamie ili nirudi mwanza kuendelea na issue nyiingine ila akaanza kuniletea habari za faida 20K wakati mimi nishapiga hesabu za mbali kabisa, nilimtoa nirudi mwenyewe mzigoni(sikutaka kumpeleka wife kule mgodini) na mambo yakaendelea kuwa mzuri na mpaka mwisho wa mwezi ule nilikunja kama 1.2M benki. Biashara ya Guest Ilianza kuzorota maana ilifikia hatua chumba ikaw ni 3k baada ya guest kuwa nyingi.

CHANGAMOTO KUBWA:

Baada ya kama miezi miwili mambo yalianza kwenda kombo yani nikawa nauza msosi kwa raia wengi ila usiku wakati wa mahesabu hakuna hela hadi naanza kubembelezana na wafanyakazi kuwalipa hela, nikaanza kuchukua hela nje ya biashara ili kuinusuru, niliwaza labda naibiwa na wafanyazi ila kwakua mimi ndo nilikuwa mshika hela sikufikiria hivyo sana. Mimi huwa ni si muumini wa wa mambo ya tiba asilia na nilikuwa na msimamo sana ila baada ya kuona vyakula vinaisha ila hela haionekani jioni nikaamua kuomba ushauri, kila mtu akawa anadai bariadi wachawi sana na kwamba sitatoka na kitu nikizubaa. Nikaamua kumshirikisha mjomba wangu mmoja aliyekuwa anafanya kazi GGML ambaye alikuwa ni tajiri sana kutokana na biashara zake nyingi( RIP), alinisisitiza sana swala la kwenda kwa mganga nilikataa sana ila baadae niliingia kwenye line kisha akaniunganisha na mzee fulani hivi (sitaki maswali PM) nikaenda kuaguliwa japo kishingo upande, niliambiwa kuwa kulikuwa na chuma ulete kwenye biashara yangu na kwamba hela zikikuwa hazikai.

Niliporudi ofisini mambo yalichachamaa kaisi kwamba ikanilazimu kuongeza wahudumu kutoka wanne hadi 9 ili kuendana na kasi ya wateja, watu walitoka mbali (namba 2 na 7 kuja kula Calfonia ambayo ipo namba 1), kikuweli niliuza sana kisha baadae niliongeza biashara ya chips na nyama choma ambayo nayo ilinipa faida sana, swala la kuweka 90K- 120K kama faida likawa la kawaida sana au la lazima kabisa na kila mwisho wa mwezi benki ilibaki 900K- 1.4M (haikuwa constant kwasababu ya matumizi ya kijinga ikiwemo betting)

Hili swala la betting nilishashindwa kabisa kuliacha, na hata humu Jf mimi ni member mzuri tu wa jukwaa la mikeka😄.

Maisha yalikuwa mazuri sikuwa na hitaji kufanya kingine kabisa tofauti na mgahawa wangu, Mwanza nikawa naingia weekend (ijumaa- jpili) na nikifika na kula bata na marafiki na jamaa na kila aliyeuliza mishe yangu mpya nilimwambia nipo mgodini😄.

Baada ya mwaka mmoja mgodi ulienda unapunguza idadi ya watu walihamia Kakola na sikuwa na mpango wa kukimbizana nao hasa nikiangalia faida niliyoipata ndani ya muda huo, taratibu mauzo yalipungua mpaka ilipofikia mwezi wa tatu nikaamua kuibomoa nili nirudi kutulia nyumbani.

Mpaka nafunga biashara benki nilikuwa na 17.6M achilia mbali zile ambazo nilikuwa na kula au zile ambazo nilikuwa naliwa kwenyr betting.

NILICHOJIFUNZA

👉🏽Biashara ni location, huo mgahawa ukiuleta Mwanza mjini ungeonekana local kabisa na pengine nisingepata haya mauzo kabisa.

👉🏽Kwenye biashara utajikuta tu unaingia kwenye ushirikina kutokana na nature ya wateja ambao utawapokea (wapo wasio na nia nzuri ) unless uwe mcha Mungu thabiti kitu ambacho wengi hatuwezi.

👉🏽Ningekuja kuomba ushauri humu jf kwa mtaji ambao nilianza nao pale basi ningekata tamaa, maana humu nilishawahi kuona jamaa anasema hata mtaji wa 12M hauwezi kukupa faida ya 2M daaah😄.

👉🏽Kuna mishe zinaonekana za kijishusha viwango sana ila kiuhalisia ni zinalipa sana kama utaamua kuweka aibu pembeni.

NB; Sijaeleza yote, mengine nitakuwa naeleza huko chini kutokana na maswali ya wadau.
I will apply
 
Bora utoto wenye akili kuliko ukubwa wenye kujaa imani potofu. Hivi kweli karne hii unataka tukuamini eti kuna mtu mwenye uwezo wa kuchukuwa fedha za mauzo ya biashara kwa miujiza? Hili nakupia ni wajinga tu watakaoamini.
Kwakua bado unafugwa kwa shemeji yako huwezi kuelewa, wenye akili hawawezi kupinga uwepo wa hilo swala kwenye niashara, ndiomaana nikasisitiza either kumuomba sana Mungu au njia nyingine.

Sasa kwa haya matusi yako sijui ungechagua upande gani, maana kwa Mungu sikuoni.
 
Kwakua bado unafugwa kwa shemeji yako huwezi kuelewa, wenye akili hawawezi kupinga uwepo wa hilo swala kwenye niashara, ndiomaana nikasisitiza either kumuomba sana Mungu au njia nyingine.

Sasa kwa haya matusi yako sijui ungechagua upande gani, maana kwa Mungu sikuoni.
Umeumba picha isiyo kichwani mwako. Mimi biashara nimezifanya sana sana. Ujinga siyo tusi. Ujinga ni hali ya kutojua. Kudhani kuna chumaulete ni ujinga
 
Huwa niko interested na hiyo biashara ya guest house za machimboni ila taarifa za wadau humu huwa hazijitoshelezi.

Tofauti na guest za mijini ni nyumba kujengwa kwa mabati tu au kuna tofauti zingine mf vitanda,mabafu etc.
 
Na mimi nataka nithubutu kwenye ndizi na piga fuso yangu ya ndizi kutoka kiwira mbeya nauza mabibo sokoni naanza na 3M siku moja nitaleta feedback [emoji2187][emoji2187][emoji2187]
 
Kwenye migodi ya huko kahama maeneo ya kakola,Nyamishiga,nyangalata kote nimepita huko watu ni wengi sana na pesa iko njenje ukiuza hata maji,juice,soda tu unapiga pesa sana mzee watu wanapiga hela laana shida ni hiyo tu ni machimbo ya kuhama hama inabidi na wewe nyumban wakusahau
Madem wanauza K hadi buku mbili na maisha yanaenda ila ukimwi nje nje
 
Hongera sana mkuu ,biashara ni upepo mi kuna kipindi nilifungua biashara ya mgahawa nikiangalia location iko poa ila hela hamna ,duh mwisho wa siku nikaacha.

Sasa miaka ya karibuni kuna biashara moja halali upepo uliniendea ndani ya miezi miwili nilipata mil 16 ,nikaenda kutoa sadaka ya shukrani mil 1.

Baada ya hapo naendelea ila upepo sio kama wa mwanzo haipipi kabisa ,mara upepo unakuja tena gafla ila sifikii hata nusu ya niliyooteaga. But pia sometimes nahisi mtu ukianza kupata hela unaweza kupunguza ufanisi kwenye kazi na faida kushuka au unawaza mambo mengine makubwa kwa wakati mmoja hadi unafeli kwenye kile ulichofanikiwa.
Sure mkuu biashara ni upepo tu.nishawai ingiza per day 400k hadi 200k .ila now unafukuzia elfu 5 kwa siku.we acha tu

Sent from my vivo 1907 using JamiiForums mobile app
 
Sure mkuu biashara ni upepo tu.nishawai ingiza per day 400k hadi 200k .ila now unafukuzia elfu 5 kwa siku.we acha tu

Sent from my vivo 1907 using JamiiForums mobile app
na ukipata huo upepo hapo hapo unatakiwa usichezee hela fanya ishu ya maana,kama nyumba jenga ,gari nunua maana baada ya upepo kupita kurudi ni ishu hata kisaikolojia unaweza kuharibika utadhani umelogwa
 
na ukipata huo upepo hapo hapo unatakiwa usichezee hela fanya ishu ya maana,kama nyumba jenga ,gari nunua maana baada ya upepo kupita kurudi ni ishu hata kisaikolojia unaweza kuharibika utadhani umelogwa
Ushauri mzuri sana, nimekupenda bure
 
Bora utoto wenye akili kuliko ukubwa wenye kujaa imani potofu. Hivi kweli karne hii unataka tukuamini eti kuna mtu mwenye uwezo wa kuchukuwa fedha za mauzo ya biashara kwa miujiza? Hili nakupia ni wajinga tu watakaoamini.
Nimewahi kuwa na mawazo haya kwamba huenda kuna chuma ulete anaiba pesa zangu. Nikafunga safari mpaka Tanga sehemu fulani vijijini nikaenda kwa mganga aniague kwanini napata hela lakini sina kitu cha maana, mganga aliniambia anayeniloga ni mke wangu na akanipa dawa kadhaa nikifika Dar Es Salaam nifanye hili na lile na hizo dawa. Nikiwa njiani nilitafakari sana na kuona utapeli fulani yule mganga amenifanyia. Alidai nimetupiwa majini na nimefungwa vifungo 7.

Nikiwa bado njiani natoka Tanga narudi Dar Es Salaam nilitafakari sana na kuja kugundua ni mimi mwenyewe ndiyo nilikuwa na matumizi ya hovyo na sikuwa na nidhamu ya pesa. Nikazitupa zile dawa na kubadilika mimi mwenyewe binafsi bila dawa.

Nilifanikiwa hatimaye japo kwa shida lakini Nilifanikiwa bila mganga wala masharti ya mganga.

Siamini bado mambo hayo ya waganga na biashara.
 
Habari zenu humu ndani? Mimi si muandishi mzuri sana wa nyuzi humu jf ila leo nimejisikia kushare kitu kidogo na nyinyi juu ya biashara, nikiamini kwamba naweza kubadili fikira za baadhi ya vijana na wazee humu juu ya biashara.

Kwa taaluma mimi ni Civil Engineer na huwa napata vikazikazi ambavyo husukuma maisha yangu kwa kipato cha kawaida tu ila mwaka 2021 nilienda na jamaa yangu mmoja kama msindikizaji (kupoteza muda na kujifunza kitu kuhusu biashara ya dhahabu) sehemu moja inaitwa Dutwa ambako machimbo ya dhahabu yalizuka, kwa watu wa dhahabu watakuwa wanapajua vizuri. Sasa ile kufika kule nikakuta pilika za watu wengi balaa na huduma za jamii zinatolewa kwa bei ya juu kabisa, kwamfano watu walikuwa wanalala kwenye tugest tudogo twa mabati kwa 10K pre day so ukikuta mtu anavyumba 20 anakunja 200K yake kwa siku vizuri kabisa tena kwa kugombaniwa.

Nilivyorudi nyumbani Mwanza nikaa na kujiuliza sana mwisho wa siku nikaamua kuja na wazo la kwenda kuuza chakula kule, nilipojaribu kukusanya mawazo kutoka kwa watu nilikatishwa sana tamaa maana wengi walisema biashara kwenye migodi ya kulipuka huwa sio za kudumu kwana watu huhama mara kwa mara. Nilifikiria sana baadae nikaamua kujitoa mhanga, nikaandaa 2M kwaajili ya kujenga guesthouse za mabati na mgawaha na vyote nilivipa jina la CALFONIA HOLEL & CALFONIA GUEST (kwa wale waliowahi kufika dutwa namba moja watakuwa wanazijua), hazikuwa za kisasa sana ila kwa kiasi fulani niliset standards ukilinganisha na vimigahawa vingine vidogovidogo na guest za pale kihuduma.

MWANZO WA BIASHARA:
Nilinunua kila kitu kinachotakiwa kuanzisha mgahawa na ilinigharimu kama 1M nyingine, nilidhamiria kuuza kila kitu tofauti na wengine ambao walikariri chapati na chai, wali maharage nyama. Mimi nilitafuta mpishi mzuri kwaajili ya bites tu(chapati, Af cakes, na vitumbua na chai) ambae nilimlipa 10K siku, kisha nikatafuta pishi wa ugali na wengine wawili kwajili ya vitu vingine (Nyama, Samaki, wali, kuku, mbogamboga, maharage, maini...nk). Wahudumu nilitafuta wanne ambao niliwashonea sare kabisa.

Nilivyoanza sikutaka kucheka na nyani kwakua vitu vilikuwa standard nilikuja na bei ambazo hazikuwako kabisa. Kwamfano:-

Chapati 500Tsh (wao 300)
Andazi 500Tsh (wao 200)
Kitumbua 250Tsh (wao 200)
Wali nyama 3500Tsh (wao 2000)
Wali roast 4000Tsh (wao 3000)
Supu 2000Tsh (wao 1000)
Kipande kimoja cha nyama ya kuku ilikuwa ni 6000.
Samaki mzima nilikuwa nauza 10K hadi 12 wakati mimi nilikuwa nawachukulia 5k hadi 7K pale Ramadi, yani ni kwamba nilinunua vitu kwa bei ndogo na kuuza mara mbili yake. Nilizingatia usafi wa eneo langu na wahudumu wangu muda wote.

Siku ya kwanza hadi ya nne mauzo hayakuwa mazuri sana ila yalienda yanaongezeka,nadhani walikuwa wanapeana habari. Wiki ya pili nilianza kuuza hadi nilishangaa maana watu wa kule wakikaa kula hakuna kujibana, kwenye mgahawa wangu watu walipishana wengi sana ambao kwa mjini ili uwapate unahitaji uwe na mtaji mkubwa sana, nilipata tenda hadi kwenye ofisi za shamba ambako walikaa wale makota wa dhahabu. Mauzo ya chai na supu(7Kg) yalifika hadi 120K-140K kutokana na siku, mchana hadi usiku kwa pamoja nilikuwa nakusanya mauzo si chini ya 350K-400K (watu mtashangaa ila uhalisia ulinishangaza hata mimi)

Baada ya hesabu na kuwalipa wafanyakazi kukunja 60k-70k kama faida ilikuwa ni swala la kawaida kabisa. Nikikaa pale kama cashier kwa wiki tatu kisha baada nikaleta ndugu asimamie ili nirudi mwanza kuendelea na issue nyiingine ila akaanza kuniletea habari za faida 20K wakati mimi nishapiga hesabu za mbali kabisa, nilimtoa nirudi mwenyewe mzigoni(sikutaka kumpeleka wife kule mgodini) na mambo yakaendelea kuwa mzuri na mpaka mwisho wa mwezi ule nilikunja kama 1.2M benki. Biashara ya Guest Ilianza kuzorota maana ilifikia hatua chumba ikaw ni 3k baada ya guest kuwa nyingi.

CHANGAMOTO KUBWA:

Baada ya kama miezi miwili mambo yalianza kwenda kombo yani nikawa nauza msosi kwa raia wengi ila usiku wakati wa mahesabu hakuna hela hadi naanza kubembelezana na wafanyakazi kuwalipa hela, nikaanza kuchukua hela nje ya biashara ili kuinusuru, niliwaza labda naibiwa na wafanyazi ila kwakua mimi ndo nilikuwa mshika hela sikufikiria hivyo sana. Mimi huwa ni si muumini wa wa mambo ya tiba asilia na nilikuwa na msimamo sana ila baada ya kuona vyakula vinaisha ila hela haionekani jioni nikaamua kuomba ushauri, kila mtu akawa anadai bariadi wachawi sana na kwamba sitatoka na kitu nikizubaa. Nikaamua kumshirikisha mjomba wangu mmoja aliyekuwa anafanya kazi GGML ambaye alikuwa ni tajiri sana kutokana na biashara zake nyingi( RIP), alinisisitiza sana swala la kwenda kwa mganga nilikataa sana ila baadae niliingia kwenye line kisha akaniunganisha na mzee fulani hivi (sitaki maswali PM) nikaenda kuaguliwa japo kishingo upande, niliambiwa kuwa kulikuwa na chuma ulete kwenye biashara yangu na kwamba hela zikikuwa hazikai.

Niliporudi ofisini mambo yalichachamaa kaisi kwamba ikanilazimu kuongeza wahudumu kutoka wanne hadi 9 ili kuendana na kasi ya wateja, watu walitoka mbali (namba 2 na 7 kuja kula Calfonia ambayo ipo namba 1), kikuweli niliuza sana kisha baadae niliongeza biashara ya chips na nyama choma ambayo nayo ilinipa faida sana, swala la kuweka 90K- 120K kama faida likawa la kawaida sana au la lazima kabisa na kila mwisho wa mwezi benki ilibaki 900K- 1.4M (haikuwa constant kwasababu ya matumizi ya kijinga ikiwemo betting)

Hili swala la betting nilishashindwa kabisa kuliacha, na hata humu Jf mimi ni member mzuri tu wa jukwaa la mikeka[emoji1].

Maisha yalikuwa mazuri sikuwa na hitaji kufanya kingine kabisa tofauti na mgahawa wangu, Mwanza nikawa naingia weekend (ijumaa- jpili) na nikifika na kula bata na marafiki na jamaa na kila aliyeuliza mishe yangu mpya nilimwambia nipo mgodini[emoji1].

Baada ya mwaka mmoja mgodi ulienda unapunguza idadi ya watu walihamia Kakola na sikuwa na mpango wa kukimbizana nao hasa nikiangalia faida niliyoipata ndani ya muda huo, taratibu mauzo yalipungua mpaka ilipofikia mwezi wa tatu nikaamua kuibomoa nili nirudi kutulia nyumbani.

Mpaka nafunga biashara benki nilikuwa na 17.6M achilia mbali zile ambazo nilikuwa na kula au zile ambazo nilikuwa naliwa kwenyr betting.

NILICHOJIFUNZA

[emoji1428]Biashara ni location, huo mgahawa ukiuleta Mwanza mjini ungeonekana local kabisa na pengine nisingepata haya mauzo kabisa.

[emoji1428]Kwenye biashara utajikuta tu unaingia kwenye ushirikina kutokana na nature ya wateja ambao utawapokea (wapo wasio na nia nzuri ) unless uwe mcha Mungu thabiti kitu ambacho wengi hatuwezi.

[emoji1428]Ningekuja kuomba ushauri humu jf kwa mtaji ambao nilianza nao pale basi ningekata tamaa, maana humu nilishawahi kuona jamaa anasema hata mtaji wa 12M hauwezi kukupa faida ya 2M daaah[emoji1].

[emoji1428]Kuna mishe zinaonekana za kijishusha viwango sana ila kiuhalisia ni zinalipa sana kama utaamua kuweka aibu pembeni.

NB; Sijaeleza yote, mengine nitakuwa naeleza huko chini kutokana na maswali ya wadau.
Asante Sana bro kwa mrejesho wa experience yako katika maisha na hasa biashara...
Binafsi nimekuwa nikisumbuliwa Sana na mawazo Kama yako na nimekuwa na ndoto za kufanya mgahawa hasa maeneo hayohayo ya migodi maana nimepitapita huko nikaona maisha ya migodini yanavyokutaka kuspend pesa nyingi kwa huduma ya kawaida kabisa Kama chakula, malazi na mavazi. (Kwa wanaopajua katoro nilikuwa Rwamgasa wakati panahila)
Nilivutiwa na maeneo hayo na nikahamasika kuwekeza kwenye mgahawa, gest , bar na duka la bidhaa pia.
Umenifungua macho, umenipa experience ambayo sikuwahi kuipata kwa mtu yoyete na umeyapa uhai mawazo na ndoto zangu na nakuhaidi mwakani mpaka mwezi wa pili ntakuwa napambana huko kwenye hiyo migodi maana nipo kwenye process za kuhamia geita kabisa (kwa sasa nipo kibondo) nitakutafuta kwa maongezi zaidi [emoji39][emoji39][emoji39].
THANKS ALOT JAMAA
 
Natamani nikueleze kwa upana ila sijui niazlnzie wapi, kiufupi pamoja na uzoefu wangu katika biashara, elimu na umakini wangu ilifikia hatua nikataka kukata tamaa.

Kwenye biashara kuna mambo mengi mkuu, hivyo ni vyema kuchagua upande mmoja kati ya mbili kisha ushikamane nao haswa. Muombe Mungu bila unafiki ikiwa mengine huwezi kuliko kuishi bila kujua unasimamia wapi, vinginevyo utakuwa msindikizaji siku zote.
Ukisoma historia nyingi za self made millionaires utagundua kitu kimoja kwa wote, nacho ni 'ilikuwa kidogo nikate tamaa na kuacha kila kitu'.

Kwahiyo kwenye biashara mafanikio mara nyingi huja unapokaribia kukata tamaa au pale umekata tamaa tayari ndiyo mafanikio yanakuja.

Biashara chache sana unaweza kuanza na kufanikiwa moja kwa moja bila kukata tamaa kwanza.

Kusali kwa Mungu siyo lazima kutwa nzima ushinde kanisani au msikitini masaa 12. Unaweza kusali dakika 15 tu kila baada ya masaa matatu na bado Mungu atakusikia. Amekupa uhai bure atashindwa vipi kukupa hiyo biashara?
 
Kwenye migodi ya huko kahama maeneo ya kakola,Nyamishiga,nyangalata kote nimepita huko watu ni wengi sana na pesa iko njenje ukiuza hata maji,juice,soda tu unapiga pesa sana mzee watu wanapiga hela laana shida ni hiyo tu ni machimbo ya kuhama hama inabidi na wewe nyumban wakusahau
Madem wanauza K hadi buku mbili na maisha yanaenda ila ukimwi nje nje
Anayekubishia ni yule ambae hajafika maeneo ya migodi hiyo lakini kwa aliyewahi kwenda hata kuona kwa macho tu ame experience hayo yote Tena ndani ya muda mfupi tu
 
Back
Top Bottom