Mkianza kuadisiana kila mmoja hapa story zake database za jf ntazijaza kwa uwongo wakutunga
Wewe umilia tu tuburudike masaa yasogee,
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkianza kuadisiana kila mmoja hapa story zake database za jf ntazijaza kwa uwongo wakutunga
Dubai UAE pesa still upo ukiwa na mtaji , Connection na uaminifu..Umenikumbusha jinsi wazanzibar walivopiga pesa dubai, ilikua inaenda kununuliwa gari used dubai, mule ndani siti zinatolewa zote kama ni corola inajazwa mzigo unapangwa vizuri laptops, tv flat screen, na makorokoromengine vioo vinapigwa tinted milango inakua locked kabisa, ngoma ikifika bandarini kinacholipiwa ushuru ni ile gari bidhaa nyingine zote zile zinapita free soko la unguja likawa na vitu vya electronic kibao wapemba wakakuza mitaji then wakaona wahamie kariakoo jamaa walipiga bingo enzi zile basi tu,
Mwarabu umpate wa Oman ..Ila mje kuishi bongo.Kwa waarabu hata sikushauri😂😂 heri mzungu
Ila wewe umezidi kusafiri au unauza ngada mkuu[emoji850][emoji850]..mara niko india mara abudhabi[emoji1787][emoji1787]! Uje kwangu sasa...nikienda sana naishia sirari .hahha..nipe uzoefu wa Kampala mkuu...nzuri sana kutembea aisee
Mbona Nongwa MwanawiseMkianza kuadisiana kila mmoja hapa story zake database za jf ntazijaza kwa uwongo wakutunga
Hapana kabisa hizo...hatari sanA..namfikiriaga shamim nakosa rahaChelewa kupata pesa, pata faida kidogo, usijaribu habari za unga au kutapeli, wauza ngada na matapeli mwisho wao hua ni mbaya sana sana,
Unga kibongo bongo sio ukiotewa unakula nyundo nyingi,Unga inchi Za ulaya kidogo afadhali.Chelewa kupata pesa, pata faida kidogo, usijaribu habari za unga au kutapeli, wauza ngada na matapeli mwisho wao hua ni mbaya sana sana,
Hapana kabisa hizo...hatari sanA..namfikiriaga shamim nakosa raha
Unga kibongo bongo sio ukiotewa unakula nyundo nyingi,Unga inchi Za ulaya kidogo afadhali.
Dah vuruga huko Musoma unaibukia kule juu Singita grunet ..Geita uzuge kiaina unarukia Mwanza, unakula sato na sangara unakaa kidogo siku mbili vuruga malaika , sijui villa then hapo unawaza utokee serengeti huko uitafute Arusha mbele utajiongeza
UMESHASEMA DADA WA KICHAGA. FULL STOPAisee wapo sema humu sijui kama wapo, kuna Dada mmoja mchaga jina sitomtaja niliwahi kukutana nae hotelin sehemu moja inaitwa Mambasa njia ya kwenda kisangani ilikua safari yake ya kwanza lakini alibeba pea kibao viatu vya kimasai alikua anafuata dhahabu/ Oro mapori ya kisangani huko nilipotea miaka kama sita sijarudi kule siku moja nafika tena kisangani nikamuuliza dreva mmoja wa classic za Butembo kisangani huyu dreva anaitwa aggrey ni mtu wa songea, akanipa story za Dada yetu kumbe alikomaa akatoboa akawa ameshanunua truck Benzi kama nne hivi anafuata mizigo viwandani kenya kupeleka Congo, huyu sister hua napenda angekuja akasimulia siku moja maana hakua mdangaji alikua jasiri kwa mtoto wa kike hawa wa oya oya asingethubutu kukata mbuga moshi, uganda then congo bila kua na ndugu.
Hahahahahahhaah nacheka .inAkera ..miafrica ndo tulivyoHalafu unakutana na Mbwiga wa Idara ya Uhamiaji anasema hatoi Pasi mpaka upeleke sababu za Safari
Wengi wa hao maafsaa wamepewa hizo nafasi kiushemeji na asili yao ni kula kulala.
Hawajui kuhangaika.
Unataka ukajilipue dubai kwenye mahotel kama hamisa mobeto?Mauaji hayo mie hPana mie najifutika huko Dubai....
Hahhhhaaa ilishindwa hata kufanya convention kwenye simu kujua kwcha moja sawa na tsh ngapi? Siku nyingine usivuke boda bila kuchange hela mzee watu wale wKiwa upande wao wanKuwa wasumbufu balaa. Ila ungekuwa upande wa tz ungepewa ushirikiana hata na watoa change wa kibongoSEHEMU YA TANO
Wakuu nitajitahidi kuandika kwa urefu na nitajitahidi kuandika kila kitu ili mtu mwengine aweze kujifunza kitu. Hata matukio yangu ya aibu pia nitawaeleza ili mtu ajifunze kitu kupitia story yangu na Kama kuna Makosa nilifanya basi iwe rahisi kwa mtu mwengine kujifunza na kurekebisha.
Nilivyorudi kwa yule Dada wa Uhamiaji, alifungua Passport yangu bila kusema chochote aligonga Mhuri nikaondoka zangu. Nikajua kumbe mwanzoni alisema vile ili kunitengenezea mazingira ya kutoa rushwa.
Nilivyotoka tu pale Kaunta, wale Vishoka wakanifuata ili niwarudishie ile Pesa yao, Kwacha 50. Kumbuka hapo nilikuwa bado sijabadili pesa za Kigeni. Nikawauliza wale Jamaa, Kwacha 50 ni sawa na shilingi ngapi za Kitanzania ili niwarudishie pesa yenu, wakaniambia "Wewe tupe Laki Moja tu"
Nikaona wananiletea Ujinga, nikatoka mpaka nje kwa Jamaa ambae alikuwa anawabadilishia watu fedha, Wale Vishoka wapo nyuma yangu tu. Nikataka kubadilisha Pesa yule Jamaa akakataa akasema "Malizana kwanza na hao Jamaa zako".
Nikamwambia kuhusu hawa Jamaa niachie Mimi, wewe nipe huduma tu ya Kubadilisha Pesa, Jamaa alikataa. Nikamwambia basi niambie Kwacha 50 ni sawa na shilingi ngapi za Kitanzania, Hata hilo nalo alikataa aliendelea kusema " Maliza kwanza na hao Jamaa".
Nikaondoka pale kurudi kwenye Bus ili nimuulize Dereva au Konda, Wale Vishoka wapo tu nyuma yangu. Dereva na Konda nao walikataa kutoa ushirikiano kwa madai ya kwamba nimalizane kwanza na wale Vishoka.
Hapo Vishoka wanatoa maneno yote ya Shombo. Lakini nilijifanya kama Siwasikii vile, mwisho wa siku nikawaambia oya nyie sikilizeni Mimi hiyo Laki Moja sina fanyeni mnachotaka kufanya. Tukaanza kuvutana vutana pale na kurushiana maneno. Abiria wengine wapo kimya wanatusikiliza tu.
Mwisho wa Mabishano nilikubali kuwapatia Elfu 50. Roho iliniuma sana. Nilijua fika hapa nimepigwa. Baadae nilikuja kujua kuwa Kwacha 50 ilikuwa kama Elfu Nane ya Kitanzania. Ndo hivyo nilishapigwa.
Baada ya wale Vishoka kushuka ndani ya Bus niliwauliza Dereva na Konda kwa nini walikataa kunisaidia. Wakaniambia kuwa wao ile njia wanapita kila siku na hao Vishoka wapo hapo Boda ya Tunduma miaka na miaka. Kwa hiyo kama wangenisaidia basi Bus lao lingefanya kazi katika Boda hiyo kwa tabu sana pengine wangeweza kutobolewa matairi kila watakapokuwa wanapita hapo. Kwa kweli niliwaelewa.
Aisee kumbe sikuwa peke yangu niliyepigwa usiku ule. Mara waliingia Abiria wengine na Vishoka wengine wakigombana kama ilivyokuwa kwangu. Moyoni nikasema hapa itakuwa kuna mchezo unachezwa kati ya Maafisa Uhamiaji na hawa Vishoka. Ndo mana wanaruhusiwa kuingia hadi ndani.
Tulilala ndani ya Bus hadi asubuhi ndo tukaendelea na safari ya kuelekea Zambia.
Hongera kwa hilo[emoji122][emoji122][emoji122]Ha haa Mimi ni mama wa familia. Muhenga kabisa
Ndio anakukuta huko Kisangani wakati huo keshafukuzwa kazi halafu wewe teyari una Passport ya South SudanHahahahahahhaah nacheka .inAkera ..miafrica ndo tulivyo
Soma vyema...panda huko.juu utaelewa mkuu...MIMI SIO FUKARAUnataka ukajilipue dubai kwenye mahotel kama hamisa mobeto?
Nimekuelewa, ntakujulishaIla siku ukitak kwenda kwa yule shost nistue...au hamjawah panga kwendaga...kumtembelea
Hahahahhahahaa....hahahhaNdio anakukuta huko Kisangani wakati huo keshafukuzwa kazi halafu wewe teyari una Passport ya South Sudan
Kinachofatia ni unamtumbukiza kwenye Mto Kongo kwa gazabu