Nilivyokwenda Afrika Kusini bila kuwa na Ndugu wala Rafiki kule

Nilivyokwenda Afrika Kusini bila kuwa na Ndugu wala Rafiki kule

Hao wanaigeria ujuaji wao unawacost kila sehemu hawakubaliki kutokana na tabia zao za kishenzi,utapeli,wizi etc
Kinachosababisha wakimbie kwao ni umasikini na kwa sasa nchi yao hali ya kisiasa sio nzuri muda wowote kitawaka
Nani amekwambia hawakubaliki???....mfukoni wako vizuri

Wewe ambaye ukienda "unakubalika"..... Umefaidika nini??

Umasikini wa Naijeria na Huku kwetu wapi kuna nafuu???

Unajua ni hela kiasi gani zinaingia Nigeria kutoka kwa Diaspora?? Ambazo zinasaidia jamii yao??

Hayo mawazo ya kutaka " kukubalika" ndio utopolo tuliojazwa toka tunakua yani mpaka saivi vijana wanahangaika wazazi wanataka wote waajiriwe serikalini( SU-Soma Ule/Shirika la umma) matokeo yake vijana wamebaki kuwa na stress tu. Kasomesha mtoto na hana msaada mzazi kastaafu halafu mtoto anashindwa hata kumsaidia utaleta "kukubalika" kwenye kikao cha familia kumchangia mshua Aende Apollo India matibabu??

Kuna siku nilikua na demu mmoja wa Kiswana kutoka sauzi nikaanza kuongea huo utopolo wa Nyerere kaisaidia South Afrika nikitaka "nikubalike" wakati huyo dada hata Nyerere hamjui wala Tanzania haijui ananishangaa tu na "kukubalika" kwangu kwamba waafrika kusini ndugu zetu😂😂

Matatizo ya Ujamaa hayo......dunia hii ni yq ubepari fanya vyovyote kuwa na hela utakubalika tu. Unadhani tunawapenda sana Wazungu??? Madola wanayoyaleta ndo "tunawakubali"

Badilisheni mindsets hizo,kuweni na uthubutu
 
Mkubwa nina kama Nyundo 2 hivi na misumali kadhaa sijakanyaga mitaa ya Pta. Vipi wale wamasai waliojazana mitaa ya Bosman karibu na park station bado wapo? Mara ya kwanza kuwaona wamasai hapa kaburu ilikuwa ni mitaa hiyo. Afu hawa jamaa ninachowapendea wao unga, bangi usiwatembezee, kazi au shughuli yao kubwa ni kusuka.

Wakikamata kichwa mkongo mwenyew anangoja. Wanachoniuzi wakitembea wanakuwa wengi wengi kama mabata. Mkubwa ukimaliza stori zako karibu jozi kwa watoto wa "mbwa mwitu" uone tunavyowakalisha wazawa, na masela koko kutoka nchi Mbali mbali za East, South, North and West. Sisi ndo wabongo original kutoka Mburahati to Mabibo ilipoanzia komando yosso, Red Soldier.

Wape hi watani zangu wote watoto wa kinondweni kina baba ubaya, marashi ya pwani, sefu kalawa nk, yu no wari am say!!
 
Kweli chief, hata Lema au Lissu pasipo kujilipua leo hii wasingekuwa mamtoni huko 😁!
Ndo hivyo ikitokea fursa unajilipua tu. Unatia na uwongo uwongo mwingi natishiwa maisha ntauliwa unaomba hifadhi mamtoni.

Kizazi cha kwanza cha pili unadhani familia ya Lissu/Lema watakua sawa na familia ya Lusinde tena??
 
Umenikumbusha jinsi wazanzibar walivopiga pesa dubai, ilikua inaenda kununuliwa gari used dubai, mule ndani siti zinatolewa zote kama ni corola inajazwa mzigo unapangwa vizuri laptops, tv flat screen, na makorokoromengine vioo vinapigwa tinted milango inakua locked kabisa, ngoma ikifika bandarini kinacholipiwa ushuru ni ile gari bidhaa nyingine zote zile zinapita free soko la unguja likawa na vitu vya electronic kibao wapemba wakakuza mitaji then wakaona wahamie kariakoo jamaa walipiga bingo enzi zile basi tu,
Kwasasa nafikiri watakuwa washabuni mbinu mpya....?
 
Unatuandikia stori kama vile unamtumia demu text vile..fupi fupi..

Mkuu fanya kuandika aisee..page hata moja bado ila stori tayari ina episodes tano.

Najua hatukulipi lakini em fanya namna.
Aisee umenichekesha Sana Ngoja nilale niiamkie Kesho Duuu hii story Ni tamu y
Tujifunzeeeee Mambo ya Duniani
 
Leta story nipo chirundu hapo
Hivi kwa Nini Nilipotea kwa muda humu?? Niliacha mautamu haya? Aisee hujajua nilivochekaa Sasa kumwita mwenzio Chirundu wkt Ni sehemu tu aliyofikia ndo Nini.Aisee too much fun.
Tomorrow jamaa endelea nitaikuta Kesho
Aiseeee humu Ndani Kuna wachekeshaji sana
 
Halafu unakutana na Mbwiga wa Idara ya Uhamiaji anasema hatoi Pasi mpaka upeleke sababu za Safari

Wengi wa hao maafsaa wamepewa hizo nafasi kiushemeji na asili yao ni kula kulala.

Hawajui kuhangaika.

Hua nawachek najisemea hawa kuvaa uniform zao na kujua salamu za lugha kadhaa wanaona washamaliza, wewe toa kitabu watu wasonge mbele, mimi kikiishaga nazama makao yao makuu namaliza mchezo naondoka zangu,
Yaaani na haya matatizo ya ajira ilitakiwa kila graduate akipewa cheti anapewa na gamba lake akiamua akafie mbele huko au aliweke chini ya godoro liliwe na panya

Na vijana wakizamia huko mbele wakirudishwa hapa(deported) hamna kuwafunga wala kesi wamwage mtaani waanze upya kutafuta chaka nyingine za kulowea

Sasa wao na mentality yao ya kikomunisti wanasema passport ni dokumenti ya kiusalama.....mawazo ya miaka ya 70 huko😂😂

Nakuhakikishia miaka 10 tu matokeo tungeyaona. Familia nyingi sana zingekua na msaada kwa diaspora sio kama saivi vijana wamebaki kuwa mzigo kwa familia

Bila "Conquering new frontiers" hatutoboi ng'o

Kina Livingstone, Speke,Stanley nk bila kuja kufanya upelelezi mpaka Ku(tu)gundua wala sio Mjeruman wala Muingereza angejua kuwa kuna watu bado washamba wanatakiwa kutawaliwa kuwa makoloni kwa manufaa yetu(wazungu)

Wale ni vijana walijilipua kuja sehem unknown to the world na waliua,walifanya kila aina ya unyama nqwengine walifia huku ila walileta mafanikio kwa mataifa yao.

Sio kujifungia tu huko kijijini Matombo toka umezaliwa mpaka unakufa kwa ajili ya uoga
 
Mkubwa nina kama Nyundo 2 hivi na misumali kadhaa sijakanyaga mitaa ya Pta. Vipi wale wamasai waliojazana mitaa ya Bosman karibu na park station bado wapo? Mara ya kwanza kuwaona wamasai hapa kaburu ilikuwa ni mitaa hiyo. Afu hawa jamaa ninachowapendea wao unga, bangi usiwatembezee, kazi au shughuli yao kubwa ni kusuka. Wakikamata kichwa mkongo mwenyew anangoja. Wanachoniuzi wakitembea wanakuwa wengi wengi kama mabata. Mkubwa ukimaliza stori zako karibu jozi kwa watoto wa "mbwa mwitu" uone tunavyowakalisha wazawa, na masela koko kutoka nchi Mbali mbali za East, South, North and West. Sisi ndo wabongo original kutoka Mburahati to Mabibo ilipoanzia komando yosso, Red Soldier. Wape hi watani zangu wote watoto wa kinondweni kina baba ubaya, marashi ya pwani, sefu kalawa nk, yu no wari am say!!


Haaah haaah!!Jozi pande zipi mwana?
 
Nataka nipeleke Bangi ya Arusha mpaka S. Africa.
Mliofika mnaweza kunipa details
Nina rafiki yangu, ana rafiki yake alizamia SA kitambo hadi leo hii yupo huko anafanya hiyo biashara ya bangi tu!
Anaishi ushuani, hivyo wateja wake wengi ni wakishua ...

Alioa huko huko now ana watoto wawili na maisha yake yanasonga... wakiwa kwenye apartment matata....
 
Wajinga Sana, vi much know Sana maringo mengi,malaya malaya,vitisho Sasa🙄 sie wa mipakani wanatuonea Sana na pua zetu ndefu mi kunipa gamba ilibidi kwenda kuwaonyesha kaburi la babu mzaa babu upande wa baba, ovyo kabisa Yani wanakwamisha watu wengi mno kuvuka mipaka kwenda nje kusaka maisha, wanataka tubanane humu tunuke kana kunguni😏😏 kuwakomoa niliondoka na wawili walifutwa kazi.
Ulipiga simu 1 tu upstairs?
 
Hahhhhaaa ilishindwa hata kufanya convention kwenye simu kujua kwcha moja sawa na tsh ngapi? Siku nyingine usivuke boda bila kuchange hela mzee watu wale wKiwa upande wao wanKuwa wasumbufu balaa. Ila ungekuwa upande wa tz ungepewa ushirikiana hata na watoa change wa kibongo
Mara nyingi hizi hela nyingine huwezi kubadilisha mpaka ukiwa boda

Kwa mfano unaweza kuhangaika kupata hela ya Zambia au ya Rwanda/Burundi ukiwa Dar ila ukifika boda zipo za kutosha

Na hao wabadilisha hela was kibongo ndo hao hao wanashirikiana na vishoka kukupiga. Wala sio wa Zambia, umenisoma mkuu??
 
Nimeshtuka saa 8:33 za usiku Cha Kwanza nilikuja kuona kun jipya duh keagan wew badal nipige Sala naanzakuangali epsod zako
 
MCHAWI PALE KURASINI.
yaani wanaona passport ni Mali kuliko dhahabu.
Yaaani tumetengenezwa kizazi cha uoga sana na kuwaza mipango mipango mipango mpaka mtu anazeeka alikua anapanga tu

Huko serikalini sasa ndo kila siku mchakato,Tuko mbioni,upembuzi yakinifu,tunaandaa mpango mkakati mpaka kitu kije kufanyika mshachelewa sana

Kwa hili aisee ndo nilimkubali Msee Marehemu. Mipango hakuna unajilipua kila kitu kitajulikana mbele kwa mbele. Ukishakua na hii spirit lazima utapata njia tu ya kutatua ya huko mbele

Wanaijeria nawafahamu vizuri sana wale jamaa yaani wahalifu,wanafanya kazi halali,majinias,waliosoma,kina kalume kenge wale ni kujilipua tu hawaogopi kitu na inawasaidia sana kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja na kwa familia pia

Wakenya nao hawako nyuma na wanajua kushikana mikono sana....yaan US mbongo ukiongea Lafudhi tu wanadhani Mnaija[emoji23][emoji23]

Sie tumejifungia huku nyumbani Madibila tunakula Pitiku na ugali tunaridhika tunaogopa
 
Back
Top Bottom