Nilivyokwenda Afrika Kusini bila kuwa na Ndugu wala Rafiki kule

Nilivyokwenda Afrika Kusini bila kuwa na Ndugu wala Rafiki kule

SEHEMU YA KUMI NA TATU

Basi nilikaa pale Kanisani mpaka Asubuhi, wakati najiandaa kuondoka nikakutana tena na Yule Dada. Nakumbuka aliniuliza naishi wapi, nikamwambia Pretoria. Akasema mbona unaishi mbali sana, Gari za Kanisa lao halina rut za huko. Akaniambia kama sitojali, Kanisa kuna nyumba limewapangishia waumini wake wale ambao wanajitolea Kanisani. Akasema ataongea na Jamaa mmoja anaishi room peke yake, kama huyo jamaa atakubali basi atanipigia simu kuniambia.

Ukweli Yule Dada alionesha kunichangamkia sana. Basi nikaondoka zangu pale mpaka Pretoria kwa washkaji zangu wa Kibongo. Ukweli kama nilivyosema mwanzo, Mbongo yeyote ukianza kufanya harakati zako tofauti na wenzio wanaanza kukusema sema. Hili natoa kama angalizo kwa mtu ambae hajawai kufika South, lakini inabidi uwe na moyo mgumu kuweza kufuata ndoto zako.

Basi nikafika mpaka kwa Jamaa Y, akaniuliza kuhusu habari za Kanisani nikamjibu kwa ufupi tu kuwa ni safi tu. Sikutaka kumwambia kila kitu kilichoendelea kule kwa sababu ningewapa mada ya kunijadili zaidi. Kichwani niliwaza endapo Yule demu atanicheki kuniambia kuwa amepata chumba kule Midrand basi hawa jamaa nitawadanganya kuwa kule Midrand nilikutana na HomeBoy wangu Kabisa wa Mtaa mmoja hapa Temeke. Homeboy amesema nikaishi nae. Nilipanga kuwadanganya hivyo ili wasijue chochote kuhusu mpango wangu.

Basi siku zikaenda, kama kawaida asubuhi tunaenda kusimama kule Barabarani na Jamaa Y. Tayari nilishafikia hatua ya kupewa Kazi mbili tatu za kuwapelekea jamaa Fulani madawa, nilikuwa nafanya hivyo, lakini moyoni sikuwa comfortable, Nilikuwa najiuliza, ina maana mimi South nimekuja kuuza Madawa? Najisemea Hapana. Hapa lazima niendelee kutafuta Mchongo wa Halali. Jamaa Y alikuwa akikutuma kumkatalia unashindwa, kumbuka unaishi kwenye chumba ambacho yeye ndo analipia Kodi. Muda mwingi unakula chakula chake. Kwa hiyo akikutuma huwezi kumkatalia. Basi nikawa napiga michongo hiyo hapo ya hapa na pale, Siku nikipata nafasi ndo nilikuwa naenda kule Midrand Kanisani. Wale Vijana ambao Jamaa Y amewaleta South yan utawaonea huruma, wanapiga Kazi kama punda. Wao wanainjoi tu kuishi Ghorofani, Kuvaa vizuri na kula KFC.

Mpaka siku ambayo Yule demu wa Kanisani alinicheki kwa simu na kuniambia Jamaa amekubali nikaishi nae. Nilifurahi sana. Jamaa zangu ziliwadanganya kama nilivyopanga. Jamaa Y alikubali niondoke lakini sura yake ilionesha kutokupendezwa na mimi kuaondoka pale. Alikuwa ananiambia maneno Fulani hivi ya kunitaka niwe makini. Alisema majamaa wengine sio wazuri sana kuishi nao. Nikamwambia mimi naenda lakini nitakuwa narudi hapa mara kwa mara. Jamaa alikubali kishingo upande. Hata sikuchelewa zangu nikawaaga jamaa, nikabeba begi langu nikasepa.

Kwa kifupi nilikuja kujua kwamba Yule demu wa Kanisa anaitwa KANYA, Alikuwa ni mmoja wa waimba kwaya muhimu pale Kanisani. Waimbaji wote walikuwa wanaishi kwenye nyumba nzima ambayo walipangishiwa na Kanisa. Alivyonicheki aliniambia tukutane sehemu mmoja inaitwa KALFONTEEN, Sio mbali sana na Midrand. Aisee nakumbuka ile siku hadi kufika huko KALFONTEEN nilipotea sana. Yan kilichotokea ni kwamba mfano wewe hapa Dar unaishi Tegeta halafu mtu akwambie njoo tukutane Makumbusho, Halafu wewe upande daladala mpaka Kariakoo, ukifika Kariakoo ndo utafute Daladala za Makumbusho uende zako Makumbusho. Wenzetu miji yao mikubwa, barabara nyingi mpaka mtu unachanganyikiwa.

Hatimae nilifika mpaka aliponiambia Kanya tukutane, hapo nina begi langu Mgongoni. Hao mdogo mdogo kwa mwendo wa miguu akanipeleka kwa huyo jamaa ni raia wa Ghana anaitwa Thomas. Maisha yangu mapya yalianzia hapo Kalfonteen. Yan kwenye Chumba tulipokuwa tunaishi na Thomas na kule Wanapoishi Wadada waimbaji sio mbali sana. Tuliishi kwenye Chumba Kimoja kikubwa, Jiko na Choo. Hakukuwa na Sebure. Thomas alikuwa na visa vingi sana, kwa sababu kabla ya mimi kufika pale yeye na rafiki zake wengine wa Kanisani ndo walikuwa wana date na wale wadada waimba kwaya, nilivyofika mimi kibao kikageuka. Basi pale maisha yangu na Thomas yakawa magumu mno mpaka nikawachukia Waghana wote. Mpaka Nikatamani kurudi Pretoria kwa Jamaa Y.

Sehemu inayofuata nitaelezea maisha yangu na Thomas yalivyokuwa, Mapenzi yangu na Kanya yalivyoanza na Harakati zangu za kuanza kutafuta mchongo wa Halali.
 
@Noelia unajua huwa tunakosea sana sisi wabongo...

Passport ni hati au kibali cha kusafiria na tena kukutambulisha wewe kwa taifa jingine kama ni Mtanzania...

Sasa tujiulize wote tu, kama hauna mpango wa kwenda nchi nyingine, kwa nini uhitaji passport?

Halafu pia restrictions zinakuwa nyingi sababu kuna watu wanatumia passport kufanikisha shughuli zao za kiharamia kama kupitisha madawa ya kulevya n.k, sasa kama taifa huwezi tu kuwa unatoa passport ili kufanikisha mauharamia...

Mfano kipindi tulipokuwa na passport ya zamani (ile ya gamba la kijani), passport ya bongo ilikuwa shamba la bibi, watu wa mataifa mengine waliitumia sana kufanya mambo yao especially kwa zile nchi ambazo mbongo anaingia kwa kupata entry visa airport...
Ukienda kwenye ofisi zao wameorodhesha mahitaji yote ili kuweza kupata hiyo pasi, unakamilisha masharti yao yote ikiwemo sababu ya kuomba passport km ni barua ya mwaliko unawaonyesha lakini bado jamaa watasumbua tu tena mie walinitamkia mpaka nitoe chochote la sivyo hawangenipa nikazifoward kwa mamlaka ya juu, wakapunguzwa kazini, sikutoa hata Mia na gamba nikapata ila kwa mvutano,

Uhamiaji Ni jipu usiwatetee kabisa
 
Ukienda kwenye ofisi zao wameorodhesha mahitaji yote ili kuweza kupata hiyo pasi, unakamilisha masharti yao yote ikiwemo sababu ya kuomba passport km ni barua ya mwaliko unawaonyesha lakini bado jamaa watasumbua tu tena mie walinitamkia mpaka nitoe chochote la sivyo hawangenipa nikazifoward kwa mamlaka ya juu, wakapunguzwa kazini, sikutoa hata Mia na gamba nikapata ila kwa mvutano,

Uhamiaji Ni jipu usiwatetee kabisa
Kwa situation yako sidhani kama kulikuwa na sababu ya kuzungushwa, najua ni wengi pia hukutana na mausumbufu ili tu kuwekewa mazingira ya kuombwa mlungula...

Hapo niliandika in general, sababu kuna mtu yeye huwa anataka kuwa na passport tu halafu basi...

Ngoja tuendelee kumsoma mleta uzi tutoe arosto...ciao ciao!!!
 
Kwa situation yako sidhani kama kulikuwa na sababu ya kuzungushwa, najua ni wengi pia hukutana na mausumbufu ili tu kuwekewa mazingira ya kuombwa mlungula...

Hapo niliandika in general, sababu kuna mtu yeye huwa anataka kuwa na passport tu halafu basi...

Ngoja tuendelee kumsoma mleta uzi tutoe arosto...ciao ciao!!!
Watu wengi wanawalalamikia Sana hawa jamaa

Tuko pamoja, enjoy the story
 
SEHEMU YA KUMI NA TATU

Basi nilikaa pale Kanisani mpaka Asubuhi, wakati najiandaa kuondoka nikakutana tena na Yule Dada. Nakumbuka aliniuliza naishi wapi, nikamwambia Pretoria. Akasema mbona unaishi mbali sana, Gari za Kanisa lao halina rut za huko. Akaniambia kama sitojali, Kanisa kuna nyumba limewapangishia waumini wake wale ambao wanajitolea Kanisani. Akasema ataongea na Jamaa mmoja anaishi room peke yake, kama huyo jamaa atakubali basi atanipigia simu kuniambia.

Ukweli Yule Dada alionesha kunichangamkia sana. Basi nikaondoka zangu pale mpaka Pretoria kwa washkaji zangu wa Kibongo. Ukweli kama nilivyosema mwanzo, Mbongo yeyote ukianza kufanya harakati zako tofauti na wenzio wanaanza kukusema sema. Hili natoa kama angalizo kwa mtu ambae hajawai kufika South, lakini inabidi uwe na moyo mgumu kuweza kufuata ndoto zako.

Basi nikafika mpaka kwa Jamaa Y, akaniuliza kuhusu habari za Kanisani nikamjibu kwa ufupi tu kuwa ni safi tu. Sikutaka kumwambia kila kitu kilichoendelea kule kwa sababu ningewapa mada ya kunijadili zaidi. Kichwani niliwaza endapo Yule demu atanicheki kuniambia kuwa amepata chumba kule Midrand basi hawa jamaa nitawadanganya kuwa kule Midrand nilikutana na HomeBoy wangu Kabisa wa Mtaa mmoja hapa Temeke. Homeboy amesema nikaishi nae. Nilipanga kuwadanganya hivyo ili wasijue chochote kuhusu mpango wangu.

Basi siku zikaenda, kama kawaida asubuhi tunaenda kusimama kule Barabarani na Jamaa Y. Tayari nilishafikia hatua ya kupewa Kazi mbili tatu za kuwapelekea jamaa Fulani madawa, nilikuwa nafanya hivyo, lakini moyoni sikuwa comfortable, Nilikuwa najiuliza, ina maana mimi South nimekuja kuuza Madawa? Najisemea Hapana. Hapa lazima niendelee kutafuta Mchongo wa Halali. Jamaa Y alikuwa akikutuma kumkatalia unashindwa, kumbuka unaishi kwenye chumba ambacho yeye ndo analipia Kodi. Muda mwingi unakula chakula chake. Kwa hiyo akikutuma huwezi kumkatalia. Basi nikawa napiga michongo hiyo hapo ya hapa na pale, Siku nikipata nafasi ndo nilikuwa naenda kule Midrand Kanisani. Wale Vijana ambao Jamaa Y amewaleta South yan utawaonea huruma, wanapiga Kazi kama punda. Wao wanainjoi tu kuishi Ghorofani, Kuvaa vizuri na kula KFC.

Mpaka siku ambayo Yule demu wa Kanisani alinicheki kwa simu na kuniambia Jamaa amekubali nikaishi nae. Nilifurahi sana. Jamaa zangu ziliwadanganya kama nilivyopanga. Jamaa Y alikubali niondoke lakini sura yake ilionesha kutokupendezwa na mimi kuaondoka pale. Alikuwa ananiambia maneno Fulani hivi ya kunitaka niwe makini. Alisema majamaa wengine sio wazuri sana kuishi nao. Nikamwambia mimi naenda lakini nitakuwa narudi hapa mara kwa mara. Jamaa alikubali kishingo upande. Hata sikuchelewa zangu nikawaaga jamaa, nikabeba begi langu nikasepa.

Kwa kifupi nilikuja kujua kwamba Yule demu wa Kanisa anaitwa KANYA, Alikuwa ni mmoja wa waimba kwaya muhimu pale Kanisani. Waimbaji wote walikuwa wanaishi kwenye nyumba nzima ambayo walipangishiwa na Kanisa. Alivyonicheki aliniambia tukutane sehemu mmoja inaitwa KALFONTEEN, Sio mbali sana na Midrand. Aisee nakumbuka ile siku hadi kufika huko KALFONTEEN nilipotea sana. Yan kilichotokea ni kwamba mfano wewe hapa Dar unaishi Tegeta halafu mtu akwambie njoo tukutane Makumbusho, Halafu wewe upande daladala mpaka Kariakoo, ukifika Kariakoo ndo utafute Daladala za Makumbusho uende zako Makumbusho. Wenzetu miji yao mikubwa, barabara nyingi mpaka mtu unachanganyikiwa.

Hatimae nilifika mpaka aliponiambia Kanya tukutane, hapo nina begi langu Mgongoni. Hao mdogo mdogo kwa mwendo wa miguu akanipeleka kwa huyo jamaa ni raia wa Ghana anaitwa Thomas. Maisha yangu mapya yalianzia hapo Kalfonteen. Yan kwenye Chumba tulipokuwa tunaishi na Thomas na kule Wanapoishi Wadada waimbaji sio mbali sana. Tuliishi kwenye Chumba Kimoja kikubwa, Jiko na Choo. Hakukuwa na Sebure. Thomas alikuwa na visa vingi sana, kwa sababu kabla ya mimi kufika pale yeye na rafiki zake wengine wa Kanisani ndo walikuwa wana date na wale wadada waimba kwaya, nilivyofika mimi kibao kikageuka. Basi pale maisha yangu na Thomas yakawa magumu mno mpaka nikawachukia Waghana wote. Mpaka Nikatamani kurudi Pretoria kwa Jamaa Y.

Sehemu inayofuata nitaelezea maisha yangu na Thomas yalivyokuwa, Mapenzi yangu na Kanya yalivyoanza na Harakati zangu za kuanza kutafuta mchongo wa Halali.
Ndio ndioo leta episodes mkuu
 
Wakuu tunaendelea Muda sio Mrefu, Mnisamehe Leo nitajitahid kuandika sana

Pole Sana kiongozi tuna tambua nawe una pilika nyingi Sana za kimaisha lakini tambua jana usiku watu wame subili uzi waka lala waka amka waka chungulia tena kimya.Tuna shukuru kwa kujali hope leo uta kuwa na come back ya maana kwetu wapata elimu
 
Hili tunaweza kusaidiana kujibu,barabara Tanzania bado sana tena sana,hii T1 yetu ni bado sana,Zambia wanajitahidi sana hasa barabara ya Lusaka to Livingstone,ya kwenda Chilindu sio mbaya sana ILA kuna tatizo kubwa mno btn Nakonde na Mpika ni shida sana(hii kwangu ni sabotage wanayotufanyia wazambia maana wameelekeza nguvu nyingi kusini but pure kibiashara)Chilundu hadi Beitbrige wanaifanyia ukarabati na nzuri in general,na N1 ya kutoka Beitbrige hadi cape town ni first class road ni super,na ukija Botswana nao ni super kuanzia ile A3 hadi A1,border ya zambia na Namibia sio safi hasa Zambia side ila upande wa pili ni super.Tanzania tuache siasa ni vema hii T1 yetu tuitengeneze ili tuchukue even 40%ya mizigo ya DRC(hii ndio future ya kibiashara Africa)
Wabongo hamuelewek aliyekua anajenga barabara mlimpiga Vita eti diktera Leo hii mnaanza kudemka mnasema Tena barabara
 
Nani amekwambia hawakubaliki???....mfukoni wako vizuri

Wewe ambaye ukienda "unakubalika"..... Umefaidika nini??

Umasikini wa Naijeria na Huku kwetu wapi kuna nafuu???

Unajua ni hela kiasi gani zinaingia Nigeria kutoka kwa Diaspora?? Ambazo zinasaidia jamii yao??

Hayo mawazo ya kutaka " kukubalika" ndio utopolo tuliojazwa toka tunakua yani mpaka saivi vijana wanahangaika wazazi wanataka wote waajiriwe serikalini( SU-Soma Ule/Shirika la umma) matokeo yake vijana wamebaki kuwa na stress tu. Kasomesha mtoto na hana msaada mzazi kastaafu halafu mtoto anashindwa hata kumsaidia utaleta "kukubalika" kwenye kikao cha familia kumchangia mshua Aende Apollo India matibabu??

Kuna siku nilikua na demu mmoja wa Kiswana kutoka sauzi nikaanza kuongea huo utopolo wa Nyerere kaisaidia South Afrika nikitaka "nikubalike" wakati huyo dada hata Nyerere hamjui wala Tanzania haijui ananishangaa tu na "kukubalika" kwangu kwamba waafrika kusini ndugu zetu😂😂

Matatizo ya Ujamaa hayo......dunia hii ni yq ubepari fanya vyovyote kuwa na hela utakubalika tu. Unadhani tunawapenda sana Wazungu??? Madola wanayoyaleta ndo "tunawakubali"

Badilisheni mindsets hizo,kuweni na uthubutu
Tabia zao kishenzi wameharibu kila sehemu wezi,matapeli,
 
SEHEMU YA KUMI NA TATU

Basi nilikaa pale Kanisani mpaka Asubuhi, wakati najiandaa kuondoka nikakutana tena na Yule Dada. Nakumbuka aliniuliza naishi wapi, nikamwambia Pretoria. Akasema mbona unaishi mbali sana, Gari za Kanisa lao halina rut za huko. Akaniambia kama sitojali, Kanisa kuna nyumba limewapangishia waumini wake wale ambao wanajitolea Kanisani. Akasema ataongea na Jamaa mmoja anaishi room peke yake, kama huyo jamaa atakubali basi atanipigia simu kuniambia.

Ukweli Yule Dada alionesha kunichangamkia sana. Basi nikaondoka zangu pale mpaka Pretoria kwa washkaji zangu wa Kibongo. Ukweli kama nilivyosema mwanzo, Mbongo yeyote ukianza kufanya harakati zako tofauti na wenzio wanaanza kukusema sema. Hili natoa kama angalizo kwa mtu ambae hajawai kufika South, lakini inabidi uwe na moyo mgumu kuweza kufuata ndoto zako.

Basi nikafika mpaka kwa Jamaa Y, akaniuliza kuhusu habari za Kanisani nikamjibu kwa ufupi tu kuwa ni safi tu. Sikutaka kumwambia kila kitu kilichoendelea kule kwa sababu ningewapa mada ya kunijadili zaidi. Kichwani niliwaza endapo Yule demu atanicheki kuniambia kuwa amepata chumba kule Midrand basi hawa jamaa nitawadanganya kuwa kule Midrand nilikutana na HomeBoy wangu Kabisa wa Mtaa mmoja hapa Temeke. Homeboy amesema nikaishi nae. Nilipanga kuwadanganya hivyo ili wasijue chochote kuhusu mpango wangu.

Basi siku zikaenda, kama kawaida asubuhi tunaenda kusimama kule Barabarani na Jamaa Y. Tayari nilishafikia hatua ya kupewa Kazi mbili tatu za kuwapelekea jamaa Fulani madawa, nilikuwa nafanya hivyo, lakini moyoni sikuwa comfortable, Nilikuwa najiuliza, ina maana mimi South nimekuja kuuza Madawa? Najisemea Hapana. Hapa lazima niendelee kutafuta Mchongo wa Halali. Jamaa Y alikuwa akikutuma kumkatalia unashindwa, kumbuka unaishi kwenye chumba ambacho yeye ndo analipia Kodi. Muda mwingi unakula chakula chake. Kwa hiyo akikutuma huwezi kumkatalia. Basi nikawa napiga michongo hiyo hapo ya hapa na pale, Siku nikipata nafasi ndo nilikuwa naenda kule Midrand Kanisani. Wale Vijana ambao Jamaa Y amewaleta South yan utawaonea huruma, wanapiga Kazi kama punda. Wao wanainjoi tu kuishi Ghorofani, Kuvaa vizuri na kula KFC.

Mpaka siku ambayo Yule demu wa Kanisani alinicheki kwa simu na kuniambia Jamaa amekubali nikaishi nae. Nilifurahi sana. Jamaa zangu ziliwadanganya kama nilivyopanga. Jamaa Y alikubali niondoke lakini sura yake ilionesha kutokupendezwa na mimi kuaondoka pale. Alikuwa ananiambia maneno Fulani hivi ya kunitaka niwe makini. Alisema majamaa wengine sio wazuri sana kuishi nao. Nikamwambia mimi naenda lakini nitakuwa narudi hapa mara kwa mara. Jamaa alikubali kishingo upande. Hata sikuchelewa zangu nikawaaga jamaa, nikabeba begi langu nikasepa.

Kwa kifupi nilikuja kujua kwamba Yule demu wa Kanisa anaitwa KANYA, Alikuwa ni mmoja wa waimba kwaya muhimu pale Kanisani. Waimbaji wote walikuwa wanaishi kwenye nyumba nzima ambayo walipangishiwa na Kanisa. Alivyonicheki aliniambia tukutane sehemu mmoja inaitwa KALFONTEEN, Sio mbali sana na Midrand. Aisee nakumbuka ile siku hadi kufika huko KALFONTEEN nilipotea sana. Yan kilichotokea ni kwamba mfano wewe hapa Dar unaishi Tegeta halafu mtu akwambie njoo tukutane Makumbusho, Halafu wewe upande daladala mpaka Kariakoo, ukifika Kariakoo ndo utafute Daladala za Makumbusho uende zako Makumbusho. Wenzetu miji yao mikubwa, barabara nyingi mpaka mtu unachanganyikiwa.

Hatimae nilifika mpaka aliponiambia Kanya tukutane, hapo nina begi langu Mgongoni. Hao mdogo mdogo kwa mwendo wa miguu akanipeleka kwa huyo jamaa ni raia wa Ghana anaitwa Thomas. Maisha yangu mapya yalianzia hapo Kalfonteen. Yan kwenye Chumba tulipokuwa tunaishi na Thomas na kule Wanapoishi Wadada waimbaji sio mbali sana. Tuliishi kwenye Chumba Kimoja kikubwa, Jiko na Choo. Hakukuwa na Sebure. Thomas alikuwa na visa vingi sana, kwa sababu kabla ya mimi kufika pale yeye na rafiki zake wengine wa Kanisani ndo walikuwa wana date na wale wadada waimba kwaya, nilivyofika mimi kibao kikageuka. Basi pale maisha yangu na Thomas yakawa magumu mno mpaka nikawachukia Waghana wote. Mpaka Nikatamani kurudi Pretoria kwa Jamaa Y.

Sehemu inayofuata nitaelezea maisha yangu na Thomas yalivyokuwa, Mapenzi yangu na Kanya yalivyoanza na Harakati zangu za kuanza kutafuta mchongo wa Halali.
Ukija kuendelea pia udokeze kidogo namna ulivyofanikiwa kuongeza muda wa kibali chako kukaa huko (maana mwanzoni ulisema ulipewa kibali cha mwezi mmoja tuu). Na harakati zote hizi, na assume kuwa mwezi ulishaisha kitambo. Au kuextend muda wa kibali ukiwa huko sio issue sana?
Otherwise, ni story very interesting na yenye mafunzo mengi sana kuhusu harakati za utafutaji na kujilipua kwetu vijana.
Keagan Paul
 
Back
Top Bottom