Keagan Paul
JF-Expert Member
- Jul 19, 2018
- 510
- 3,178
- Thread starter
- #821
SEHEMU YA KUMI NA TATU
Basi nilikaa pale Kanisani mpaka Asubuhi, wakati najiandaa kuondoka nikakutana tena na Yule Dada. Nakumbuka aliniuliza naishi wapi, nikamwambia Pretoria. Akasema mbona unaishi mbali sana, Gari za Kanisa lao halina rut za huko. Akaniambia kama sitojali, Kanisa kuna nyumba limewapangishia waumini wake wale ambao wanajitolea Kanisani. Akasema ataongea na Jamaa mmoja anaishi room peke yake, kama huyo jamaa atakubali basi atanipigia simu kuniambia.
Ukweli Yule Dada alionesha kunichangamkia sana. Basi nikaondoka zangu pale mpaka Pretoria kwa washkaji zangu wa Kibongo. Ukweli kama nilivyosema mwanzo, Mbongo yeyote ukianza kufanya harakati zako tofauti na wenzio wanaanza kukusema sema. Hili natoa kama angalizo kwa mtu ambae hajawai kufika South, lakini inabidi uwe na moyo mgumu kuweza kufuata ndoto zako.
Basi nikafika mpaka kwa Jamaa Y, akaniuliza kuhusu habari za Kanisani nikamjibu kwa ufupi tu kuwa ni safi tu. Sikutaka kumwambia kila kitu kilichoendelea kule kwa sababu ningewapa mada ya kunijadili zaidi. Kichwani niliwaza endapo Yule demu atanicheki kuniambia kuwa amepata chumba kule Midrand basi hawa jamaa nitawadanganya kuwa kule Midrand nilikutana na HomeBoy wangu Kabisa wa Mtaa mmoja hapa Temeke. Homeboy amesema nikaishi nae. Nilipanga kuwadanganya hivyo ili wasijue chochote kuhusu mpango wangu.
Basi siku zikaenda, kama kawaida asubuhi tunaenda kusimama kule Barabarani na Jamaa Y. Tayari nilishafikia hatua ya kupewa Kazi mbili tatu za kuwapelekea jamaa Fulani madawa, nilikuwa nafanya hivyo, lakini moyoni sikuwa comfortable, Nilikuwa najiuliza, ina maana mimi South nimekuja kuuza Madawa? Najisemea Hapana. Hapa lazima niendelee kutafuta Mchongo wa Halali. Jamaa Y alikuwa akikutuma kumkatalia unashindwa, kumbuka unaishi kwenye chumba ambacho yeye ndo analipia Kodi. Muda mwingi unakula chakula chake. Kwa hiyo akikutuma huwezi kumkatalia. Basi nikawa napiga michongo hiyo hapo ya hapa na pale, Siku nikipata nafasi ndo nilikuwa naenda kule Midrand Kanisani. Wale Vijana ambao Jamaa Y amewaleta South yan utawaonea huruma, wanapiga Kazi kama punda. Wao wanainjoi tu kuishi Ghorofani, Kuvaa vizuri na kula KFC.
Mpaka siku ambayo Yule demu wa Kanisani alinicheki kwa simu na kuniambia Jamaa amekubali nikaishi nae. Nilifurahi sana. Jamaa zangu ziliwadanganya kama nilivyopanga. Jamaa Y alikubali niondoke lakini sura yake ilionesha kutokupendezwa na mimi kuaondoka pale. Alikuwa ananiambia maneno Fulani hivi ya kunitaka niwe makini. Alisema majamaa wengine sio wazuri sana kuishi nao. Nikamwambia mimi naenda lakini nitakuwa narudi hapa mara kwa mara. Jamaa alikubali kishingo upande. Hata sikuchelewa zangu nikawaaga jamaa, nikabeba begi langu nikasepa.
Kwa kifupi nilikuja kujua kwamba Yule demu wa Kanisa anaitwa KANYA, Alikuwa ni mmoja wa waimba kwaya muhimu pale Kanisani. Waimbaji wote walikuwa wanaishi kwenye nyumba nzima ambayo walipangishiwa na Kanisa. Alivyonicheki aliniambia tukutane sehemu mmoja inaitwa KALFONTEEN, Sio mbali sana na Midrand. Aisee nakumbuka ile siku hadi kufika huko KALFONTEEN nilipotea sana. Yan kilichotokea ni kwamba mfano wewe hapa Dar unaishi Tegeta halafu mtu akwambie njoo tukutane Makumbusho, Halafu wewe upande daladala mpaka Kariakoo, ukifika Kariakoo ndo utafute Daladala za Makumbusho uende zako Makumbusho. Wenzetu miji yao mikubwa, barabara nyingi mpaka mtu unachanganyikiwa.
Hatimae nilifika mpaka aliponiambia Kanya tukutane, hapo nina begi langu Mgongoni. Hao mdogo mdogo kwa mwendo wa miguu akanipeleka kwa huyo jamaa ni raia wa Ghana anaitwa Thomas. Maisha yangu mapya yalianzia hapo Kalfonteen. Yan kwenye Chumba tulipokuwa tunaishi na Thomas na kule Wanapoishi Wadada waimbaji sio mbali sana. Tuliishi kwenye Chumba Kimoja kikubwa, Jiko na Choo. Hakukuwa na Sebure. Thomas alikuwa na visa vingi sana, kwa sababu kabla ya mimi kufika pale yeye na rafiki zake wengine wa Kanisani ndo walikuwa wana date na wale wadada waimba kwaya, nilivyofika mimi kibao kikageuka. Basi pale maisha yangu na Thomas yakawa magumu mno mpaka nikawachukia Waghana wote. Mpaka Nikatamani kurudi Pretoria kwa Jamaa Y.
Sehemu inayofuata nitaelezea maisha yangu na Thomas yalivyokuwa, Mapenzi yangu na Kanya yalivyoanza na Harakati zangu za kuanza kutafuta mchongo wa Halali.
Basi nilikaa pale Kanisani mpaka Asubuhi, wakati najiandaa kuondoka nikakutana tena na Yule Dada. Nakumbuka aliniuliza naishi wapi, nikamwambia Pretoria. Akasema mbona unaishi mbali sana, Gari za Kanisa lao halina rut za huko. Akaniambia kama sitojali, Kanisa kuna nyumba limewapangishia waumini wake wale ambao wanajitolea Kanisani. Akasema ataongea na Jamaa mmoja anaishi room peke yake, kama huyo jamaa atakubali basi atanipigia simu kuniambia.
Ukweli Yule Dada alionesha kunichangamkia sana. Basi nikaondoka zangu pale mpaka Pretoria kwa washkaji zangu wa Kibongo. Ukweli kama nilivyosema mwanzo, Mbongo yeyote ukianza kufanya harakati zako tofauti na wenzio wanaanza kukusema sema. Hili natoa kama angalizo kwa mtu ambae hajawai kufika South, lakini inabidi uwe na moyo mgumu kuweza kufuata ndoto zako.
Basi nikafika mpaka kwa Jamaa Y, akaniuliza kuhusu habari za Kanisani nikamjibu kwa ufupi tu kuwa ni safi tu. Sikutaka kumwambia kila kitu kilichoendelea kule kwa sababu ningewapa mada ya kunijadili zaidi. Kichwani niliwaza endapo Yule demu atanicheki kuniambia kuwa amepata chumba kule Midrand basi hawa jamaa nitawadanganya kuwa kule Midrand nilikutana na HomeBoy wangu Kabisa wa Mtaa mmoja hapa Temeke. Homeboy amesema nikaishi nae. Nilipanga kuwadanganya hivyo ili wasijue chochote kuhusu mpango wangu.
Basi siku zikaenda, kama kawaida asubuhi tunaenda kusimama kule Barabarani na Jamaa Y. Tayari nilishafikia hatua ya kupewa Kazi mbili tatu za kuwapelekea jamaa Fulani madawa, nilikuwa nafanya hivyo, lakini moyoni sikuwa comfortable, Nilikuwa najiuliza, ina maana mimi South nimekuja kuuza Madawa? Najisemea Hapana. Hapa lazima niendelee kutafuta Mchongo wa Halali. Jamaa Y alikuwa akikutuma kumkatalia unashindwa, kumbuka unaishi kwenye chumba ambacho yeye ndo analipia Kodi. Muda mwingi unakula chakula chake. Kwa hiyo akikutuma huwezi kumkatalia. Basi nikawa napiga michongo hiyo hapo ya hapa na pale, Siku nikipata nafasi ndo nilikuwa naenda kule Midrand Kanisani. Wale Vijana ambao Jamaa Y amewaleta South yan utawaonea huruma, wanapiga Kazi kama punda. Wao wanainjoi tu kuishi Ghorofani, Kuvaa vizuri na kula KFC.
Mpaka siku ambayo Yule demu wa Kanisani alinicheki kwa simu na kuniambia Jamaa amekubali nikaishi nae. Nilifurahi sana. Jamaa zangu ziliwadanganya kama nilivyopanga. Jamaa Y alikubali niondoke lakini sura yake ilionesha kutokupendezwa na mimi kuaondoka pale. Alikuwa ananiambia maneno Fulani hivi ya kunitaka niwe makini. Alisema majamaa wengine sio wazuri sana kuishi nao. Nikamwambia mimi naenda lakini nitakuwa narudi hapa mara kwa mara. Jamaa alikubali kishingo upande. Hata sikuchelewa zangu nikawaaga jamaa, nikabeba begi langu nikasepa.
Kwa kifupi nilikuja kujua kwamba Yule demu wa Kanisa anaitwa KANYA, Alikuwa ni mmoja wa waimba kwaya muhimu pale Kanisani. Waimbaji wote walikuwa wanaishi kwenye nyumba nzima ambayo walipangishiwa na Kanisa. Alivyonicheki aliniambia tukutane sehemu mmoja inaitwa KALFONTEEN, Sio mbali sana na Midrand. Aisee nakumbuka ile siku hadi kufika huko KALFONTEEN nilipotea sana. Yan kilichotokea ni kwamba mfano wewe hapa Dar unaishi Tegeta halafu mtu akwambie njoo tukutane Makumbusho, Halafu wewe upande daladala mpaka Kariakoo, ukifika Kariakoo ndo utafute Daladala za Makumbusho uende zako Makumbusho. Wenzetu miji yao mikubwa, barabara nyingi mpaka mtu unachanganyikiwa.
Hatimae nilifika mpaka aliponiambia Kanya tukutane, hapo nina begi langu Mgongoni. Hao mdogo mdogo kwa mwendo wa miguu akanipeleka kwa huyo jamaa ni raia wa Ghana anaitwa Thomas. Maisha yangu mapya yalianzia hapo Kalfonteen. Yan kwenye Chumba tulipokuwa tunaishi na Thomas na kule Wanapoishi Wadada waimbaji sio mbali sana. Tuliishi kwenye Chumba Kimoja kikubwa, Jiko na Choo. Hakukuwa na Sebure. Thomas alikuwa na visa vingi sana, kwa sababu kabla ya mimi kufika pale yeye na rafiki zake wengine wa Kanisani ndo walikuwa wana date na wale wadada waimba kwaya, nilivyofika mimi kibao kikageuka. Basi pale maisha yangu na Thomas yakawa magumu mno mpaka nikawachukia Waghana wote. Mpaka Nikatamani kurudi Pretoria kwa Jamaa Y.
Sehemu inayofuata nitaelezea maisha yangu na Thomas yalivyokuwa, Mapenzi yangu na Kanya yalivyoanza na Harakati zangu za kuanza kutafuta mchongo wa Halali.