Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
"Hapo ni upalestina tu unyama unyama"NILIVYOMKOMESHA TAPELI WA VIWANJA KIVULE
Sehemu ya 5
Baada ya kutoka pale nikamvutia uzi mwanangu yule hakimu kule Singidani nikamwambia hakimu aliyesimamia show ndio huyo huyo mwanao akasema poa nitampigia jioni tumpange tuone jambo linakuwaje,dah jioni mwana akapigiwa na nikapewa namba yake tukafanya conference call tukayajenga maana nilimpa sakata lote kuanzia pale Staki shari wakati wakufungua hadi kufikia ile siku akasema poa ntakusaidia na kwa kuwa yule mwanae ni mshkaji wangu nimlinde tukakubaliana kukutana weekend kwani alikuwa anakuja pale Ilala mtaa wa Arusha kwenye mafremu ya kanisa la Anglikana floor ya juu kulikuwa na gym (kwa wale wenyeji wa maeneo hayo watakuwa wamepafahamu) so jumamosi angekuja tupange zaidi nami nikamwambia poa.
Jumamosi akafika na tukayajenga nami nikamwambia hiyo laki ntakupa ila kwa awamu mbili na ile siku pesa yote nilikuwa nayo ila nikaiweka katika tigo pesa na nikamwambia nakutumia 50 leo maana siko vizuri akasema poa,nikamuwekea muhamala wake na tukaacha na baada ya wiki mbele ndio ikawa siku ya kwenda tena kule Madafu (kumbuka ile siku hadi mahakama inafungwa Kasangu wadhamini wake hawakuwa wametimiza vigezo ila wakati wa maongezi yale ya jioni kati yangu,mshkaji wa singida na hakimu,hakimu alisema alidhaminiwa).
Nimefika zangu kama kawaida na siku hii nilikuwa nimeongozana na yule mwanajeshi mwenye eneo ambaye ndio nimeuziwa kiwanja chake na ndugu yangu ambaye alisimama kama shahidi wakati wa mauziano,muda wa shauri ulipofika yule Kasangu hakuwepo na mheshimiwa akasema ameambiwa anaumwa akaahirisha tena wiki 2 tukaondoka zetu.
Udhulio la tatu nikaenda tena nikiwa na yule ndugu yangu bila ya yule mjeshi mtuhumiwa alifika na wakati tunangojea kuingia ndugu zake wakanifata eti tuyamalize pembeni nikawatukana tena nikawaambia wasinisogelee (natamba tena si najua hakimu mwana ndugu yao namkomesha) dah nilijidanganya kwani aliposomewa tena shtaka akakana hivyo tukatakiwa date inayofuata tuje na mashahidi wetu,tukandoka zetu na ilipofika jioni nikampigia mheshimiwa inakuwaje? Kwa maana apeleke jambo mpela mpela nitoke nikafanye yangu,hakimu akanambia niwe mpole kesi imekaa vizuri upande wangu na yule jamaa ana kesi kama 15 pale zote za mambo ya viwanja ila atamkomesha safari hii nikasema sasa hakimu si ndio huyu,ndugu yangu kama unaweza kumalizana na mtuhumiwa wako uko uko kitaani malizana nae hawa mahakimu hawa,hawa wazee wa baraza hawa we acha tu.
Siku ya siku nimewabeba mashahidi wangu mtuhumiwa hola hajafika,goma likalala,date nyingine kimya goma likalala tena nikimuuliza mheshimiwa ananipiga sound nikasema wewe utafurahi na wana Sikinde!
Siku hiyo nafika mahakamani na mshkaji wangu mshtakiwa kaja namuuliza mheshimiwa huyu mtu kafika lakini sioni akiulizwa alikuwa wapi,sioni wakiitwa wadhamini wake kutoa maelezo kwani mimi ni muhathirika wa hili shauri je nieleweje kuhusu hilo? Hakimu ananiambia mahakama inazo taarifa nikamuuliza je sipaswi kuzijua? Wale wazee wa baraza wakawa wananikaripia eti sioneshi utii kwa mheshimiwa niwawajibu siulizi ya mtu mwingine hapa napigania haki yangu,hakimu akanisoma kama nimepaniki na akajua huyu anapoelekea anaweza kumwaga mbona akapiga tarehe ya kuleta mashahidi,nikamstua mjeshi na yule ndugu yangu kuhusu hiyo date.
Siku ya siku mtuhumiwa kaja na mashahidi wangu wakaja na wakatoa ushahidi wao na walipomaliza akiulizwa kama ana maswali kwao akasema hana ila sasa wale wazee wa baraza ndio wakawa wanauliza maswali kibao,hatimaye siku ikaisha tukala date.
Date mpya tulipofika yule jamaa mtuhumiwa akawa hajaja kama mara 3 na hakuna lolote ninaloelezwa nikihoji wale wazee wa baraza hasa yule bibi dah alikuwa hanipi pumzi kama mie ndio mwizi kumbe nimeumizwa mie ilifika hatua nikifika pale namuona kama nini sijui,namuomba Mungu anisamehe tu ila yule mja wake najua yeye ni mjuzi zaidi anajua lakumfanya🙏🏼.Hakimu nikawa sasa nikimpigia mara anakata na ujumbe unakuja ule "i'll call you back" mara "on meeting" na mengineyo nikasema huyu hanijui sasa ndio atajua joto ya jiwe,nikamtumia ule ujumbe wa muhamala wa tigo pesa yule mwanangu wa Singidani kwani niliusave kwenye draft then nikampigia nikamwambia mwanao anajifanya mjanja pesa yangu lala,wazee wake wa baraza wananizingua,simu zangu hapokei,mtuhumiwa hafiki na anamtetea sasa wewe unanijua kinagaubaga najua ANAYETOA NA ANAYEPOKEA RUSHWA WOTE NI WAKOSAJI sasa mie kuku wa kienyeji napeleka TAKUKURU huu ujumbe twende jela mimi na yeye tuone watoto wa nani watakaoteseka na mshkaji akaniplease sana,nikamwambia tatizo sio mimi tatizo mwanao ama arudishe changu apeleke kesi anavyotaka ama afate atende haki kinyume na hapo ni UPALESTINA TU (Najitoa mhanga nae)
Itaendelea!
Ukatili unakuja tu wenyewe throu matukio!hawa matapeli unaweza fanya jambo ambalo hujawahi fikiria
Santo sana rafiki naona mwamba anataka kugecha watuuu!
Katafute wakukukuna marinda!Mtoa mada umeshawahi kusimama mahakamani kweli wewe?, eti Hakimu akakuplease mbona huwa sio taratibu kwa kauli zako hapo mahakamani na utovu wa kutii mahakama ungefungwa japo wiki mbili, sijui kama kweli unaifahamu korti wewe.
Merci!Mwamba Hauna mbambambaa kabisa!
safi sana[emoji106]
Shindwaaaaaaaa kabisa
Ndio unamwita mwenzio pulizio 🙄sijapenta😂
Tena na kilemba kama cha Arafat kile!"Hapo ni upalestina tu unyama unyama"
Hakuna kusurrender [emoji123]
Treis bien! 👍👍👍Merci!
Sawa fame gayUnadhani basi naweza matusi,matusi tulishawaachia nyie mnaoweza kutukana!
Hakii ulitakiwa uwe mjeshi hakuna kucheka na kimaa!!👽Tena na kilemba kama cha Arafat kile!
NILIVYOMKOMESHA TAPELI WA VIWANJA KIVULE
Sehemu ya 6
UTAJUA HUJUI
Yule mshkaji wangu wa Singida dah nilimuonea huruma kwani alijuta kuniunganisha katika lile jambo na akawa amemueleza mshkaji na mshkaji akawa anajitetea kuwa mara nyingi ninapompigia anakuwa kwenye maombi au bize kupitia kesi ambazo yeye akiwa kama mkuu wa mahakama pale aweze kuzitolea ripoti,nikamtumia ule ujumbe wa tigo pesa na yeye nikamwambia sikublack mail ila tambua simamia tulichopatata na najua umekula pesa wewe na wazee wako wa baraza sasa mimi ntakuja kuitoa kesi hapo kuipeleka mbele kwakuwa sina imani na mwenendo mnaoupeleka dah jamaa akaniomba sana msamaha ndio nikawaza inawezekana mtu akisema hana imani na mahakama husika waliopo pale kunawaletea picha chafu basi sasa ule mramaha wake ndio kama ulimponza sasa nikawa hakimu mimi yeye ndio mshtaki😂😂 na nikamwambia nataka siku ya date mshtakiwa awepo sijui utampataje na akubali kosa na alipe changu (hapo nshaclaim gharama zote zimefika M3.3) we bwana pema hapa ninapohadithia siku ya siku nimekaa benchini mtuhumiwa kaja na ndugu zake wawili wakike na wakiume wakaniita nje wakaniomba sana sana nikawambia nyie wekeni m3.3 ubaoni mi nabwaga kesi wakawa wanataka wanipe kwa awamu tena kianzia laki 5 nikawaambia kampeni hakimu hiyo pesa mi ninataka nipoteze tu wakatoka wamelowa! Muda wa kesi tukaitwa na alipoulizwa alipokuwepo akadai alikuwa anaumwa nikanyoosha mkono naomba kupata vielelezo vya hospitali akasema alipelekwa kwa mganga! Dah dunia hii nyie acheni,mheshimiwa akapotezea akaendelea na kesi mara mtuhumiwa akanyoosha tena mkono akamawambia hakimu yeye amekubali kosa na yuko tayari kunilipa ila sio hiyo pesa yote kwani mimi nilimpa yeye M2 tu (alijichanganya wakati mimi nimempa M1.3 na vichenji,sikuwa nimemalizia) na ananiomba twende mimi na yeye kule site kuhesabu gharama zangu za ujenzi kujua gharama halisi nikakubali na kesho yake nikatakiwa kwenda nae kule kwa mama Anna Mkapa.
Asubuhi nampigia kujua tunakutanaje akanambia wala nisiende yeye kaamua atalipa tu hayo madai yangu anaona tutasumbuana,nikaendelea na shughuli zangu kusubiria siku ya kwenda kule mahakamani.Siku ikafika na muda wa kuingia tukaitwa wakati hakimu anatuuliza natoa maelezo akanikana na kusema yeye hajaniona wala sijampigia dah kama mtu ameiona ile sinema ya kihindi ANDHAL KANOON ndio nilikuwa natamani pale Amita Batchan alipomshindilia bisu yule mzee ndio nilitamani nifanye pale yaani nilitoa maneno ambayo wote pale walibutwb nikamwambia "mheshimiwa naona danadana zimekuwa nyingi sasa nasema mbele ya mahakama hii nikijua wazi kama kutamka maneno ya kutishia kudhuru ni kosa kisheria ila hadi muda huu huyu jamaa keshaharibu maisha yangu,utu wangu,muda wangu na anaendelea kuniletea dharau sasa kwakuwa kadhamilia kuharibu maisha yangu basi ingawa sijawahi kuua ila huyu jamaa familia yake haitokaa salama nipo tayari kwa lolote kutoka sasa na wewe nakuachia ukumbi hukumu hii kesi kwa mizani yako unayoona sawa" dah hakimu jasho linamtoka na yule bibi akadakia unatishia mbele ya mahakama,kiujasiri nikamjibu simtishi na hii kesi ndio itakuwa yake ya mwisho kuja hapa wakati huo sio yeye wala mimi tunaojua litakalotokea! Bibi ananitizama huku natetemeka nasema kama mbwai iwe mbwai!
Hakimu akawa ananiplease kaka acha hasira,acha hasira haki yako utaipata ndugu haya yanazungumzika nikamjibt mimi sitaki huruma ya mahakama wewe toa hukumu tu,akawa anamwambia Kasangu ndugu unasikia hayo maneno? We unayaona yanatoka tu mdomoni na unadhani kutakuwa hakuna utekelezaji? Please mpe pesa yake tusije kuingia matatizoni wote,Kasangu akawa kakaa kimya na mheshimiwa akapiga date ndefu kama mwezi kamili!
Sasa wakati tunatoka ukiwa unaelekea pale kituoni kupanda daladala mimi na ndugu yangu yule Juma Kasangu akawa nae anakuja na ndugu zake akawa ananiambia "mtani mtani we mtani wangu bwana usikasirike ebu njoo tuyajenge bwana" haloo ilinitoka ngumi hiyo Juma chini! Nikamtimba kifuani yule ndugu yangu akanipush nikamponyoka nikawa namfata tena kuendelea kumchapa akanyanyuka akawa anakimbia kurudi kule mahakamani yeye mbele mimi nyuma hadi kati viunga vya mahakama akadumbukia ndani mimi nikageuza nikaondoka zangu wale ndugu zake wananitizama tu wanaogopa hata kufunua midomo yao.
Usiku hakimu akanipigia ooh kaka usifanye hivyo punguza hasira nikamwambia kavukavu nyie kuleni pesa ila mtajua tu siku moja uchungu tunaoupitia tunaodhulumiwa, akaniomba sana nikamwambia haki isipotendwa ama zake ama zangu na huyo fala.
Baada ya mwezi tukaenda tena mahakamani Juma hajaja,ikapigwa date hajaja tena,date ya tatu ndio kama alafu sasa anasema atalipa kwa awamu sita nikasema pesa yangu haikuwa mkopo nataka yote kila mtu akaendelee na hamsini zake na hakimu akamsisitizia kama amekubali kulipa alipe yote kikubwa atoe tamko ni muda gani,nikadakia iwe ndani ya mwezi (natamba mie tena hakimu na mtuhumiwa wote wapo kiganjani)wakakubali hivyo nikapewa tarehe kama ile kwa mwezi unaofuata,tukatakiwa twende kwa mhasibu wa mahakama kwenda kuandikishiana kumbe wakati wote huyo mama mhasibu alikuwepo pale mlangoni anafatilia tena ile kesi ikawa ikifika muda wa kusomwa ingawa ilikuwa inasomwa chumbani watu wengi walikuwa wanajaa hadi hakimu anawaomba wapungue pale mlangoni.
Tulipofika pale yule mama mhasibu akawa ananiambia "wewe mjinga badala ya kuchukua hata kidogo kidogo unakataa,utasumbuka" nikamjibu "mama fanya kazi yako kitengo chako cha hesabu pesa hauna shea nayo mama yangu"
Akakaa kimya akatuandikia maelezo nikaondoka zangu.
Mwezi uliofata nikatimba eneo la tukio na mwanangu tukahesabiwa mpunga wetu alafu yule mama mhasibu akawa ananambia "sinywi hata soda" nikamjibu "mama we nisamehe tu mimi sidili na upande wa upinzani" akanipa makaratasi nikasaini nikatia pesa kwenye begi nikaenda na kwa hakimu kuna makaratasi nikasaini nikatoka na mwanangu hao,nikampigia Chacha nikamuukiza nikulindaje akasema wewe usijali nipe 50 kibingwa na yule Marwa nikamtia 50 nae nikasepa zangu
IMEISHA HIYO
NB:Yule hakimu miaka michache mbele alikamatwa kwa kesi ya rushwa na hadi leo hajarejeshwa kazini kwakuwa malakamiko yalikuwa mengi sana juu yake tena ni rafiki yangu fb eti nae anaweka nyimbo za mapambio kujifanya mwema😂😂 kuna siku nikacomment katika moja ya post yake "PRACTICE WHAT YOU PREACH!" Ila kitambo sijamcheki kama bado anapost post na akiendelea kupost kujifanya mwema mtamuweka hadharani NWAMA YULE! MLA RUSHWA NA MPOTEZA HAKI ZA WATU! (nilitaka kuandika za wanyonge nikajipima nikagundua simo kundi hilo)
IMEISHA WANDUGU!
Nisamehe sitorudia Lovelovie pulizii oooShindwaaaaaaaa kabisa
Umefanya vizuri hakuna kupoteza mudaaaa...Komaa kwani mie nimekomaa kuiandika leo tu tena kwa kutumia simu nilikuwa naandika napost whatsapp,naandika napost uko hadi nilipopata 4 ndio nikawa napost moja moja
Mie sungusungu tu! Au wale suma jkt!Hakii ulitakiwa uwe mjeshi hakuna kucheka na kimaa!![emoji89]