NILIVYOMKOMESHA TAPELI WA VIWANJA KIVULE
Sehemu ya 3
KAMA NOMA NA IWE NOMA
Siku ya jumatatu asubuhi na mapema nikiwa na akili zangu za usiku nikatoka zangu Magomeni kuelekea pale Staki shari mapema tu moja kasoro kadhaa niko pale nikawakuta maaskari wanajipanga kwa ajili ya lokoo ya kuanza siku mpya na kulikuwa na kiongozi wao yeye akiwa amevaa combat kama za wale field force mtu mzima hivi mfupi na mweupe kiasi nikamngojea awakague wale maaskari na nikamwendea nikidhani ndio mkuu wa kituo nikamsalimu na kumuelezea changamoto zangu na akanambia yeye sio mkuu ila nipite pale kolidoni na nikate kulia nisome vibao juu ya milango na nikae nje ya mlango ulioandikwa MKUU WA KITUO,nikamshukuru na nikaingia ndani kufata maelezo niliyopewa,nilipofika kaunta askari aliyekuwepo akaniuliza ninapoenda na nikamuelezea ninapoenda,nikasoma vibao na nikafika eneo husika uzuri wake kulikuwa na kibenchi nikakaa pale kimya,sasa wakati nimekaa pale kumbuka maaskari wengi si wananifahamu wakawa wananiuliza kulikoni nikawa namngojea mkuu na nadhani katika wale maaskari walionikuta pale wakaenda kumtonya yule mpelelezi mzee Juma akaja pale anajifanya kama anaongea peke yake kuwa najisumbua tu uko ninapotaka kwenda nami wala sikumjibu kwani ilibidi nijiusie mwenyewe moyoni kwani nilikuwa na donge limenibana sana nikifikiria nadai changu naonekana msumbufu? Tena mtuhumiwa nimemkamata amempa dhamana alafu ananambia nikakae nyumbani hadi atakapopatikana eti ndio atanipigia,leo ananiona mimi ndio tatizo,nikajiambia nisifungue mdomo acha alopoke tu.
Mara akafika askari aliyekuwa amevaa kiraia na akatoa ufunguo na kufungua kile chumba na nyuma yake akiwa ameongozana na kundi la watu kama watano hivi na yule kiongozi akanisalimu huku akiwa ameshafungua mlango nami nikajibu salamu yake na akaniuliza tatizo langu maana yeye hakuwa na muda kwani alitakiwa kwenda uwanja wa ndege kusimamia msafara kuna ugeni unakuja kwahiyo lazima awepo eneo la tukio ila kwakuwa ni jumatatu anataka kufanya kikao kidogo na watendaji wake kupata details za yaliyojiri kwa wiki nzima iliyopita,wakati huo ananipa maelezo hayo tukawa yeye na mimi na wale wenzake tumeshaingia ndani ya kile chumba na akanitaka kama sitojali nimngojee hadi atakapotoka uwanja wa ndege ila nikamuomba sana anipe japo dakika 5 tu kwangu zingenitosha kujua hatima ya shauri langu naye akanipa!
Nikajitambulisha na kumueleza suala langu na aliyekuwa na faili na matukio yote toka kumkamata na hadi kuachiwa na kutakiwa nijae nyumbani hadi atakapopatikana mtuhumiwa na nikahitimisha kwa kumuomba kuwa "yeye ndio mtu wa mwisho katika kituo ambacho faili la kesi yangu lipo naomba kauli yako kuwa kituo kimeshindwa kutatua tatizo langu na unanipa ruksa ya kwenda mbele kusaka haki yangu" tena yule mzee Juma aliwa ameitwa na miongoni mwa waliokuwa pale kumbe kulikuwa na mkuu wa upelelezi wa kituo na maofisa wengine,yule mzee Juma anaulizwa hana analosema lenye mashiko na mkuu akawauliza "toka mmeanza kufanya kazi kwenu mmeshakutana na mwananchi mwenye uthubutu wa kudai haki yake katika mfumo huu? Huu ni mtego kwani kama ameweza kuja hadi kwangu je anashindwa kwenda wapi? Mtuhumiwa kamleta mmemtoa,mwendelezo hamtoi je afanyaje?" Yule mzee Juma akajitdmtea kuwa nitoe pesa ya mafuta ya gari ili waende kumsaka na yule mkuu akaniuliza je nipo tayari kutoa pesa ya mafuta? nikamjibu pale pale nishapoteza pesa na mtuhumiwa nishamleta sina hiyo pesa na huyu mpelelezi yeye kama kutoa ndio atoe kwani alijiridhisha akampa dhamana,sina hiyo pesa,yule mkuu akaona huu mziki sasa akanambia sara naomba japo siku 3 nitakupatia jibu nikamwambia poa ntakuja ijumaa na nikatoka zangu huyooo!
Ile ijumaa mimi sikuenda nikakaa kama wiki kadhaa ndipo huo msemo wa MUNGU SI ATHUMAN ukachukua nafasi tena kwani yule bwana Juma Kasangu akawa anaendelea na utapeli wake sijui walimtapeli mama gani uko waliuza nyumba yao ya familia uko Buguruni na yule mama akaenda kununua kiwanja na kwakuwa alikuwa na pesa tayari ujenzi ukaanza mara moja na mama ujenzi umefika kwenye rinta akaja kuelezwa kuwa eneo analojenga sio lake na kule jirani na eneo ambalo mimi nimeuziwa kulikuwa na eneo kubwa sana lilikuwa linamilikiwa na taasisi flani inaitwa UVIKIUTA sijajua wanajihusisha na nini na hawa kina Kasangu wakawa wanaenda kuwauzia watu viwanja kule na wale jamaa uwa wakifanya operesheni inakuwa kama vita wanakwenda kamili na field force na mabomu ya machozi kutokana na historia ya eneo lenyewe na asilimia kubwa ya wakaazi wa maeneo yale walikuwa Wakulya na kama unavyojua hawa ndugu zetu,tatizo kule mpaka wa wale Uvikiuta hakukuwa na mipaka yenye kuonekana wazi sasa unaweza kuwa hapa ukaambiwa upo nje pale ukaambiwa upo ndani yaani wanaweza kuja awamu hii ukaachwa na wakaja awamu nyingine ukatolewa mkukumkuku sasa wale kina Kasangu ndio wakawa wanatumia huo kutokuwepo na mipaka ya wazi kama njia ya kuwapiga wananchi.
Sasa kumbe yule bwana Juma Kasangu akiwa na vijana wake waliuza sijajua eneo gani na nasikia walipata kama milioni 8 hivi yule bwana akawa amewadhulumu wenzake na kati ya aliowashirikiana nao kuna jamaa anaitwa Chacha😂,huyu bwana nadhani alipewa namba yangu na yule Marwa kwani alinipigia siku hiyo sina hili wala lile akataka kuonana nami nikamuelekeza na akaja mara moja Ilala tulikutania pale Ilala mtaa wa Kigoma na Moshi kulikuwa na duka la Mangi,akanieleza mikasa mingi na kueleza waziwazi kuwa amesikia kuhusu ishu yangu na yule wamefanya tukio pamoja na amewazika yeye na wenzake sasa hasira zake anataka kuzihamishia kwa kumkomoa kupitia mimi,ule msemo wa "adui wa adui yako ni rafiki yako" ukachukua nafasi na akanambia jinsi tunatakiwa tufanye na yeye atafanya yake kadri ya uwezo wake na kazi alitaka ifanyike mapema iwezekanavyo nami nikimshirikisha mshkaji wangu mmoja anaitwa Kindamba na Kindamba akampigia Kasangu na kumwambia anataka eneo kwani amepewa namba kupitia rafiki yake,Kasangu akamuuliza kuwa anakaa wapi naye akamjibu kuwa anakaa Mwananyamala A na akamwambia atakuja jioni akitoka kazini ili aje aone maeneo (tulipanga iwe jioni kwa sababu mbalimbali nazo ni kuweza kufika eneo wakati ofisi za serikali ya mtaa kumefungwa,mimi kutoonekana kwakuwa giza litakuwa lishashuka na kuepusha wambea kuwa wengi na kupata kujipanga vyema)
Itaendelea...