shikamkono01
JF-Expert Member
- Mar 26, 2016
- 685
- 2,055
NILIVYOMKOMESHA TAPELI WA VIWANJA KIVULE
Habari zenu wadau wa JF!
Leo nami nimeonelea niwasimulie kisa changu jinsi nilivyomkomesha tapeli maarufu wa viwanja maeneo ya Kivule ajulikanaye kama Juma Kasangu,mnamo mwaka 2014 mwanzoni nikiwa katika harakati zangu za kutaka kujipatia eneo nikamshirikisha rafiki yangu mmoja ambaye yeye alishakuwa na eneo kule Kivule maarufu kama kwa mama Anna Mkapa
Huyu jamaa yangu alishaanza na ujenzi akawa ameshaweka msingi ila kutokana na changamoto za kiuchumi akawa ameliacha kwanza avute nguvu ndipo nami baada ya kumueleza tamanio langu naye akanipeleka nikapaone eneo analojenga nami baada ya kufika kiukweli nikapapenda sana kwanza pako tambarare, mazingira rafiki, mji ulikuwa umepangiliwa kwani Serikali ya mtaa ilichora njia kabisa na walikuwa wakali hadi kufikia kupita mara kwa mara kwenye maeneo ya ujenzi kuhakikisha hakuna anayejenga kiholela, mpangilio wa mitaa ulitiliwa mkazo sana, hizo ni mojawapo wa sifa kuu zilizopelekea kupapenda eneo lile.
Sasa kwakuwa huyu jamaa yangu alinunua eneo kutoka kwa huyu Juma Kasangu nami akaniunganishia kwake ili niweze kupata eneo maeneo karibu na eneo la kwake,(waweza kushangaa imekuwaje nimpe sifa ya utapeli wakati aliyenipeleka nae aliuziwa eneo na huyo huyo tapeli😂😂)
Kiukweli huyu Kasangu ni mbwa miongoni mwa mambwa koko wakubwa sana kiukweli sijui hatima yangu na namuomba sana Mungu anijaalie mwisho mwema ila huyu jamaa ana mzigo mzito sana kesho mbele ya muumba wake kama hajajirekebisha (sina uhakika kama bado yuko hai).
Huyu jamaa yangu nae wakati wa kimbembe changu ndipo akaja kupewa mkanda wake ponapona yake ilikuwaje hadi kutofikia kutapeliwa, kumbe kilichomuokoa ni kuwahi kuanza kujenga lile eneo kwani kumbe pale alipouziwa jamaa yangu mwenye eneo ni baba mkwe wake Kasangu (baba wa mkewe) na walipoona pameshaanzwa ujenzi ikabidi wakamalizane kiukwe na kutoyatoa hadharani (naamini hata huyo baba mkwe hakupewa chochote)
Turudi sasa katika sakata langu, siku hiyo mimi na jamaa yangu na ndugu yangu mwingine baada ya kumpanga bwana Kasangu, Jumamosi moja tukatoka makwetu wakati huo mimi nakaa Ilala Sharifu Shamba na wenzangu walikuwa wanatokea maeneo ya Ilala sokoni (kiuzawa mimi nimezaliwa maeneo ya Ilala sokoni) tukaelekea eneo la tukio kwa kupanda gari hadi Banana pale tukapanda hadi Kivule napo tukatembea mdogo mdogo kwenda huko kwa mama Mkapa (kulikuwa hakuna vigari wakati huo ni bodaboda tena hazikuwa kihivyo kuna mchanga sana ila nasikia siku hizi daladala zinafika)
Kasangu akaja na vijana wake wawili (Kasangu kikabila ni mnyamwezi)hao vijana walikuwa ni wakurya nao ni Marwa na mwingine sikuwa nimemtambua kwa jina vizuri maana ni siku hiyo tu sikumuona tena wakati wote wa sakata hili
Marwa nilimtambua kwakuwa uko mbele pia nilipata msaada wake, sasa tukafika eneo la tukio na akatuonesha viwanja vitatu ambavyo viko kama mita 120-150 kutoka eneo ambalo jamaa yangu ameuziwa, tukavikagua na mwishowe nikakichagua cha kukichagua na ikafika muda wa kufanya malipo na yule mtu aliyekuja nae pamoja na Marwa alinitambulisha kama mjumbe wa eneo lile kwani pia alikuwa na mihuri kabisa na mauzo yalikuwa ni 1,200,000/= (mauzo yote yalikuwa ni 1,500,000) nikampatia pesa na mashahidi wakaweka saini zao na nikamtaka lazima twende Serikali ya mtaa kukamilisha makubaliano ndio nimmalizie hiyo 300,000 yake
Tukatoka eneo la tukio salama na jamaa yangu akanisisitiza kuanza ujenzi japo msingi wa vyumba viwili kwani jambo la moto unalifanya na moto wake nisipoe tena nami baada ya kama miezi minne nakumbuka nikaanza kujipanga na kuanza ujenzi (pesa yake iliyobaki nikawa nampa kidogo kidogo mara 50 mara 20)
Itaendelea...
Habari zenu wadau wa JF!
Leo nami nimeonelea niwasimulie kisa changu jinsi nilivyomkomesha tapeli maarufu wa viwanja maeneo ya Kivule ajulikanaye kama Juma Kasangu,mnamo mwaka 2014 mwanzoni nikiwa katika harakati zangu za kutaka kujipatia eneo nikamshirikisha rafiki yangu mmoja ambaye yeye alishakuwa na eneo kule Kivule maarufu kama kwa mama Anna Mkapa
Huyu jamaa yangu alishaanza na ujenzi akawa ameshaweka msingi ila kutokana na changamoto za kiuchumi akawa ameliacha kwanza avute nguvu ndipo nami baada ya kumueleza tamanio langu naye akanipeleka nikapaone eneo analojenga nami baada ya kufika kiukweli nikapapenda sana kwanza pako tambarare, mazingira rafiki, mji ulikuwa umepangiliwa kwani Serikali ya mtaa ilichora njia kabisa na walikuwa wakali hadi kufikia kupita mara kwa mara kwenye maeneo ya ujenzi kuhakikisha hakuna anayejenga kiholela, mpangilio wa mitaa ulitiliwa mkazo sana, hizo ni mojawapo wa sifa kuu zilizopelekea kupapenda eneo lile.
Sasa kwakuwa huyu jamaa yangu alinunua eneo kutoka kwa huyu Juma Kasangu nami akaniunganishia kwake ili niweze kupata eneo maeneo karibu na eneo la kwake,(waweza kushangaa imekuwaje nimpe sifa ya utapeli wakati aliyenipeleka nae aliuziwa eneo na huyo huyo tapeli😂😂)
Kiukweli huyu Kasangu ni mbwa miongoni mwa mambwa koko wakubwa sana kiukweli sijui hatima yangu na namuomba sana Mungu anijaalie mwisho mwema ila huyu jamaa ana mzigo mzito sana kesho mbele ya muumba wake kama hajajirekebisha (sina uhakika kama bado yuko hai).
Huyu jamaa yangu nae wakati wa kimbembe changu ndipo akaja kupewa mkanda wake ponapona yake ilikuwaje hadi kutofikia kutapeliwa, kumbe kilichomuokoa ni kuwahi kuanza kujenga lile eneo kwani kumbe pale alipouziwa jamaa yangu mwenye eneo ni baba mkwe wake Kasangu (baba wa mkewe) na walipoona pameshaanzwa ujenzi ikabidi wakamalizane kiukwe na kutoyatoa hadharani (naamini hata huyo baba mkwe hakupewa chochote)
Turudi sasa katika sakata langu, siku hiyo mimi na jamaa yangu na ndugu yangu mwingine baada ya kumpanga bwana Kasangu, Jumamosi moja tukatoka makwetu wakati huo mimi nakaa Ilala Sharifu Shamba na wenzangu walikuwa wanatokea maeneo ya Ilala sokoni (kiuzawa mimi nimezaliwa maeneo ya Ilala sokoni) tukaelekea eneo la tukio kwa kupanda gari hadi Banana pale tukapanda hadi Kivule napo tukatembea mdogo mdogo kwenda huko kwa mama Mkapa (kulikuwa hakuna vigari wakati huo ni bodaboda tena hazikuwa kihivyo kuna mchanga sana ila nasikia siku hizi daladala zinafika)
Kasangu akaja na vijana wake wawili (Kasangu kikabila ni mnyamwezi)hao vijana walikuwa ni wakurya nao ni Marwa na mwingine sikuwa nimemtambua kwa jina vizuri maana ni siku hiyo tu sikumuona tena wakati wote wa sakata hili
Marwa nilimtambua kwakuwa uko mbele pia nilipata msaada wake, sasa tukafika eneo la tukio na akatuonesha viwanja vitatu ambavyo viko kama mita 120-150 kutoka eneo ambalo jamaa yangu ameuziwa, tukavikagua na mwishowe nikakichagua cha kukichagua na ikafika muda wa kufanya malipo na yule mtu aliyekuja nae pamoja na Marwa alinitambulisha kama mjumbe wa eneo lile kwani pia alikuwa na mihuri kabisa na mauzo yalikuwa ni 1,200,000/= (mauzo yote yalikuwa ni 1,500,000) nikampatia pesa na mashahidi wakaweka saini zao na nikamtaka lazima twende Serikali ya mtaa kukamilisha makubaliano ndio nimmalizie hiyo 300,000 yake
Tukatoka eneo la tukio salama na jamaa yangu akanisisitiza kuanza ujenzi japo msingi wa vyumba viwili kwani jambo la moto unalifanya na moto wake nisipoe tena nami baada ya kama miezi minne nakumbuka nikaanza kujipanga na kuanza ujenzi (pesa yake iliyobaki nikawa nampa kidogo kidogo mara 50 mara 20)
Itaendelea...