Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua Nyumbani

Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua Nyumbani

Mnafanya biashara za haramu halafu hamna codes za mawasiliano??!! Criminal gang lazima iwe na code hata kama ameshikwa na polisi akianza kuongea tu kwenye simu mwenzake lazima ajue kuwa hali sio hali au unatoa muda feki wa kufika eneo la tukio then unafika mapema sana kucheki mazingira ukiona hali haieleweki unapotea tu.
Hata mimi nimeshangaa sana. "^Uko wapi ? Njoo nyumbani."
 
Wewe ndiye uliyeniquote, sikuwa naongea na wewe, guess what, mwenye shobo ni nani kama siyo wewe?

Kuanzia sasa naku-ignore, wewe ni mjinga na unaonekana ukielekezwa na wakubwa wako hujifunzi.
Ninachofanya ni kukueleza tu kwa wema kuwa utaposwa acha shobo bwamdogo,acha kudandia usiyoyajua
 
Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 12.



Niliendelea kumtazama dogo kwa makini asije kuwa anakuja na watu ili ikiwezekana nichukue hatua katika mbio!.Baada ya kujiridhisha ya kwamba alikuwa akija yeye mwenyewe nilikaa kwa kutulia nikiendelea kumsubiria!.

Dogo "Bro jamaa kasema akupatie ngapi!"

Mimi "Sijakuelewa!"

Dogo "Jamaa ameniambia waweza taka pesa ngapi kwa ile exchange!?"

Mimi "Kwani jamaa huwa anabadili kiasi gani kwa kila Tsh 10,000!"

Dogo "Sikia bro kwanini nisikupeleke kwa huyo mjamaa ukaelewane nae!"

Mimi "Jamaa anafanyia kazi zake wapi?"

Dogo "Yuko tu hapo ng'ambo na hata siyo mbali!"

Mimi "Hakuna wanoko?"

Dogo "Ati unasema aje!?"

Mimi "Hakuna tatizo nikienda kwake?"

Dogo "Wala hakuna problem yeyote,jamaa yuko fiti tu!"


Sasa baada ya mazungumzo na yule dogo kumbe alimuachia huyo jamaa ile hela na jamaa akawa amemwambia aje aniulize ili kujua kwenye ile laki mimi angenipatia kiasi gani,basi kiukweli niliogopa sana na nikaona uenda ulikuwa ni mchongo wa mimi kudakishwa!.Lakini nilipompeleleza yule dogo sana akaniambia jamaa anauza vifaa vya magari,hivyo pia huwa anabadilishaga na hela!.Basi ili kuonekana sikuwa na wasiwasi nikamwambia dogo tuelekee kwa yule jamaa!.Tulitembea kwa takribani dakika 4 tukawa tumefika kwa yule jamaa ambaye alikuwa na duka la spare za magari!.Kiukweli niliamua kujiamini na niliamua kuiweka hofu kando,sasa yule jamaa alikuwa ni mkenya ambaye alionekana kiswahili kukifahamu vizuri japo kuna muda pia alikuwa akichapia!.

Jamaa "Mambo vipi bro"

Mimi "Poa kabisa"

Jamaa "Ni wewe ndiye umemwagiza Mkamilifu?"

Mimi "Yes ni mimi!"

Jamaa "Oooh hapo iko poa,maana hata sikumuelewa"

Aliendelea "Ulitaka sasa bro nikupee pesa ngapi?"

Mimi "Wewe huwa unabadili kiasi gani kwa kila Tsh 10,000?"

Jamaa "Mimi bro nitakupea Ksh 3500!"

Mimi "Ok sawa haina tatizo"

Basi kimoyo moyo nilikuwa namshukuru Mungu sana kukutana na yule jamaa maana kiukweli kama angekuwa mjuaji pale nisingechomoka!.Jamaa aliingia dukani akawa amenipa Ksh 3500 ambapo na mimi nilimpatia yule dogo Ksh 500.Sasa jamaa akaniambia kama nilikuwa ninapesa nyingine nimpelekee maana baada ya siku mbili alikuwa anatoka!,sasa yeye alichoamini ni kwamba kupitia hela ile angejipatia faida mara dufu,kuna muda nilikuwa naona kabisa natenda dhambi lakini sikuwa na namna kwasababu mimi nilichotaka ni pesa tu!.

Jamaa "Bro kama uko na pesa ingine waweza tu niletea nikubadilishie!"

Kimoyo moyo nikasema "wewe humjui umughaka vizuri,ngoja nikuonyeshe mimi ni nani".Basi nilimwambia ningerudi jioni kuleta hela kiasi fulani anichenjie.Basi tuliondoka na dogo huku tukiendelea kupiga stori za hapa na pale,nilimwambia dogo anionyeshe maduka ya nguo ili ninunue sweta nivae maana kwa kipindi kile kulikuwa na baridi ya kiaina hapo Migori!.Baada ya kununua sweta mimi nilirudi lodge na dogo akaelekea kuendelea na mishe zake!.

Sasa ilipofika mida ya saa 12 jioni sikumuoma dogo nikajua uenda atakuwa ametingwa na majukumu,basi nikachomoa tena mle kwenye begi shilingi laki moja nikaelekea kwa yule jamaa.Nilipofika jamaa alinipatia Ksh 3500 kama kawaida na kiukweli alikuwa akinishangaa sana na alitaka kufahamu kwa Tanzania nilikuwa natokea maeneo gani,mimi nilimdanganya ni mwenyeji wa Mwanza!.Kama nilivyosema hapo awali ya kwamba,baada ya kujishughulisha na hiyo shughuli haramu hata muonekano wangu ulibadilika sana na ulikuwa ukiniangalia huwezi amini kama mimi ni mpiga debe pale Sirari!.Sasa baada ya jamaa kunipatia ile hela nililipa pale lodge pesa ya siku mbili nikawa nimebaki na pesa kadhaa!.Nilitaka nikae pale Migori ndani ya siku 3 halafu nigeuke zangu Sirari ili nikaone kama mambo yalikuwa yamepoa!.Niliamini ya kwamba kama jamaa angetoka akaenda kubadili zile hela halafu wakamshitukia basi najua angemtafuta dogo Joe akawaleta pale Lodge nikapata kashikashi,hivyo nilipanga nichomoke mapema kabisa!.

Sasa kabla ya kuondoka nilinunua begi dogo la mgongoni kisha nikanunua na suruali ya jeans moja nikawa nimebadilisha,zile hela niliziweka kwenye lile begi la mgongoni pamoja na ile shati niliyokuwa nimevaa siku naingia hapo Migori,ile sweta na jeans nikavaa nikawa sasa na muonekano mpya!.Sasa siku naondoka nilienda kuonana na yule dogo Joe pale stendi nikamkabidhi lile begi nikampatia na hela kiasi cha elfu 50 ya Tanzania,sasa ilikuwa ni juu yake kuzibadili ili aionjoi maisha,kama walidamka basi ni yeye na mungu wake!.

Nilipanda zangu shuttle za Isebania nikageuka zangu.Nilipofika pale Isebania nilishuka nikaingia zangu kitaani kupita njia isiyokuwa rasmi kuingia Sirari,ile njia walikuwa wakiipita watembea kwa miguu hivyo hakukuwa na bugudha toka kwa mamlaka zote mbili!.Ilijulikana ya kwamba watu wa Kenya wanapita kuingia Tanzania na watanzania walikuwa wanaingia Kenya kununua bidhaa na mahitaji.Sasa nilipofika hapo Sirari,sikutaka kabisa kwenda moja kwa moja nyumbani,nilianzia kwanza kijiweni!.Nilipofika pale niliwakuta wadau wangu wakiwa wanaendelea na kazi huku wengine wakishangaa na kuniuliza ndani ya siku mbili tatu hizo nilikuwa wapi!.Mshikaji wangu Nyamori sikumuona hapo kijiweni hivyo nikaelekea dukani kwa yule mama kununua vocha ili nimpigie simu.

Nilimpigia simu yake ikawa inaita tu bila kupokelewa,basi nilipoona haipokelewi nikaamua kuachana nae,sasa ikabidi nimpigie Gabriel,nilipoipiga namba yake ikawa haipatikani!,nikarudia tena lakini haikupatikana!.Sasa sikutaka kumtafuta kabisa yule mwanamke wake kwasababu nilikuwa nakifahamu kichwa chake kilivyokuwa kibovu!.Nia ya mimi kumtafuta Gabriel nilitaka kujiridhisha kama yuko hewani ili anieleze kilitokea nini siku ile,sasa nilipomkosa niliamua kupiga kimya!.Sasa wakati nikiwa naendelea kutafakari,kuna mshikaji alikuwa mdau hapo kijiweni nae alikuwa mpiga debe,huyu alikuwa akiitwa Magesa!.Sasa jamaa akawa ananiambia kuna jamaa toka juzi alikuwa akinitafuta hapo kijiweni na hata asubuhi ametoka hapo kuniulizia!.

Mimi "Jamaa yukoje?"

Magesa "Ni jamaa mmoja hivi tolu halafu blaki!"

Mimi "Alikuwa anasemaje?"

Magesa "Aisee hata sijui maana juzi ameshinda hapa na hata leo pia amekuja lakini hakukaa!"

Mimi "Alikuwa na gari?'

Magesa " Sijajua kama ana gari maana hapa hakuja na gari"

Baada ya Magesa kuniambia vile kiukweli moyo wangu ulilipuka tena kwa hofu,kwa namna alivyozitaja sifa chache za huyo mtu nilijiridhisha kabisa ya kwamba hakuwa Gabriel.Sasa baada ya muda kidogo nikiwa pale kijiweni simu yangu ikawa inaita,kuangalia nikakuta ni Nyamori alikuwa akinipigia.

Nyamori "Mwanangu ulikuwa wapi?,mbona simu yako ilikuwa haipatikani!"

Mimi "Mwanangu nilienda hapo Migori mara moja"

Mimi " Nipo hapa kijiweni lakini sikuoni!"
Nyamori "Mi nilitoka niko Nyamongo tangu jana,kuna mzee tumemletea ng'ombe hivyo nitarudi jioni au kesho asubuhi"

Aliendelea "Sasa sikia,kuna jamaa mmoja ni askari namjua,toka juzi anakusarandia hapo kijiweni Mwanangu"

Basi baada ya jamaa kuniambia vile sikutaka kabisa kupoteza muda pale kijiweni nikawa nimeondoka,sasa ndipo nikaunganisha na yale maelezo ya magesa nikaona kumbe bado kulikuwa na msako unaoendelea kimya kimya!..

Nyamori " Mwanangu kwani kuna ishu gani?

Mimi "Mwanangu bado ni ile ishu ya deni!".

Nyamori "Kwanini usimwambie mshikaji uwe unamlipa kidogo kidogo mpaka umalize ili aache kukusumbua!"

Mimi "Nitajua cha kufanya Mwanangu!"

Yeye hakufahamu kwamba ni lile dili haramu ndilo lilikuwa likiniangaisha,alichofahamu na nilichomwambia ni kwamba nilikuwa ninadaiwa!.

Basi nikaondoka zangu nikawa natembea haraka uelekeo wa Tarime ili nikapande gari nielekee Tarime mjini,sasa sikutaka kunyooka na lami,nilipita pembezoni mwa barabara ili nikifika mbele nidandie gari mpaka Tarime!.Wazo la kurudi tena pale geto kwangu sikuwa nalo kabisa na niliamua kama ni vitu ngoja viozee ndani lakini si kwenda kujikamatisha!.

Sasa namshukuru Mungu nilifika Tarime na niliamua kupita njia nilizokuwa nazifahamu kuelekea nyumbani kwetu ambako Mzee miezi michache iliyopita alikuwa amenitimua!.Nilipofika hapo nyumbani nilimkuta binti ambaye nilikuwa simfahamu na nilipomuuliza wenyeji wameenda wapi akawa ameniambia Mzee hajui alipo kwenda ila mama yangu alikuwa ameenda sokoni na dogo Amos yeye alikuwa shule!,sasa niliondoka mdogo mdogo kuelekea sokoni ambako mama yangu alikuwa akifanyia biashara zake!.
Umughaka unacheza mchezo wa hatari sana, kuendelea kubaki sirare au tarime unatafuta matatizo makubwa zaidi, ulipojithibitishia polisi bado wanakuwinda ilikua uhame kabisa mkoa, Piga ruti ndefu kajichimbie zako Chitogholi- Tandahimba Mkoani Mtwara.
 
Wewe ndiye uliyeniquote, sikuwa naongea na wewe, guess what, mwenye shobo ni nani kama siyo wewe?

Kuanzia sasa naku-ignore, wewe ni mjinga na unaonekana ukielekezwa na wakubwa wako hujifunzi.
Uliingilia majibizano yangu mimi na yule mwanamke mwenzako ndio maana nakueleza ukweli choko wewe
 
Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 11.




Nililipa kiasi cha Ksh 50 kwenye Hiace(Shuttle) iliyokuwa ikielekea Kisumu na niliwaambia waniache Migori.Migori ni mji ambao ulikuwa ni mkubwa tu na hapo kabla sikuwahi kufika lakini katika stori za washikaji walikuwa wakidai ni mji ambao ulikuwa jirani sana na Isebania,nilichokua nimepanga ni kwamba nikifika hapo mji wa Migori nitajua cha kufanya,jambo la msingi ni kutoka kwanza hapo Sirari ambapo hali ya hewa ilikuwa imechafuka!.

Nikiwa kwenye gari nilikuwa nimekumbatia kile kibegi ambacho hakikuwa kizito na kiukweli nilikuwa kama nimepagawa na kuduwazwa na ile hali ya hofu niliyokuwa nayo!.Tulitumia takribani nusu saa mpaka dakika arobaini kufika hapo mjini Migori!.

Nilipofika nilishuka na nilitembea kuelekea juu kama narudi tena Sirari,sasa nilipofika kwa mbele nilikutana na jamaa nikamuuliza anielekeze ilipo Guest House ili niende nikapumzike,sasa kwa wale jamaa wao walikuwa wanaita Lodge,ulikuwa ukiuliza neno Guest House kidogo wanakushangaa,basi jamaa akawa amenionyesha Lodge moja ambayo haikuwa mbali na ile stage(stand).

Nilifika pale nikauliza vyumba nikaambiwa ni Ksh 350,nilichomoa hela nikawa nimempa kisha nikaonyeshwa chumba changu!.Kiukweli baada ya kuingia chumbani akili yangu ilitulia sasa!,niliingia bafuni kuoga na nilipomaliza nililala sana na nimekuja kushituka ikiwa mida ya 12 jioni!,basi nikaamua kuamka ili niende kutafuta mahali walipokuwa wanauza msosi ili nitwange nirudi ndani,sasa nilijaribu kumuuliza yule jamaa wa pale mapokezi akawa amenionyesha kimgahawa ambacho hakikuwa mbali na lile eneo,sasa baadae nilikuja kufahamu kumbe mwenye ule mgahawa ndiye aliyekuwa mwenye ile Lodge!.

Nilipofika hapo Migori kiukweli kilichonichanganya ni namna ya kuitumia hela ya Kenya kiusahihi,kuna muda nadhani nilikuwa naibiwa kwasababu sikuwa na muda wa kuanza kuhesabu hesabu vichenji vilivyokuwa vinabaki!.

Sasa wakati natoka Sirari,kwenye lile begi nilikuwa na kiasi cha Tsh milioni 5,na sikufahamu nitazifanyia nini nikiwa hapo Migori!,Sasa asubuhi kulipokucha niliamka mida ya 4 asubuhi nikanawa uso na kupiga mswaki kisha nikaondoka kuelekea pale kwenye kile ki-mgahawa ili kupata chai!.Ule mgahawa ilionekana kwa lile eneo ulikuwa unauza sana kwasababu ile jioni na hata asubuhi nilipoingia nilikuta kuna watu wengi wakipata vyakula mbalimbali,sasa wakati nimeagiza chai na chapati nikiwa nasubiria,ghafla waliingia jamaa wawili wakiwa wamevaa makoti ya kijeshi na suruali za kijani huku wakiwa na bunduki!,nilipata hofu sana lakini nikawa mtulivu,sasa kumbe wale jamaa walikuwa ni askari wa Kikenya na ndivyo walivyokuwa wakivaa,haukupita muda waliongezeka na wengine wawili wakiwa na silaha kama wenzao!.Basi nao walikaa wakawa wameagiza chai wakaendelea kunywa!.

Muda huo nilijikausha kama sina habari na mtu,namshukuru Mungu pia na wao hawakuwa na habari na mtu!,walipomaliza walinyanyuka wakawa wameondoka,sasa nilikuja kugundua kumbe lile eneo nililokuwepo halikuwa mbali na kituo cha polisi hapo Migori na kituo chenyewe kilikuwa barabarani kabisa,niliona lile eneo si sahihi kwangu,hivyo nikapanga ikifika mchana niondoke lile eneo nikatafute Lodge nyingine ambayo itakuwa mafichoni kidogo!. Kiukweli ile hela niliyokuwa nimebadili ilimalizika siku hiyo baada ya kutafuta Lodge nyingine iliyokuwa pembeni ya mji kama unaelekea Kisumu,sasa hofu ilianza kunijaa namna nitakavyoweza kusavaivu kwa kipindi chote nitakachokuwa huko!.

Ilipofika mida ya jioni nilitoka nikaelekea pale stendi kwa mguu na nilipofika jamaa walidhani ni abiria wakaanza kunichangamkia na niliwaeleza mimi si abiria,nilikaa pembeni kujaribu kuangalia namna wanavyofanyakazi lakini kila nikijaribu kuangalia mdau angalau nilete mazoea lakini hola!,kiukweli sikufahamu nitaishije yale mazingira ambayo sikuyazoea!.Utofauti niliuona pale stendi ni kwamba jamaa walionekana kujitahidi kuchangamka lakini bado washikaji na wahuni niliokuwa nikifanya nao kazi pale Sirari walikuwa wamewazidi wale wajaluo kwa uchangamfu!.Basi siku hiyo niliamua kurudi zangu pale Lodge ambako nililala mpaka asubuhi,ilipofika mida ya saa 3 asubuhi nilitoka zangu nikarudi pale stendi kushangaa,sasa nikasogea zilipokuwa zinapaki gari za kuelekea Isebania,pale niliwakuta jamaa wanaongea kikurya hivyo nikajiona kabisa kama nipo Sirari,sasa kuna dogo alikuwa konda akiita abiria kwenye zile shuttle na alikuwa amevaa tisheti iliyokuwa na picha ya Chege na Temba huku ikiwa imeandikwa TMK WANAUME,sasa baada ya kumcheki kwa muda mrefu yule dogo ni kama alinivutia kwa namna alivyokuwa mchangamfu!,sasa baada ya kuitia ile shuttle na kujaza,nilimsogelea kutaka angalau mazoea nae ili ikiwezekana yeye ndiye aifanye ile kazi ya kubadili zile hela wakati nikiwa kule!.

Mimi "Mwanangu mambo niaje?"

Dogo "Ni bomba bro!"

Mimi "Una muda mrefu sana hapa eeh!"

Dogo "Yes bro tuko hapa kitambo!"

Sasa wakati naongea nae hakusita kuniuliza kama mimi ni Mtanzania maana ongea yangu na yake ilikuwa tofauti kabisa!.

Mimi "Unaitwa nani mwanangu?"

Dogo "Mimi naitwa Joe lakini wengi huniita Mkamilifu!"

Dogo "Na wewe bro majina yako nani?"

Mimi " Mimi naitwa Umughaka"

Dogo "Its your first time hapa Migori?"

Mimi "Hapana,huwa nakuja mara kibao tu!"

Dogo "Mi pia huwa nakwenda Sirare kwa jamaa zangu"

Sasa wao kwa kule badala ya kuita Sirari,wao walikuwa wakiita Sirare na hata shuttle zao zote za kuelekea Sirari zilikuwa zimeandikwa Sirare,nadhani ilikuwa ni lafudhi tu lakini walikuwa wakimaanisha Sirari!.Sasa dogo alionekana kupafahamu vizuri Sirari na hata maeneo baadhi niliyomtajia alionekana kuyafahamu!.Pia nilimdanganya kwamba hapo Migori mimi sikuwa mgeni ili isije akawa mkora akatafuta genge la kihalifu wakanifanya kitu mbaya!.

Sikutaka stori nyingi kwasababu sikuwa na hela ya kunivusha siku itakayofuata,nilitaka yeye ndiye akawe chambo wa kubadili zile hela na nilipanga endapo kikinuka basi ningechafua hapo Migori kuendelea kusonga mbele!.


Mimi "Hivi hapa ni maeneo gani wanabadili hela"

Dogo "Ooh kwani una haraka sana bro,huwezi subiri nimalize hii job then nikuonyeshe!"

Mimi "Sawa haina noma"

Basi dogo akaendelea kupambana na ile kazi ya kuita abiria mpaka akawa amejaza tena gari ya pili,hiyo ilikuwa mida ya saa 7 mchana!.

Dogo "Naweza kukuelekeza sasa"

Basi dogo akawa amenichukua mpaka kwenye jengo moja ambalo tukaingia ndani tukakuta maduka kibao,sasa mimi baada ya kuingia mle ndani kiukweli niliona siwezi kubadili zile hela kwenye mazingira yale kwasababu ningedakwa tu!.Sasa nilimchukua dogo nikatoka nae nje nikamwambia twende mpaka kwenye ile Lodge niliyofikia kisha nikamwambia nitamlipa hela ili kufidia muda wake!.Tulipofika kwenye ile Lodge nilimuacha dogo pale mapokezi nikamwambia anisubiri,nilifungua lile begi nikatoa laki moja kisha nikaitia mfukoni nikawa nimefunga kile chumba na kutoka nje!.

Mimi "Nakupa hizi hela naomba ukabadili sehemu nyingine tofauti na pale pa mwanzo kwasababu wale jamaa wanakata hela kubwa"

Dogo "Ok bro kuna jamaa mmoja yupo hapo ng'ambo nampelekea huwa ana-exchange pesa ya Tz,nikukute basi hapa"

Mimi "Nitakulipa vizuri ukifanya vizuri!"

Dogo "Sawa bro nikukute hapa,sa hii tu nakuja!"

Mimi "Uwe muaminifu"

Dogo "Ahahaha bro ndiyo maana nikaitwa Mkamilifu,we uliza watu wote kwa pale stage hakuna ambae hanijui!"

Mimi "Sawa nakusubiri".


Basi dogo alitoka akikimbia akielekea kwa huyo jamaa kubadili ile hela niliyompatia,ile hela kama nilivyosema hapo awali ya kwamba,ulikuwa ukiiangalia kiukweli hakukuwa na shaka yeyote kwamba ilikuwa ni pesa halali kwa matumizi,uenda kama ungeiweka kwenye mashine au ungekuwa na utambuzi wa hela feki ndipo ungeifahamu!.Nilipompa dogo ile hela nilikuwa nina mambo niliyokuwa nayafikiria kichwani,kama angekimbia basi kwangu isingeniuma kwasababu nilikuwa nazo za kutosha,na kama angefanikiwa kubadili basi ndiye angekuwa rafiki yangu kwa kipindi ambacho ningekuwa hapo,lakini pia kama wangemdaka nilipanga kutoweka kama kipanga!.

Basi baada ya kama nusu saa nikiwa pale nje,nilimuona dogo kwa mbali akiwa anakuja!.
Mzee Umughaka hongera sana asee umebarikiwa sana kipaji cha kusimulia
 
Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 13.

Mimi "Mama nyakuru Mwita"

Mama "Tata sabhoke"

Ilikuwa ni heshima na salamu ambayo nilimpatia mama yangu baada ya kuwa nimefika hapo sokoni kwenye meza aliyokuwa akifanyia biashara!.

Mama "Ulienda wapi baba?"

Mimi "Nilikuwepo tu mama!"

Mama "Mbona umenenepa hivyo,au umepata kibarua huko baba!?"

Mimi "Nabangaiza tu hivyo hivyo!"

Mama "Nilimpigia mama yako mkubwa lakini akaniambia uliondoka na akajua labda ulirudi nyumbani"

Mimi "Mama nilienda kupambana na maisha yangu!".

Mama "Sasa baba utaendelea kuhangaika hivi hadi lini,rudi nyumbani mimi niliongea na baba yako na akasema hayo yameisha"

Mimi "Mama kwa umri huu siwezi kukaa tena pale nyumbani"

Mimi "Nilipita tu kuwasalimia"

Mama "Ulipita nyumbani?"

Mimi "Nimeanzia huko ndiyo nikaja hapa"

Mama "Dada yako alikuja na amemaliza kuondoka wiki iliyopita!"

Aliendelea "Chukua namba yake utawasiliana nae alisema ukirudi nikwambie umtafute"

Basi baada ya mazungumzo na mama nilichukua ile namba ya dada yangu mkubwa(Sarah)kisha nikaondoka zangu!.Mama yangu mara zote alikuwaga rafiki yangu kipenzi,pamoja na lile seke seke la mzee lakini bado alitaka nirudi pale nyumbani kitu ambacho kisingewezekana kwa wakati huo!.Sasa wakati naondoka nilimpigia dada yangu simu ili kumjulia hali maana tangu nilivyokuwa nimemaliza shule sikuwahi kuongea nae kwasababu yeye alikuwa ameolewa huko Mwanza!.

Baada ya kuongea na dada kwa dakika kadhaa alishangaa sana kwa kile kitendo ambacho mzee alinifanyia na alilaumu sana kwanini nilishindwa kumshirikisha kwa muda wote huo nikawa kimya!.

Da'Sarah "Sasa sikuhizi unafanya kazi gani hapo Tarime?"

Sikutaka kabisa kumficha kitu dada nilimwambia niliamua kuwa mpiga debe angalau maisha yaendeleee,alinishangaa sana ya kwamba nawezaje kuwa na elimu halafu niende kupiga debe!.

Da'sarah "Nilimwambia baba ukweli na kama ni kuchukia ngoja achukie,haiwezekani pesa anamalizia kwa mama yake Robina halafu sisi tunahangaika!"

Aliendelea "Kwahiyo sasa ulikuwa unakaa wapi?"

Mimi "Niliamua kupanga hapo Sirari!"

Da'Sarah "Ngoja nimwambie shemeji yako aje akutumie nauli uje huku"

Aliendelea "Na huyo mzee wala usimwambie chochote,muacheni na hela zake,yeye si anaona mama yetu hana maana!"

Mimi "Mimi nishamsahau na wala sihitaji hata kumi yake!"

Mimi " Halafu dada kama huko kuna sehemu ya kufikia hilo suala la nauli kwangu alinisumbui,we hata usimsumbue shem we kama inawezekana hata leo nianze safari"

Da'Sarah " Sasa hivi kweli kuna gari za kutoka hapo kuja Mwanza?"

Mimi "Hilo suala wewe niachie mimi,mimi nikifika nitakwambia"

Da'Sarah " Sawa wewe panda gari uje kama una nauli na ngoja nimpigie shemeji yako simu muda huo!"

Ile kauli ya Dada kunitaka niende Mwanza nikama ilinisaidia maana mpaka wakati huo nilikuwa sielewi hatma yangu!.Basi nilielekea mpaka stendi ambako nilikuwa nikitembea kwa umakini na tahadhari kubwa ili nisije kujikuta naangukia mkoni mwa mapongo,wakati huo begi langu lilikuwa na hela lipo mgongoni sikutaka kabisa kuliachia!.Basi nilipofika pale stendi nilidandia Hiace za Musoma ambako nilipanga nikifika pale Zero zero( Makutano) nisubiri gari zinazoenda Mwanza kutokea Musoma mjini!.Nilifika pale Makutano mida ya saa 9 alasiri na nikatelemka kusubiri gari za Mwanza.

Sikutaka kupandia gari za Mwanza pale Tarime mjini maana kulikuwa na wajuaji wengi hivyo nikawa naogopa kukamatishwa!.Basi haukupita muda nikawa nimepanda gari za Mwanza na nikawasiliana na dada nikawa nimemjulisha nishapanda gari!.,Kiukweli akili yangu mpaka wakati huo ilikuwa inawaza mambo mengi sana,sikujali ya kwamba Sirari nimeacha vitu vyangu wala nini,mimi nilichojali ni usalama wangu na kama ni vitu niliona ningevifata hali ambapo ingetulia!.

Wakati nikiwa kwenye gari nilimtafuta mshikaji wangu Mtatiro ambaye niliamini yupo Mwanza na nilipanga nikifika Mwanza tuonane!.


Mimi "Mwanangu vipi?"

Mtatiro "Mwanangu umekuwa adimu sana kama mate ya nyoka!"

Mimi "Ahahahaa ahahaaa,nambie mwanangu"

Mtatiro "Nimekutafuta juzi kati ulikuwa hupatikani!"

Mimi "Kuna mahali nilikuwepo mtandao ulikuwa haushiki kaka"

Mimi "Nipo njiani mwanangu nakuja M-Z-A"

Mtatiro "Unakuja lini,leo!?"

Mimi "Yeah nipo njiani"

Mtatiro "Umefika wapi?"

Mimi "Tunakaribia Kiabakari"

Mtatiro "Mimi sipo Mwanza mwanangu"

Mimi "Ulirudi Tarime?"

Mtatiro "Hapana,nipo hapa Bunda kuna ki mgodi kimetema ndiyo tupo na brother"

Mimi "Duuu!"

Mtatiro "Mwanza unaenda kwa nani?"

Mimi "Naenda kwa sista Sarah!"

Mtatiro "Mwanangu achana na habari za Mwanza kwanza,we kama vipi telemkia hapo Bunda mimi nitakufata uje tuone kama tutapata chochote"


Mtatiro alinishawishi hadi nikajikuta tena safari ya Mwanza kama imetoweka moyoni mwangu,nilichokuwa namshukuru Mshikaji wangu Mtatiro alikuwaga kila fursa haachi kunishirikisha kama rafiki yake,iwe haramu au iwe halali,kiukweli kwenye hilo sitamsahau jamaa yangu(Kwasasa anaishi Uganda).

Mtatiro "We mwambie Konda akushushe kituo kinaitwa Nyasura"

Aliendelea "Akikushusha hapo Nyasura ndiyo itakuwa jirani na huku nilipo!"

Mimi "Sawa"

Basi safari ikawa inaishia Bunda ingawa nilishalipa nauli ya Mwanza moja kwa moja,sikuona taabu kwasababu bado fungu nilikuwa nalo la kutosha.Ingawaje pesa niliyokuwa nayo ilikuwa haramu lakini ilikuwa inanipa kujiamini kwingi sana!.

Baada ya safari ya dakika kadhaa tukawa tumefika pale Bunda na mimi kushushwa hapo Nyasura kama Mtatiro alivyokuwa amenielekeza!.Basi nilimpigia simu Mtatiro nikamueleza ya kwamba nishafika hapo Nyasura,jamaa akawa amenitaka nipumzike sehemu aje kunifuata maana alipokuwepo yeye kulikuwa na umbali mrefu kidogo!.
Umenikumbusha kwetu. Bunda nyasura, machimbo yaliwahi kuibuka hapo Nyasana
 
Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 13.

Mimi "Mama nyakuru Mwita"

Mama "Tata sabhoke"

Ilikuwa ni heshima na salamu ambayo nilimpatia mama yangu baada ya kuwa nimefika hapo sokoni kwenye meza aliyokuwa akifanyia biashara!.

Mama "Ulienda wapi baba?"

Mimi "Nilikuwepo tu mama!"

Mama "Mbona umenenepa hivyo,au umepata kibarua huko baba!?"

Mimi "Nabangaiza tu hivyo hivyo!"

Mama "Nilimpigia mama yako mkubwa lakini akaniambia uliondoka na akajua labda ulirudi nyumbani"

Mimi "Mama nilienda kupambana na maisha yangu!".

Mama "Sasa baba utaendelea kuhangaika hivi hadi lini,rudi nyumbani mimi niliongea na baba yako na akasema hayo yameisha"

Mimi "Mama kwa umri huu siwezi kukaa tena pale nyumbani"

Mimi "Nilipita tu kuwasalimia"

Mama "Ulipita nyumbani?"

Mimi "Nimeanzia huko ndiyo nikaja hapa"

Mama "Dada yako alikuja na amemaliza kuondoka wiki iliyopita!"

Aliendelea "Chukua namba yake utawasiliana nae alisema ukirudi nikwambie umtafute"

Basi baada ya mazungumzo na mama nilichukua ile namba ya dada yangu mkubwa(Sarah)kisha nikaondoka zangu!.Mama yangu mara zote alikuwaga rafiki yangu kipenzi,pamoja na lile seke seke la mzee lakini bado alitaka nirudi pale nyumbani kitu ambacho kisingewezekana kwa wakati huo!.Sasa wakati naondoka nilimpigia dada yangu simu ili kumjulia hali maana tangu nilivyokuwa nimemaliza shule sikuwahi kuongea nae kwasababu yeye alikuwa ameolewa huko Mwanza!.

Baada ya kuongea na dada kwa dakika kadhaa alishangaa sana kwa kile kitendo ambacho mzee alinifanyia na alilaumu sana kwanini nilishindwa kumshirikisha kwa muda wote huo nikawa kimya!.

Da'Sarah "Sasa sikuhizi unafanya kazi gani hapo Tarime?"

Sikutaka kabisa kumficha kitu dada nilimwambia niliamua kuwa mpiga debe angalau maisha yaendeleee,alinishangaa sana ya kwamba nawezaje kuwa na elimu halafu niende kupiga debe!.

Da'sarah "Nilimwambia baba ukweli na kama ni kuchukia ngoja achukie,haiwezekani pesa anamalizia kwa mama yake Robina halafu sisi tunahangaika!"

Aliendelea "Kwahiyo sasa ulikuwa unakaa wapi?"

Mimi "Niliamua kupanga hapo Sirari!"

Da'Sarah "Ngoja nimwambie shemeji yako aje akutumie nauli uje huku"

Aliendelea "Na huyo mzee wala usimwambie chochote,muacheni na hela zake,yeye si anaona mama yetu hana maana!"

Mimi "Mimi nishamsahau na wala sihitaji hata kumi yake!"

Mimi " Halafu dada kama huko kuna sehemu ya kufikia hilo suala la nauli kwangu alinisumbui,we hata usimsumbue shem we kama inawezekana hata leo nianze safari"

Da'Sarah " Sasa hivi kweli kuna gari za kutoka hapo kuja Mwanza?"

Mimi "Hilo suala wewe niachie mimi,mimi nikifika nitakwambia"

Da'Sarah " Sawa wewe panda gari uje kama una nauli na ngoja nimpigie shemeji yako simu muda huo!"

Ile kauli ya Dada kunitaka niende Mwanza nikama ilinisaidia maana mpaka wakati huo nilikuwa sielewi hatma yangu!.Basi nilielekea mpaka stendi ambako nilikuwa nikitembea kwa umakini na tahadhari kubwa ili nisije kujikuta naangukia mkoni mwa mapongo,wakati huo begi langu lilikuwa na hela lipo mgongoni sikutaka kabisa kuliachia!.Basi nilipofika pale stendi nilidandia Hiace za Musoma ambako nilipanga nikifika pale Zero zero( Makutano) nisubiri gari zinazoenda Mwanza kutokea Musoma mjini!.Nilifika pale Makutano mida ya saa 9 alasiri na nikatelemka kusubiri gari za Mwanza.

Sikutaka kupandia gari za Mwanza pale Tarime mjini maana kulikuwa na wajuaji wengi hivyo nikawa naogopa kukamatishwa!.Basi haukupita muda nikawa nimepanda gari za Mwanza na nikawasiliana na dada nikawa nimemjulisha nishapanda gari!.,Kiukweli akili yangu mpaka wakati huo ilikuwa inawaza mambo mengi sana,sikujali ya kwamba Sirari nimeacha vitu vyangu wala nini,mimi nilichojali ni usalama wangu na kama ni vitu niliona ningevifata hali ambapo ingetulia!.

Wakati nikiwa kwenye gari nilimtafuta mshikaji wangu Mtatiro ambaye niliamini yupo Mwanza na nilipanga nikifika Mwanza tuonane!.


Mimi "Mwanangu vipi?"

Mtatiro "Mwanangu umekuwa adimu sana kama mate ya nyoka!"

Mimi "Ahahahaa ahahaaa,nambie mwanangu"

Mtatiro "Nimekutafuta juzi kati ulikuwa hupatikani!"

Mimi "Kuna mahali nilikuwepo mtandao ulikuwa haushiki kaka"

Mimi "Nipo njiani mwanangu nakuja M-Z-A"

Mtatiro "Unakuja lini,leo!?"

Mimi "Yeah nipo njiani"

Mtatiro "Umefika wapi?"

Mimi "Tunakaribia Kiabakari"

Mtatiro "Mimi sipo Mwanza mwanangu"

Mimi "Ulirudi Tarime?"

Mtatiro "Hapana,nipo hapa Bunda kuna ki mgodi kimetema ndiyo tupo na brother"

Mimi "Duuu!"

Mtatiro "Mwanza unaenda kwa nani?"

Mimi "Naenda kwa sista Sarah!"

Mtatiro "Mwanangu achana na habari za Mwanza kwanza,we kama vipi telemkia hapo Bunda mimi nitakufata uje tuone kama tutapata chochote"


Mtatiro alinishawishi hadi nikajikuta tena safari ya Mwanza kama imetoweka moyoni mwangu,nilichokuwa namshukuru Mshikaji wangu Mtatiro alikuwaga kila fursa haachi kunishirikisha kama rafiki yake,iwe haramu au iwe halali,kiukweli kwenye hilo sitamsahau jamaa yangu(Kwasasa anaishi Uganda).

Mtatiro "We mwambie Konda akushushe kituo kinaitwa Nyasura"

Aliendelea "Akikushusha hapo Nyasura ndiyo itakuwa jirani na huku nilipo!"

Mimi "Sawa"

Basi safari ikawa inaishia Bunda ingawa nilishalipa nauli ya Mwanza moja kwa moja,sikuona taabu kwasababu bado fungu nilikuwa nalo la kutosha.Ingawaje pesa niliyokuwa nayo ilikuwa haramu lakini ilikuwa inanipa kujiamini kwingi sana!.

Baada ya safari ya dakika kadhaa tukawa tumefika pale Bunda na mimi kushushwa hapo Nyasura kama Mtatiro alivyokuwa amenielekeza!.Basi nilimpigia simu Mtatiro nikamueleza ya kwamba nishafika hapo Nyasura,jamaa akawa amenitaka nipumzike sehemu aje kunifuata maana alipokuwepo yeye kulikuwa na umbali mrefu kidogo!.
Hukumwachia mama hata hela kidog0?
 
Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 13.

Mimi "Mama nyakuru Mwita"

Mama "Tata sabhoke"

Ilikuwa ni heshima na salamu ambayo nilimpatia mama yangu baada ya kuwa nimefika hapo sokoni kwenye meza aliyokuwa akifanyia biashara!.

Mama "Ulienda wapi baba?"

Mimi "Nilikuwepo tu mama!"

Mama "Mbona umenenepa hivyo,au umepata kibarua huko baba!?"

Mimi "Nabangaiza tu hivyo hivyo!"

Mama "Nilimpigia mama yako mkubwa lakini akaniambia uliondoka na akajua labda ulirudi nyumbani"

Mimi "Mama nilienda kupambana na maisha yangu!".

Mama "Sasa baba utaendelea kuhangaika hivi hadi lini,rudi nyumbani mimi niliongea na baba yako na akasema hayo yameisha"

Mimi "Mama kwa umri huu siwezi kukaa tena pale nyumbani"

Mimi "Nilipita tu kuwasalimia"

Mama "Ulipita nyumbani?"

Mimi "Nimeanzia huko ndiyo nikaja hapa"

Mama "Dada yako alikuja na amemaliza kuondoka wiki iliyopita!"

Aliendelea "Chukua namba yake utawasiliana nae alisema ukirudi nikwambie umtafute"

Basi baada ya mazungumzo na mama nilichukua ile namba ya dada yangu mkubwa(Sarah)kisha nikaondoka zangu!.Mama yangu mara zote alikuwaga rafiki yangu kipenzi,pamoja na lile seke seke la mzee lakini bado alitaka nirudi pale nyumbani kitu ambacho kisingewezekana kwa wakati huo!.Sasa wakati naondoka nilimpigia dada yangu simu ili kumjulia hali maana tangu nilivyokuwa nimemaliza shule sikuwahi kuongea nae kwasababu yeye alikuwa ameolewa huko Mwanza!.

Baada ya kuongea na dada kwa dakika kadhaa alishangaa sana kwa kile kitendo ambacho mzee alinifanyia na alilaumu sana kwanini nilishindwa kumshirikisha kwa muda wote huo nikawa kimya!.

Da'Sarah "Sasa sikuhizi unafanya kazi gani hapo Tarime?"

Sikutaka kabisa kumficha kitu dada nilimwambia niliamua kuwa mpiga debe angalau maisha yaendeleee,alinishangaa sana ya kwamba nawezaje kuwa na elimu halafu niende kupiga debe!.

Da'sarah "Nilimwambia baba ukweli na kama ni kuchukia ngoja achukie,haiwezekani pesa anamalizia kwa mama yake Robina halafu sisi tunahangaika!"

Aliendelea "Kwahiyo sasa ulikuwa unakaa wapi?"

Mimi "Niliamua kupanga hapo Sirari!"

Da'Sarah "Ngoja nimwambie shemeji yako aje akutumie nauli uje huku"

Aliendelea "Na huyo mzee wala usimwambie chochote,muacheni na hela zake,yeye si anaona mama yetu hana maana!"

Mimi "Mimi nishamsahau na wala sihitaji hata kumi yake!"

Mimi " Halafu dada kama huko kuna sehemu ya kufikia hilo suala la nauli kwangu alinisumbui,we hata usimsumbue shem we kama inawezekana hata leo nianze safari"

Da'Sarah " Sasa hivi kweli kuna gari za kutoka hapo kuja Mwanza?"

Mimi "Hilo suala wewe niachie mimi,mimi nikifika nitakwambia"

Da'Sarah " Sawa wewe panda gari uje kama una nauli na ngoja nimpigie shemeji yako simu muda huo!"

Ile kauli ya Dada kunitaka niende Mwanza nikama ilinisaidia maana mpaka wakati huo nilikuwa sielewi hatma yangu!.Basi nilielekea mpaka stendi ambako nilikuwa nikitembea kwa umakini na tahadhari kubwa ili nisije kujikuta naangukia mkoni mwa mapongo,wakati huo begi langu lilikuwa na hela lipo mgongoni sikutaka kabisa kuliachia!.Basi nilipofika pale stendi nilidandia Hiace za Musoma ambako nilipanga nikifika pale Zero zero( Makutano) nisubiri gari zinazoenda Mwanza kutokea Musoma mjini!.Nilifika pale Makutano mida ya saa 9 alasiri na nikatelemka kusubiri gari za Mwanza.

Sikutaka kupandia gari za Mwanza pale Tarime mjini maana kulikuwa na wajuaji wengi hivyo nikawa naogopa kukamatishwa!.Basi haukupita muda nikawa nimepanda gari za Mwanza na nikawasiliana na dada nikawa nimemjulisha nishapanda gari!.,Kiukweli akili yangu mpaka wakati huo ilikuwa inawaza mambo mengi sana,sikujali ya kwamba Sirari nimeacha vitu vyangu wala nini,mimi nilichojali ni usalama wangu na kama ni vitu niliona ningevifata hali ambapo ingetulia!.

Wakati nikiwa kwenye gari nilimtafuta mshikaji wangu Mtatiro ambaye niliamini yupo Mwanza na nilipanga nikifika Mwanza tuonane!.


Mimi "Mwanangu vipi?"

Mtatiro "Mwanangu umekuwa adimu sana kama mate ya nyoka!"

Mimi "Ahahahaa ahahaaa,nambie mwanangu"

Mtatiro "Nimekutafuta juzi kati ulikuwa hupatikani!"

Mimi "Kuna mahali nilikuwepo mtandao ulikuwa haushiki kaka"

Mimi "Nipo njiani mwanangu nakuja M-Z-A"

Mtatiro "Unakuja lini,leo!?"

Mimi "Yeah nipo njiani"

Mtatiro "Umefika wapi?"

Mimi "Tunakaribia Kiabakari"

Mtatiro "Mimi sipo Mwanza mwanangu"

Mimi "Ulirudi Tarime?"

Mtatiro "Hapana,nipo hapa Bunda kuna ki mgodi kimetema ndiyo tupo na brother"

Mimi "Duuu!"

Mtatiro "Mwanza unaenda kwa nani?"

Mimi "Naenda kwa sista Sarah!"

Mtatiro "Mwanangu achana na habari za Mwanza kwanza,we kama vipi telemkia hapo Bunda mimi nitakufata uje tuone kama tutapata chochote"


Mtatiro alinishawishi hadi nikajikuta tena safari ya Mwanza kama imetoweka moyoni mwangu,nilichokuwa namshukuru Mshikaji wangu Mtatiro alikuwaga kila fursa haachi kunishirikisha kama rafiki yake,iwe haramu au iwe halali,kiukweli kwenye hilo sitamsahau jamaa yangu(Kwasasa anaishi Uganda).

Mtatiro "We mwambie Konda akushushe kituo kinaitwa Nyasura"

Aliendelea "Akikushusha hapo Nyasura ndiyo itakuwa jirani na huku nilipo!"

Mimi "Sawa"

Basi safari ikawa inaishia Bunda ingawa nilishalipa nauli ya Mwanza moja kwa moja,sikuona taabu kwasababu bado fungu nilikuwa nalo la kutosha.Ingawaje pesa niliyokuwa nayo ilikuwa haramu lakini ilikuwa inanipa kujiamini kwingi sana!.

Baada ya safari ya dakika kadhaa tukawa tumefika pale Bunda na mimi kushushwa hapo Nyasura kama Mtatiro alivyokuwa amenielekeza!.Basi nilimpigia simu Mtatiro nikamueleza ya kwamba nishafika hapo Nyasura,jamaa akawa amenitaka nipumzike sehemu aje kunifuata maana alipokuwepo yeye kulikuwa na umbali mrefu kidogo!.
Woyoo! Mzigo huu hapa
 
Back
Top Bottom