Nilivyonusurika kuuawa na wananchi wenye hasira kali miaka 15 iliyopita. Tanzania kufariki ni dakika 0 tu!

Pole sana mrembo 😂😂
 
Wanawake uwa wanakurupuka sana, hapo anawezakua alimfananisha tu
 
Mimi Kuna siku nilikuwa msibani sehemu Fulani hapa Dar es salaam,Sasa nilibanwa na haja ndogo na hiyo sehemu kulikuwa Kuna kajumba kimuonekano ni kama bafu la kuogea Nikawa nawaza niende kumbe Ile ni nyumba ya mtu.Yaani Bahati nzuri kabla ya Mimi kutaka niingie mwenye nyumba akawa ameingia na kutoa kiti kidogo.Siku hiyo siwezi kuisahau maana ningeingia ningeonekana kama naenda kuiba.Nyumba za watu wa dar ni kiboko
 
Na Masikini tulivyo na hasira ulikua unaisha mzee
 
Nashkuru Mungu kwenye maisha yangu yote sijawahi kupiga mwizi na sintowahi kamwe.

Siyo kila anaeitiwa mwizi ni mwizi.
 
Mungu ashukuriwe sana kwa kukulinda na kukuokoa...
Kama bado hujaenda kumshukuru yule mama mjumbe na kumpelekea zawadi walau pea ya Kitenge utakuwa umechelewa Ila fanya hivyo. Huyo ndiye Mungu alimpa kibali cha kukuokoa....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…