Nilivyonusurika kuuawa na wananchi wenye hasira kali miaka 15 iliyopita. Tanzania kufariki ni dakika 0 tu!

Nilivyonusurika kuuawa na wananchi wenye hasira kali miaka 15 iliyopita. Tanzania kufariki ni dakika 0 tu!

Ni miaka 15 sasa imepita tangu ninusurike kuuawa na walimwengu. Nilikuwa nikiishi Tabora, na jioni moja, nilikuwa natembea mjini Tabora. Wakati natembea, nikajihisi kubanwa haja ndogo, nikawa nakatiza mtaa wa Salimini. Kwa wale wenyeji wa Tabora, mnafahamu ule mtaa ulivyo wa Kiswahili. Nikawaona niingie kwenye nyumba moja mtaani hapo ili niombe sehemu ya kujisaidia haja ndogo (chooni).

Nje ya nyumba ile alikuwa amesimama kijana mwenye umri wa miaka 18 au 19, nilimuomba na akaniielekeza nipite kwenye korido niende mpaka uwani. Wakati napita kwenye korido, nilikutana na mwanamke na mwanaume wakiwa wanazungumza. Niliwasalimia, na mimi nikaendelea na safari yangu kuelekea uwani. Nilipofika uwani, kabla ya kuingia chooni, nikawa ninakunja suruali yangu mpaka ukaribu na magotini (kawaida yetu Waislamu huwa tunafanya hivi ili utakapokuwa unajisaidia haja ndogo, zile cheche za mikojo zisirukie nguo). Ghafla nilisikia sauti ya mwanamke ikitokea nyuma ikiita "mwiziiiiii, mwiziiiiii."

Ile kugeuka, namuona yule mwanamke niliemuona kwenye korido anakuja mbio huku akakamata kuni. Akaanza kunipigia na ule ukuni sehemu za mabegani huku mimi nikihangaika kupangua kile kipigo na kujitetea kuwa mimi sio mwizi. Yule mwanamke alipoona ananipiga na ukuni na mimi sianguki, akabeba sufuria iliyokuwa na maji ya moto ili animwagie usoni. Dah, lahaula! Akatokea yule mwanaume aliyekuwa nae akamuambia "achaaaaa!" Kujinusuru, nilibidi nirukie kwenye korido nitokee mlango wa mbele ili nikimbie (hapa nilifanya kosa kubwa). Nilianza kukimbia barabarani huku yule mwanamke akiendelea kuita "mwiziiii, mwiziiiiii."

Watu wakaanza kunikimbiza. Kadiri nilivyokuwa nakimbia, watu walizidi kuongezeka, huku wengine wakiwa wamebeba mapanga. Niliingiwa na fikra za haraka za kuingia kwenye nyumba ya mtu ili ninusuru maisha yangu. Bahati nzuri, nyumba ile niliyoingia ilikuwa ya mjumbe wa serikali ya mtaa. Alichokifanya yule mjumbe (mwanamke wa makamo) aliniambia niingie nijifiche chumbani na yeye akafunga mlango. Lile kundi la watu wenye mapanga walifika kwenye nyumba ile niliyokuwa nimejificha na wakaanza kumlazimisha yule mjumbe anitoe nje huku wakiimba "tunamtaka mwizi weeetúu."

Yule mjumbe alisimama mlangoni na kuwaambia wale watu, "Simtoi nje huyu kijana, ila nitakachofanya, napiga simu polisi waje wamchukue, mtamkuta kituoni." Hii ndiyo ilikuwa salama yangu. Haikupita masaa mawili, walikuja polisi na kunichukua kwenye gari lao. Polisi mmoja alinipiga vibao huku akisema, "Kumbe jamaa mwenyewe mrembo!" (Mimi nina asili ya ushombe shombe kwa mbali).

Nilipofikishwa kituoni, nilijieleza kwa ufasaha na pia nikatoa vitambulisho vyangu ili viwe ni uthibitisho wa kile nilichokizungumza. Bahati nzuri, mfukoni nilikuwa na shilingi laki moja, nikatoa 30,000/- nikawapa wale askari, wakawa wameniachia niende nyumbani usiku ule na kesho yake niende kuripoti. Kesho yake niliripoti polisi, na askari walinikabidhi vitambulisho na kuniambia hakuna kesi. Nikaendelea na majukumu yangu.
Niliwahi koswa koswa kupondwa na mawe mtaroni kisa mlevi mmoja tabata.

Nilikua nimepaki gari kipindi hiko bar inaitwa BL karibu na bar ya camp mtaa wa st. Marry. Sasa ikafika muda nikataka kusepa. Ile nataka kuondoka nikaona mtu kapaki boda nikashuka nikaenda kumwambia nataka kutoka.

Hapa na pale akatokea mwenzake kalewa. Akaanza nyie wenye magari mna dharau blaah blaah kibao. Ghafla watu wakaanza kukusanyika. Wakati nashangaa mara teke mara nipo mtaroni mtu anaita mwizi mara naona mtu kabeba bonge la jiwe anataka kulishusha kichwani. Sijui nani alimzuia yule mtu.

Baada ya hapa na pale nikaweza kuondoka ila nikamkariri yule jamaa.

Nilimripoti pahala jamaa yangu akampata. Alishughulikiwa vilivyo ila jamaa hakutaka kunionyesha anaishi wapi.

Mpaka leo imepita miaka zaidi ya 10 niliapa yule jamaa siku nikikutana naye lazima nitalipa kisasi tu.

Kila nikikumbuka hili tukio huwa natetemeka sana...

Ningekufa kibwege sana.
 
Wananchi wengi hatupo tayari kufuata sheria ila ndo tuko mstari wa mbele kulalamikia watekaji na viongozi wasiofuata sheria. Tanzania watembea kwa miguu wengi huvunja sheria za barabara ila hawawajibishwi. Tukiamka na kuanza kuheshimu sheria itapunguza uhalifu hasa mauaji.
 
Ni miaka 15 sasa imepita tangu ninusurike kuuawa na walimwengu. Nilikuwa nikiishi Tabora, na jioni moja, nilikuwa natembea mjini Tabora. Wakati natembea, nikajihisi kubanwa haja ndogo, nikawa nakatiza mtaa wa Salimini. Kwa wale wenyeji wa Tabora, mnafahamu ule mtaa ulivyo wa Kiswahili. Nikawaona niingie kwenye nyumba moja mtaani hapo ili niombe sehemu ya kujisaidia haja ndogo (chooni).

Nje ya nyumba ile alikuwa amesimama kijana mwenye umri wa miaka 18 au 19, nilimuomba na akaniielekeza nipite kwenye korido niende mpaka uwani. Wakati napita kwenye korido, nilikutana na mwanamke na mwanaume wakiwa wanazungumza. Niliwasalimia, na mimi nikaendelea na safari yangu kuelekea uwani. Nilipofika uwani, kabla ya kuingia chooni, nikawa ninakunja suruali yangu mpaka ukaribu na magotini (kawaida yetu Waislamu huwa tunafanya hivi ili utakapokuwa unajisaidia haja ndogo, zile cheche za mikojo zisirukie nguo). Ghafla nilisikia sauti ya mwanamke ikitokea nyuma ikiita "mwiziiiiii, mwiziiiiii."

Ile kugeuka, namuona yule mwanamke niliemuona kwenye korido anakuja mbio huku akakamata kuni. Akaanza kunipigia na ule ukuni sehemu za mabegani huku mimi nikihangaika kupangua kile kipigo na kujitetea kuwa mimi sio mwizi. Yule mwanamke alipoona ananipiga na ukuni na mimi sianguki, akabeba sufuria iliyokuwa na maji ya moto ili animwagie usoni. Dah, lahaula! Akatokea yule mwanaume aliyekuwa nae akamuambia "achaaaaa!" Kujinusuru, nilibidi nirukie kwenye korido nitokee mlango wa mbele ili nikimbie (hapa nilifanya kosa kubwa). Nilianza kukimbia barabarani huku yule mwanamke akiendelea kuita "mwiziiii, mwiziiiiii."

Watu wakaanza kunikimbiza. Kadiri nilivyokuwa nakimbia, watu walizidi kuongezeka, huku wengine wakiwa wamebeba mapanga. Niliingiwa na fikra za haraka za kuingia kwenye nyumba ya mtu ili ninusuru maisha yangu. Bahati nzuri, nyumba ile niliyoingia ilikuwa ya mjumbe wa serikali ya mtaa. Alichokifanya yule mjumbe (mwanamke wa makamo) aliniambia niingie nijifiche chumbani na yeye akafunga mlango. Lile kundi la watu wenye mapanga walifika kwenye nyumba ile niliyokuwa nimejificha na wakaanza kumlazimisha yule mjumbe anitoe nje huku wakiimba "tunamtaka mwizi weeetúu."

Yule mjumbe alisimama mlangoni na kuwaambia wale watu, "Simtoi nje huyu kijana, ila nitakachofanya, napiga simu polisi waje wamchukue, mtamkuta kituoni." Hii ndiyo ilikuwa salama yangu. Haikupita masaa mawili, walikuja polisi na kunichukua kwenye gari lao. Polisi mmoja alinipiga vibao huku akisema, "Kumbe jamaa mwenyewe mrembo!" (Mimi nina asili ya ushombe shombe kwa mbali).

Nilipofikishwa kituoni, nilijieleza kwa ufasaha na pia nikatoa vitambulisho vyangu ili viwe ni uthibitisho wa kile nilichokizungumza. Bahati nzuri, mfukoni nilikuwa na shilingi laki moja, nikatoa 30,000/- nikawapa wale askari, wakawa wameniachia niende nyumbani usiku ule na kesho yake niende kuripoti. Kesho yake niliripoti polisi, na askari walinikabidhi vitambulisho na kuniambia hakuna kesi. Nikaendelea na majukumu yangu.
Mazali kama haya ya kusingiziwa na kuitwaa mwizi natamani yanitokee yani huo mkono ntakavyoutembeza maamaee.
 
Watanzania wana uwezo mdigo wa akili Sana .

Kipindi nipo Bukoba waliua jamaa mmoja ambaye alikuwa sio mwizi yaani hawafikirii kwa kina waswahili.

Pia nakumbuka kipindi kile Bukoba kuna yale mauaji ya Koromeo around 2014/2015.

Nakumbuka siku moja usiku natoka zangu nyumbani naenda Saloon alikuepo Kijana Fundi umeme anaitwa Baraka alikamatwa na kuanza kupewa kipigo kikali eti anaua watu .

Kumpekua walimkuta na kisu , bisibisi prize Ilawalivyoona hivyo kipigo kikazidi kumbe zilikuwa zana za Kazi yake ya umeme.

Hii kitu ilinifanya nifikirie Sana japo huyo jamaa aliokolewa na police dk kama ya 70%

Ukisikia kelele za mwizi usikurupuke kuua ni hatari Sana.
 
Ni miaka 15 sasa imepita tangu ninusurike kuuawa na walimwengu. Nilikuwa nikiishi Tabora, na jioni moja, nilikuwa natembea mjini Tabora. Wakati natembea, nikajihisi kubanwa haja ndogo, nikawa nakatiza mtaa wa Salimini. Kwa wale wenyeji wa Tabora, mnafahamu ule mtaa ulivyo wa Kiswahili. Nikawaona niingie kwenye nyumba moja mtaani hapo ili niombe sehemu ya kujisaidia haja ndogo (chooni).

Nje ya nyumba ile alikuwa amesimama kijana mwenye umri wa miaka 18 au 19, nilimuomba na akaniielekeza nipite kwenye korido niende mpaka uwani. Wakati napita kwenye korido, nilikutana na mwanamke na mwanaume wakiwa wanazungumza. Niliwasalimia, na mimi nikaendelea na safari yangu kuelekea uwani. Nilipofika uwani, kabla ya kuingia chooni, nikawa ninakunja suruali yangu mpaka ukaribu na magotini (kawaida yetu Waislamu huwa tunafanya hivi ili utakapokuwa unajisaidia haja ndogo, zile cheche za mikojo zisirukie nguo). Ghafla nilisikia sauti ya mwanamke ikitokea nyuma ikiita "mwiziiiiii, mwiziiiiii."

Ile kugeuka, namuona yule mwanamke niliemuona kwenye korido anakuja mbio huku akakamata kuni. Akaanza kunipigia na ule ukuni sehemu za mabegani huku mimi nikihangaika kupangua kile kipigo na kujitetea kuwa mimi sio mwizi. Yule mwanamke alipoona ananipiga na ukuni na mimi sianguki, akabeba sufuria iliyokuwa na maji ya moto ili animwagie usoni. Dah, lahaula! Akatokea yule mwanaume aliyekuwa nae akamuambia "achaaaaa!" Kujinusuru, nilibidi nirukie kwenye korido nitokee mlango wa mbele ili nikimbie (hapa nilifanya kosa kubwa). Nilianza kukimbia barabarani huku yule mwanamke akiendelea kuita "mwiziiii, mwiziiiiii."

Watu wakaanza kunikimbiza. Kadiri nilivyokuwa nakimbia, watu walizidi kuongezeka, huku wengine wakiwa wamebeba mapanga. Niliingiwa na fikra za haraka za kuingia kwenye nyumba ya mtu ili ninusuru maisha yangu. Bahati nzuri, nyumba ile niliyoingia ilikuwa ya mjumbe wa serikali ya mtaa. Alichokifanya yule mjumbe (mwanamke wa makamo) aliniambia niingie nijifiche chumbani na yeye akafunga mlango. Lile kundi la watu wenye mapanga walifika kwenye nyumba ile niliyokuwa nimejificha na wakaanza kumlazimisha yule mjumbe anitoe nje huku wakiimba "tunamtaka mwizi weeetúu."

Yule mjumbe alisimama mlangoni na kuwaambia wale watu, "Simtoi nje huyu kijana, ila nitakachofanya, napiga simu polisi waje wamchukue, mtamkuta kituoni." Hii ndiyo ilikuwa salama yangu. Haikupita masaa mawili, walikuja polisi na kunichukua kwenye gari lao. Polisi mmoja alinipiga vibao huku akisema, "Kumbe jamaa mwenyewe mrembo!" (Mimi nina asili ya ushombe shombe kwa mbali).

Nilipofikishwa kituoni, nilijieleza kwa ufasaha na pia nikatoa vitambulisho vyangu ili viwe ni uthibitisho wa kile nilichokizungumza. Bahati nzuri, mfukoni nilikuwa na shilingi laki moja, nikatoa 30,000/- nikawapa wale askari, wakawa wameniachia niende nyumbani usiku ule na kesho yake niende kuripoti. Kesho yake niliripoti polisi, na askari walinikabidhi vitambulisho na kuniambia hakuna kesi. Nikaendelea na majukumu yangu.
kuna Mwaka mmoja uliwahi kucomment kwenye uzi mmoja hivi ile comment iliweza kumaliza wiki yangu yote kazini comment ilikuwa inasomeka hivi

mleta mada we ni muongo Acha kukaa kwa shemeji acha kupiga nyeto🤣🤣
 
Nilipomaliza chuo nilizunguka sana kutafuta AJIRA hasa kwenye majiji makubwa kama mwanza, Dodoma na na Daressalam huko kote niliambulia holaaaa, nilikaa nikafikiria sana nikaona sehemu pekee ya kwenda kutafuta maisha ni mikoa ambayo haijaendelea kwa sababu ushindani katika sekta ya ajira unakuwa ni mdogo na uhitaji unakuwa ni mkubwa pia, nikaona Bora niende tabora huko nilifanikiwa kupata ajira japo nilikuwa nalipwa mshahara mdogo sana..Mimi ni mtaalamu wa Afya ya binadamu japo kwa sasa najishughulisha na biashara niliisha Toka huko....soko la ajira aliliharibu zaidi magufuri likawa gumu balaa......
Pole sana ndugu yangu
 
Ni miaka 15 sasa imepita tangu ninusurike kuuawa na walimwengu. Nilikuwa nikiishi Tabora, na jioni moja, nilikuwa natembea mjini Tabora. Wakati natembea, nikajihisi kubanwa haja ndogo, nikawa nakatiza mtaa wa Salimini. Kwa wale wenyeji wa Tabora, mnafahamu ule mtaa ulivyo wa Kiswahili. Nikawaona niingie kwenye nyumba moja mtaani hapo ili niombe sehemu ya kujisaidia haja ndogo (chooni).

Nje ya nyumba ile alikuwa amesimama kijana mwenye umri wa miaka 18 au 19, nilimuomba na akaniielekeza nipite kwenye korido niende mpaka uwani. Wakati napita kwenye korido, nilikutana na mwanamke na mwanaume wakiwa wanazungumza. Niliwasalimia, na mimi nikaendelea na safari yangu kuelekea uwani. Nilipofika uwani, kabla ya kuingia chooni, nikawa ninakunja suruali yangu mpaka ukaribu na magotini (kawaida yetu Waislamu huwa tunafanya hivi ili utakapokuwa unajisaidia haja ndogo, zile cheche za mikojo zisirukie nguo). Ghafla nilisikia sauti ya mwanamke ikitokea nyuma ikiita "mwiziiiiii, mwiziiiiii."

Ile kugeuka, namuona yule mwanamke niliemuona kwenye korido anakuja mbio huku akakamata kuni. Akaanza kunipigia na ule ukuni sehemu za mabegani huku mimi nikihangaika kupangua kile kipigo na kujitetea kuwa mimi sio mwizi. Yule mwanamke alipoona ananipiga na ukuni na mimi sianguki, akabeba sufuria iliyokuwa na maji ya moto ili animwagie usoni. Dah, lahaula! Akatokea yule mwanaume aliyekuwa nae akamuambia "achaaaaa!" Kujinusuru, nilibidi nirukie kwenye korido nitokee mlango wa mbele ili nikimbie (hapa nilifanya kosa kubwa). Nilianza kukimbia barabarani huku yule mwanamke akiendelea kuita "mwiziiii, mwiziiiiii."

Watu wakaanza kunikimbiza. Kadiri nilivyokuwa nakimbia, watu walizidi kuongezeka, huku wengine wakiwa wamebeba mapanga. Niliingiwa na fikra za haraka za kuingia kwenye nyumba ya mtu ili ninusuru maisha yangu. Bahati nzuri, nyumba ile niliyoingia ilikuwa ya mjumbe wa serikali ya mtaa. Alichokifanya yule mjumbe (mwanamke wa makamo) aliniambia niingie nijifiche chumbani na yeye akafunga mlango. Lile kundi la watu wenye mapanga walifika kwenye nyumba ile niliyokuwa nimejificha na wakaanza kumlazimisha yule mjumbe anitoe nje huku wakiimba "tunamtaka mwizi weeetúu."

Yule mjumbe alisimama mlangoni na kuwaambia wale watu, "Simtoi nje huyu kijana, ila nitakachofanya, napiga simu polisi waje wamchukue, mtamkuta kituoni." Hii ndiyo ilikuwa salama yangu. Haikupita masaa mawili, walikuja polisi na kunichukua kwenye gari lao. Polisi mmoja alinipiga vibao huku akisema, "Kumbe jamaa mwenyewe mrembo!" (Mimi nina asili ya ushombe shombe kwa mbali).

Nilipofikishwa kituoni, nilijieleza kwa ufasaha na pia nikatoa vitambulisho vyangu ili viwe ni uthibitisho wa kile nilichokizungumza. Bahati nzuri, mfukoni nilikuwa na shilingi laki moja, nikatoa 30,000/- nikawapa wale askari, wakawa wameniachia niende nyumbani usiku ule na kesho yake niende kuripoti. Kesho yake niliripoti polisi, na askari walinikabidhi vitambulisho na kuniambia hakuna kesi. Nikaendelea na majukumu yangu.
Inaendelea au mwisho.
 
Coincidence gani ya kuzama kwenye nyumba halafu bahati ikawa nyumba ya mjumbe?
Hii ilikuwa ni kama bahati Tu iliyosababishwa na MUNGU..nimekutana na matukio mengi sana kwenye maisha yangu miaka ya nyuma sana niliwahi kupewa kesi ya unyang'anyi wa kuitumia siraha ( armed robbery), wakati nikisubili Vyeti vyangu niliamua kazi ya ulinzi kwenye kampuni moja ya kichina huko jijini. Siku moja Mimi nikiwa nipo mapumzikoni ( sikuingia shift) usiku majambazi walivamia eneo lile . Walinzi wawili walikuwa lindo usiku Huo walifungwa mikono na miguu na kutishiwa kuuawa endapo Tu wangepiga kelele. Wale majambazi walifanikiwa kulizingira eneo lile na baadhi ya wachina waliokuwa wanaishi eneo lile walijeruhiwa kwa mapanga na baadhi ya vitu kama pesa taslimu , simu na kompyuta viliibiwa. Kesho yake ya tukio ilikuwa ni ziara ya waziri mkuu , Katika hotuba yake katika ziara hiyo alisititiza zaidi walinzi wanaolinda eneo hilo ndio kundi linalotakiwa kukamatwa na kutoa maelezo zaidi huenda tukio lile tunalifahamu au sisi ndio tulitengeneza njama ya kuvamiwa wachina hao. Itaendelea............
 
Kinachoniuma Kwa askari wetu hawana maswali yaani unabebwa.na hela unatoa huku kosa huna.

Hata chembe ya aibu hawana.
 
Back
Top Bottom