Nilivyoweza kujinasua kwenye gharika la ndugu omba omba, Nilionekana mbahili lakini wanaanza kunielewa, pesa yangu siwezi kuitoa bila uwajibikaji

Kama kujitafuta kwako mpaka unajipata ndugu hawakushiriki una haki ya kuwakataa lakini kama viatu vya shule kanunia mjomba,uniform kanunia bamdogo,kaka alikulipia ada lazima uwajibike kwao ....otherwise funga mdomo wako.
Kuna wengine hata pen hakuna lakini wee pata kazi ndiyo utaanza kuona simu zakusalimiwa
 
Wasaidien ndugu zenu acheni roho mbaya

Unakuta mtu mmoja umejilimbikizia uchumi mwingi sana alafu ndugu zako wote masikin mafukara wa kutupwa

Hata ikitokea umekufa hakuna hata ndugu yako mmoja mwenye uwezo wa kununulia hata jeneza la laki mbili
Fukara yeyote ni maamuzi yake kuwa fukara,hupaswi kumuonea huruma.
 
Miezi 3 nyumba nilipata heka heka za kibarua, Ikabidi nimuombe ss anipige tafu.

Aloo, Tusaidiane jamn pale panapo wezekana, Isingekua ss kunishika mkono ningeteseka mno.

Now kidogo nimesimama
 
1. Saida ukiwa na uwezo wa kusaidia.

Mapato yako yaruhusu kutoa msaada tofauti na hapo unajitengenezea majanga.

2. Saidia watu SAHIHI. Siyo kila mtu unapaswa kumsaidia haijalishi ni ndugu au siyo ndugu.

Isikilize sauti yako ya ndani ikikuambia toa, toa kweli ila ikikuambia usitoe hatakama unayo nyingi kiasi gani USITOE!

Binadamu ni viumbe ambavyo vinabadilika.

Usije ukaanza kujilaumu baadae ukianza kuona uhalisia wao ukiwa hauna kitu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…