Niliwaambia wazazi wasubiri niweke mambo yakae sawa wakanigomea, sasa naona yakitimia

Hauna busara wala hofu ya Mungu, ninaamini hata wazazi wake wanakuona wewe ni mjuaji, mkaidi n.k

Rudi kwa wazazi wako kama wadau walivyokushauri hapo juu, ni dhahiri pande zote mbili zinaona una shida, ni rahisi upande wa mwanamke kufanya mazungumzo na wazazi wako kuliko wewe sababu umeshajitia doa.

Jaribu kuheshimu wazazi kile wanachokwambia, Mungu akusaidie usije ukapata mtoto asiyekusikiliza na asiyejikita ktk imani kama wewe.
 
Yah, hapo lazima aipange familia yake aende tu hiyo tarehe, kuna makosa alishayafanya na ndo yamezaa yote haya.
 
Hehe... sawa.
 
Tuma mshenga wakazungumze uone kama watabadili msimamo wakikataa tulia watakutafuta
 
Yaah sure ni dharau.

Kwa wanyabi hua tunaishi nao kigumu bila pande zote kujua. Ila hii ya kua pande zote zinajua na wewe hutaki kwenda kwao kwasababu unazojua wewe ni dharau kwa familia ya mwanamke.

Jitahidi ukutane na wazee wako muliweke sawa, ila chonde usiumize uchumi wako.
 
Ushauri murua kabisa huu.
 
Nilijipanga kwa mwezi wa 3/4 itakapoangukia pasaka kwasababu january hii hela hamna lakini pia ni ngumu hata kumualika mtu akakuelewa.
Ni kweli... Kaa nao uwaeleweshe.. After all yanabaki kuwa maamuzi yako, mtu asikupangie.
 
Ulizingua ulivyomgomea binti kwenda kwao na hutambuliki kitaratibu, hayo mengineyo waachie wazee na mshenga watayaweka sawa ila jiandae mfuko usiwe mtupu.
Swali je huyo binti umemkuta bikra?
Kama jibu ni ndio basi mwamba anatakiwa kabla ya tarehe 15 aende wasikilizane na sio kulipia
Unalipia mtu ili aje akutwishe mizigo ya maisha yake yote??
Mimi ninapingana na hizi hoja za kuwalipia mahari mabinti zetu..
Kwasababu wao wenyewe wamekuwa hawatabiriki yaani hawajali gharama tunazowatolea zaidi wanadhani eti kisa wana kitobo tu wanastahili kulipiwa
Hawajui kama vigezo na masharti vinatakiwa kuzingatiwa..
 
Kwahyo kama hakumkuta bikra amuache?
 
Mbona hii match unaamua wew na ndugu zako, maana mke wako ni mjamzito,huna haja ya kuwanyenyekea wakwe zako,maana wao ndo wamezingua
 
Tatizo ni kwamba nimeshtukizwa kwa kitu ambacho nilishakiona kitakuja tokea baadae, naona dalili za kutengeneza single mother bila kupenda.
Duu kumbe sheikhe na vitu vya maandalizi ukweni,unaenda toa wewe,je ni kabila gani hilo sheikhe lenye tamaduni hizo ,mahali ukatoe,faini ya kumtia mimba mtoto wao au kuish nae ukapigwe na bado na gharama za mpunga ukazichangie duu?
 
wazazi wako wanaingiloaje kwenye mambo yako?
 
Kataa ndoa, ndoa ni upotevu wa muda.

Angalia kijana usije ukawehuka ukashindwa hata kufika mjini, ukapata ajali kisa mawazo.

Hao watakuoa wewe usipoangalia, kuwa na msimamo kama umeshamtia KIBENDI vimba tu. Wacha waneng'eneke wakichoka mtoto wao atarudi mjini na hiyo sijui sherehe( upotevu wa rasilimali) itakuja baadae maana wewe kwanza bado huna ECONOMIC FREEDOM( wewe ni apeche alolo).

Kaza hao wakwe ukilegea watakuoa wewe.Simamia misimamo yako wewe ndo unaoa na kutoa mahari, kama wewe ndo unaolewa na kutolewa mahari endele kuwaendekeza hao wakwe.

# kataa ndoa,ndoa ni utapeli!!
 
We nae hakuna kitu kabisa hapo inshu ni hela sio kuwasikiliza wazazi. Upande wa mke wanatama hela wewe unasema jamaa ana kiburi sasa hata akiwa mpole inatakiwa hela
 
Iliwahi kunikuta Mimi pia hii,

Hapo wazazi wake wamekupiga "sanction", yaani "upati utelezi Tena mpaka ukaonekane officially".

Hapo wanamaanisha,
"Harudi Tena kwako ,mpaka ukaonekane ukweni"

Mtego wao Ni kwamba,
"Ukipuuza mpk akajifungua kwao, Mtoto atakaezaliwa sio Mali Yako"

Pia,
"Ukienda kuonekana ashajifungua, watajipatia pesa kutokana na faini ya uchafuzi"

Hivyo wanamtumia Binti yao Kama "bargaining chip" au "ndoano" kukunasa Wewe unaejifanya kupiga piga chenga SUALA LA KURASIMISHA.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…