Kama ni kuishi usijenge na Wala usijenge nyumba kubwa sana angalau vyumba vitatu basi na sebule jiko labda na stoo ila uwe na eneo kubwa ni vema ili upande miti ufurahi maana siku ukizeeka na familia ikitawanyike nyumba itakupa upweke sanaSiwezi jiroga kujenga ghorofa kama hata nyumba ya kwanza ya kuishi sina! Kujenga ghorofa hela zinateketea halafu huoni hata hatua uliyopiga
PCHA YA NYUMBA TUNAOMBA KWA NJE TUBinafsi naamini sana kuwa na sehemu yako ya kuishi bila bugudha ya kodi wala maudhi ya wapangaji wengine,
Mambo machacho kuhusu mimi
1. Niko under 30
2. Kipato changu ni kati ya 500k - 550 k kwa mwezi
Baada ya kununua kiwanja، nilianza kununua maatofali kidogo kidogo.
Mambo niliojifunza
1. Anza kujenga na ulicho nacho, kwenye fungu ndio kwenye nyongeza, ukishaweka tofali kama kweli unania ya kugenga kichwa kitapata moto, Mungu atakufungulia
2. Msingi wa nyumba ndio kila kitu, nilipoanza kujenga nilikua na bajeti ndogo, ujenzi ulikuaa wa kimasikini kweli, matokeo yake, sasa nyumba imeisha ila msingi uko chini na kuna vitu ningetamani vingekuepo ila ndo nyumba ishamalizika, hili silijutii kwani ni funzo, hata hapa nilipofika sikutegemea kufika.
3. Hata kama fundi unamuamin, ni muhimu sana kuwepo wakati wa ujenzi, kuna makosa mengi ambayo yanaweza kutokea, kusimamia ujenzi sio kwa kuzuia uizi tu bali hapa usahihi wa nyumba unavyotaka iwe. Nyakati muhimu za kuwepo ni wakati wa kuset msingi wa nyumba, wakati wa kufunga mkanda wa nyumba, ukataji wa madirisha na milango, na kufunga lenta makosa mengi yanatokea hapa
4. Ujenzi hauna gharama kamili, kama ulipiga bajeti ya milioni 30, hakikiaha una milioni tano ya extra. Mengi yanatokea, ikiwemo vitu kupanda bei
5. Kuna muda utakua unajua kua fundi amekula hela ila hakuna jinsi, ikiwa hujui vifaa vya plumbing au umeme, chukua bei ya fundi, nenda madukani kaulizie, ukipata tofauti isio kubwa na ukiwa na uhakika wa kuletewa kitu original ambacho wewe unahofu ya kuuziwa fake , basi mpe tu fundi hela ( kwa wasio na uzoefu)
6. Siku unayomaliza kupaua ndio ujenzi unaanza, kati ya vitu ambayo ni kuhimu katika nyumba na vina gharama kubwa ni kama mfumo wa maji, umeme, milango ya mbao na grill, hivi vitu usivichukulie kirahisi kwenye budget, gharama zake hua ni M M tu.
7. Unapotaka jugenga aim for high, nilikua nimeingia mtego wa kutaka kujenga chumba kimoja na sebure, ila nilipoamua kujenga nyumba ya vyumba vitatu niliona kabisa kama ni kitu ambaacho hakiwezekani ila hatimae imewezekana, lesson-- panga kwa kuangalia wewe unakua au unataka kua nani nani na si sasa hivi una hali gani .
Plan besed on who you want to be not who you are, by this utaepuka regret za kujenga kitu ambacho baadaae hukifurahii sana
DAAAAHNingeweka picha ila nahofia watu wa karibu kujua ID yangu siunajua anonymity
Mimi nimenunua ALAF bati la maxcover Geji 28, mita moja 18320, kwa bati iliokatwa kwa mita 3 roughly ni 55,000 kwa bati moja, kwa nyumba yangu invoice ilikua Mil. 4.5,Nimenunua 28,000 migongo mipana na Niko site aisee kuwa makini mno na Mungu akuongoze Kuna wakati mafundi wanatupiga
Mi nimepaua hivo mkuu mahesabu mengine ya mita ngapi na ngapi siyajui kwa kweli ila geji ni 28 bati 80 na bei ni 2240000Mimi nimenunua ALAF bati la maxcover Geji 28, mita moja 18320, kwa bati iliokatwa kwa mita 3 roughly ni 55,000 kwa bati moja, kwa nyumba yangu invoice ilikua Mil. 4.5,
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] jamaa anajifanya mgumu nini!Inakuwaje hajajibu hadi sasa?[emoji4]
Je ni Original?? maana nimeshughudia nyumba nyingi zuri ila bati ndani ya mwaka zimepauka na kuchuja mwishowe test ya nyumba inapotea kabisaNimenunua 28,000 migongo mipana na Niko site aisee kuwa makini mno na Mungu akuongoze Kuna wakati mafundi wanatupiga
Hongera sana, maisha ni nyumba[emoji4]Nimejenga dar es salaam mkuu
Unakopa hela benkiUkisevu 250K kwa mwezi, kwa miaka 3 ni only 9 Million. Haitoshi hata msingi wa nyumba ya vyumba 3 na makolombwezo mengine. Labda uwe na chanzo kingine cha pesa. Ila kwa laki tano na nusu kwa mwezi, ukitoa matumizi ya mwezi. Hata miaka 9 bado utakuwa unajenga. Mimi naona kujenga kutegemea mshahara pekee ni ngumu sana, labda mshahara uwe mamilioni kwa mwezi
Mimi nimejenga nyumba ya vyumba 4 kwa milioni 118 ( 118,000,000/-)Si tunazungumzia nyumba yeye analeta habari za kujenga vibanda, hivi nyumba standard kabisa ya vyumba vitatu utajenga hadi kupaua kwa 7.5M? [emoji28]
Sikatai mkuu maana mimi mwenyewe nimetumia 32M hadi kupaua tu. Nyumba ni vyumba vitatuMimi nimejenga nyumba ya vyumba 4 kwa milioni 118 ( 118,000,000/-)
Siwezi kukataa, kwasasa ukitaka kujenga nyumba standard kabisa tena ya vyumba vinne hela lazima ikutoke. Huwezi kusema eti ujenge nyumba kubwa kwa 7.5 M pesa ambayo inaishia kwenye msingi tu.Mimi nimejenga nyumba ya vyumba 4 kwa milioni 118 ( 118,000,000/-)
Ukisema upige finishing ya viwango, itafika 52M.Sikatai mkuu maana mimi mwenyewe nimetumia 32M hadi kupaua tu. Nyumba ni vyumba vitatu
Hizi ndio mnazoita nyumba afu mnatutisha wa mikoani kwamba tunajenga mabanda? 😁😁Mi nimepaua hivo mkuu mahesabu mengine ya mita ngapi na ngapi siyajui kwa kweli ila geji ni 28 bati 80 na bei ni 2240000View attachment 2119237
Watu wa Dar mnapenda Sana kutisha Watu,nitakuja na picha ya nyumba ya mil.8Siwezi kukataa, kwasasa ukitaka kujenga nyumba standard kabisa tena ya vyumba vinne hela lazima ikutoke. Huwezi kusema eti ujenge nyumba kubwa kwa 7.5 M pesa ambayo inaishia kwenye msingi tu.
Achana na Dar mkuu, hata mikoa mingine kama Mwanza, Arusha,Dodoma, ni ngumu sana kujenga kwa huo mchanganuo wako.Watu wa Dar mnapenda Sana kutisha Watu,nitakuja na picha ya nyumba ya mil.8
Inawezekana kwa mikoa ambayo hakuna burnt bricks na udongo wa mfinyanzi ni majangaAchana na Dar mkuu, hata mikoa mingine kama Mwanza, Arusha,Dodoma, ni ngumu sana kujenga kwa huo mchanganuo wako.
Kila kitu hapo,kwetu fundi anapewa 350,000 kujenga msingi wa mawe..
NYie watu wa Dar hamtakaa mumiliki nyumba maana gharama za ujenzi huko ni kubwa Sana..
Wakati mimi nanunua tofari za kuchoma hadi site kwa 120,, wewe block moja kwa bei ya chini ni 1,000 .
Yeah, ni kati ya 52M hadi 90M pamoja na fensi. Bila fensi ni kati ya 52 hadi 70MUkisema upige finishing ya viwango, itafika 52M.
Mkuu nyumba hizo za bei nafuu zinawezekana kwa mikoa ambayo wanatumia tofali za kuchoma na kujengea udongo baadala ya saruji. Ukienda Mafinga, ujenzi wa aina hiyo ni kawaida kabisa, gharama zinakuwa kubwa kwenye kupaua tu. Vilevile kwa uzoefu wangu ujenzi kwa baadhi ya mikoa, labour charge zipo chini sana, mtu nyumba nzima kuanzia msingi hadi kukamilisha boma ambalo halijaezekwa anakuambia laki 8. Wakati kwa Dodoma nyumba hiyo hiyo utajenga kwa labor chaji ya 3.5M hadi 4.5M. Mikoani huko, labour chaji ya kupaua unaweza kuta laki tatu tu lkni njoo Dodoma utakuta haipungui 1MInawezekana kwa mikoa ambayo hakuna burnt bricks na udongo wa mfinyanzi ni majanga