Niliyoyaona baada ya kuita roho za giza kwa kutumia OUJIA board (don't try this at home)

Niliyoyaona baada ya kuita roho za giza kwa kutumia OUJIA board (don't try this at home)

Tumekubaliana majini hayachagui lugha 😹😹😹
Hukuona mleta mada katumia kinge kuwakwepa vibwengo vya kiswahili??
We BHANA.
Mie sizungumzii vinafsi vichafu vipepo holela alivyoviita mleta mada ambavyo hata kwenye vikombe wanakaa.
Hapa nawazungumzia marohani wa majina ya kijani wa koo za falme za kirohani ambao kuwakuta kwao ni Baharini,Misitu minene,Mapango makubwa ama chini ya ardhi.
Hao unawaita kwa qassam za kiarabu maana hiyo ndio lugha yao ya kwanza.
Ila wakishafika unaweza kuongea nao lugha yeyote.
Hao sio poa hawakai chooni au kwenye vikombe.
 
Ambao majaribu mtaleta mrejesho mmepona Nini Ili na sisi tujaribu
 
😂😂😂😂😂 Mbona nimeanza kumfanyia mambo mkuu Hammaz !?
We muulize,na leo usiku namtupia nondo mkuu mzee wa Hallelujah!
We hujui kiarabu sasa😂😂😂😂😂.
Kama unajua sema nikurushie.
Mkuu, una kesi ya kujibu bhana!

Kesi ya kuongopa! 😂😂😂

Watu wanataka wavione vitu!
 
Njia yoyote ambayo haimkufuru Mungu waweza kutumia ilimradi ufanikiwe the bad thing is to die broke while there's a lot of ways to make money.
Mkuu, lengo langu halikuwa kutafuta pesa au kitu chochote, nilifanya kama moja ya tafiti zangu binafsi, sio kwamba nilifanya ili nipate hela.

Nadhani labda haujasoma uzi mpaka mwisho.
 
Mkuu, una kesi ya kujibu bhana!

Kesi ya kuongopa! 😂😂😂

Watu wanataka wavione vitu!
😂😂😂😂😂😂Anayesema hivyo ni mamaa wa Kvant na Hanson's Choice pamoja na Heineken,anawaonaje just simple like that!?
Akitaka ajipange halafu twende sehemu ila asije akanililia tu kwenye mabega😂😂😂😂😂😂😂
 
Aaaagh wee unaweza kufa ama kujikojolea.
😂😂😂😂Is not that simple maana kwanza wengi wao wakija huja na macho ya kijani sanaa ama blue sanaa,pia urefu wa futi 7 sio chini ya hapo.
Japo wanakuja wanavutia wowowo hilo😂😂😂😂😂.
Ila macho na urefu noop is such a fvcking disaster.
hivi huwa wanajua kuwa wanatisha?
 
Kipo ila kuna namna wanakupa huo utajiri.
Labda chama ambacho ni local na kina husisha ulozi, lakini vyama vile vya kimataifa havitoi utajiri.

Wanakupa influence au mvuto, huo ndyo utakuletea pesa nyingi. Mfano kama wewe ni msanii, mwana michezo, mwansiasa, kiongozi wa dini au Karia yoyote ile

Pesa zitakuja baadae utakapo vuma na kupata ushawishi mkubwa kwa wafuasi wako.
 
😂😂😂😂😂😂Anayesema hivyo ni mamaa wa Kvant na Hanson's Choice pamoja na Heineken,anawaonaje just simple like that!?
Akitaka ajipange halafu twende sehemu ila asije akanililia tu kwenye mabega😂😂😂😂😂😂😂
Hahahah!
Lamomy kuna ujumbe wako hapa!

Unaambiwa upunguze vyombo ndipo mambo yatakwenda sawa! 😁
 
Nataka nilitume Jini pale Swiss Bank likakombe pesa zote za mafisadi wa bongonyo, kisha aniletee huku milimani kwenye hekalu la wajerumani kudadadeki.

Hallelujah!!!
 
Bob Manson
You tube kuna channel inaitwa "Mind Seed Tv" inahusiana na paranormal activity kuna vitu utavipata.

Angalia kuanzia za mwaka (2023).
 
Bob Manson
You tube kuna channel inaitwa "Mind Seed Tv" inahusiana na paranormal activity kuna vitu utavipata.

Angalia kuanzia za mwaka (2023).
Sawa mkuu nitapita huko nitazame then nitakupa mrejesho
 
Mkuu, lengo langu halikuwa kutafuta pesa au kitu chochote, nilifanya kama moja ya tafiti zangu binafsi, sio kwamba nilifanya ili nipate hela.

Nadhani labda haujasoma uzi mpaka mwisho.

Kuita ROHO zilizokufa hii nilipewa kitabu ambacho kimeandikwa kwa Arabic na kiingereza kufanya translation.


Nilijfunza mambo kadhaa ikiwemo kuita ROHO zilizokufa hapa duniani kwa lengo la kuzitumia kufanikisha mambo yako Fulani.


Hiyo njia uliyotumia ni hatua za mwanzo za kucheza na demons pamoja na spirit mbalimbali.


Next time waweza kusafiri hadi kufikia kiwango cha kugeuza tafiti kuwa fursa
 
Habari za wakati huu wana jukwaa

Duniani hatupo peke yetu, vipo viumbe au roho ambazo kwa macho hatuwezi kuziona, zipo katika dimension nyingine, lakini ipo namna tunaweza kuwasiliana au kutengeneza ukaribu nao.

Swala hili halina uhusiano wowote na imani yangu bali ni jambo ambalo niliona katika baadhi ya harakati na tafiti zangu binafsi, kujaribu na kudadisi mambo mapya ni moja ya hulka na tabia yangu.

OUJIA board ni nini?

View attachment 3045441

Ni kipande au ubao ulioundwa kwa mbao na kuandikwa kwa mpangilio wa herufi na namba ambazo hutumika kuita au kufanya mawasiliano na roho za giza. Upande wa kushoto kuna neno YES na upande wa kulia NO, upande wa chini lipo neno linalo someka GOOD BYE.

Ubao huu huambatana na kitufe au kipande kidogo cha mbao ambacho huitwa planchettes, hii hutumika kama pointer, kimbao hicho huwa na umbo la kopa na kishimo kidogo katikati yake.

Matumizi ya vitu hivi viwili yana lengo la kutafuta au kuita roho ambazo zipo karibu yetu katika mazingira tuliyopo kwa wakati huo kwa kuzungusha kipande kidogo juu ya ubao wa OUJiA board.

Baada ya kufuatilia kwa ukaribu mchezo huu na kugundua una uhalisia na kuleta matokeo, ndipo na mimi nikaona ni vyema kujaribu na kujua ni nini hasa hutokea au huonekana.

Nilikuwa na rafiki ambaye anajihusisha na uagizaji wa bidhaa katika soko la Amazon, ndipo nikamuomba tufanye order ya OUJIA board, nilifanikiwa kuipata bidhaa ikiwa katika hali nzuri kama yalivyokuwa matarajio yangu.

Nilikaa nayo kwa muda mrefu pasipo kujaribu kuitumia, sababu ni bado nilikuwa najifunza kwa kutazama videos ili nijue njia sahihi ya kutumia ubao huo. Japo katika video hizo niliona matukio ya kutisha lakini bado niliamini naweza kufanya kwa usahihi bila kupata au kuona madhara yoyote.

Mnamo tarehe 24/ 11/2022, baada ya kurejea nyumbani Mida ya saa tatu usiku, ndipo nikatoa ubao ule na kuutazama kwa dakika kadhaa, nikaona hii ndyo siku sahihi ya kufanya majaribio.

Nikauchukua ubao na kuuweka chini, nikawasha mishumaa mitatu na kuiweka pande tofauti yani mbele, nyuma na pembezoni mwa ubao. Nikatia nia na kufungua zoezi kwa kutamka maneno maalum. Hofu ilinijaa lakini sikusita kwani tayari nilikuwa na kusudi la kujaribu.

Nilianza kuzungusha kipande kidogo cha mbao katika herufi na namba zilizoandikwa katika OUJIA board, sikuona wala kusika chochote. Nikajaribu tena kwa mara nyingine huku nikiuliza kwa sauti "Is there any presence of spirits? " Am I alone? "

Nilichagua kutumia Lugha ya kingereza kwa kuhofia labda kiswahili kinaweza sababisha nikaita vigagura au vibwengo vya kiswahili. Wakati bado nazungusha kipande cha mbao (pointer) juu ya ubao, ndipo nikahisi kuna sauti nasikia bila kujua zinatoka wapi.

Nilihisi labda ni woga tu niliokuwa nao, niligeuka nyuma na sikuona kitu, lakini bado nilihisi sauti na upepo kutokea upande wa nyuma. mkono wangu uliokua juu ya ubao ukaanza kusogea bila idhini yangu, hapo nikajua tayari nimepata ugeni.

Nikauliza "what is your name"? Mkono ukasogeza ile pointer mpaka kwenye herufi "J", nikauliza "how old are you" pointer ikajisogeza yenyewe wakati nimeishika mpaka kwenye namba 34.

Nikauliza "do you wish to harm or attack me" pointer ikasogea Mpaka upande ulio andikwa NO. Bado nikawa nahisi upepo au hewa kali inatokea upande wa nyuma nilipokuwa nimekaa, lakini nikigeuka sioni kitu.

Uoga ulinizidi kwani ilikuwa ni usiku sana na nilikuwa pekeyangu, nikaamua nisitishe zoezi na kumalizia mchezo.

Kwa utaratibu wa mchezo huu, baada ya kutosheka na maongezi na Spirit husika, unapaswa kusogeza pointer katika maneno yaliyo andikwa Good bye ili kuruhusu roho hiyo kuondoka na kumaliza game, lakini nilishindwa kufanya hivyo kwani mkono ulikuwa hauwezi kabisa kusogeza kile kibao.

Nikatoa mkono na kuacha ile pointer, ajabu ni kwamba ilianza kuzunguka yenyewe na kurejea kwenye herufi 'J' kisha namba 34. Ubao niliuweka chini kabisa hivyo usidhani kwamba labda ulikuwa kwenye meza na chini kuna sumaku au kitu kingine. Ni kweli kabisa niliona pointer inazunguka yenyewe juu ya ubao pasipo kuguswa na mtu.

Niliogopa sana na nilifanikiwa kutoka nje haraka. Siku ile sijarudi nyumbani kabisa na nikaenda kulala kwa rafiki. Nilipo rejea asubuhi nikachukua ubao ule na nikautupa, ila badae niliurejea na kuuchoma moto kabisa.

Nadhani nilikosea sheria au taratibu za mchezo, pia niligundua sio jambo sahihi kutafuta mawasiliano au ukaribu na roho za giza. Kuanzia siku hiyo mpaka leo, nikilala kwenye chumba changu naota lakini sikumbuki ndoto yoyote, tofauti na sehemu nyingine. Nahisi bado kuna tatzo ndani ya chumba changu, itabidi nihame nijaribu sehemu nyingine.

Hili tukio ni la kweli na nilikutana nalo wala sio hadithi au story ya kutunga, kama yupo atakaye hitaji kujaribu, nipo tayari kumpa maelekezo lakini atambue kwamba ni mchezo hatari sana na sio vyema kuufanya ukiwa pekeyako.

Shukran kwa kusoma andiko hili, karibu share maoni au experience yako kuhusu OUJIA board.

View attachment 3045421


______________________



#BM
Mkuu unamaanisha mtu ajaribu akiwa kazini? Au msikitini?
 
Back
Top Bottom