Niliyoyashuhudia Jeshini

Niliyoyashuhudia Jeshini

Duuh asee hakuna kitengo ninachokipenda na ninachokiona rahisi jeshini kama kwata huwa sielewi kwanini watu wanakichukia na kukiona kigumu

Yani mimi kwangu kwata ndio ilikuwa sehemu ya kupoozea machungu ya jeshi, maana mimi sipendi mabio wala mazoezi nakumbuka mwishoni mwa six weeks za kwanza, nilikosa kuwepo kwenye pass of square tu roho iliniuma sana

Nikasema kwenye graduu lazima niingie kitengo cha kwata, na kweli graduu nilikuwa kwata coy sema kimbembe kuweka silaha begani, hadi mfupa wa bega ukaanza kuuma nikawa naweka handkerchief

Yani mimi kiujumla jeshini vitu nilivyovipenda ni chenja, kwata, range (japo niliishia kulenga mijusi), syndicate na route march (kutembea tu), ila ukishaniambia nikimbie daah nilikuwa najionea tabu tu

Na yale maovyoovyo mengine nilikuwa siyapendi kabisa
mimi nina mwili ambao mwalimu wa kwqta akiuona Lazima aniunge kwenye Bogi la kwata dakika 15 tu za mwanzo ata nichoka na kunitimua...

kwata ina watu wake mimi pia ni miongoni mwa watu ambao kwata imetu kataa😭😭😭😭​
 
SEHEMU YA 7
Nashangaa muda unaenda mbona haturuhusiwi kwenda kulala?
Yule bakabaka akastopisha kwata akasema hivi sasa ni saa 2 usiku muda bado kabisaa! 😂
Kuruta tunaulizana muda bado kivipi akati tumetumia muda mwingi kombania.
kuruta wakisinzia wanapewa kazi ya kushindana kukimbia
Mimi sikua nasinzia nilikua najipa moyo muda simrefu tunaenda kulala ila wapiiiii.... kila muda bakabaka anasema ndo kwanza saa 2 kamili usiku.

Tunaimba chenja, mazoezi ya viungo kwenye mazoezi nilikua napenda viroba (squats) hata 100 nashuka tu nasihisi kuchoka. then bakabaka anasema hapohapo ulipo jilaze ulale! Basi watu fasta tunajilaza kwenye vumbi
Dakika 5 nyingi anasema inuka rukaruka kichura😄
Kuruta tulipata hasira hadi wengine wakaanza kusonya.

Hapa nilishangaa kitu! Kuruta anamsonya bakabaka halafu hafanywi kitu zaidi tu anasmile halafu anasema "kuruta fungua moyo huo"
Ila walikua wanaudhi fikiria mtu anakuambia lala ghafla ruka kichura anarudia mara nyingi zile hasira plus usingizi watoto wengine hawana adabu wanamsonya na yeye anablush tu.

Hamuwezi amini alfajiri ilifika tukishuhudia kwa macho! Sasa tunaulizana "mbona leo hatujaenda kulala?" Tutafanya nini ndo ishapita hiyoo😄

Tukapanga foleni mabio yakaanza, kama nilivyosema muda wa mabio niliupenda sana zile chenja ndo ugonjwa wangu nikawa nakimbia bila kutegea nafurahia kukimbia.

Tumerudi jogging uelekeo shambani, tukitoka shambani chai kuipata hadi ukimbie 2km, tukitoka chai uelekeo kwata
Sikupenda kwata nilikua nanga nimekula mabao mengi tu mpaka bakabaka akanichoka! Akaniambia labda utaweza vitu vingine kama ngoma coy, karate au kazi mchanganyiko.

Ratiba iliendelea mpaka wiki ikakata hatukurudi angani hatukulala wiki nzima!

Baada ya wiki sasa bila kulala! vituko vilianza mtu anachuma machungwa huku kafumba macho anaota kabisa😄
Mimi ile mabio nikawa nakimbia huku nasinzia, chenja naitikia miguu inaenda mbele lakini nimelala ila naota nakimbia.
Unaweza usiamini lakini hali ndio hiyo.

Bakabaka wakawa wanasema hawa itabidi leo wakalale wasije kutufia bure hapa!
Kitengo cha kuvuna machungwa tulikua tunapiga story sana na bakabaka.
Wiki ilipita bila kuoga.


Usiku ukafika mimi najua kabisa leo tunaenda kulala, nikawa na furaha , sasa muda unaenda ila haturuhusiwi, njaa ikawa inaniuma nikasema subiri nitoroke niende kunywa chai jikoni halafu nirudi fasta kombania nilihisi tulidanganywa leo tena tunakesha.

Lahaula nilijuta kwanini nilitoroka........

Itaendelea.
Uandishi mzuri👍👍👍
 
mimi nina mwili ambao mwalimu wa kwqta akiuona Lazima aniunge kwenye Bogi la kwata dakika 15 tu za mwanzo ata nichoka na kunitimua...

kwata ina watu wake mimi pia ni miongoni mwa watu ambao kwata imetu kataa[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]​
Aahh yani mimi kwata ndio my best na sijawahi kuwa nanga wa kwata zile steps kwangu zilikuwa very easy to capture, sasa mimi mwendo wa pole unaniboa mimi napenda goose march mwendo wa haraka halafu muwe mnapigiwa ngoma na matarumbeta bwana wee, mimi hata maadhimisho ya sherehe za kitaifa huwa napenda kuangalia lile gwaride la mwendo wa haraka wakifika pale kwenye heshima kulia wanavyochapa zile silaha aahh
 
Hahaha mkuu umenichekesha sana aisee, mdogo wangu wa kiume alipangiwa maramba Tanga, Sasa yeye ni mweupe, siku amerudi ile wiki moja wanayopewa ya kuapply chuo na mkopo aisee kawa mweusi, kakondaa, mama alipomuona akamkumbatia tu huku machozi yanamlenga, kila saa tunampa mara matunda, mara supu, hafokewi yaani tulimhandle with care, baba na mama wote wamepita jkt ile mujibu ya mwaka mmoja na kaka etu mkubwa yupo jwtz wakampa mbinu mbinu na kumtia moyo hapo akarudi Tena.Ile program ilimtransform Sana dogo kwanza alirudi ile miezi mitatu ilipoisha ana furaha, self discipline ilikua juu sana, zamani kusafisha tu chumba chake mpaka mgombane, maji anaoga ya Moto lakini alipotoka kule anaoga mara 2 kwa siku bila kuambiwa Tena maji baridi anafanya mambo yake kwa wakati, yupo active, nilimfurahia Sana nikasema Jeshi kumbe linabadilisha watu.Mpaka leo anasoma MD mwaka wa 3 yeye ni mtu wa mazoezi tu , anacheza mpira wa miguu na kukimbia hizi mbio fupi, yupo kwenye timu ya chuo.Nilisema nikipata mtoto wa kiume lazima aende JKT mwaka mmoja.
Kwahiyo kwenu mnafokewa sana.
 
Hakika,, kuna vitoto viko hivyo. Lakini binafsi siioni katika kudeka, sijui ni mazoea ya makuzi.
Mfano mdogo, nimekulia kwenye nyumba ambayo haina ndoo za lita 20. Ni tank, majaba na vindoo vya lt 10.

Nimemaliza heka heka za kusoma, nikapata tempo mkoani. Mshua akagoma nisitoke nyumbani kwenda kuishi mwenyewe ama laa niende huo mkoa nikakae kwa ndugu flani, nikakubali kwenda kwa huyo ndugu.

Hilo eneo nikakuta maji kukatika week nzima ni kawaida tu na hawana tank. Wana madumu na mandoo kibao ya Lt20, mimi siwezi kuyabeba.. yule mtu anapiga simu home kunisemelea kwamba najifanyisha. Home wananitetea kidizain aendelee kunizoesha kidogo kidogo.

So hapo napo ni kudeka? Hapana ni mazoea ya makuzi.
Nachukia kuumwa, ile moment mwili unakuwa unconfortable uwa siipendi. So najikuta ndio nimeshalia.

Mazoea ya kusindikizana pia, sijui umeagizwa wapi unaenda na mdogo wako, ama unaenda wapi umeenda na mama. Haya yalinifikia mpaka huku utu uzimani.. nikitoka job imetokea ninaondoka mwenyewe, nashindwa kutembea mwenyewe, naangalia contact list nimpigie nani mpk nifike stand.

kuna mtu humu anaitwa Lenie, nimemsumbua sana. Nikitoka nampigia tustorike mpaka navyopanda hiace. 😂

So ni mazoea na sio madeko… mtoto kamzoea baba ake, akimuona lazima amgande gande. Nyie ndo mnaona madeko? Hapana 😂😂😂
Wenye trauma hawawezi kukuelewa
 
SEHEMU YA 11

2. NGOMA COY

Nilimwambia Anna mimi kwata nishafukuzwa, akanishauri nihamie ngoma coy.
Ngoma coy wanajihusisha na sanaa kuimba, kucheza, kuigiza hivyo.

Nikapiga picha mimi kuigiza, kucheza, kuimba siwezi nitafanyaje sasa? Nikajipa moyo kesho nikaongozana na Anna kitengo.

Nimefika pale bakabaka akaniambia bora umekuja ngoma coy huku utawala kama wote! hamna jua wala kutumia nguvu. Sasa kuna mchujo humu huingii bure, wote unaowaona hapa wamefanya vizuri kipindi cha mchujo.

"Aya imba tukusikie sasa ndo mchujo huu usifanye masihara"
Mimi kuimba sijui
"Sasa hujui kuimba, hapa umefata nini? Aya cheza tuone"
Kuna mziki kabisa kwenye lile hall! Navyokwambia ngoma coy utawala ujue utawala kweli!!
Mziki unapiga nicheze! Anna ananiangalia anacheka tu, nikajikaza kucheza😄

Naona kuruta wananicheka na mimi najua hapa naharibu tu.
"Weeee! Kuruta kucheza unajua lakini sasa hapa tumeshajaa tupo wengi, jaribu vitengo vingine" akaniambia bakabaka

Majibu hayo tu nikajua nimeboronga kucheza hivyo kanikataa kiaina kama walijua wamejaa kwanini hakuniambia tokea mwanzo?......

Sasa niende wapi! Ngoma coy sijafit ila ningekubaliwa hapa ingekua utawala kama wote.
Nikarudi hangani mapema, sababu muda ulikua umebaki mwingi kuruta wapo vitengoni.
Hairuhusiwi kwenda hangani muda wa kazi hivyo nililala chini ya deka ili bakabaka wakipita wasinione.

Usiku kama kawaida kombania! Ukifika unakaa chini vumbi kama lote. Kipindi hiki tushamaliza zile first weeks za mateso hivyo tukawa hatupewi mazoezi magumu hivyoo!

Tunanyanyua viroba (squats) tukichoka tunaimba chenja mambo yakizidi tunaekewa mziki tucheze bakabaka wetu alikua na speaker ndogo.


3. KITENGO CHA KAZI MCHANGANYIKO
Nilivyotoka ngoma coy nikaja huku sasa.
Kazi mchanganyiko wanadeal na kufyatua tofali na kubeba, kuchimba visiki, kuvuna machungwa na kupukuchua mahindi, kumwagilia bustani ya mbogamboga bondeni, kusafisha vyoo, kufyeka nyasi.

Mwanzo nilijitahidi nikaekwa kundi la kuvuna machungwa! Bakabaka walituambia kula machungwa hadi usaze kubeba hairuhusiwi hivyo nilikula utawala sana shambani.

Mpaka shamba likawa jeupe tumevuna kila kitu
Hivyo kazi ya machungwa baada ya kama wiki ikafa tukawa hatuendi tena.

Nikawa najila ili niende kundi la bustani nikafanikiwa, kule pia utawala sana tunamwagilizia michicha spinach ila tatizo likaja bustani kwenda ni asubuhi na jioni tu. Mchana tunaambiwa twende shambani kung'oa visiki.

Huko shambani mbali kama 2km nikaona hiki kipengele kila siku kubeba visiki nikawa nalalamika sana.
Anna akaniambia kwanini usiende kitengo cha karate?

Nikafunga ukurasa na kazi mchanganyiko nikahamia karate rasmi!

Itaendelea.

Muendelezo soma Niliyoyashuhudia Jeshini
 
Hahaha mkuu umenichekesha sana aisee, mdogo wangu wa kiume alipangiwa maramba Tanga, Sasa yeye ni mweupe, siku amerudi ile wiki moja wanayopewa ya kuapply chuo na mkopo aisee kawa mweusi, kakondaa, mama alipomuona akamkumbatia tu huku machozi yanamlenga, kila saa tunampa mara matunda, mara supu, hafokewi yaani tulimhandle with care, baba na mama wote wamepita jkt ile mujibu ya mwaka mmoja na kaka etu mkubwa yupo jwtz wakampa mbinu mbinu na kumtia moyo hapo akarudi Tena.Ile program ilimtransform Sana dogo kwanza alirudi ile miezi mitatu ilipoisha ana furaha, self discipline ilikua juu sana, zamani kusafisha tu chumba chake mpaka mgombane, maji anaoga ya Moto lakini alipotoka kule anaoga mara 2 kwa siku bila kuambiwa Tena maji baridi anafanya mambo yake kwa wakati, yupo active, nilimfurahia Sana nikasema Jeshi kumbe linabadilisha watu.Mpaka leo anasoma MD mwaka wa 3 yeye ni mtu wa mazoezi tu , anacheza mpira wa miguu na kukimbia hizi mbio fupi, yupo kwenye timu ya chuo.Nilisema nikipata mtoto wa kiume lazima aende JKT mwaka mmoja.

Ahh mimi nilitoka na hasira hasira kwa sababu naturally tu sipendi kupangiwa vitu vya kufanya , sasa imagine unakabidhi maisha yako kwa mtu mwingine kwa miezi mingi, halafu nirudi home mtu anipangie nilikuwa natamani nimkate makofi 😁😁

Ila baada ya muda nilikaa sawa japo jeshi kiukweli linakuondoa zile deko deko flani za kikawaida. Mfano ukiumwa kidogo unabagua vyakula au hufanyi chochote hadi upone, na ile ya kushindwa kuishi na watu wa tabia flani au kutokuwa responsible maana kule ukiibiwa sahani,hupewi nyingine..kazi kwako utaipata wapi ili ule 😁😁

JKT ina faida japo natamani itengenezwe kuendana na mazingira ya sasa haswa kwenye zile stadi za kazi. Tusifikirie tu kilimo pekee, kuna vingi vya kuongezwa ili mtu akitoka, asione kapoteza muda
 
Kule kwenye kuku nlikuwa naenda mara Moja Moja, ile mwanzoni nlizozana na serviceman Moja aisee nkapangwaga kwenye ujenzi uwanjani hlo tofali kulinyanyua😁siku kama hakuna ujenzi tunaenda kuangalia ruvu shooting wakifanya mazoezi
Yaani ukitaka tu shughuli uliyofanya naweza kujua wewe ni kuruti wa mwaka gani mfano wewe ulikuwa wa kujitolea op makao
 
🤣🤣🤣🤣 nilijua tuuu utawataja wale wachina...enzi napita hapo kulikuwa na mbu wengi sana Kuruta tulisumbuliwa sana na maralia...ilikuwa ngumu pia kujongomea...porini kulikuwa na chatu wakubwa...harafu wewe kama ulipita enzi za Mbuge itakuwa ilikuwa OP Kikwete...? au miaka 55 ya uhuru...?
Mbuge aliondoka kipindi cha kati ya op magufuli na op mererani akaenda kusimamia ujenzi wa ukuta wa mererani kisha akaenda Dodoma akisimamia ujenzi mpaka alipopelekwa kwenye madaraka ya ukuu wa wilaya
 
Mbuge aliondoka kipindi cha kati ya op magufuli na op mererani akaenda kusimamia ujenzi wa ukuta wa mererani kisha akaenda Dodoma akisimamia ujenzi mpaka alipopelekwa kwenye madaraka ya ukuu wa wilaya
Mbunge licha ya kuaondoka alikua anarudi sana pale kambini Kuna kipind alikua anarudi kuangalia maendeleo ya ujenzi wa Ruvu jkt club, anaenda hadi shadidi kule
 
Mi ni mujibu wa sheria.... natamani nikurahisishie code ila naona umeanza mwenyewe! Haya endelea kijana wa Ngonyani baba lao😁
Yes nimejichanganya nlimaanisha wa mujibu, wa kujitolea walikuja nyinyi mkiwa mnakaribia Kumaliza lakini mlikuwa mnafoleni pamoja usiku ila mnatenganishwa ninyi na wao.
Siku ya sherehe yenu nilicheka sana mayanga alipokuwa amevaa yale majani(kikundi cha singe)

Ujenzi wa uwanja walikamilisha wa kujitolea op makao
 
Back
Top Bottom