Niliyoyashuhudia Jeshini

mimi nina mwili ambao mwalimu wa kwqta akiuona Lazima aniunge kwenye Bogi la kwata dakika 15 tu za mwanzo ata nichoka na kunitimua...

kwata ina watu wake mimi pia ni miongoni mwa watu ambao kwata imetu kataa😭😭😭😭​
 
Uandishi mzuri👍👍👍
 
mimi nina mwili ambao mwalimu wa kwqta akiuona Lazima aniunge kwenye Bogi la kwata dakika 15 tu za mwanzo ata nichoka na kunitimua...

kwata ina watu wake mimi pia ni miongoni mwa watu ambao kwata imetu kataa[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]​
Aahh yani mimi kwata ndio my best na sijawahi kuwa nanga wa kwata zile steps kwangu zilikuwa very easy to capture, sasa mimi mwendo wa pole unaniboa mimi napenda goose march mwendo wa haraka halafu muwe mnapigiwa ngoma na matarumbeta bwana wee, mimi hata maadhimisho ya sherehe za kitaifa huwa napenda kuangalia lile gwaride la mwendo wa haraka wakifika pale kwenye heshima kulia wanavyochapa zile silaha aahh
 
Kwahiyo kwenu mnafokewa sana.
 
Wenye trauma hawawezi kukuelewa
 
SEHEMU YA 11

2. NGOMA COY

Nilimwambia Anna mimi kwata nishafukuzwa, akanishauri nihamie ngoma coy.
Ngoma coy wanajihusisha na sanaa kuimba, kucheza, kuigiza hivyo.

Nikapiga picha mimi kuigiza, kucheza, kuimba siwezi nitafanyaje sasa? Nikajipa moyo kesho nikaongozana na Anna kitengo.

Nimefika pale bakabaka akaniambia bora umekuja ngoma coy huku utawala kama wote! hamna jua wala kutumia nguvu. Sasa kuna mchujo humu huingii bure, wote unaowaona hapa wamefanya vizuri kipindi cha mchujo.

"Aya imba tukusikie sasa ndo mchujo huu usifanye masihara"
Mimi kuimba sijui
"Sasa hujui kuimba, hapa umefata nini? Aya cheza tuone"
Kuna mziki kabisa kwenye lile hall! Navyokwambia ngoma coy utawala ujue utawala kweli!!
Mziki unapiga nicheze! Anna ananiangalia anacheka tu, nikajikaza kucheza😄

Naona kuruta wananicheka na mimi najua hapa naharibu tu.
"Weeee! Kuruta kucheza unajua lakini sasa hapa tumeshajaa tupo wengi, jaribu vitengo vingine" akaniambia bakabaka

Majibu hayo tu nikajua nimeboronga kucheza hivyo kanikataa kiaina kama walijua wamejaa kwanini hakuniambia tokea mwanzo?......

Sasa niende wapi! Ngoma coy sijafit ila ningekubaliwa hapa ingekua utawala kama wote.
Nikarudi hangani mapema, sababu muda ulikua umebaki mwingi kuruta wapo vitengoni.
Hairuhusiwi kwenda hangani muda wa kazi hivyo nililala chini ya deka ili bakabaka wakipita wasinione.

Usiku kama kawaida kombania! Ukifika unakaa chini vumbi kama lote. Kipindi hiki tushamaliza zile first weeks za mateso hivyo tukawa hatupewi mazoezi magumu hivyoo!

Tunanyanyua viroba (squats) tukichoka tunaimba chenja mambo yakizidi tunaekewa mziki tucheze bakabaka wetu alikua na speaker ndogo.


3. KITENGO CHA KAZI MCHANGANYIKO
Nilivyotoka ngoma coy nikaja huku sasa.
Kazi mchanganyiko wanadeal na kufyatua tofali na kubeba, kuchimba visiki, kuvuna machungwa na kupukuchua mahindi, kumwagilia bustani ya mbogamboga bondeni, kusafisha vyoo, kufyeka nyasi.

Mwanzo nilijitahidi nikaekwa kundi la kuvuna machungwa! Bakabaka walituambia kula machungwa hadi usaze kubeba hairuhusiwi hivyo nilikula utawala sana shambani.

Mpaka shamba likawa jeupe tumevuna kila kitu
Hivyo kazi ya machungwa baada ya kama wiki ikafa tukawa hatuendi tena.

Nikawa najila ili niende kundi la bustani nikafanikiwa, kule pia utawala sana tunamwagilizia michicha spinach ila tatizo likaja bustani kwenda ni asubuhi na jioni tu. Mchana tunaambiwa twende shambani kung'oa visiki.

Huko shambani mbali kama 2km nikaona hiki kipengele kila siku kubeba visiki nikawa nalalamika sana.
Anna akaniambia kwanini usiende kitengo cha karate?

Nikafunga ukurasa na kazi mchanganyiko nikahamia karate rasmi!

Itaendelea.

Muendelezo soma Niliyoyashuhudia Jeshini
 

Ahh mimi nilitoka na hasira hasira kwa sababu naturally tu sipendi kupangiwa vitu vya kufanya , sasa imagine unakabidhi maisha yako kwa mtu mwingine kwa miezi mingi, halafu nirudi home mtu anipangie nilikuwa natamani nimkate makofi 😁😁

Ila baada ya muda nilikaa sawa japo jeshi kiukweli linakuondoa zile deko deko flani za kikawaida. Mfano ukiumwa kidogo unabagua vyakula au hufanyi chochote hadi upone, na ile ya kushindwa kuishi na watu wa tabia flani au kutokuwa responsible maana kule ukiibiwa sahani,hupewi nyingine..kazi kwako utaipata wapi ili ule 😁😁

JKT ina faida japo natamani itengenezwe kuendana na mazingira ya sasa haswa kwenye zile stadi za kazi. Tusifikirie tu kilimo pekee, kuna vingi vya kuongezwa ili mtu akitoka, asione kapoteza muda
 
Kule kwenye kuku nlikuwa naenda mara Moja Moja, ile mwanzoni nlizozana na serviceman Moja aisee nkapangwaga kwenye ujenzi uwanjani hlo tofali kulinyanyua😁siku kama hakuna ujenzi tunaenda kuangalia ruvu shooting wakifanya mazoezi
Yaani ukitaka tu shughuli uliyofanya naweza kujua wewe ni kuruti wa mwaka gani mfano wewe ulikuwa wa kujitolea op makao
 
Mbuge aliondoka kipindi cha kati ya op magufuli na op mererani akaenda kusimamia ujenzi wa ukuta wa mererani kisha akaenda Dodoma akisimamia ujenzi mpaka alipopelekwa kwenye madaraka ya ukuu wa wilaya
 
Mbuge aliondoka kipindi cha kati ya op magufuli na op mererani akaenda kusimamia ujenzi wa ukuta wa mererani kisha akaenda Dodoma akisimamia ujenzi mpaka alipopelekwa kwenye madaraka ya ukuu wa wilaya
Mbunge licha ya kuaondoka alikua anarudi sana pale kambini Kuna kipind alikua anarudi kuangalia maendeleo ya ujenzi wa Ruvu jkt club, anaenda hadi shadidi kule
 
Mi ni mujibu wa sheria.... natamani nikurahisishie code ila naona umeanza mwenyewe! Haya endelea kijana wa Ngonyani baba lao😁
Yes nimejichanganya nlimaanisha wa mujibu, wa kujitolea walikuja nyinyi mkiwa mnakaribia Kumaliza lakini mlikuwa mnafoleni pamoja usiku ila mnatenganishwa ninyi na wao.
Siku ya sherehe yenu nilicheka sana mayanga alipokuwa amevaa yale majani(kikundi cha singe)

Ujenzi wa uwanja walikamilisha wa kujitolea op makao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…