Niliyoyashuhudia Jeshini

Niliyoyashuhudia Jeshini

hakuna jeshi laini duniani nasema hakuna. nilikutana na dogo mkorea kusini wao service kwa mujibu ni 2 years. mwendo wa shuluba yaan baruti bin cheche bin kujamba.
Lakini tofauti na majeshi ya nchi zilizoendelea huku kwetu bado tunachapana kama punda, kule kwa wenzetu ni matusi tu kama kawa lakini drill instructors hawaruhusiwi hata kumkunja recruit, huku kwetu afande anamnyuka kuruti utasema anapiga mtoto wake
 
Bustani utawala mwingi uwe kwenye nyanya au chainizi unapiga kazi chapu ukimaliza unazama kwenye mikorosho unakula mabibo mpaka sauti haitoki

Mwanzoni tulivofika ukiwekewa msosi ulikua unabaki, Baada ya kimbembe kuanza aisee unakula A coy ukimaliza unawahi C coy unamaliza E coy!

Wakaanzaga utaratibu wanapeana code kwenye kombania zao maana kuruti zinarudia msos kwenye coy mbali mbali lkn tulikula sana[emoji16]
Nahisi ulikuwa Op Magufuli, kama ulimkuta Private Kwaro alikuwaga na msemo wake mmoja "kuruti kama hujashiba wahi bombani", maana yake usirudie msosi we kabwie mimaji tu utashiba
 
Hata mimi sikuwa interested kabisaaa ila nilivyoingia kwenye lile geti nikafungua moyo

Sikuwahi kudoji na hata baada ya muda zilipopatikana chance za kutoka, niliwahi toka one time tu. Nilisubiri hadi siku ifike niondoke

Na wajeda baadhi walikuwa wananiheshimu kwa sababu nilikuwa naenda na mfumo na nilikuwa sio lopolopo. Kuna baadhi walinambia kama naweza jifikiria kuingia ila nilijua haiwezekani..

japo nakumbuka ile siku narudi home baba alishtuka na ndugu yangu mmoja alinisahau kabisaa, sikuwahi pata extra care kama ile siku 😁😁😁
Hahaha mkuu umenichekesha sana aisee, mdogo wangu wa kiume alipangiwa maramba Tanga, Sasa yeye ni mweupe, siku amerudi ile wiki moja wanayopewa ya kuapply chuo na mkopo aisee kawa mweusi, kakondaa, mama alipomuona akamkumbatia tu huku machozi yanamlenga, kila saa tunampa mara matunda, mara supu, hafokewi yaani tulimhandle with care, baba na mama wote wamepita jkt ile mujibu ya mwaka mmoja na kaka etu mkubwa yupo jwtz wakampa mbinu mbinu na kumtia moyo hapo akarudi Tena.Ile program ilimtransform Sana dogo kwanza alirudi ile miezi mitatu ilipoisha ana furaha, self discipline ilikua juu sana, zamani kusafisha tu chumba chake mpaka mgombane, maji anaoga ya Moto lakini alipotoka kule anaoga mara 2 kwa siku bila kuambiwa Tena maji baridi anafanya mambo yake kwa wakati, yupo active, nilimfurahia Sana nikasema Jeshi kumbe linabadilisha watu.Mpaka leo anasoma MD mwaka wa 3 yeye ni mtu wa mazoezi tu , anacheza mpira wa miguu na kukimbia hizi mbio fupi, yupo kwenye timu ya chuo.Nilisema nikipata mtoto wa kiume lazima aende JKT mwaka mmoja.
 
Lakini tofauti na majeshi ya nchi zilizoendelea huku kwetu bado tunachapana kama punda, kule kwa wenzetu ni matusi tu kama kawa lakini drill instructors hawaruhusiwi hata kumkunja recruit, huku kwetu afande anamnyuka kuruti utasema anapiga mtoto wake
hapo ndipo chanzo cha kuambukizana ukimwi...fimbo imchape yule, huyu...na yule...😭😭😭

jeshi limeoza...asilimia 75 wapo kwenye grid ya Taifa😭😭😭​
 
Hilo neno mteru nimekumbuka mbali kuna wadau walikuwa ni vipande vya mwanakwetu ila sasa mteru kama wote,wakishikiliwa kidogo tu utawahurumia..
Kutolewa uraia lazima mtu uive..
TPDF ukidoji ukatoboa wewe mwamba ila majeshi mengine ni kosa kubwa..
Kuruti hafi,kuruti mdudu!!!
Hapo kudoj Tpdf elezea kidogo mkuu kwamba hutoboi vp?kwa maana kwamba Kuna msako mkali au vipi
 
SEHEMU YA 3
Watu tunang'oa visiki huku tunasinzia, yule mjeda namesake akanifata "njoo huku" nikaenda sasa kuna vichaka vingi akanipeleka kichaka flani hivi majani yamekaa kimduara katikati uwazi upepo unapita. Akaniambia "lala hapo muda wa kuondoka ukifika nitakufata" nikapiga zangu mbonji.

Nakuja kushtuliwa na mateke, nimekurupuka namuona bakabaka ananitizama tena ana nyota mbili (bakabaka - mwanajeshi aliyeajiriwa) "toka huko chuchumaa hapa haraka" nikatii amri mzee.
Umefikaje huku? Swali nimepigwa...

Nikafikiria nikaona siwezi kumchoma mjeda namesake ni vyema nipambane na hali yangu.
Nikaanza kujitetea pale, "Mimi naumwa vidonda vya tumbo nimezidiwa nikaona nipumzike hapa" akamwita mjeda hana cheo akamwambia naomba umshughulikie huyu.
Yule mjeda akaniambia "adhabu yako utabeba kisiki kikubwa peke yako kupeleka kambini". Nikaona nishaanza kupata msala mapema muhimu nikurudi nyumbani.

Nimekaa kihuzuni mjeda namesake akaja "nimekutafuta kule sijakuona" nikamwambia nilifumwa nikampa mkasa wote akaniambia nisijali atanisaidia. Kweli saa 4 ikafika filimbi ikalia kisiki kimoja mnabeba watu wawili kwenda kambini. Yule bakabaka akasema yule mwenye adhabu yangu yuko wapi? Nikaenda akanipa kisiki kikubwa machozi yakaanza kunilenga.

Akaniambia unatoka mkoa gani nikamwambia Dar! Akacheka sana "mbona watu wa dar wajanja? Wewe kitu kidogo unalia ebu acha usen....."

Nikapewa kisiki kikubwa peke yangu yeye akaondoka, namesake akawapasia kile kisiki kuruta wengine, akawaita wakaka wawili akawaambia kisiki chao wanipe mimi changu wabebe. Hawakupinga fasta wakabeba.
Kama kawaida uelekeo kambini, umbali kutoka pale shamba hadi huko ni kama 2km, kutembea ni mchakamchaka.

Tumefika tukaenda dining, tukakuta bakabaka kama wote
"Aya kila mtu ana kikombe chake! chukua ndoo nenda kituoni kajaze mchanga ulete hapa ndo uchukue chai"
Kituoni ni kule siku ya kwanza tuliposhuka na gari
Njaa inauma, muda huo nikawa sisikii tena kulia ila hasira kama zote nikajuta kwenda jeshi.

Kufika huko kituoni michanga yenyewe ina maji, nikatiliwa mchanga nikamuomba yule mjeda aniwekee ndoo nusu sababu kipara plus ndoo ya mchanga nzito, akaniwekea.
Niliporudi jikoni kumbe bakabaka wanakagua kama ndoo imejaa au ipo nusu........

Tupo kwenye foleni ya kukaguliwa machozi yananilenga najua kabisa narudishwa nikajaze ndoo, akaja mjeda namesake akaniuliza "ndoo yako imejaa? Nikamwambia hapana
Basi kuna kuruta alikua anapita amerudishwa akajaze ndoo mjeda namesake akamwambia chukua mchanga wako muongezee huyu wewe ukajaze tena!

Yule akupinga akanijaziwa ndoo nikakaguliwa imejaa nikachukua chai na mkate.
Uzuri chai imekolea sukari na mkate mzuri mkubwa nikala nikashiba ila majonzi yakawa palepale ninayo moyoni.
Yaani siwezi kupewa msosi mpaka jasho linitoke???
Nikipata upenyo lazima nimpigie mama aje kunifata.
Mmh nisingeweza uwiii
Hongera
 
SEHEMU YA 10
VITENGO

Jeshi kuna vitendo vingi kama Ngoma coy, Kwata, karate na kitengo cha kazi mchanganyiko

Kipindi cha kupewa vitengo ukawadia sasa hapa nitaanza kuelezea kitengo kimoja hadi kingine sababu vyote nilipita, nilipita ila sio kwa kupenda ni vile tu maswahibu yaliniandama.

1. KWATA
Service man walituambia siku ya graduation kuna watu hawatovaa kombat na mabuti "Nyie fikirieni mtu yupo kitengo cha kazi mchanganyiko siku ya gradu avae kombati ya nini? Ila ukiwa kwata kombati lazima uvae, tena nyie ndo mnaanza kupewa" akasema

"Ooh! Kumbe kwata kuna kuvaa kombati na mabuti ya jeshiii! Hicho kitengo ndo nakitaka" hapo namwambia Anna

Anna akasema mimi nitaenda ngoma coy kwata siwezi. Mimi kwata ilinishinda tokea kombania usiku tulivyokua tunafundishwa lakini nikasema acha niende ili nivae kombati siku ya graduu....

Wa kwata tukaambiwa tupange mistari uelekeo uwanja wa nyuma ya jeshi! Nimeusahau jina lake. Tunaenda kwa kuchapa mkono bega la kushoto umelikaza[emoji1]
Hao tukaanza kutembea huku tunachapa! Chapa chapa... mpaka tukafika.

Tukaekwa kimakundi, nikaangukia kundi la Afande nampa jina afande mzee sababu age ilikua imeshamtupa mkono.
Akaanza kutupa intro pale halafu akasema kupima uwezo wenu, wote tulale tumbo juu tuangalie jua hakuna kukwepesha macho.

Ule uwanja una jua kalii kichizi! Tukitoka kambini hali ya hewa nzuri tukiingia ule uwanja jua kali kinoma.
Kuruta tumelala macho juu! Ole wako ujile kazi unayo
Macho hadi yanatoa machozi watu tunakodorea jua.

Baada ya hapo kazi ikaanza
"Kwa mwendo wa pole mbele tembeaaa...
Nyuma geuka....
Mbele geuka kushota geuka....
Aya chap mguu..."
Wazee tunapiga kwata!!

Mwanzoni wengi tulikua nanga, afande mzee akawa anatuelekeza kwa upole pale, kadri muda unaenda mananga yanapungua ila mimi nilikua nanga pro...
Kuchapa mkono sijui, mguu siwezi!

Afande mzee ananiambia "kaza tako hilo mwendo wa polepole chapa mkono kwa ukakamavu"
Ikafika muda hadi mabao nikawa nakula
Hapo nilijuta nikasema kwata siwezi! Bora nihame kitengo

Muda wa kwata umeisha afande mzee akaniambia "kesho nisikuone kwenye kundi langu, sitaki mananga mimi"
[emoji1][emoji1]Nilijisikia unyonge ila nikasema nakaza hukuhuku kwata! ili nivae kombati siku ya graduu.....

Usiku muda wa kombania service man akawa ananielekeza kwata pale kidogo nikapata mwanga nikasema kesho nitaweza.
Kweli bhana kesho nikawa nimejitahidi afande mzee akaridhika niendelee kubaki kundi lake.
Mpaka siku ya tatu wiki haijaisha style nyingi za kwata tukawa tumefundishwa, hapo mzozo kwangu ukaanza.

Nilikua nachanganya madensa.
Ikitajwa style hii mimi nafanya style nyingine.

" kuruta wewe hama kitengo kabla muda haujaenda! Kama kombati utavaa hata lililochakaa, waziiii!?
Nikamwambia wazii Afande!

Safari yangu na kwata ikawa imeishia hapoo!
Wiki haijaisha kule kwenye kwata lakini mwili una mabadiliko mengi hii ilikua kwa wote sanasana wacheza kwata.
nikivua nguo mwili una alama mbili nyeusi na weupe

Sehemu iliyofunikwa na nguo kweupe rangi niliyotoka nayo nyumbani, sehemu ambayo inabaki wazi nikivaa imekua nyeusi kama mkaa! Uso wote mweusii shingo nusu nyeupe nusu nyeusi.

Itaendelea.......
Karibu upande wa pili, huku hakuna kuchimba visiki wala hutaenda kuvuna mahindi.
 
SEHEMU YA 10
VITENGO

Jeshi kuna vitendo vingi kama Ngoma coy, Kwata, karate na kitengo cha kazi mchanganyiko

Kipindi cha kupewa vitengo ukawadia sasa hapa nitaanza kuelezea kitengo kimoja hadi kingine sababu vyote nilipita, nilipita ila sio kwa kupenda ni vile tu maswahibu yaliniandama.

1. KWATA
Service man walituambia siku ya graduation kuna watu hawatovaa kombat na mabuti "Nyie fikirieni mtu yupo kitengo cha kazi mchanganyiko siku ya gradu avae kombati ya nini? Ila ukiwa kwata kombati lazima uvae, tena nyie ndo mnaanza kupewa" akasema

"Ooh! Kumbe kwata kuna kuvaa kombati na mabuti ya jeshiii! Hicho kitengo ndo nakitaka" hapo namwambia Anna

Anna akasema mimi nitaenda ngoma coy kwata siwezi. Mimi kwata ilinishinda tokea kombania usiku tulivyokua tunafundishwa lakini nikasema acha niende ili nivae kombati siku ya graduu....

Wa kwata tukaambiwa tupange mistari uelekeo uwanja wa nyuma ya jeshi! Nimeusahau jina lake. Tunaenda kwa kuchapa mkono bega la kushoto umelikaza[emoji1]
Hao tukaanza kutembea huku tunachapa! Chapa chapa... mpaka tukafika.

Tukaekwa kimakundi, nikaangukia kundi la Afande nampa jina afande mzee sababu age ilikua imeshamtupa mkono.
Akaanza kutupa intro pale halafu akasema kupima uwezo wenu, wote tulale tumbo juu tuangalie jua hakuna kukwepesha macho.

Ule uwanja una jua kalii kichizi! Tukitoka kambini hali ya hewa nzuri tukiingia ule uwanja jua kali kinoma.
Kuruta tumelala macho juu! Ole wako ujile kazi unayo
Macho hadi yanatoa machozi watu tunakodorea jua.

Baada ya hapo kazi ikaanza
"Kwa mwendo wa pole mbele tembeaaa...
Nyuma geuka....
Mbele geuka kushota geuka....
Aya chap mguu..."
Wazee tunapiga kwata!!

Mwanzoni wengi tulikua nanga, afande mzee akawa anatuelekeza kwa upole pale, kadri muda unaenda mananga yanapungua ila mimi nilikua nanga pro...
Kuchapa mkono sijui, mguu siwezi!

Afande mzee ananiambia "kaza tako hilo mwendo wa polepole chapa mkono kwa ukakamavu"
Ikafika muda hadi mabao nikawa nakula
Hapo nilijuta nikasema kwata siwezi! Bora nihame kitengo

Muda wa kwata umeisha afande mzee akaniambia "kesho nisikuone kwenye kundi langu, sitaki mananga mimi"
[emoji1][emoji1]Nilijisikia unyonge ila nikasema nakaza hukuhuku kwata! ili nivae kombati siku ya graduu.....

Usiku muda wa kombania service man akawa ananielekeza kwata pale kidogo nikapata mwanga nikasema kesho nitaweza.
Kweli bhana kesho nikawa nimejitahidi afande mzee akaridhika niendelee kubaki kundi lake.
Mpaka siku ya tatu wiki haijaisha style nyingi za kwata tukawa tumefundishwa, hapo mzozo kwangu ukaanza.

Nilikua nachanganya madensa.
Ikitajwa style hii mimi nafanya style nyingine.

" kuruta wewe hama kitengo kabla muda haujaenda! Kama kombati utavaa hata lililochakaa, waziiii!?
Nikamwambia wazii Afande!

Safari yangu na kwata ikawa imeishia hapoo!
Wiki haijaisha kule kwenye kwata lakini mwili una mabadiliko mengi hii ilikua kwa wote sanasana wacheza kwata.
nikivua nguo mwili una alama mbili nyeusi na weupe

Sehemu iliyofunikwa na nguo kweupe rangi niliyotoka nayo nyumbani, sehemu ambayo inabaki wazi nikivaa imekua nyeusi kama mkaa! Uso wote mweusii shingo nusu nyeupe nusu nyeusi.

Itaendelea.......
Duuh asee hakuna kitengo ninachokipenda na ninachokiona rahisi jeshini kama kwata huwa sielewi kwanini watu wanakichukia na kukiona kigumu

Yani mimi kwangu kwata ndio ilikuwa sehemu ya kupoozea machungu ya jeshi, maana mimi sipendi mabio wala mazoezi nakumbuka mwishoni mwa six weeks za kwanza, nilikosa kuwepo kwenye pass of square tu roho iliniuma sana

Nikasema kwenye graduu lazima niingie kitengo cha kwata, na kweli graduu nilikuwa kwata coy sema kimbembe kuweka silaha begani, hadi mfupa wa bega ukaanza kuuma nikawa naweka handkerchief

Yani mimi kiujumla jeshini vitu nilivyovipenda ni chenja, kwata, range (japo niliishia kulenga mijusi), syndicate na route march (kutembea tu), ila ukishaniambia nikimbie daah nilikuwa najionea tabu tu

Na yale maovyoovyo mengine nilikuwa siyapendi kabisa
 
Duuh asee hakuna kitengo ninachokipenda na ninachokiona rahisi jeshini kama kwata huwa sielewi kwanini watu wanakichukia na kukiona kigumu

Yani mimi kwangu kwata ndio ilikuwa sehemu ya kupoozea machungu ya jeshi, maana mimi sipendi mabio wala mazoezi nakumbuka mwishoni mwa six weeks za kwanza, nilikosa kuwepo kwenye pass of square tu roho iliniuma sana

Nikasema kwenye graduu lazima niingie kitengo cha kwata, na kweli graduu nilikuwa kwata coy sema kimbembe kuweka silaha begani, hadi mfupa wa bega ukaanza kuuma nikawa naweka handkerchief

Yani mimi kiujumla jeshini vitu nilivyovipenda ni chenja, kwata, range (japo niliishia kulenga mijusi), syndicate na route march (kutembea tu), ila ukishaniambia nikimbie daah nilikuwa najionea tabu tu

Na yale maovyoovyo mengine nilikuwa siyapendi kabisa
Mimi kitu pekee ambacho kilikua kinaniudhi ni kuhesabu namba Kila dak. As ware nyingi
 
Back
Top Bottom