Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Inatokea post namba 223.


Nimeona tuwekane wazi kidogo. Kisa kilichokwisha post namba 223 kimeelezea nilipokabidhiwa majini na babu yangu, yeye alikuita kufunguliwa macho. Kwa kiwango fulani kweli nilifunguliwa macho.

Kisa kilochofatia nikaonesha safari yangu ya kwanza baada ya kuoa, ilionipeleka Shinyanga na majini wakafanikiwa kumfanyia tiba mwanamke aliekua anasumbuliwa na majini. Ieleweke kua sijatibu mimi na wala sijui walitibu vipi zaidi ya mimi kumshika kichwa tu yule mwanamke na walichonielezea hao majini siku ile na baadae.



Kisa hicho ni cha miaka mingi sana nyuma, sasa hivi ni mtu mzima. Babu yangu alishatangulkia mbele ya haki. Shamba letu la ufukweni Duga, lipo mpaka leo, wanaokaa pale kwa sasa ni watoto na wajukuu wa babu walioamua kuishi pale. Watoto waliopo pale ni mmoja mkubwa kwa baba yangu wa kike. Na wakiume na mkewe na wanawe ni kwa mama mwingine na baba yangu, wanachangia baba tu.

Binafsi huwa nakwenda sana Duga shamba la babu, kwa sana namaanisha kila msiumu wa kamba huwa tunaenda mimi na mzee kuvuna kamba. Licha ya kamba, kwa babu kuna minzi mingi sana, kuna miembe mingi. Babu yangu alikua anapenda sana miti ya kudumu, kuna miembe ya aina )ofautoi isiopungua 500 na minazi zaidi ya 1000 aliyoiacha marehemu babu.

Bahati watoto zake wote wanajiweza, wana shughuli zao na mali zao, na wawili, mkubwa wa kike na kiume na watoto zao na mkubwa wa kiume wa tumbo lingine ndio wanaoishi huko full time. Waliamua wenyewe waishi huko ili shamba lisikose mtu na lina utajiri wa kutosha. Mbali ya minazi na miembe alioicha babu, kuna miti mingi ya hapa na pale ya matunda, ambayo haipo kwa kiwango cha biashara. Babu alipanda kila aina ya matunda kidopo kidogo, shamba la babu ni kubwa sana, sio la kitoto. Lina minai mingi, nazi karibia kila siku zinangushwa, na pesa wanagawa kwa kila ndugu, Hakuna tatizo, wasimamizi ni wazuri sana na wacha Mungu.

mambo ya tiba na pango kuna wanafunzi wa babu lakini hawako kwa kiwango cha babu. ilimradi wapo tu. Umaarufu wa kwenda kutibiwa watu kwa mzee Mabruki uliisha alipoondoka mwenyewe. Mimi binafsi sijairithi kazi ya uganga ya babu, kabisa tena. Wapo majini, ingawa wenyewe wanasema ni watu, alioniwachia babu. ikitokea, wao ndio wanatibu watu bila mimi kujua wanachokifanya zidi ya kunijulisha tu.

Arsis yupo, pete yake naivaa kila siku. Jini wa bakora yupo na bakora ya babu aliirithi binti yake ambae anakaa shamba kwa sasa, yeye ndio anaitumia kwa tiba watu wakienda. Anaelewa mwenyewe anatibu vipi, mimi simuingilii wala simuulizi. Ni shangazi yangu, yeye ananipenda sana na anawaambia kila mtu., mimi ndio mrithi wa babu kwenye uganga.

Visa vinavyofatia sana sana vitakua vya mahojiano kati yangu na Arsis, nitajitahidi kuvifanya vyepesi vieleweke, ingawa mimi sio mwandishi.

Arsis mpaka leo ni rafiki yangu na anakuja kila nikimuita zile sehemu zake za kumuita. Mwenyewe anapenda sana kila nikija kwenye msimu wa kamba nimuite kila siku tuongee. Mpaka leo kwa Dar nikitaka kumuita nakwenda pale oshen road, pia alinionesha na sehemu nyingine mtajijua wakati kisa kinaende;lea. Hii ipo nje ya mji kidogo.

Visa vijavyo vina elimu kubwa sana ya Arsis, sio yangu. Mimi najifunza kwake.

Kuna watu wengi wanaongelea kuhusu majini waongo, wazuri, wabaya. Kwenye mahojiano na Arsis tutapata mwanga mkubwa sana kwa mujibu wa Arsis.

Napenda ieleweke, Arsis anasisitiza sana nijifundishe kusoma uandishi ili niandike vizuri, ananambia yeye atanisaidia kumbukumbu kwa nilioyasahau na atanisaidia kunielezea yale amapya nitayohisi yanahitaji aelezee zaidi.

Nawaahidi nitapitia post moja moja za nyuma na kurekebisha maandishi, kupunguza au kuzidisha na kurekebisha nilipokosea na kuyakusanya kwenye post moja ikiwezekana, yaani kufanyia editing. Arsis kanambia kuna makosa mengi sana.

Nafahamu kua anausoma huu uzi, sifahamu kama ni member JF au hapana, nimemuuliza hilo akanambia " mimi nimekwambia nasoma tu, usiniulize zaidi kuhusu hilo". Hiyo ni kawaida yake Arsis, mtajionea mbele huko namuuliza mpaka anakasirika.lakini ni mtu mwema sana. Mwenyewe anashikilia nimwite mtu. Ingawa kiukweli sijui ni kiumbe wa aina gani. Mimi nachukulia ni mtu kama mimi lakini hataki aonekane. Isipokua anasema umeshaniona mara nyingi lakini hujui kama ni mimi. Anasisitiza anakuja kwa sura na muonekano tofauti bila mimi kufahamu.


Itaendelea.
 
1. Mahojiano na Arsis

Yafuatayo ni mahojianao yangu (nitajiita simba kuanzia sasa) ambayo sio ya kwanza kati yangu na Arsis, lakini nimeyaweka namba 1 kwa kua nahisi yataleta mpangilio mzuri wa mahojiano yatakayofatia.

Mimi; Arsis, Arsis, Arsis, upooo?

Baada ya kumwita ikapita kama nusu dakika hivi.

Arsis; Nipo Simba, vipi hali yako?
Mimi; Mimi mzima kabisa na wewe?
Arsis; Mimi nipo salama namshukuru Muumba wetu.
Mimi; Arsis, leo nina swali moja tu, nataka nikuulize utakaponijibu ndio naweza kua na maswali mengine.
Arsis; Uliza Simba.

Mimi; Arsis kuna siku nilikuuliza wewe umejuana vipi na Babu yangu, nikahisi kama kuna vitu umenificha hukunieleza vyote. Ulinielezq umefahamu kupitia Jini wa bakora, nikahisi umenip9ga [piga chenga. Leo nieleze bila chenga, tumeshakua marafiki muda sasa.

Kabla ya kujibu Arsis akacheka kma mtu aliyefurahi. Naomba kusisitiza hapa, Arsis ni kiumbe mmoja ambae ukiongea nae utaona raha sana, hacheki kwa majivuno au kwa kebehi, unamhisi anacheka kwa kua anacheka kweli.

Arsis; Sikiliza, leo umenifutrahisha sana, nilikua nangoja siku uwe serious kama leo ili unielewe vizuri. Nilikua nakuhisi kama ninayokwambia yanakuingia na kutoka. Nisikilize kwa makini.

Simba, mimi nilikua kifungoni kwa miaka zaidi ya 900, ndio ni 925 alaiejitahidi mpaka nikafunguliwa kifungoni ni babu yako kupitia jini wa bakora. Simba nataka uelewe, jini wa bakora ni jini mwenye heshima sana katika majini. Nafahamu kua ukoo wake walikua na uhusiano na ukoo wa babu yako, yaani ukoo wako kwa baba yako kwa muda mrefu sana., karne nyingi sana, vizazi na vizazi, lakini ni wachache sana katika ukoo wenu siku za nyuma wakaweza kukabidhiwa bakora kama uliopewa wewe. Wote wengine waliopewa bakora au wanapewa bakora za ukoo tu, lakini babu yako alipewa bakora kutoka kwa mwenyewe jini bakora, lakini liitengeza, sio ya kurithi. Bakora ya jini bakora ya kurithi kwa wazeewake ni ile uliopewa wewe tu. Ile bakora kuwepo tu kwako ni kinga kubwa na heshima kubwa sana kutoka kwa majini wote watakao kuona nayo. Nakushangaa wewe umeifungia chumbani.

Miimi; Nimeiweka Arsis, siwezi kutoka na kutembea nayo kila mahali.
Arsis; Nafahamu hilo na Jini bakora anafahamu hilo, dunia ya siku hizi hambebi bakora kama zamani, ni watu na makabila machache sana yenye kujua thamni ya mwanamme kubeba bakora. Mimi nakwambia jizoeshe kua nayo katribu zaidi ile bakora. Usiwe na wasi wasi, Jini bakora hasikii haya maongezi yetu wala hawezi kusogea hapa kusikiliza tunachoongea, tunaheshimiana sana.

Mimi; Arsis; Unaanza kunipiga chenga tena? Hujajibu swali langu.
Arsis; Tafadhali tumia lugha nzuri ukiongea na mimi, kqnza mimi ni mtu mazima sana kwako kwa kiwango chochote kile, halafu mimi ni Mwalimu wako. Acha lugha hizo mitaani. Sikupigi chenga, nipo katika kukujibu swali lako lakini nataka uelewe kwa undani zaisi, fanya dsubira.
Mimi; Samahani, unajua lugha zetu za siku hizi, Nitakua mwangalifu.
Arsis; Usijali Simba. Nisikilize kwa makini. Babu yako alikutana na watu kutoka Pemba wakati anaishi Tanga, hao watu walikuja kutafuta mali za Mjetrumani, miaka mingi sana nyuma.
Mimi: Hujui mwaka gani?
Arsis; Najua ilikuwa mwaka gani, ni mwaka wa 1072 kwa miaka ya dunia ya kwanza, hii dunia tuliopo. Hawa watu, alikua ni kijana mmoja ambae alihadithiwa na babu yake kabla hajafa, kua Tanga, nje kidogo ya mji kuna mali ya Wajerumani imefukiwa. Babu yake alimwabia na yeye kahadithiwa na rafiki yake ambae ameshfariki, lakini ameandika jina ya hio sehemu na alama zilizowekwa. Aliambiwa kua asijaribu kwenda boila kutafuta mwenye nguvu za majini na mwenyeji wa Tanga. Bila hivyo itakua ni hatari sana. Ataekwenda tu bila ulinzi wa nguvu za majini anaweza kufa.

Huyo kijana ndio akaanza kutafuta mtu mwenye nguvu hizo kwao Pemba, wapemba kila akiwaambia au wengine wanadhatrau hio habari au wengine wanaogopa. Ukapata mtu mmoja akamwabia kuna mama wa Kipenda yupo Darisalam, anajua kua huyo mama ana majini wakubwa anawatumia kwa kuondoa matatizo ya watu. Ndio kafunga safari akaja Mjini Dar. Akafanikiwa kumuona huyo mama, huyo mama kweli alikua na majini wakubwa sana na anapandisha kichwanikwake. Walipokuja wale majini wakasema sisi hatujui kuhusu hizo mali lakini kuna mganga mmoja yupo Tanga, huyo mganga ni mtu wa Lamu, Mgunya lakini anaishi Tanga, yeye ana majini wakubwa wa kutokea Tanga wanaweza kujua Yule jini wa mama akawapa anuani mpaka mtaa watakapompata huyo mganga wa kigunya, alikua barabara ya tisa, karibusana na sokoni pale Tanga.

Yule mama wa Kipemba hafanyi ile kazi yake peke yake, yeye anapandisha jini lakini mtu anaetafsiri na lazima anakua karibu yake ni mume wake. Yule mume akasikia kisa chote kile akawa na yeye kapata tamaa ya mali.

Mimi; Arsis kumbe ni mtu wa mikasa mingi wewe.
Arsis; Leo umesikia mali ndio unasikiliza kwa makini? Subiri nimalize, usije kusema nakupiga chenga, nyamaza usikilize mpaka nimalize, usitie neno lako.
Mimi; sawa Arsis, mbona leo unakua mkali hivi?
Arsis; Umeuliza kitu ambacho inabidi nikueleze kwa yundani, vipi nimejuana na babu yako, au hutaki tena kujua?Nyamaza. usijibu.

Nikanyamaza kimya.

Arsis; Leo huondoki hapa mpaka nimalize kukufahamisha.

Basi yule mume na ytule kijana wakahangaika kufanya safari ya kuja Tanga kwa mganaga wa Kigunya, alikua hodari sana wa kusoma vitabu huyo mganga, mtu mzima sana, lakini alikua anajulikana sana kwa kutibu watu na alikua anaweza kuita majini wakubw wakubwa sana. Alikua na maarifa mingi sana.

Baada ya muda, wakafanikiwa kuja Tanga, wakakutana na yule Mzee wa Kigunya wakamueleza ile habari. Yule mzee akawasikiliza kawaambia basi nyinyi kaeni hapa kwangu wakati mimi nafanya uchunguzi wa hiyo habari. Watu wengi wanakuja kuuliza habari za mali za Wajerumani, na wanakwenda kuhangaika san, hakuna alierudi kwangu akanambia kama kafanikiwa au hajafanikiwa, lakini inasemekana zipo, wapi mimi sijui, Kwa sababu mmenipa jina ya hio sehemu, wacheni mimi ntauliza nipeni siku mbili tatu, nikipata jibu lolote nitawajulisha.

Basi wale mabwana wakakaa pale siku ya tatu akwaita. Akawaambia nisikilieni kwa umakini sana.

Hapa Tanga Wajerumani wamekaa sana na njia hio mlionambia kuna mtu hapa anfanya kazi serikalini, ni fundi mkubwa sana, huyu amerithi majini wakubwa sana wa ukoo wake, bipi nimejua hii habari msiniulize. Lakini mimi simjui huyo mtu. Nyie tafdoiteni wenyeji wakepelekeni ile sehemu ya serikali wanapotengeza mashine na magari yao, Muulize fundi mkubwa wa pale, mkimpata njooni nae hapa tuongee nae.

Wale wageni hawakupata tabu kuna baraza ya kahwa na hakua pale jirani waklikua wameshizoea na watu wanacheza bao. Wakauliza pale. Kuna mtu akawaambia kuna fundi pale nyumba ile wa hukohuko karakana, ngija tumtume mtoto akamuite kama yupo.

Basi akatumwa mtoto akaenda, kuuliza akaambiwa hajarudi lakini akirudi watampa salaa kua kuna wageni wao kwenye kahawa atakuja, basi akija kama hampo hapa tutawafata hapo kwa Sheikh.


Basi kufika jioni wanarudi kusali alasiri hawjakaa sana wakaja kuitwa wakedna kibaraza cha kahawa, wakampata yule mtu wakamuita pembeni wakamwabia wao wageni kuna mtu wanamtafuta lakinihamwajui jina isipokua ndio fundi mkubwa wa serikali. Yule mtu akawauliza mzungu huyo au mtu wa hapa tanga? maana pale mimi ndipo ninapofanya kazi, kuna Mzungu ndio Worksjop manager. Na kuna funid wetu mkubwa, mtu wa hapa hapa Tanga maarufu sana anaitwa Mabruki. Wakasema itakua huyo wa Tanga. Maana ingekua mzungu wangetuambiwa mzungu. Akawaambia kama ni huyto basi mmeshampata turudi tukanywe kahawa niwape mtoto awapeleke nyumnai kwake, hayupo mali yupo hapo usagrfam barabara ya saba mwisho kule.

Wakarudi kwenye kahawa, akwaambia wale waliokwenda kumwita , hawa wanamtafuta Mabruk sio mimi jamani. Watu wakasheka, walikua hawamjui jina wanaemtafuta, mbona wangeshafika zamani kwa Mabruki.

Wakapewa mtoto akawapeleka kwa babu yako. Wal wakamwabia unaitwa na Sheikh Mgunya katutuma tuje kukita. Huyu Sheikh Mgunya wa barabara ya tisa? Wakamwabia ndio yeye anakuhitaji kwa ajili yetu. Akawaabia haya, tangulieni nikisha sali magharibi nakiuja huko. Mwambieni ikisha magaharib tu mguu wake huu.

Wakaondoka, kweli baada ya kusali magharibi babu yako akaenda, w)alipofika Mzee wa Kigunya kawaambia haya muhadithieni na mwenyeji wa hapa. Mbruki akmwambia mzee Mgunya, wewe ushaoa wake wanne Tanga mimi nakuona wewe kuaniz mdogo hata huko ugunyani kwenu sijui kama unapajua tena, unasema mi mi mwenyeji. Wewre mwenyeji zaidi yangu bwana.

Mzee wa kigunya kawaambia wale wageni wampoishe kidogo aongee faragha na babu yako wakanywe kahawa akiwa tauayari wataenda kuitwa. Mzee Mgunya akamwabia kwanini alimwita yeye, alimwabia mimi nimeongea na majini wakubwa sana, wao wakanmbia wewe una jini mkubwa mwenye hiyo bakora ulioibeba, yeye mwenyeji wa mitaa hiyo walioitaja, si umeisikia bwana wametaja Amboni lkini sio mapangomi upande unaotazama mapango kwa bharini. Nikaambiwa wewe una wenyeji wa huko watatoa mwangza ndio kisa cha kukuita bwana Mabruki.

Babu yako aksema usemayo kweli lakini hio mali sijawahi kusikia, ningeisikia si ningeshakwenda kuichukua? Mzee mgunya akmwabia akmwabia kweli huijui, hata mimi siijui lakini uradi uliopo hapa, ni uwaulize hao wakubwa huko, tutapata fununiu. Babu yako akasema swa atawaita kwa muda wao wampe siku mbili tatu ataleta majibu.

Wakakubalina hivyo. Wakaitwa wlae mbawna waendelee kusubiri, ikwa yule bwana Mihamed hawei kusuniri tena, akrudimDar, yule kijana akasema miminitasubiri. Mzee Mgunya kamwabia wewe subiri na usiwe na shka ni mgeniwa y. Tuombe iwe heri tu. Tumsubiri Mabruki atupe jibi lake na yeye.


Itaendelea.
Simba.
 
inatokea post namba 227

Arsis: Babu yako aliporudi nyumbani akaita jini wa bakora, Akamueleza yote kama alivyoelezwa kwa Sheikh Mgunya na wale wageni.

Jini Bakora akmwambia babu yako ampe muda alifanyie kazi suala, mpka siku ya pili amuite atamueleza kafikia wapi. Siku ya poili babu yako akamuita. Jini bakora akafika akaanza kumweleza babu yako.

Jini Bakora; Mbaruki umefungua mambo makubwa sana, jana nimeenda mpaka Amboni, unajua pango letu ndio hilo hilo linakwenda mpaka mlango wa Amboni, hakuna jini kwenye hayo mapango aliyewahi kuona hiyo sehemu isipokua wapo waliosikia sikia tu. Hao waliosikia tu nao hawana uhakika ya walichosikia, kwa hio ni kama hadithi tu.

Jini Bakora; Kwa hio kabidi niende nikaongee na majini wa baharini, nahati nzuri tunaheshimiana nao sana. Nikaonana na mkubwa wao kabisa kwa upande huu wa mlango wa Ambini, akanambia habari hizo hata yeye amezisikia tu lakini hana uhakika nazo hakuna aliemuuliza kabla. Lakini huyu akanipa ushauri. Akanambia kuna kazi nzito inabidi ifanyike, kuna jini ana kitabu, lakini huyu Jini yupo dunia ya tatu, dunia ya tatu inabidi lango lake lifunguliwe ili huyo jini apate kutoa kitabu na kurudi. Inabidi mumpate jini au mtu mwenye uezo wa kwenda dunia ya tatu na kurudi na yule jini mwenye kitabu, na jini asie na nguvu akienda huko harudi tena huku. Na hakuna anaeweza kuja na hicho kitabu isipokua huyo jini mwenye hicho kitabu. Kwa hio Mabruk niwache niendelee na hii kazi, wacha niendelee kutafuta jini mwenye uwezo huo. wapo tutawapata, usiwe na shaka, lakini inabidi kazi kubwa ifanyike. Hivi vitabu vya majini vina kazi na hatari kubwa sana kwetu sisi majini. Mbaruk ukikipata hicho kitabu utawamiliki majini wa dunia nzima, sio mchezo.

Mbaruki: Sasa wewe fnya njia zako na mimi nafanya njia zangu, tukutane hapa baada ya siku tatu. Mimi nitakuita.


Mabruki siku ya pili, akenda kwa Mgunya akamueleza kilichopo, Mgunya nae akaahidi atafanyia kazi baada ya siku tatu wakutane. Ikawa kazi sasa ipo pande tatu, Jini Bakora na Majini wa Mgunya na Babu yako na vitabu vyake na majini wake wengine.

Siku ya tatu wakutana wote watatu, kila mmoja akaeleza alichokipata. Akaanza Mgunya akasema mimi nimepata jina la hicho kitabu kinachoongelewa, na zipo nuskha (kopi) lakini sio nzuri zimechezewa sana na watu waongo waongo. Kwa kifupi hakifai, mpaka kipatikane kwa huyo jini.

Jini Bakora; Hata mimi nimepata jina la hicho kitabu na nimepata ufumbuzi mwepesi kidogo. Kuna mtu amefungwa na majini hapa hapa duniani, huyu akitolewa kifungoni anaweza kwenda na kurudi kuleta hicho kitabu, kazi ya kumtoa kifungoni sio ndogo lakini inawezekana, na anaeweza kumtoa huyo ni binadam tu, sio Jini, kwa sababu majini wote wanaogopa, atakae mtoa huyo atauliwa. Mimi nimeweza kupata jini ataetuonesha kafungwa wapi na vipi tutamtoa inabidi apatikane binadam asie na uoga na anaejua kusoma Qur'an, Qur'an ndio kinga pekee itakayo mkinga na majini wanaomlinda huyo mtu aliefungwa, akipatikana ndio atumike. Haya Mabruki wewe umepata nini?

Mabruki: Mimi nilichokipata hakuna zaidi isipokua ahadi za kufanyiwa kazi tu. Kwa hio naendelea kusikiliza. lakini kama anatakiwa binadam aifanye hio kazi kama ulivyosema, nipo mimi nitaifanya.

Mgunya akasema shabash, mimi naahidi kuwapa ushirikiano wowote mtakao uhitaji kutoka kwangu tumpate huyo mtu.

Mabruki; Haya tunafanya baada ya hapa?

Jini Bakora:; Wacha nikaandae majeshi kwanza tupapate alipofungwa huyo mtu, halafu tujue namna kufika na kutoa kifungoni.

Mgunya: Tukijuwa kafungwa wapi, kama ni dunia hii, namna ya kufika niwachieni mimi, kuna elimu ya kupafika hata kuwe na ulinzi vipi wa majini, mradi isiwe dunia nyingine tu. Dunia yetu hii halafu jini aytushinde ujanja kwetu? Sisi ni viumbe bora kabisa. Mimi nasema tukutane kesho, wewe Bakora, kafanye uchunguzi wko, umeleta habari nzuri sana, na mimi nitafanya uchunguzi wangu, na wewe Mabruki usichooke, kesho njooni tukutane hapa. sasa tuna muelekeo.


Wakaondoka, ikabidi mgunya amueleze yule kijana wa Kipemba, kua haya mambo ni marefu inabidi aende gtu kwao, yakoiwiva atapelekewa habari aje.

Mpemba: Sasa nitapataje habari?
Mgunya; usiwe na shaka utapata tu habari, usofikiri kuna mtu ataifanya hio kazi akudhulumu, umetupa mtihani mkubwa sana. Mimi nakuonea huruma kuendelea kukaa hapa. Wewe nakushauri nenda tu.
Mpemba; Mimi nakwenda lakini baada ya mwezi kama sikusikia kitu nitarudi kuja kusikiliza.
Mgunya; Inshallah utapata habari kabla ya mwezi kwisha ili tukupunguzie gharama za nenda rudi, ukija hapa inatakiwa ujue iunakuja unaondoka na mali sio mikono mitupu.


Basi wakakubaliana Mpemba aondoke na wao wakutane siku ya pili yake.


Itaendelea.
 
inatokea post namba 227

Arsis: Babu yako aliporudi nyumbani akaita jini wa bakora, Akamueleza yote kama alivyoelezwa kwa Sheikh Mgunya na wale wageni.

Jini Bakora akmwambia babu yako ampe muda alifanyie kazi suala, mpka siku ya pili amuite atamueleza kafikia wapi. Siku ya poili babu yako akamuita. Jini bakora akafika akaanza kumweleza babu yako.

Jini Bakora; Mbaruki umefungua mambo makubwa sana, jana nimeenda mpaka Amboni, unajua pango letu ndio hilo hilo linakwenda mpaka mlango wa Amboni, hakuna jini kwenye hayo mapango aliyewahi kuona hiyo sehemu isipokua wapo waliosikia sikia tu. Hao waliosikia tu nao hawana uhakika ya walichosikia, kwa hio ni kama hadithi tu.

Jini Bakora; Kwa hio kabidi niende nikaongee na majini wa baharini, nahati nzuri tunaheshimiana nao sana. Nikaonana na mkubwa wao kabisa kwa upande huu wa mlango wa Ambini, akanambia habari hizo hata yeye amezisikia tu lakini hana uhakika nazo hakuna aliemuuliza kabla. Lakini huyu akanipa ushauri. Akanambia kuna kazi nzito inabidi ifanyike, kuna jini ana kitabu, lakini huyu Jini yupo dunia ya tatu, dunia ya tatu inabidi lango lake lifunguliwe ili huyo jini apate kutoa kitabu na kurudi. Inabidi mumpate jini au mtu mwenye uezo wa kwenda dunia ya tatu na kurudi na yule jini mwenye kitabu, na jini asie na nguvu akienda huko harudi tena huku. Na hakuna anaeweza kuja na hicho kitabu isipokua huyo jini mwenye hicho kitabu. Kwa hio Mabruk niwache niendelee na hii kazi, wacha niendelee kutafuta jini mwenye uwezo huo. wapo tutawapata, usiwe na shaka, lakini inabidi kazi kubwa ifanyike. Hivi vitabu vya majini vina kazi na hatari kubwa sana kwetu sisi majini. Mbaruk ukikipata hicho kitabu utawamiliki majini wa dunia nzima, sio mchezo.

Mbaruki: Sasa wewe fnya njia zako na mimi nafanya njia zangu, tukutane hapa baada ya siku tatu. Mimi nitakuita.


Mabruki siku ya pili, akenda kwa Mgunya akamueleza kilichopo, Mgunya nae akaahidi atafanyia kazi baada ya siku tatu wakutane. Ikawa kazi sasa ipo pande tatu, Jini Bakora na Majini wa Mgunya na Babu yako na vitabu vyake na majini wake wengine.

Siku ya tatu wakutana wote watatu, kila mmoja akaeleza alichokipata. Akaanza Mgunya akasema mimi nimepata jina la hicho kitabu kinachoongelewa, na zipo nuskha (kopi) lakini sio nzuri zimechezewa sana na watu waongo waongo. Kwa kifupi hakifai, mpaka kipatikane kwa huyo jini.

Jini Bakora; Hata mimi nimepata jina la hicho kitabu na nimepata ufumbuzi mwepesi kidogo. Kuna mtu amefungwa na majini hapa hapa duniani, huyu akitolewa kifungoni anaweza kwenda na kurudi kuleta hicho kitabu, kazi ya kumtoa kifungoni sio ndogo lakini inawezekana, na anaeweza kumtoa huyo ni binadam tu, sio Jini, kwa sababu majini wote wanaogopa, atakae mtoa huyo atauliwa. Mimi nimeweza kupata jini ataetuonesha kafungwa wapi na vipi tutamtoa inabidi apatikane binadam asie na uoga na anaejua kusoma Qur'an, Qur'an ndio kinga pekee itakayo mkinga na majini wanaomlinda huyo mtu aliefungwa, akipatikana ndio atumike. Haya Mabruki wewe umepata nini?

Mabruki: Mimi nilichokipata hakuna zaidi isipokua ahadi za kufanyiwa kazi tu. Kwa hio naendelea kusikiliza. lakini kama anatakiwa binadam aifanye hio kazi kama ulivyosema, nipo mimi nitaifanya.

Mgunya akasema shabash, mimi naahidi kuwapa ushirikiano wowote mtakao uhitaji kutoka kwangu tumpate huyo mtu.

Mabruki; Haya tunafanya baada ya hapa?

Jini Bakora:; Wacha nikaandae majeshi kwanza tupapate alipofungwa huyo mtu, halafu tujue namna kufika na kutoa kifungoni.

Mgunya: Tukijuwa kafungwa wapi, kama ni dunia hii, namna ya kufika niwachieni mimi, kuna elimu ya kupafika hata kuwe na ulinzi vipi wa majini, mradi isiwe dunia nyingine tu. Dunia yetu hii halafu jini aytushinde ujanja kwetu? Sisi ni viumbe bora kabisa. Mimi nasema tukutane kesho, wewe Bakora, kafanye uchunguzi wko, umeleta habari nzuri sana, na mimi nitafanya uchunguzi wangu, na wewe Mabruki usichooke, kesho njooni tukutane hapa. sasa tuna muelekeo.


Wakaondoka, ikabidi mgunya amueleze yule kijana wa Kipemba, kua haya mambo ni marefu inabidi aende gtu kwao, yakoiwiva atapelekewa habari aje.

Mpemba: Sasa nitapataje habari?
Mgunya: usiwe na shaka utapata tu habari, usofikiri kuna mtu ataifanya hio kazi akudhulumu, umetupa mtihani mkubwa sana. Mimi nakuonea huruma kuendelea kukaa hapa. Wewe nakushauri neda tu.
Mpemba; Mimi nakenda lakini baada ya mwezi kama sikusikia kitu nitarudi kuja kusikiliza.
Mgunya" Inshallah utapata habari kabla hya mwezi kwisha ili tukupunguzie gharama za nenda rudi, ukija hapa inatakiwa ujue iunakuja unaondoka na mali sio mikono mitupu.


Basi wakaubaliana Mpemba aondoke na wao wakutane siku ya pili yake.


Itaendelea.
Upo vizuri kaka,...
 
mkuu Corazon Espinado,tunajua majini wana elimu kubwa sana mfano hao wako kina Arsis wala hupati tabu kujua shida za watu yaani mgonjwa hana haja ya kujieleza nini kinamsibu wao majini wanajua kila kitu na kipi wafanye kumaliza tatizo,sasa ww umesema hufanyi hizo ishu za uganga wala hutaki sasa watu wakija kwako hasa baada ya kuona hu uzi wanasaidika vp? je,unaweza kumuomba Arsis amchunguze fulani ajue matatizo yanayomsibu na ipi tiba yake kwa atakayo yaona kwa huyo mtu. si umesema nae yupo Jf anasoma uzi huu
 
Nimefurahi sana kwa hilo swali lako, hilo amenielezea zamani sana. Ni kisa kirefu kidogo,

Kwanza alikua ananielezea kuhusu dunia, kwanza yeye anakataa kua dunia haipo duara kama tunavyoaminishwa na sayansi. Pili anasema hiz nyita wanasema ni kubwa ni waongo wana sayansi, hizo nyota anasema ni kama ilivyosemwa kwenye Qur'an ni mapambo kwa hii dunia. Pia anasema hakuna nyoita inayozidi tani kumi ukubwa wake, wanasayansi ni waongo. Na vimondo ndio hizo nyota. Ka ufupi sana jibu ndio hilo, mbele huko kisa kikifika sehemu hiyo nilipouliza utakisikia kwa kina.

Majibu ya Arsis yanaweza kukuachia maswali mengi sana. Ni vizuri kua hilo alinijibu zamani.
Kweli nina maswali mengi sana,,lkn ngoja tuendelee kupata story zaidi
 
Kikapu kikajaa kamba............

Hii stori kamba wametajwa kuliko kitu kingine chochote
WE tulia tuendelee kula kamba
Typos zimekuwa nyingi mpaka inakuwa vigumu kusoma kwanini usipitie spelling errors na kuzirekebisha watu wengi sio waandishi wazuri lakini hawaandiki kwa kutojali kama wewe inaonekana una haraka mno ya kuandika
KIkubwa tu Arsis haja mind, bas hakuna shida
 
Inatokea post namba 197.

Safatri yetu ya kuelekea DOM ikawa nzuri sana haina pirika wala vituko Dereva akawa anaendelea kunipoiga story tu.

Dareva: Waarabu wa Morogoro wana pesa bwana, ule mzigo wao, Halima kanilipa na wao wamenilipa, tena nimewaambia nimeshapewa nauli ya huu mzigo na Halima, wakanambia hiyo sio nauli, hizo zako, Kafurahi na wewe. Wakanambia siku wakiambiawa mimi ndio naleyta mzigo wanafurahi, maredereva wengine wanawakata mirungi yao wanaenda kuuza juu kwa juu ghiyo.
Mimi; Mbona wewe unakula?
Dereva; Mimi yangu ananipa Halima, tena toka Sofi yupo pale ndio alizowesha, mimi nilikua sili mirungi mshikaji, Sofi kila nikienda ananipa, sema nashukuru siili hii mpaka nbipewe pale, sijawahi kununua wala kuwachomolea mirungi yao Waarabu. Mie nimelelewa kwetu mshikaji. Siijui jaa mimi, kwetu masikini lakini hatukosa riziki, tunakula wali na mboiga nne mshikaji wangu.
Nikawa nacheka jinsi anavyoongea.

Dereva: Mshikaji wewe kama mimi hupendi kula kula njiani, mimi bwana nyama nyama sijui kuku, sijui nani kachinja, sili kabisa, tutalishwa vibudu njiani, Humu. Hivi hapa kula yangu mimi Dodoma, kwa Sharifu, uhindini au wiumpy, na yeye sharifu vile vile, Kule tena nikimkuta habiba Jamal pale wimpy silipi kitu, Mwenye ananiita sheikh wake. Unajua mwenye wimpy Dodoma?
Mimi; Hapana sikjui, mimi nimeahi kupita tu Dodoma, sijuani na watu.
Dereva: basi leo nitakupeleka ukamjue Al Habiba Jamal wa wimpy. Mimi nilijuana nae kuna siku walikua wanagawa sadaka, wakaja chuoni kwetu nyumbani, nikawapiga dua, pale hajanisahau toka siku hiyo. Ananniita Sheikh wangu. Tena unaweza kuwajua wewe, wanasema alikua na wimpy Dar wakaiuza.
Mimi; Labda mzee wangu atawajua, mi isiwafahamu.
Drereva; Usijali mshikaji, mradi upo na mimi utawajua watu wa maana nia hii, wananijua mimi kama shilingi.

Nikawa nacheka tu uongeaji wake, haikupita muda tukafika Gairo, akanambia hapa mshikaji hatuingii mjini huko, tutasimama pembeni hapo kuna kituo cha mafuta na kuna shehemu ya chai nzuri tu, ukitaka kula pia, hakuna wasiwasi.
Mimi; Mimintamenya nanasi na machungwa nile, sijisikii kula sasa hivi.
Dereva: Mwili ra tizi huo, kula mshikaji usione haya.

Akapaki vizuri kituo cha mafuta, kunajamaa pale akamwabia, wewe kila ukija hapa nakwambia paki kule pambeni unajifabya huelewi sio?
Dereva; Nashau mshikaji wangu, mhapa najiona nimefika nyumbani, nipo huru.

Yule jamaa akamwabia, hapo nakwambia kwa usalama, wako wagtakukwangua, madereva wengine walevi.
Dereva: kwli mwanagu wacha niiweke pembeni.

Akaiweka pembeni akafungua buti nyuma akanambia lete hayo machungwa kama kumi hivi watatumenyea hapa, leta na manasi mawaili, moja lako moja langu. Mshikaji usiwe na wasi wasi na wasiwasi tutakula martinda tu leo kama timbiri, sem mananasi na machungwa tutakojoa sana njiani.
Mimi:; Nimeona msikiti pale, wacha nikapige safar kidogo nakiuja, sasa hivi sichelewi.
Dreva' Nenda mshikaji wangu dua kwa wingi tu usiwe na wasi wasi. dua muhimu sana. Mimi nikishaunganisha zangu, ningekuja na wewe. Utakuta hapo kwenye kiduka hicho, kun mrfembo humo ndani, halafu naambiwa kawachwa na mumewe.


Mimi nikaondoka, nikajua huyu hanyamazi sasa hivi. Nikasali nikarudi nikaingia kwenye kimgahawa, dah kweli, nikamkuta mwanamke mzuri kweli sio mchezo. Mshikaji wangu sikumuona.

Yule mwanamke akaniuliza wewe ndio umekuja jna yue dereva wa IT?
Mimi; Ndio sister

Alikua anaonesha ana umri mkubwa kwangu lakini bado ni kijana. mafa mshikaji akaja, bumetoka mumenya vitu, pale, hawa wakaguru hapa hawajui kumenya machungwa wala mananasi.

Dada: Kw akujidai huyu, wewe uje na machngwa yako nani akumenyee? Unaleta ujanaja wa mitaani hapa?
Dereva: Usisemee mbovu, ningepajua kwenu ningeshapelka posa. mtoto mzuri kama wewe unaka poarini huku? Ningekuweka mjini wewe.
Dada; Nipishe huko, nani alikwambia ana shida ya kuolewa? Una maneno ya kijinhga jinga.
Dereva: basi poa, nimekuletea zawadi, ngoja nikuletee.

Akatoka akaenda kwenye gari akarudi na nanasi moja kubwa na machungwa kwenye bakuli kubwa tu.
Dada; Nilifikiri utalisahau bakuli langu.
Dereva; Sina akili ya kusahau mimi. Ukila nanasi tu hilo, nimelisomea hilo, ujue hunikatai tena.
Dada: tna ndio nalila kwanza hilo, hariufu yake tu linaonesha limewiva, sasa weewe unajida zawadi kumbe kinanasi kimpoja tu?
Dereva; Mwanangu, hiku kanielekea mimi, hakuna mwanamke mwenye shukurani duniani isipokua mama yako mzazi tu. Si unamuona huyu mwanamke, mimi nimemuwazia zawadi, nilikua sina sababu ya kusimama hapa zaidi ya kukuletea wewe zawadi, halafu unaiponda zawadi yangu. Na siku ingine.
Dada: Kwani leo hukusimama kwa ajili ya kusali?
Dereva: Mimi nimeshaunganisha sala ya safari, unajua sala ya safari wewe? Nimesimama kwa ajili yako tu.
Dada; Haya ahsante, Mungu akuzidishie.
Dereva; Hayo ndio maneno, twende zetu mshikaji wangu, anaweza kunizuwia huyu nisiondoke hapa, anajidai tu.
Dada; Nipishe huko, nani akuzuwie wewe. Tena usimfundishe huyo kijna, mwenyewe anaonesha mpole.
Dereva: Mpole? Simba mwenda kimya huyo. Au nimwache yeye mimi nitangulie?
dda: Huyu, mwache ahamie hapahapa patapendeza hapa, sio wewe. Haya kwaherini.

Aaingia ndani. na sisi tukaondoka zetu.
Dereva: mwanangu lazima ujue nituo vyua njiani, sio unajisimamia hovyo tu. Usione tabu mwanangu, umenabia wewe fundi, unaweza kufata migari mibovu huku ujue wapi pa kula, wapi pa kupumzika. Hapa kuna wajjaguru, wachawi kama nini.

Tukaendelea na safari pka nje nje ya Dodoma akanambia mshikaji kuna mawili, au tutafute sehemu gtulale hapa Dom au tutembee mpaka Singda, unasemaje?
Mimi; Mimi vyoivyote vile niko poa tu.
Dereva; usijali mwanangu, tulale hapa, alfajiri tuondoke haina haja ya kukimbizana barabra usiku.


Tukaenda moja kwa moja mpaka ki gesti kimoja kipo mjini kabisa, gari inaingia mpaka ndani, akiweka gari akanambia mshikaji, Sasa kama kukoga kutawadha, tukutane hapa nje kama nusu saa hivi twenda kwa wimpy tulkle mapema, halafu tuke kupumzika mapema, alfajiri sana tukijaaliwa tuondoke. Tutasali kwa Gadafi. Kuna msikiti mkubwa mbele hapo unaitwa kwa Gadafi.

Akaingia chumbani kwake na mimi nikaingia chumbani kwangu, ilikua ndio mara ya kwanza kulala gesti namna ile. Kilikua k9i gesti fukani kidogo lakini ksafi. Nikakoga kuna choo ndani, nikagtoika nje. Baada ya muda akaja, tukaondoka tukaenda wimpy, bahati akamkuta rafiki yake anaitwa Jamali, tukaulizana pale, tukala, Jamali akakataa kabisa kupokea pesa, akasema nyie wageni wangu, Huyu Sheikh wangu. Mtakuepo Dodoma?

Dereva: hapana mjomb Jamal. sisi tuombee dua sharofu, alfajiri ytunachoma.
Jamal: Woi safari hii?
Dereva" Mimi kule kule Burundi, huyu mshikaji anaishia Shinyanga.
Jamal": Kuna kaka yangu pale Shinyanga, chukua namba zake, nhgoja nikuandikie, ukiwa na mwenyeji ni vizuri zzaidi. Jamal alikua namwili wa unene na mtu mzima makamo ya mzee wangu akanipa namba, SAkasema mimi nitamoigia na wewe ukifika usiache kwenda kumuona, au mwenyeji wewe Shinyanga. Nikamwambia hapana, mimi nafata gari tu limeharibika huko.
Jamal; Wrewe fundi au unapeka spea, unaonesha bado kijana mdogo sana?
Mimi: Mimi fundi, tuna gereji kwetu, nimekulia gereji.
Jamal; Basi uone kaka yangu anaitwa Ali, maarufu sana Shinyanga.

Mimi; sawa nitampigia nikifika.
Jamali: Mwambie hata huyu mwezako akupeleke kama hana haraka, anapajua nishampa mizigi ya Ali matra nyingi ampelekee.
Dereva; Nitamuonesha Sharifu, siwezi kukuvunja hata siku moja kijukuu cha mtume.

Tukala pale tiukaondoka, tukatembea mwendo kido mpaka kwa gadafi tukakuta wamesha sali isha, sisi tikasali, tukaunganisha jamaa na wengine waliochelewa kama sisi. Tukarudo hoiteli


Ikawa mimi nimekosa usingizi na sijachoka nikatoka nje, niliona shemu kama garden hivi wakat tunaenda na kurudi msikitini, nikaenda pale, kinyaa hakuna mtu kabisa, nikasema ngoja nimwite Arssis. Nikamwita kimya kimya akaja kweli, nikaanz akusikia sauti.

Asis; Vipi hali yako?
Mimi: Salama, sikutegemea kama utakuja.
Arsis; Hakuna neno, sehemu nzuri hii umechagua sema washenzi wanakojoa kojoa hovyo hapa. nenfda pale ulipfikia nje kuna baraza zuri, tutaonea pale. Najua una maswali. Titaonana baadae kidogo.

Nikaondoka pale, kweli nikaanz akusikia harufu ya mikojo, nikarudi hoteli, nikakaa nje pembeni kibarazani, kumwita tu Arsis akaja.

Arsis; Vipi hali? Unaona hapa pazuri, unasemajje?
Mimi: Arsis; leo nilikua naongea na yule jini mwanamke, mboina yeye anakubali ni jini, wewe unasema sio jini?
Arsis: Mimi nimekwambia naweza kua chochoite kile, naweza kua mtu, naweza kua jini, naweza kua mti. Wewe hilo usijali, amini ninachokwambia.
Mimi; Sijui nianzie wapi?
Arsis: Anza popte tu usiwe na wasiwasi.

Mimi; Yule jini wa kike kasema yeye yuko na mimi ananifundisha, ananifundisha nini? Nani kampa hio kazi ya kunifundusha?
Arsis: Mimi nimempa kazi, kuna mengu sana hayajui. Anayoweza yeye atakujulisha asioweza mimi nitakufundisha.
Mimi; Kwanini mimi?
Arsis: haya mambo yanakua kiukoo, ni viapo vua ukoo kabla ya babu yako kuzliwa sisi tuko kwenye ukoo wenu.
Mimi: Unasema sisi, una maana mko wengi?
Arsis: Hapana, mimi niko peke yangu, yule jini wa kike na mamake, ndio wanafanya kazi kwangu, wapo chini ya himaya yangu. Babu yako sijawahi kufanya nae kazi, zema namfahamu sana nimemsaidia mara nyingi. Yeye ruhani wake aliekurithisha ni yule mwenye ile bakora. Mimi ni mkuwaba wao, eote wapo kwenye himaya yangu, kwa hio hawawezi kupinga na mimi. Mi i nasaidia tu mpaka ulipokabidhiwa wewe kwa yule mwenye bakra nikaona ujuzi ulionao usipotee bure, tulikua tunatafuta binadam siku nyingi wa kumfundisha tunayojua. Wewe ndio nimekuchagua nikufundishe.
Mimi; Mbina unasema "sisi" kama mpo wengi halafu unasema uko peke yako, unanishanganya.
Atrsis: Usichanganyikiwe, wotew wanaofanya kazi chini yangu ina maana ni sisi. Mimi kiukoo nipo peke yangu ni tofauti kabisa na jini wa bakora na hawa majini wa kike, Wao wana ukoo wao mkubwa. Bado wewe pia unakoo mwengine, huo sana upande wa mama yako, ukoo wa simba. Lakini na babu yako yupo ukoo huo, sema yeye hapendi mamboi ya uasherati yeye ameshika dini, alifanya mcheo kidogo akafanya toba yeye sasa akita anaoa tu. Unajua babu yako kishaoa, wake wangapi mpaka sasa?
Mimi: Sijamuuiza lakini zee kanambia wengi tu.
Arsis" Mkionana muulize, wengi kwacha lakini kabaaki na wawili unawaju wewe na mmoja humjui.
Mimi; Kwa hio babu sasa anawake wa tatu?
Arsis: ndio, mullize mwenyewe atakwambia.
Mimi; Hii poete ya nini> N yule mwanamke naona inafanana na hii laikini yeye kiti cha duara.

ARSIS: hiyti pete ni zawadi yako, ni ya kwangu mimi, ipo moja tu dunaiani. Kwa ajili ya mawasiliano tu mimi na wewe. na walw wanawake ni mawasiano tulakini vyao ni vito nadhahabu yawaida tuliwatengeneza alipoana kufanyua kazi na mimi, sio siku nyingi sana, walikiua wanafanya kazi na yiule mwenye bakora, sasa kanipa mimi wanisaidie kwa ajili yako. basi hakuna zaidi.
Mimi: nyinyi ni wachawi?
Arsis: Hapana mimi sio mchwawi kabisa, na wale wanawake yule mama yake zamani alikua mchawi miubwa sana, sasa hana yena uchawi, amefanya toba na sasa nimwema kabisa, akiwa mchawi watamuua wenzake. Na huyu mwanae anaekuja sana kwako, hajawahi kua mchawi, sema anajua mambo mebgi ya kichawim kwa sababu anpiugana sana na wachawi katika kazi zake. Anjua mengi yule, usione anaongea na wewe kiupole nihatari sana ytule kwa wachawi, ana jeshi kunbwa sana wanamuogopa yule. Yule anakufundisha na anakulinda. Mradi wewe unaoete hiyo, wewe ndio boss wake sasa.
Mimi: Sasa wewe nani hasa?
Arsis; Mimi nimwalimu tu ninaekufundusha vile utaweza. Hatuwezi kukufunsisha mabaya wala sina mabaya. Wewe hukukabidhwa kwangu, mimi nimekuja kwako mwenyewe. Baada ya kukuchunguza sana, yule jini wa nakora ndio jini umekabidhiwa, miubwa sana yule, usione vile.
Mimi: Naona kwa leo inatosha, maana inabidi niamke alfajiri sna, tunaondoka.
Arsis: Sawa, sema Inshaallah.
Mimi; In shaa Allah. Haya kwaheti Arsis.

Arsis; Kwaheri, siku nyingine mitakundisha kitu leo nenda kapumzike.


Nikaingia zangu kulala.

Itaendelea.
Ulivyotaja whimpy na Jamal nimeamini.
 
Ulivyotaja whimpy na Jamal nimeamini.
Ulifikiri ni "kamba"? Hiki ni kisa cha kweli kadiri ya uwezo wangu wa kukumbuka, sana sana kuna vionjo tu, kwa sababu siwezi kukumbuka kila neno au kila kitu. Isipokua, kuanzia kisa cha Mahojiano yangu na SArsis, yote yana kumbukumbu za kurekodi. Nilianza kurekodi kabla ya hizi smart phones, nilianza kwa kurekodi na tape ndogo ya mkononi, kwa muda mchache sana, nikapata "digital recorder" ndogo sana ya mkononi, hio nilikaa nayo muda kiasi mpaka zilipoingia simu za kuweza kurekodi, ndio mpaka sasa.

Kama unamfahamu Sharifu Jamal, muulize kama ana kaka yake na yupo kama nilivyoelezea. Upate uhakika zaidi.
 
maeneo yote ya kweli.wimpy hapo nimekula sana ice cream.we jamaa mwarabu mwarabu nin? usagara huko kote napajua. leo nimesjindwa kula mjini.kila mtu namuona yupo uchi. tena mama mmoja mtu mzima kaniangalia sana nikawa namkazia macho
Kula, kwa jina la Mwenyezi Mungu, hautopata madhara ya kula visivyofaa.
Simba.
 
Back
Top Bottom