Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Kuna wengi sana wanauliza maswali private, nahisi maswali hayo wangeuliza hapa yangewasaidia wengi, na yale ambayo mimi sina uwezo wa kuyajibu kuna wanaoelewa zaidi yangu watajibu. Huu ni uzi wa wazi.

Yale maswali ya private uliza kwa ID usiojulikana, lakini kuna mengine yapo general, yatasaidia wengi kupata majibu na wengi kuweza kufunguka kuuliza zaidi.
 
Sasa mbona uzi wako umejaa vitu tofauti la lengo la uzi wenyewe.
Mfano ishu ya safari yako na maongezi na huyo dereva, maongezi na mama muuza vitumbuaa..

Aloo Arsisi kama nae anafatilia huu uzi basi akwambie upunguze unnecessary stories.
 
Inatokea post namba 184;

basi tulipotoka Mdaula, dereva akawa anaongea huyo, kumbe mwenzangu alikua anakula mirungi kiaina nilikua sijamstukia mwanzo. Nilipomstukia nikawa namjibu kwa kumchokea asinyamaze nilikua na enjoy sana. Jamaa yupo fiti kweli kusafiri nae. Tukaenda vizuri mpaka kukaribia Morogoro aknambia, mshikaji, tutasimama pale Msamvu, hawa warabu wenye mzigo wao wanakuja wenyewe kuuchukuwa. Nikamwambia poa.

Basi kufika Msamvu hakuingia stendi ndani, kuna hoteli moja ipo nje inaonesha ya zamani, akanambia hapo poa, utapata kahawa ile ya kopo ya kukorogea kwenye maji ya moto, sio kama ya kwa Sofi. Mimi nakuacha hapo nazunguka nyuma hapo kidpog niwape mzigo wao. Akaniwacha akaondoka.

Aliponiwacha pale kweli pametulizana sana, kidogo akaja mhudumu, nikamwabia kahawa. Akanambia nipe dakika kama kumi hivi inabidi nikuchewmshie maji ya moto. Nikamwabia poa, akaondoka. Ile anaondoka tu, niaksikia naitwa "bwana mkiubwa", kutazama namuona yule jini wa kike, akaja kukaa namimi.
Jini 1: Sikiliza, nakushauri, siku zingine ukija sehemu kama hizi au ukiingia masokoni na madukani, kula ule mti uliopeqwa ili usionekane. Lakini mwenzako asikuome ukiula. atakuona mchawi.

Nikacheka. Nikamuuliza;
Mimi; Umekuja na nini?
Jini w: usijali, sisi tunapanda usafiri wowote ule hatuonekani na tusiotaka watuone.
Mimi; Kwa hiyo hapa unaonekana au huonekani?
Jini 1; Hapa sionekani na hakuna anaesikia kama tunaongea. Uasiwe na shaka. Mie kazi yangu nisicheze mbali na wewe mpaka utakapokomaa, kuna vitu vingi inabidi nikukumbushe mpaka uvizowee.
Mimi; Naweza kukuuliza maswali?
Jini 1; Niulize lakini mimi sijui mengi, kama una maswali muulize Arsis. Mimi akiwepo yule siwezi kuwepo, ni mkubwa sana yule.
Mimi; Mbona unapete yake?
Jini 1; Muulize yeye atakujibu, hilo siwezi kujibu. Wewe badala ya kuniuliza mambo yanayonihusu mimi, mgfano wale watu nilionesha pale ulipopanda gari. Umeshwajua?
Mimi; Nikamwabia sijawaju, lakini hilo nilikua nasema nitamuuliza Arsis.
Jini 1; Hilo naweza kukuuliza, si mimi ndio nilikuonesha? Umesahau?
Mimi; Haya nieleze.
Jini 1: Walw ukisiki misukule, wale wote ni misukule yule mwanamke mnwenye ile bar, mchawi sana, anawanunua wale waje kujiuza pale na kuvuta wateja. Hawajijui masikini ya Mungu.
Mimi; Anawanunua? Sijaelewa hapo.
Jini 1: Yule aliingizwa chama cha wachawi kwa tamaa ya utajiri. Kuna hao wakubwa zao kabisa wa hicho chama wanawauza au wanawakodisha hao misukule, mbona wapo wenhgi sana. Hujawatazama tu.
Mimi; Dah, watu hawawaoni?
Jini 1: wagtawaonaje na wanavaa nywele za kubandika na wanafanyiwa kiini macho, wasio na macho hawawaoni kaboisa. Wanaowaona wachawi wengine, lakini ka ujuavyo mchawi hatoi siri ya mchawi mwengine.
Mimi; Kwa hio na wewe ni mhawi unyaona yote hayo?
Jini w: hapana, mimi jini, wale wanatumia majini ya kichawi, mimi kazi yangu kupambana na wachawi, sipamnai na binadamu, napambana na majini wenzangu wa kichawi. Wewe unaniona mimi tu, tuna jeshi kubwa sana la kupigana maovu. Kwa sasa nipo na kazi maalum ya kukufundisha wewe haya mambo, ukitaka kujua zaidi muulize Arsis.
Jini: kahawa yako inakuja, subiri akisha kuletea kahawa tutaendelea kuongea zaidi.

Tukawa tumekaa tu hatuongei, nikawa namtazama lakini sura yake siioni vizuri, sema ana mwili mzuri, ingawa yupo ndani ya nguo, lakini anaonesha yupo poa sana, na jinasi anavyoongea kiutaratibu nikawa nawaza mengi. Mara kahawa ikaletwa, nikaletewa chupa ya maji na vikombe viwili.
Mhudu: Karibu kaka, uko peke yako? Nilionakama ulikua umekaa na mtu nilipokua kule jikoni. Nikajua mpo waewili.
Mimi; katoka kidogo, atarudi sasa hivi.
Mhudumu; Jichunge na wanawake wa msamvu, misukule wengi hapa.
Mimi ; Nikashangaa, yule jini akawa anacheka.

Mhudumu alipoondoka yule jini aksema...
Jini 1; Si umesxikia mambp hayo? Misukule wengi.
Mimi; Mbona anasema aliona kuna mtu amekaa, na wewe umesema huonekani?
Jini 1: kwanza nilikuja kwa kuonekana, nikaona niytakuzibia mengi, angenina tena hapa, unafikiri angekwambia habari ya misukule?
Mimi; Kweli.
Jini 1: sasa hivi ananiona hata akija mtu yoyogte wananiona, sema wenye macho yao watajua mimi jini, watakuogopa na wewe watajua ni mchawi.
Mimi; Wewe sio mchawi?

Jini 1: hapana mimi sio mchawi, nikijiingiza kwenye uchawi nyauliwa siku hiyo hiyo. Muulize hayo maswali Arsis atakuelekeza voizuri, imi sifahamu mengi. Mimi nippo kwa ajili hyako kwenye hii safari, tutakwenda wote tutarudi wote, akiwepo Arsis mimi sikai. Ndicho ninachojua hicho kwa sasa.
Mimi: Kwa hio upo na sisi muda wite?
Jini 1: hapana, mimi so mbea. Nakuja na kuondoka. usiwe na shaka.
Mimi; Kwanini ukanipa yule mwanamke polisi anitafutue gari?
Jini 1: Si nilikwambia, yuleekua rahisi kwangu kwa kua nimeongea na jini lake la kichawi, likaniogopa sana, likasema halitaki vita na sisi, atafanya tunachotaka. Likanambai mwambie tu hawezi kukukatalia. Ndio nikaongea nae.
Mimi: Mbona huyu dereva anamlalamikia sana?
Jini 1; Wewe hujui kwanini wanafanya kazi? Si wanafanya kazi za haranu wanajifanya za halali? Hayo mengine muuliza Arsis, mimi nikitumwa nimshughulikie atakoma ubishi, kwanza sijampenda kabisa maringo yake, anajiona yeye ndio yeye. Bahati alitulizwa na yule shjetani wake, angekoma ubishi. Ningemlaza hospitali, sina utani na watu wachafu mimi. YTena ole wako ujaribu kutenbea na mtu kama yule. Kama ukoo wa babu yako wote haukua kinyume na wewe. Babu yako ni mtu mwema sana, usimuharibie kabisa jina lake na la ukoo wenu. Kwaheri bwana tutaonana baadae.

Kabla sijamsehesemesha kaamka huuo akawa anakwenda zake, anaelkea stendi ya msamvu, ni pale pale jitrani tu, nara kidogidereva akarudi na yule bitimhudumu akaja. kumbe alikua anatuona alipokaa.

Dereva: Vipi mshikaji, ngoja na mimi ninywe kahawa tuondoke, safari ni ndefu.
Mhudumu; Kumbe upo na huyu mwanga, ngoja nikeletee kikombe.
Mimi; Kikombe si hiki hapa.
Mhudumu; Kumbe yule dada hajakitumia?
Mimi; Hajakitumia, hatumii kahawa yule.
Dereva: Mshikaji wangu ushaopoa hapahapa?Angalia hii baravra wezi wengi, Tena ukiwa na gari asikuombe mtu lifti au akijidai abiria mwanamke ukampakia. Tena wale wazuri ndio hatari kabisa.
Mimi: Kwanini, majambazi kaka, muulzie huyu binti akwambie visa vya hii barabara, ni vingi nno.
Mimi: Mbona mimi umenipakia?
Dereva; Unafikiri bila kupewa na yule askari ningekupakia? Sipakii mtu nisiemjua kabisa. Mzigowangu wa niani unanitisha kabisa, sipakii mtu kabisa. Hat huyu dada nimeshamkatalia abiria wake.
Mhudumu; Kweli kaka inabidi ujichunge sana.

Tukanywa kahawa pale tukaondoka. Akanambia mjomba mimi nishakula mafuta full tank, hii mjomba Mungu akiyujaalia kituo cha kwanza Dom.
Mimi; Poa kaka.


Tukaondoka.


Itaendelea.
ini
Patamu hapo
 
Kuna wengi sana wanauliza maswali private, Nahisi maswali hayo wangeuliza hapa yangewasaidia wengi, na yale amabyo mimi sina uwezo wa kuyajibu kuna wanayoyaelewa watajibu. Huu ni zui wa wazi.

Yale maswali ya private uliza private lakini kuna mengine yapo general, yatasaidia wengi kupata majibu na wengi kuweza kufunguka kuuliza zaidi.
Najua watu wengine wako na aibu sana,,fanya hivi,likiulizwa swali ambalo unaona linafaida kwa wengi,lilete humu toa majibu huku ukimficha muuliza swali
 
Sasa mbona uzi wako umejaa vitu tofauti la lengo la uzi wenyewe.
Mfano ishu ya safari yako na maongezi na huyo dereva, maongezi na mama muuza vitumbuaa..

Aloo Arsisi kama nae anafatilia huu uzi basi akwambie upunguze unnecessary stories.
Matukio muhimu sana hayo, utakuja kuekewa umuhimu wake baadae kidogo Usiwe na haraka.

Tena matukio ya upande wa ki simba nimeyaminya kwa makusudi kabisa. Hayo yawkuwepo kwenye ule uzi wa koo za simba.
 
Sasa mbona uzi wako umejaa vitu tofauti la lengo la uzi wenyewe.
Mfano ishu ya safari yako na maongezi na huyo dereva, maongezi na mama muuza vitumbuaa..

Aloo Arsisi kama nae anafatilia huu uzi basi akwambie upunguze unnecessary stories.
Tambua arsis anakusoma kwahiyo kuwa mpole,,naona tusimpe presha sana mtoa mada ingawa tunamshauri kama sehemu haina haja sana ya maelezo ambayo hayahusiani na tunayotaka kujua ayapotezee..

Au arsis unasemaje,,nasikia unasoma mada!!!
 
Tambua arsis anakusoma kwahiyo kuwa mpole,,naona tusimpe presha sana mtoa mada ingawa tunamshauri kama sehemu haina haja sana ya maelezo ambayo hayahusiani na tunayotaka kujua ayapotezee..

Au arsis unasemaje,,nasikia unasoma mada!!!
Arsis haiingilii mada, ispookua anasema "sio mwandishi mzuri, jitahidi kusoma namna ya uandishi".
 
Niulizie swala moja kwa huyo mwamba arsis,kwa mujibu wa quran,majini zamani walikuwa wanatabia ya kwenda mbinguni na kusikiliza mazungumzo ya huko,lkn baadae wakaja kupigwa na vimondo ili wasiende kusikiliza hizo habari za siri

Naamini maneno ya Allah ni kweli,nina hamu ya kusikia toka kwa huyo arsis anasemaje
 
Inatokea post namba 200.

Nikalala fofofo, sikumbuki hata kama niliota. Kabla ya alfajiri mshikaji dereva kanigongea mlango, akanambia twende mwanangu, usijali mimi nililipia vyumba, hata chako nimekilipia, mimi ndio nimekuchelewesha.

Nikajimwagia faster. Maji ya moto, safi kabisa kwenye shower. Tukatoka mpaka kwa Gadafi ile tunafika ndio wanakimu sala, Tukasali pale tukaondoka, nikaona hatujachelewa sana, mapema tupo Manyoni, tukapita faster tu. Dereva leo alikua haongei sana.

Dereva; Mshikaji tutapiga chai Singida.
Mimi; poa.


Dereva; Saa hizi tunaambaa vizuri, mapema tu Singida, leo mshikaji Inshallah mimi nalala Buja.

Mimi; In sha Allah.

Hayukupita muda sana tukawa tupo Singida, imetuchukua kama masaa mawili na nusu hivi. Akaiingiza gari mitaa ya mjini. Kaacha njia kuu akaingia kulia, ndio kuendea katikati ya mji wa Singida.

Dereva: Twende mwanangu, kuna kihoteli kina chakula kizuri sana, kama cha nyumbani. Kufika akanambia hapa ndio ukisikia "utemini", kuna wanawake wazuri hapa kuliko Dubai.

Tukashuka, mimi nikanywa maziwa kwanza, halafu kulikua na mzee nje ya hoteli ameweka mapande ya steki ya ng'ombe anaoka kwenye oven la kienyeji, inatamanisha.

Nikamwambia nikatie nyama, akasema bado kidogo. lakini subiri nikutazamie.

Mwenzangu alikua kishaagiza chai, sambusa na mandazi anapiga, Mimi nikapiga ile nyama ya kuoka na maziwa Nilippomaliza nikawahi kulipa bill yote ili mshikaji asinione mtu wa mserereko. Tukaondoka pale mapema tu, mchana mchana hivi tukaingia Shinyanga.

Nimeiona safari kama fupi, tukaenda moja ka moja kwa kaka yake Jamal wa wimpy ya Dodoma, mzee Ali. Mshikaji akasema nakuwacha hapo utaenda kwenye gari kutokea hapa, gari walipoiweka itanitoa mimi njiani mshikaji; haujali sio?

Mimi; Nashukuru sana, nimefika Shinyanga salama, nakutakia safari njema.

Dereva; Usijali mwanangu, tuwasiliane bwana, mimi nakuja sana Dar kufata haya magari.
Mimi; tutawasiliana, usijali, tuko pamoja mwanangu.
Dereva; umemuonaje lakini yule dada wa Gairo, si anafaa kuolewa yule?


Nikacheka, tu. Mzee Ali akasema mleteni mgeni kahawa, alikua mzee fiti sana, michapo yake akanikumbusha nyumbani. Ikaletwa kahawa pale, nikamwambia zmzee kuna machungwa na mananasi haya imekuwa ndio zawadi yako, ya chalinze haya.

Mzee Ali akasema ahsante sana. Ngoja nikupeleke mimi mwenyewe kwenye gari lenu, nimeshajua wapi, sio mbali ni karibu tu, sema yule dereva sio mwenyeji hapa.

Nikaenda na gari yake Mzee ali, ana Rav 4, anaendesha mwenyewe Tulipofika nikamwambia, ahsante sana Mzeew Ali, wewe unaweza kwenda tu.

Mzee Ali; hapana, sina haraka fannya kazi zako pengine ytahitaji kitu bwana.

Dereva wa truck nilikua nishampigia simu ikawa ananingoja pale, nikashuka nikatinga ovaroli langu, nikachukua mashine yangu nikaibandika kwenye poti yake, iakawa haisomi kitu kabisa, nikacheki betri za gari, terminal zote zipo poa, nikiweka switch on gari inakaa switch on.

Dereva; Bro hii gari mafundi wa Shy wameshindwa, wamesema mpaka ije kompyuta, sasa kompyuta kwani inakwambia nini?
Mimi; Gari hakun mawasiliano baina ya kompyuta ya garii yako kabisa. Kuna fundi waya alikuja hapa?
Dereva: ndio.
Mimi; Unaweza kumwita nijue kafanya nini hapa ili iwe wepesi, itakua kacheza na waya.
Dereva; Ngoja nimpigie simu

Wakati anampigia simu na mimi nikampigia mee nikamueleza tatizo nililokuta.

Mzee wangu kama mchawi wa magari, akanambia huyo fundi kacheza na harness muulize alisafisha ile soketi ya harness mwisho kule yenye kama swichi ndani? Nikamwambia akija nitamuuliza, ngoja jae, mimi bado sijafanya kitu mzee.

Mzee; Akichelewa mimi nitakwambia nini ufanye. Kuna rafiki yangu hapo Shinyanga, nitakurushia namba zake ukimaliza kazi umsalimie. Ukimuona mwambie nataka mchele, nikamwambia poa, nirushie namba, mzee akanirushia namba nikashuka chini ya lori kairbu ya mzee Ali, ile napiga simu nasikia inalia ya mzee Ali, Duh, maajabu haya, nikaona kumbe ni yeye alienileta kwenyue gari.

Mzee Ali; Hii simu umenipigia wewe? Namba yangu alikupa yule dereva?
Mimi ; Hapana kanipa babangu sikujua kama ni wewe, ndio nakupigia hivi,
Mzee Ali; Babako nani?

Nikamfahamisha, akanambia aah, kumbe mwanangu, ngoja nimpigie babako, akampigia palepale, akamweleza kilichotokea wakacheka pale. Mara fundi umeme akaja, akanionesha alichofanya, kweli alikichezea kile kile kitu alichosema mzee.

Mimi; Fundi umekifungua hiki?
Fundi: hapana nimekisafisha tu kwa kutumia spray ya dawa ya mbu.

Nikampigia mzee nikamfahamisha. Akanambia huyo fundi mjinga, hivyo kweli huwa vinakwama, lakini hicho ni plastiki na spray ile ni mafuta makali, amaekiharibu zaidi.

Sasa cha kufanya hapo, hicho kinataka zile bisibisi ndogo za mafundi saa ukifungue ndani, ukikwangue plastiki yote. Halafu kukiosha kwake, hicho chukua baking soda dukani tia maji gilasi moja, weka baking soda vijko viwili vya chakula. Mwambie mzee ali akutafutie fundi saa ukimpata mimi nitamwelekeza namna ya kukifungua. Akifungua kiingize chote kwenye baking soda, iwache kama robo saa, ikaushe vizuri. Hakikisha haina uchafu hata tone, angalia vi swichi vyake vya shaba vidogo sana humo ndani, msivichangue.


Nikamwambia mzee Ali, akanambia twende, tukaingia Shinyanga mjini kabisa, akanipeleka kwa fundi saa mmoja mzee wa kichaga. Kumuona Mzee Ali, Ahha Sharifu upo?

Mzee Ali' Nipo baba, msikilize kijana wangu huyu ana tatizo dogo.

Nikamuelekeza yuke mzee, akasema huna haja ya ya kumpigia mtu, nimeshaona namna ya kuifungua hiyo, akaiweka juu ya meza yake akaanza kuingiza vibisibisi vyake vile vidogo kabisa, kama dakika tu, akanambia kitu hicho. nikusafishie? Kina taka Z plastiki nyingi ndani. Nikamwabia, kisafishe lakini sio kwa mfuta aina yoyote.

Akanambia, mimi sio mjinga, mpira huo ukisafisha na mafuta unaiua hiyo, tena kuna mtu kaisafisha na mafuta, sema kidogo sana. Hiyo tunasafisha na cocacola kijana.

Mzee Ali akacheka, nikamwambia tumia baking soda mangi. Akasema hpo duka la chakula utapata, kumbe wewe fundi kijana, sisi tunatia coca cola inasafisha kama baking soda, nikaleta baking soda. Mzee wa Kichaga ni hodari sana. Vile anavofanya kazi zake kwa utulivu bila wasiwasi, nikaiona kama staili ya mzee wangu, hawana haraka kabisa.

Akachanganya na maji akajaza gilasi, akitia ile swith yote ndani ya yale maji ya baking soda, akanambia haya fundi, hii nusu saa itakua tayari. imeshapona hii, unaona swichi hizo sipo ndani? hiHzi zilikwamishwa na vumbi la plastiki na shaba, zililika sana kwenye plastiki.

Imehapona hii, iwache nusu saa, nitakisafishia ndani hiyo, inakua mpya kuliko ulaya. kama kuna swith haifai tutaibadili, usijali

Tulipomaliza akairudishia vizuri kabisa, akanambia nenda kaijaribu, hiyo ikifanya kazi ilete tuipige sili na super glue.

Tukarudi nacho kwenye gari, njiani nikampigia Mzee nikamueleza kuhusu fundi saa, Mchaga na cocacola, akasema huyo anajua. Basi usiwe na wasiwasi ulivyonieleza tu nimejua huyo fundi mzuri. Nikamwambia anatengenea mpaka saa za betri. Akasema, haya testi sasa italeta moto kwenye komputa, ikileta fanya test zako muiwashe.

Dah kuiweka komputa ikasoma kama kawaida, ikawa inainipa error ya swith ya injection. hizo nazijuliamnikaichomoa switch ile ya injection, nikaiweka sawa dakika mbili tu, kuiridishia, komputa kusoma, ikatoa majibu kila kitu bomba.

Kuipiga gari start, nusu kiki tu, chuma kikanguruma , nikamwambia Mzee. Akanambia, haya bwana gfundi mwache dereva wa watu aanze safari yake, gari ishapona hio.

Nikarudi kwa mzee Ali akanizuia nilale pale. ndio mambo ya majini yakaanza pale kwake. Kama Mungu alinipeleka pale.

Itaendelea.
 
Niulizie swala moja kwa huyo mwamba arsis,kwa mujibu wa quran,majini zamani walikuwa wanatabia ya kwenda mbinguni na kusikiliza mazungumzo ya huko,lkn baadae wakaja kupigwa na vimondo ili wasiende kusikiliza hizo habari za siri

Naamini maneno ya Allah ni kweli,nina hamu ya kusikia toka kwa huyo arsis anasemaje
Nimefurahi sana kwa hilo swali lako, hilo amenielezea zamani sana. Ni kisa kirefu kidogo,

Kwanza alikua ananielezea kuhusu dunia, kwanza yeye anakataa kua dunia haipo duara kama tunavyoaminishwa na sayansi. Pili anasema hizi nyota wanasema ni kubwa ni waongo wana sayansi, hizo nyota anasema ni kama ilivyosemwa kwenye Qur'an ni mapambo kwa hii dunia. Pia anasema hakuna nyota inayozidi tani kumi ukubwa wake, wanasayansi ni waongo. Na vimondo ndio hizo nyota. Kqa ufupi sana jibu ndio hilo, mbele huko kisa kikifika sehemu hiyo nilipouliza utakisikia kwa kina.

Majibu ya Arsis yanaweza kukuachia maswali mengi sana. Ni vizuri kua hilo alinijibu zamani.
Simba.
 
Ndio nikaingia kwenye ukumbi wa wageni wa Mzee Ali, kumbe Mzee Ali kwa kua ni Sharifu, watu walikua wanakwenda kwa matatizo yao pale.

Tymekaa kididogo akamwita kijana mmoja, akamwambia muonesheni chumba mfungulieni chumba cha Saleh, atalala kule.

Huyo Saleh ni mwanae, nikaambiwa kasafiri nchi za nje zaidi ya mwaka sasa lakini chumba chake kisafi kabisa kinafanyiwa usafi na kina chooo na bafu ndani kwa nadani, ni kizuri sana kwa ujumla.

Basi ile nimeingia kukoga, nilipomaliza, nikasali dhuhur pale pale chumbani nikaunganisha na alasiri, rakaa mbili mbili za safari.
Nilipomaliza, kujitupa kitandani nikapitiwa na kama kiusingizi nikaota Arsis ananambia yule jini mwanamke atakuja hapo ndani muda huu huu usilale.

Nikaamka, kweli ile kukaa tu yule jini akagonga mlango wangu, kufungua namuona yeye akaingia ndani akakaa juu ya kiti.

Jini 1: Akanambia sikiliza, pale ulipoondoka ukumbini, kaletwa mwanamke, kijana tu ana matatizo ya mashetani, mimi nimewaona ana mashetani wabaya sana, lakini kuwatoa wale ni dakika mbili tu, sema sikutaka kuingilia kazi za watu.

Kuna vijana wanamsomea Qur'an sasa hivi. Wakimsomea wale mashetani wanakimbia anatulizana kabisa, wakiacha kusoma wanarudi tena wanakaa kimya. Mzee Ali anajua kua hawajaondoka, kawaambia wasome tena, wale mashetani wajanja, wanakimbia kabisa, hakuna wakuwashika, itachukua muda wale vijana wanaosoma Qur'an bado hawana ujuzi wa kutoa mashetani wachafu namna ile.

Nimeongea na Arsis, katupa idhini mimi na jeshi langu tuwatoe wale tuwaue kabisa, wasimrudie tena kumtesa yule mwanakmke, wanasema wao walitumwa na mchumba aabae posa yake ilikataliwa kwao, basi mpska leo mwaka wa sita huu, kila ikiletwa posa mashetani yanapanda. Sasa tusipoteze wakati.

Wewe mwambie Mzee Ali, unaweza kusaidia, Mshike kichwa yule mwanamke, soma Qur'an unavyojua wewe. sisi tutamaliza kazi ndani ya dakika tatu. Nenda tu. usiogope.

Nikatoka chumbani, nikapiga hodi ukumbini, nikakuta kweli kuna mwanamke kafunikwa khanga anasomewa. Mzee Ali alikua kakaa kwenye kochi anatazama, nikaenda karibu yake. Nikamwambia mimi naweza kusaidia Mzee Ali.

Mzee Ali; Kusadia nini?
Mimi; Huyo mwanamke matatizo yake mimi naweza kuyaondoa.
Nzee Ali; Huyo sijui ana majini aina gani, yamisomea Qur'an yanakimbia, yanrudi, anakua katiulia kabisa anakwenda kwao, akikaa mwezi miezi miwili anapandishwa tena anarudi kazi yetu kwake ndio hii, kumsomea mpaka awe hajambo aende zake.
Mimi: Naomba kidogo vijana wasitishe kisomo, waniwachie dakika tano tu.

Mzee Ali: Fatiha.

Vijana wakasoma fatiha pale akawaambia haya kaeni poembeni. Nikaenda mimi nikamshika kichwa kama nilivyoelekewa ile kumshika kichwa tu kanigeukia akapiga kelele mpaka nikashtuka "huwezi kitu wewe". Mimi niakwa nasoma tu sra ndogo ndogo, mara kama dakika tatu hivi akaanbguka chini akazimia kabisa. Nikawaambia mwacheni apumzike, mimi nikaenda vhumbani nikamuta yule jini mwnamke, akanambia tumetoa majini watatu, wote wabaya sana, kishapona yule, kuna vitu vya kuchimbua nyumbani kwao. Basi ataamka sasa hivi mpeni maji ya kunywa kishappona yule, Harudu tena na hasigei mwengine pale atawekewa kunga na sasa ataolewa.


Nikarudi ukumbini nikakuta tule mwanamke kishaamka na ndugu zake waliomleta wako pale wanaitazama na mimi.

Mzee Ali: Haya twambie Sheikh.
Mimi: hakuna cha kuwaambia Mzee Ali, kishapona huyu,

Mzee Ali' AlhamduliLlah, haya jamani vchukueni mgnjwa wenu mkatoe sadaka kwa watoto wa madrsa, wapeni pipi, si mnajua watoto wanapenda pipi?

Basi wakaondoka pale kama hakuna kilichotokea. Nikamwacha Mzee Ai na wageni zake wengine, mimi nikarudi chumbani nikakoga tena, maana yule mwanamke wakati namsoimea alikua kaning'ang'ania shati na mikono, nilipomaliza kukoga nikatoka.nje ya nyumva kabisa, nikaanza kutemebea tembea.

Mara kidigoi nikamuona yule jini wa kike kaja akawa anatembea na mimi.

Jini1: Leo umekua abu yako . Umakua mganga wa kutooa majini.
Mimi: Mganga mimi au nyinyi mliowatoa?
Jini1: sisi nani anatuona pale, kulikua kuna jeshi zima limakuja, kutuzuwia lakini jeshi letu kunbwa na kali z*sana, wakaona watauliwa wote kwa ajjili ya majini watatu, mkubwa wao akwaamuru waondoke, tukawachukua wale mkubwa akala kiapo hamuahangaoishi tena yule mwanamke, yamekwisha. Kazi kwao sasa.
Mimi; kazi gani?

Jini1: Ushjulikana mganaga itabidi utibu watu pale.
Mimi: Niwacheni kabisa, sitaki mchezo huo, mimi nimewacha kazi zangu Dar. Tana namwabia Mzee Ali leo hii hii niondoke.

Jini1: Sawa, bira uonbdoke huku wachawi wengi sana, si unaona Mzee Ali, sio mganga, yeye anasoma Qur;an tu watu wote wanajua yeye mganga. Huu muji bora uondoke haraka sana, Hawawezi kukufanya kitu lakini ukikaa sisi vita haiishi kabisa. aknig akaondoka. Mimi nikarudi kwa Mzee Ali.



Tukakaa tunaongea ilishkua jioni sana , kas*aaguza chai,, akasema twende nje hapo tukanywe chai.

Mzee Ali'; Umjifundisha fani ya majini hii?
Mimi; Nimepea na babu yangu, yeye mganga.
mMzee Ali; Bbu yako kwa baba au kwa mama?
Mimi: Kwa baba?
Mzee Ali: ndiyomaana wamurithusha wewe babako mtundu sana, hawezi kupewa uganga yule. Akacheka.

Mimi: Mzee Ali mimi nataka niondoke haraka iwezekanavyo.

Mzee Ali; Kaa siku mbili tatu, upo nyumbani hapa. Usiwe na wasiwasi. Muulize babako kuhusu mimi tunajuana mika mingi sana, toka ujana wetu, basi tu siku hizi kila mmoja yupo mbali na mwenzake.
Mimi: Nitajjua siku nyingine nikijaaliwa, kuna kazi nyingi zinningj Dar.
Mzee Ali: Ngoja nikuulizie mgari ya lifti leo, ukikosa kesho alfajiri utapanda basi.

Mimi; Sawa.

Usiku tuliporudi msikitini, Mzee Ali akanambia tumepata gari ndogo mpaka Singida, inaondoka Allfajiri, haw wenyeji pale Singida wanasema pale watakupatia gari za kwenda Dar kesho hip hio. Sawa?

Mimi: Sawa. Tena itakua vizuri, watakuja hapa kupakia mchele wenu na kuku wawili.

tukala pale nikalala, usiku akaja yule jini mwanamke, akaniamsha, kama saasaba hivi Nikaamka, akanambia samhai kuna vitu muhimu nataka kukueleza.

Jini1: kabla hujaondoka keshomwabie, mzee Ali awaambie wale vijana waliokua wanasoma Qur'an waende wakasome kwa yile mwanamke, halafu je ya mlango wao mkubwa wachimbe atakavyotoa vyovyote kama chupa wazivunje achime moto, chochote watateketeze kabisa na moto, halafu wafanye hivyo hivyo mlangi wa uani, upo pemeni ya numbami.

Halafu nimeogea na Arsis, kanambia nikwambie ukita kuuliza chochiyte niulize usogope, kanipa idhini nikujibu chochoite cha kazi yangu au sio. kama sjui utamuuliza yeye. Futa ile kauli yangu ya nyuma, sasa nimepewa idhini kwa kua ushaanza kazi na sisi. Hatuwezi kukuficha kitu.
Mimi ; Sawa.
Jini1; Haya kwaheri, smahani nimekuamsha, mama yangu anakusalimi aliwepo leo, kakuona.
Mimi; Na yeye mpe salamu zangu. Kwaheri.

Nikajiweka sawa nikalala lakini ilinichukua muda kidogo kuupata usngizi, nilikua nawaza na kuwazua.


Itaendelea.
 
Inatokea post namba 221.

Alfajiri nikaamka kutazama saa ilikua muda wa kusali tayari, nikakoga faster nikasali. Kutoka ukumbini kwa Mzee Ali nikakuta mlango wa nje umeegeshwa tu haukufungwa moja kwa moja, nikatoa salaam. Mzee Ali akanijibu, akanambia njoo nje bwana tunywe kahawa.

Nikatoka nje nikakaa nakunywa nae kahawa, akanambia mimi muda nimeenda msikitini nimerudi, nimeona nisikusumbue. Vipi umelala salama?

Mimi; Nashukuru nimelala salama nimeamka salama, nikatia kahawa, yeye alikua kishaanza kunywa, akaniwacha huku nahisi anaitazama.

Mzee Ali; Jana nimepigiwa simu usiku na ndugu zake yule binti, wanasema kufika tu kakoga, kala vizuri, kalala mapema, sio kama kawaida yake, hakusumbua mtu, sema wanasema walikua wanaogopa asiripuke tena, maana yule huwa hali, hakogi na anasema hovyo wakimsemesha, utafikiri mwehu.

Mimi; Mwenyezi Mungu amjaalie, kishapona yule, sema kuna kazi kidogo inatakiwa ifanyike kwake, inatakiwa wale vojana waliokua wanamsomea Qur'an wakachimbe mbele ya mlango wao mkubwa wa mbele na mlango wa uani uliopo pembeni ya nyumba. Waanze na wa mbele, watachokikuta wachome moto, kama kuna chupa waivunje vilivyomo ndani wachome moto, wasiwache kitu, wateketeze kabisa. Na vya uani hivyohivyo.

Mzee Ali akawa ananitazama kama anataka kuuliza kitu, akashusha pumzi. Akatia kahawa kikombe chake na changu.

Mzee Ali; Sawa, nitawafahamisha. lakini ungekuwepo mwenyewe ingekua vizuri sana. Kwanini usibaki bwana?
MImi; Hakuna shaka Mzee Ali hayo ni mazaga zaga yao tu waliweka, tunayaondoa kabisa, isibaki hata alama yao. Lakini hakuna jipya, binti kishapona, mtanijulisha hali yake anaendelea vipi siku za usoni.

Mzee Ali; Leo hii utapata simu yangu. hawa vijana walisema wanakuja baada ya alfajiri tuwasubiri kidogo maana kuna chai nzito ya subuhi inawangoja wao tu.

Haijapita muda ikaingia landcruiser prado kuna vijana wawili tu ndani, Wakasalaimia pale.

Mzee Ali: haya twendeni ndani mpate kifungua kinywa, tulikua tunawangoja nyinyi tu, huyu ndio mwenzenu mtakwenda nae.

Tukaingia ndani tukakuta supu ya kuku na mikate ya kuoka nyumbani, maziwa fresh ya moto, tukapiga pale. Tyulipomaliza tukatoka nje.

Mzee Ali; Ngojeni jamani mpakilieni huyu mchele wake kama nilivyowaambia na kitenga chake cha kuku.

Mimi nikwaambia nakuja, ngoja nichukue kibegi changu. Nikaingia ndani nikatoka na kibegi changu chepesi tu, cha maana ndani yake ni laptop yangu na mawaya ya kuunganisha kwenye magari, na nguo zangu mbili na overoli moja, kwisha.

Nikakuta washapakia vitu tukaagana na Mzee Ali. Safari ikaanza, hatukuchelewa sana tukafka Singida, wale vijana wakanishusha kabla ya kuingia mjini, kuna kituo cha mafuta kikubwa tu kizuri, wakashusha mizigo yangu wakanikabidhisha kwa mtu mwenyeji pale, wakamwambia mtafute gari haraka iwezekanavyo yoyote atakayopata kwanza ikiwa basi au gari ndogo. Akasema, poa. Yule aliokua anaendesha akamwambia, usimdai kitu, nauli na posho yako njoo uchukue kwangu. Akasema poa. Wakaondoka.

Sijakaa sana ikaja gari, pickup ya NGO fulani, ndani yumo dereva tu. Akamfata dereva akaongea nae, ile gari ikasogea akaweka mizigo nyuma akanambia huyo na yeye katokea Shy. Anaenda Dar, mpaka nyumbani hiyo. Nikaona kamshikisha poesa pale akatuaga ytukaanza safari, tukawa tunaongea ongea na dereva, anakwenda spidi huyo, mpaka nikawa naogopa. Tukaingia Dodoma mapema tu, akapiga juu kwa juu, hakusimama kabisa Dodoma.


Kutoka toka nje ya Dodoma, akanambia ukitaka kuchimba dawa nambie ndugu yangu.
Mimi; Tusimame Gairo ikiwezekana, kuna mtu nataka kumsalimia kidogo. Akanambia poa. Tulipofika Gairo nikamwelekeza pale kituoni akaweka gari vizuri tukaingia kimgahawa cha yule dada, tukakuta kimya, kumbe alikua kwa ndani anatuona. Akasema, Karibuni.

Mimi; Ahsante, habari za hapa? Akanikumbuka haraka sana.
Dada; Yule muhuni yuko wapi?
Mimi Tuliachana Shy.
dada Niwape nini, nikamwabia kahawa ipo?
Dada; Ipo ya kopo niwape?
Mimi; Tupe.

Tukanywa kahawa, nikaona dereva kama hana raha, ana haraka, tukaaga, nikamwambia mimi sina zawadi nimeona nikusalimie tu.

Dada:;Ahsante sana, basi mimi nakupa zawadi ya hio kahawa, juu yangu msiilipie. Akacheka.

Mimi; Ahsante sana, tukaondoka.

Dereva akachoma kama kwa hasira fulani hivi, tukawa kimya hatuongei. Mbele kidogo kuna sehemu wanauza uza vitu kibao tu, akasema nachukua zawadi za nyumbani kidogo. Nikamwambia poa.

Tukashuka akanunua nyanya na vvitu vitu vingi tu, pembeni kwenye mti nikaona kuna mtu sio wa kawaida, nikasikia sauti ya Arsis, akanambia jini huyo, jifanye kama hukumuona mshenzi tu huyo. Nikasema poa kimoyomoyo.

Dereva akawa kama anabishana bei na kina mama wale, nikatoa elfu kumi nikawapa, nikawaambia chukueni hii jazilieni. Wakapokea, wakasema ahsante. Dereva akaingia kwenye gari kama kakasirika hivi.

Tukaondoka kimya kimya mpaka tunafika Dar kwenye foleni foleni zile, akanambia nikuwache wapi mimi naishia Sinza, nikamwambia niwache Sinza tu pale kijiweni nitachukuwa taxi.

Fereva; kwani unaenda wapi?
Mimi; Ilala.
Dereva; sasa badili ya taxi si unipe mimi hiyo pesa nikupeleke mpaka Ilala.
Mimi; Poa, ntakupa.
Dereva; Utanipa elfu ishirini?
Mimi; Poa usijali.

Akanipeleka mpaka Ilala, kufika, nikatoa elfu thelathini nikampa, nikamwambia na hiyo nyingine ya kiushikaji bro. Tukashusha mzigo pale akanambia si niongeze japo kumi? Sikufanya hiyana, nikatoa elfu ishirini nikampa.

Aknitazama usoni, akanambia ahsante. Nikamwambia karibu, hapa ndio kwangu. Akaondoka zake bila kusema kitu. Nikashukuru tumefika salama. Kuna mlinzi pale kwetu saa zote. Akaja, akwaita na vijana wawili wa ndani kwetu, hua wanasaidia saidia kazi za nyumbani. Wakasaidiana wakaingiza mizigo. Sikukuta mtu wa nyumbani, si mama, si wife.

Nilipokwisha ingia ndani nikakoga nikabadili nikampigia mzee, akanambia nimesikia habari zako Shinyanga, Mzee Ali anakusifu sana.

Tukaongea kidogo kwenye simu, akanambia hao wote wa hapo nyumbani wametoka, watarudi jioni. Nikamwambia. poa.

Tukaagana.

Itaendelea.
Simba.
 
Back
Top Bottom