Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

We bwana mdigo leta mambo hayo au bado unakula kamba wako ,kamba kutoka kidimbwi maalum anakijua babu yako tu hiko kidimbwi😅😅🤣
Babu yangu alijaaliwa maarifa siku nyingi sana. Alijichagulia hiyo sehemu ambayo watu wote walikua wanaiogoppa. ikawa kajichagulia katikati ya matawi mawili ya mto ambayo yote,a yanatoa kamba kwa wingi wakati wa msimu, lile tawi kubwala mashariki na lile lenye mapango ya kiajabu, yote yapo kwenye eneo la shamba lake. Ule mto wa Mashariki ndio kwa upande wa pili jamii wanapata kuvuna msimu wa kamba, mto ule ndio mpaka wa shambani kwetu, huu mto wa Magharibi ni tawi dogo tu lisilokauka, linapita katikati ya shamba letu, mapango mawili makubwa moja ni kama ukumbi tu mkubwa, hayakutani kwa ndani, yote yapo ndani ya shamba letu.

Mji wa babu bado wanakaa wana familia au wanafunzi wanaokuja hapo mpaka leo hii.

Ukifika kuanzia mpakani horohoro mpaka unafika Duga maforoni ukiuliza Mzee mabruki kwake wapi, unaletwa hata na mtoto mdogo. Babu wengi wanafikiri Mbaruki ni jina lake, lakini ukweli ni kua kuanzia anafanya kazi Tanga 'Mabruki" ulikua ni msemo wake mkubwa, akimaanisha kupongeza kila zuri utaloilfanya,anakupongeza kwa kusema "mabruk" basi ikashika ndio likawa jina lake "Mzee Mabruki". Ukija Duga Maforoni tuna kwetu, vizazi vya Mzee Mabruki mpaka kesho. Lakini kwa Mzee Mabruki alipo ni kule shamba, baharini kwenye kamba wa kufa mtu. Qengi wanajua anakaa Duga mjini, hawajui pale ni kwake anakuja kwa shughuli zake tu, lakini makazi yake hasa ni kule shamba.

Kamba wa kufuga ilishindikana kabisa kule. Walikua na kazi kubwa sana, babu akasema sina hamu nao, hawa wa msimu wanatutosha na pesa zake hatuzimalizi. Ndio miradi ya kuvuna kamba kwa mwaka mzima ikaishia kwa kauli hiyo ya babu. Sasa kuna misimu miwili tu, msimu mkubwa na mdogo, na kila msimu una aina tofauti ya kamba. Miujiza ya Muumba wetu hio.

Mpaka kesho, misimu yote ya kamba, nakua shambani kwetu, navuna kamba tu.
 
Mleta mada kaeleza mambo mengi makubwa ila juu juu (siwezi sema kakosea maana target yake ni kufikisha ujumbe kuhusu alichokiona baada ya kufunguka macho, na alhamdulillah ujumbe umefika,,,, japo utata umebaki mwingi kwenye vichwa vya watu)

Ngoja nisawazishe eneo dogo hapa kwajinsi ninavyoelewa!!
Mada kubwa mezani ni SPIRITUAL AWAKENING

Viumbe wa kiroho... Ni viumbe wote ambao hawaonekani kwa macho ya kawaida (malaika, majin n.k kila mtu anawafaham kwa mujibu wa imani yake) viumbe Hawa huwa na connection kwa watu maalum pekee

Watu maalum ni hawa 👉 Manabii na mitume, wachamungu sana, waganga wa kichawi na watu waliopendelewa

Ili uwe kwenye special group lazima uwe connected na source of power yoyote kati ya hizi
A. Mungu
B. Ibiris

Sasa viumbe wa kiroho wao pia wapo makundi mawili tu.... Kutokana na uanachama wao kweny hizo source of power (hapo either awe upande wa Mungu au Shetani🤝

Sasa hao special group pia wananamna yao ya kuwasiliana na hao viumbe.....
Baadhi ni hisia, ndoto, telepathy na kuona

(Hii njia ya kuona ndio njia ya juu zaidi tuseme ndio maqam ya mwisho.... Sasa huwa unaanza kwa kupanda daraja
Utaanza njia ya hisia, ndoto, telepathy mwisho utaona🤝

Mleta mada yupo kwenye special group upande wa watu waliopendelewa... Maana hajafata process wala hajaandaliwa ila karushwa daraja moja kwa moja

(Kwa imani ya kiislam huwa Kuna watu wanazaliwa wakiwa n mawalii wa Mwenyezi Mungu,,,,, kitu ambacho n nadra sana mtu kukipata

Au mfano mtu ufanye ibada mpk uwe nabii😁😁😁🏃
Ngum sana, nabii huzaliwa akiwa tayar ni nabii


(Dah mambo ya kiroho huwa yanamaelezo mengi sana...... Ila ukiweza kuwasiliana na viumbe wa kiroho hii Dunia umeiweza🤝
Njaa kwako sahau, kuonewa kwako sahau, kukataliwa kwako sahau,,, hii ni Siri ambayo wazungu wanaitumia sana

Ushuhuda:
Baba yangu alikuwa na uwezo wa kwenda kwenye mlima wowote au mto mkubwa, akifika anawaita watawala wa huo mto au mlima wanakuja live anawaeleza anataka nn kutoka kweny himaya yao halafu wakielewana kazi kwisha
(Anaenda kweny kaburi la mtu aliyekufa anamuamsha anaongea nae akimaliza anarudi kulala..... (Najua hapa ntaonekana muongo)
Anazama kweny maji anatoka mkavu bila kuloana
Anaweza kuchukua ile sarafu ya zaman inayotafutwa kila kona
SIMBA MBILI au Rupia (akafanya yake akamtoa yule Simba na king George wakakaa na kuanza mazungumzo

Alikuwa na uwezo wa ajabu sana.....

Note: source yake ya Power haikuwa GOD
(Kwenye hii Dunia ukitaka kuwa mtu hatari we chagua njia moja upite hiyo kikamilifu utaona balaa lake.... Kama n Mungu swali sana acha dhambi kwa ukamilifu wake utaona utavyokuwa hatari

Kama n upande wa shetwani... Roga sana, usisite kutoa mtu kafara Yani kuwa nyambisi haswaa utaona ibiris atavyokupenda😂

Fanya juu chini upate mapenzi either ya Mungu au Ibiris.... Usikubali kukaa katikati maana utakuwa mtumwa
Kamba.... Na wewe umeamua kutufunga kamba. 🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Inatokea post namba 155.

Baada ya kuagana na Arsis nikaenda kwenye gari, nikaondoka bila kukutana na yeyote, nilipofika nyumbani, mlinzi akanifungulia geti bila kuita au kupiga honi, nikaaiweka gari, nikaingia chumbani kwangu kulala. Usingizi ukawa hauji haraka. Nikaanza kuitazama ile pete, nikachukua mkebe wake nikautazama vizuri. Ulikua ni mkebe wa kizamani sana, ulikua na maandishi maatatu kama michoro yale ya Kimisri ya zamani. Nikasema nikikutana na Arsis nitamuuliza kimeandikwa nini. Nikarudisha mkebe, nikaichukua bakora nikawa naichezea, nailaza chini inanyanyuka yenyewe, naiweka upande inajisimamisha yenyewe. Mpaka nikawa nacheka tu mimi mwenyewe, Bakora haikubali kulala chini kabisa. Nikaiweka pembeni ya kitanda changu. Nikalala.

Maisha yakaendelea kama vile kabla sijaenda Tanga, haikupita muda nrefu nikawa noimeshafu ga ndoa, ilikua ndoa ya surporise kubwa kwangu, lakini hapa sio pahala kwake kuielezea.

Kuna siku, baada ya kama miezi miwili mitatu ya kuoa, nikasema leo ngoja nikamtembelee "mama mkwe" wa kwenye vitumbua asubuhi subuhi, lakini toka siku niliyoyaona Chalinze na pale kwao nikawa naogopa kula kwa mama lishe. Nikajisemea wacha niende tu nikawagtembelee. Kufika, mama mkwe akawa na bashasha kweli, "Ah bwna harusi, leo umefunguliwa?" Nikamwambia "mboina jamani saba iliisha siku nyingi/". Aaah huonekani nikajua "honey moon zenu, mwezi umekwisha bwana harusi huonekani" Nikamwabia aah si unajua tena, maisha ya ndoa tofauti na ya zamani. Akanambia "tena yafurahie bado ungali una nguvu mwanangu, usicheze na furaha yako hata kidogo> Nikamwambia 'poa".

Akanambia haya nikjupe vingapi leo? Nikamwambia nimekuja kulusalimia tu, nyumbani si wameshakuja kuchukua? Akanambia haya kula viwili, ingawa hukumngoja binti yangu lakini najua kuna siku utamuoa tu, ukwe uko pale pale. Nikamwambia, tulikua nae harusini, kumbe ni partner mkubwa wa mke wangu.

Khaa, nyinyi mmetufanyia vituko vinaogelewa Ilala nzima hii, miaka yote sisi tunajua yule dadako kumbe mmelelewa pamoja tu. Nikamwambia hata mimi nilikua najua tumezaliwa pamoja, umbe ni watoto wa mjomba na shangazi.

Mama mkwe; Aaah mkeo na binti yangu umesahau toka wadogo wako pamoja? Mimi nimewaambia na huyo mume atawaoa wote mkae pamoja.

Mimi; Mimi poa tu, wakikubaliana wenyewe mimi nipo. Nikabadilisha topic.

Vipi mama wa mandazi, sijamuona toka siku ile ya pirika?
Mama Mkwe; Kwani yaliompata madogo mwanangu, si kashikwa ana wanga huko buguruni. Kututukana na kutuita sisi wachawi, kumbe yeye ndio mchawi na mwanga mkubwa.

Mimi; hatari kubwa, sina habari.
Mama mkwe; Makubwa mwanangu hata hayasemeki. Alikua anaongea huku ananong'ona. Tena hapa mwezi ujao hatupo tena, hii nyumba imeshauzwa, tunatafuta kijiwe kingine hivi sasa. lakini mimmi sina wasiwasi, nitakua nyumbani kwangu palepale, hakuna wa kunihamisha, pale kwangu mwenyewe. Nitapika pale nitakwenda kuuza vitumbua vyangu pale nje ya msikitini mpaka tupate kijiwe.

Mimi: Kumbe tuko wote, hakuna tabu. Usihamie kijiwe kipya bila kunijiulisha.
Mama mkwe; Kumbe huna habari? Wenye nyumba hii washahama wote, wameiuza nyumba haraka haraka kwa aibu, kumbe walikua chama kimoja na yule muuza mandazi. Wameaibishwa wote, kwa aibu na jiji wamelihama.
Mimi; Kasheshe.

Mama mkwe; lakini toka wameondoka, hata uzito na mazonge zonge yamepungua, kumbe tunaishi na wanga hapahapa, sasa hivi baba kijiwe kimesafishwa hiki, ambao walikua hawaji sasa wanakuja.
Mimi; Kwani aliepanunua kawaambia muhame?

Mama mkwe; Wala hajatwambia tuhame, tena mteja wetu mzuri, anakaa hapo mtaa wa nyuma, shogake mamako , yule mwanamke mpambe wa Kiarabu?

Mimi; Aaah, nimeshamjua, ndio nilisikia kanunua nyumba nyingine, kumbe ndio hii?
Mama mkwe; Pesa imetulia pale kachukua hii na ya nyuma yake, zote kwa pamoja, pesa cash na sisi wote hapa tukapata sadaka yetu nono, tena nono kweli kweli. Hatuna manug'uniko wala masikitiko. Hatutaki tumwekee kiza akianza ujenzi, mwenyewe kasema hachelewi ataanza ujenzi. Sisi tumeona wala hana haja ya kutwambia tuhame, tumeishi nae kama ndugu miaka yote. Tena mwenzetu sana yule Mwarabu, sisi tumefurahi kununua yeye hizi nyumba, maana yule na mamako ndio kimbilio letu tukiwa na shida zetu. Mwenyezi Mungu awajaalie kila heri.

Akapiga dua ndefu hapo. Kabla hajamaliza, mama muuza uji akasema bwana harusi kombe lako hili la uji, usiseme umeshiba nimekuongezea pilipili manga njia za mkojo zifunguke vizuri.
Mama mkwe: Kwani alikwambia ana shida na njia yake?
Uji: Koma bibi wee, sisi tunajua kutunza mabwana harusi, wa Tanga mwenzangu huyu, ulikua hujui?
Mama mkwe: Nawajua sana, wote wadigo nyinyi. Mnayoyajua ndio hayo hayo tu, hana lingine.

Uji; Usitutukane kirejareja, usituingilie kabisa, tuwachie wenyewe. Bwana harusi usimsikilize huyu mzaramo, hawwana walijualo zaidi ya kutingisha makalio tu.
Mama mkwe; Mbona unamwaga razi kwa mkwe wangu?
Uji; Tupishe huko, tukaoe mzaramo sisi hatuna akili? mambo ya mafiga matatu tutayaweza wapi sisi? Nyie ndio mje kuoa kwetu msiojua kupika nyinyi.

Mama mkwe: Mkwe wangu usimsikilize huyu bibi, hata huko kwao Tanga kapasahau, toka aolewe hajaenda hata kutemmbea kwao, mzaramo alivyo mdhibiti.
Mimi; Jamani nilikua nataka kuwauliza kitu.

Wakakaa kimya wote wananisikiliza.

Mimi; Hivi kwanini hamuweki kijiwe chenu pale msikitini, kwa pembeni pale, uwanja mkubwa tu, hata mkiwa ishirini mtaenea pale.
Uji: Hwa wazaramo hawataki msikitini, wanga wakubwa wanapaogopa, mimi uji wangu nauanza na watu wa msikitini alfajiri, wakitoka tu msikitini wapo hapa. Hawa wanakua bado wameulalia.

Mama mkwe: Wewe mbona una mdomo mchafu mbele ya mkwe wangu?
Uji: Nisamehe baba, mimi uji nitauuzia pale pale msikitini nikiondoka hapa, nimeshaongea na Imamu kasema mradi nisipikie pale tu, msikiti unatakiwa uwe msafi nje na ndani. Kazi kwa hawa wachoma vitumbua na wapika chapati, watapikia wapi pale?

Mama mkwe; Tutaongea na Imamu, msikiti nyuma pale tutapajenga wenyewe.
Uji; Hilo wameshakataa kama ulikua hujui, wanasema muda si mrefu msikiti unaongezwa ule unakua mkubwa , tena wa ghorofa.

Mama mkwe: Hilo nimesikia hata mimi, lakini hawajui utaanza lini kujengwa.

Uji; Umelala sijui umeulalia wewe? Msikiti kabla nyinyi hamjaondoka hapa utakua umeshaanza kujengwa.
Mama mke; basi poa, tutawauzia haohao wanaokuja kujenga, tutabanana nao hapohapo, watakula wapi?

Uji; Tena pale cheyameni wa wauzaji chakula mimi, mtanilipa mimi kila siku, mkitaka biashara pale.
Mama mkwe; Mdigo wacha utapeli wa mali ya msikiti, huo u cheyameni akupe nani wewe mwenzangu na mimi, nipishe huko.


Nikaona niage. Nikaaga nikaondoka zangu, uji kweli ulikua na pilipili manga ya ziada.

Itaendelea.
 

Inatokea post namba 155.

Baada ya kuagana na Arsis nikaenda kwenye gari, nikaondoka bila kukuta na yeyote, nilipofika nyumbani, mlinzi akanifungulia geti bila kuita au kupiga honi, nikaaiweka gari, nikaingia chumbani kwangu kulala. Usingizi ukawa hauji haraka. Nikaanza kuitazama ile pete, nikachukua mkebe wake nikautazama vizuri. Ulikua ni mkebe wa kizamani sana, ulikua na maandishi maatatu kama michoro yale ya Kimisri ya zamani. Nikasema nikikutana na Arsis nitamuuliza kimeandikwa nini. Nikarudisha mkebe, nikaichukua bakora nikawa naichezea, nailaza chini inanyanyuka yenyewe, naiweka upande inajisimamisha yenyewe. Mpaka nikawa nacheka tu mimi mwenyewe, Bakora haikubali kulala chini kabisa. Nikaiweka pembeni ya kitanda changu. Nikalala.

Maisha yakaendelea kama vile kabla sijaenda Tanga, haikupita muda nrefu nikawa noimeshafu ga ndoa, ilikua ndoa ya surporise kubwa kwangu, lakini hapa sio pahala kwake kuielezea.

Kuna siku, baada ya kama miezi miwili mitatu ya kuoa, nikasema leo ngoja nikamtembelee "mama mkwe" wa kwenye vitumbua asubuhi subuhi, lakini toka siku niliyoyaona Chalinze na pale kwao nikawa naogopa kula kwa mama lishe. Nikajisemea wacha niende tu nikawagtembelee. Kufika, mama mkwe akawa na bashasha kweli, "Ah bwna harusi, leo umefunguliwa?" Nikamwambia "mboina jamani saba iliisha siku nyingi/". Aaah huonekani nikajua "honey moon zenu, mwezi umekwisha bwana harusi huonekani" Nikamwabia aah si unajua tena, maisha ya ndoa tofauti na ya zamani. Akanambia "tena yafurahie bado ungali una nguvu mwanangu, usicheze na furaha yako hata kidogo> Nikamwambia 'poa".

Akanambia haya nikjupe vingapoi leo? Nikamwambia nimekuja kulusalimia tu, nyumbani si wameshakuja kuchukua? Akanambia haya kula viwili, imi ingawa hukumngoja bintoi yangu lakini najua kuna siku uytamuoa tu, ukwe uko pale pale. Nikamwabi tulikua nae harusini, kumbe ni partner mkubwa wa mke wangu. Khaa, nyinyi mmetufanyia voituko vinaogelewa Ilala nzima hii, miaka yote sisi tunajua yule dadako kumbe mmelelewa pamoja tu. Nikamwabia hata mimi nilikua najua tumezaliwa pamoja. Kumbe ni watoto wa mjomba na shangazi.

Mama mkwe; Aaahmkeo na binti yangu umesahau toka wadogo wako pamoja? Mimi nimewaambia na huyo mume atawaoa wote mkae pamoja.
Mimi; Mimi poa tu, wakikubaliana wenyewe mimi nipo. Niakbadilisha topis, vipi mama wa mandazi, sijamuona toka siku ile ya pirika?
Mama Mkwe: Kwani yaliompta madogo mwanangu, si kashikwa anawanga huko buguruni. Kututukana na kutuita sisi wachawi, kumbe yeye ndio mchawi.
Mimi; hatari kubwa, sina habari.
Mama mkwe: Makubwa mwanangu hata hayasemeki. Alikua anaongea huku ananong'ona. Tena hapa mwezi ujao hatupo tena, hii nyumba imeshauzwa, tunatafuta kijiwe kingine hivi sasa. lakini mimmisina wasiwasi, nitakua nyumbani kwangu palepale, hakuna wa kunihamisha, pale kwangu mwenyewe. Nitapika pale nitakwenda kuuza vitumbua vyangu pale nje ya msikitini mpaka tupate kijiwe.
Mimi: Kumbe tuko wote, hakuna tabu. Usihame kijiwe kipya bila kunijiulisha.
Mama mkwe: Kumbe huna habari? Wenye nyumba hii washama wote, wameiuza nyumba haraka haraka kwa aibu, kumbe walikua chama kimoja nayule muuza mandazi. Wameaibishwa wote, kwa aibu na jiji wamelihama.
Mimi; Kasheshe.
Mama mkwe, lakini toka wameondoka, hata uzito na mazonge zonge yamepungua, kumbe tunaishi na wanga hapahapa, sasa hivi baba kijiwe kimesafoshwa hiki, mbao walikua hawaji sasa wanakuja.
Mimi; Kwani aliepanunua kawaambia muhame?
Mama mkwe; Wala hajatwambia tena mteja wetu mzuri, anakaa hapo mtaa wa nyuma, shogake mamako , yule mwanamke mpambe wa Kiarabu? Aaah, nimeshamjua, ndio nilisikia kanunua nyumba nyingine, kumbe ndio hii?
Mama mkwe; Pesa imetulia pale kachukua hii na ya nyuma yake, zote kwa pamoja, pesa cash nq sisi wotw hapa tukapata sadaka yetu nono, tenono kweli kweli. Hatuna manug'uniko wala masikitiko. Hatutaki tumewekee kiza akianza ujenzi, mwenyewe kasema hachelewi ataanza ujenzi. Sisi tumeona wala hana ya kutwambia tuhame, tumeishi nae kama ndugu miaka yote. tena mwenzetu sana yule Mwarabu, sisi tumefurahi kununua yeye hizi nyumba, maana yule na mamako ndio kimbilio letu tukiwa na shida zetu. mwenyezi Mungu awajaalie kila heri, akapiga dua ndegu hapo. Kabla hajamaliza, mama muuza uji akasema bwana harusi kombe lako hili la uji, usiseme umeshiba nimekuongezea pilipili manga njia za mkojo zifunguke vizuri.
Mama mkwe: Kwani alikwambia ana shida na njia yake?
Uji: Koma bibi wee, sisi tunajua kutunza mabwana harusi, Watanga mwenzangu huyi, ulikua hujui?
Mama mkwe: Nawaju, wote wadigoi nyinyi.
Uji: Kwa hio usituingilie kabisa, tuwachie wenyewe. Bwana harusi usimsikilize huyumzaramo, hana alijualo zaidi kutingisha makalio tu.
Mama mkwe; Mboina unamwaga razi kwa mkwe wangu?
Uji; Tupishe huko, tukaoe mzaramo sisi hatuna akili? Nyie ndio mje kuoa kwetu msiojua kupika nyinyi.
Mama mkwe: Mkwe wangu usimsikilize huyu bibi, hata huko kwao Tanga kapasahau, toka aolewe hajaenda hata kutemnbea kwao, mzaramo alivyo mdhibiti.
Mimi; Jamani nilikua nataka kuwauliza kitu.

Wakakaa kimya wote wananisukiliza.

Mimi; Hivi kwanini hamuweki kijiwe kwenu pale msikitini kwa pembeni pale, uwanja mkubwa tu, hata mkiwa ishirini mtaenea pale.
Uji: Hwa wazaramo hawataki msikitini, wanga wakubwa wanapaogopa, mimi uji wangu nauanza na watu wa msikitini alfajiri, wakitoka tu msikitini wapo hapa. Hawa wanakua bado wamulalia.
Mama mkwe: Wewe mboina una mdomoi mchafu mbele ya mkwe wangu?
Uji: Nisamehe baba, mimi uji niytauuzia pale pale msikitini nikiondoka hapa, nimeshaongea na imamu kasema mradi nisipike pale tu, msikiti unatakiwa uwe msfi njje na ndani. Kai kwa hawa wachoma vitumbua na wapika chapati, watapoikia wapi pale?
Mama mkwe; Tutaongea na msikiti nyum aple tutapajenga wenyewe.
Uji; Hilo wameshakataa kama ulikua hujui, wanasema muda si mrefu msikiti unaongezwa ule unakua mkubwa na tena wagorogfa.
Mama mkwe: Hili nimesikia hata kimi, lakini hawajui lini utaanza lini.
Uji; Umelala wewe, msikiti kabla nyinyi hamjaondoka hapa utakua umeshaanza kujengwa.
Mama mke: basi poa, tutawauzia hao hao wanaokuja kujenga, tutabanana nao hapo hapo, watakula wapi?
Uji; Tena pla cheyameni wa wauzaji chkula mimi, mtanilipa mimi kila siku, mkitaka biashara pale.
Mama mkwe: Mdigo wacha utapeli wa mali ya msikiti, huo u cheyameni akupe nani wewe mwenzangu na mimi, nipishe huko.


Nikaona niage. Nikaaga nikapondoka zangu, uji kweli ulikua na pilipili manga ya ziada.

Utaendelea.
Hivi hilo jina .... Arsis ndo hili Osiris (au hao ni wawili tofauti
 
Kamba.... Na wewe umeamua kutufunga kamba. 🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
😂😂😂😂😂😂😂..... Haya mambo huwa yapo hvyo, ukisikia lazima uone ni kamba!!!

Siku nikiamka vizuri ntaleta kisa changu hapa.
(Maana mm nilikabidhiwa kwa mashetwan toka nikiwa mdogo, baadae wakasalitiwa nikanyang'anywa mikononi mwao ilikuwa n vita kali sana..... Wakamgeuka mzee wangu wakamuua kikatili, mzee akaona ni bora yeye afe kuliko mwanae awe mfalme wa mashetwan na wachawi🚶🚶

Siku moja nikiamka vizuri ntaisimamisha jf kwa muda😂

Maana ni visa vya mfululizo kwanzia miaka 4 mpk Sasa hivi nnavyoandika hii comment bado vita inaendelea 🏃
 
Hivi hilo jina .... Arsis ndo hili Osiris (au hao ni wawili tofauti
Ni tofauti kabisa, umewahi sana kuliuliza, niliwahi kumuuliza Arsis akanijibu;

Mimi; Arsis, wewe ndiyo Osiris?
Arsis; Hahahaa, Osiris ni Mungu wa mafirauni, mimi sio Mungu, sijawahi kuwa na wala sitokuwa Mungu wa yeyote, mimi naamini Mwenyezi Mungu ni mmoja alietuumba sisi sote.
Mimi; Arsis, wewe ulishwahi kuniambia mi Mason pia, vipi Mason halafu unaamini kuna Mwenyezi Mungu mmoja?
Arsis; Mimi naweza kuwa chochote kwa kazi zangu nilizopangiwa na Muumba wangu. Udsiniulize sana kuhusu mambo ya imani. Amini ninavyokwambia.

kwa ufupi huo ilikuwa mjadala wangu kadiri ya kumbukumbu zangu, tuliongea mengi sana siku hiyo, ilikua nimeshazoweana nae na nilikua nimeanza kupata mwangaza wa mengi kupitia kwake. Leo imebidi niweke kipande hicho kwa ajili ya swali lako.

Arsis ni mwalimu mzuri sana, ambae kila alichonifundisha alinisisitiza na mimi nijisomee, historia na mambo mengine mengi tu. Msimamo wake ni tofauti na mtu yeyote yule. Anashangaza sana.
 
Inatokea post namba 174.

Maisha yakaendelea, koo za ki simba na mambo na nidhamu zake, ambazo sitaki kuzihusisha sana na hiki kisa cha viumbe visivoonekana.

Kitu kimoja kingine muhimu kilinitokea safarini, nilikua nasafiri na gari kubwa, nimepewa lift na mteja wetu mmoja tunaemtengezea gari zake, alikua anaelekea Mwanza na mimi naelekea Shinyanga kwa kazi nilotumwa na mzee, kazi zetu za ufundi.

Tumeondoka Dar vizuri Alfajiri sana, dereva akanambia ana mke mdogo hapo mbele kidogo ya Kongowe , Kibaha. kwahiyo atasimama hapo kwa muda awasalimie, mimi kama nina haraka sana atanitafutia lifti hapo check point ya TRA ndipo alipo paki gari. Alisema hapo kuna usalama zaidi kwa gari. Nikamwambia, wewe nenda tu, nikiondoka nitakupigia simu. Akachukua boda boda, akamwacha kwenye gari utingo wake na mimi. Nikashuka, kuna vijimgahawa vingi vingi tu, pako na hekaheka na pirikapirika nyingi za hapa na pale. Pamechangamka.

Nikaingia kwenye kimgahawa kimoja, nikaagiza maziwa ya moto Nikaletewa, kulikua na mtu nje hapo anakaanga chips kuku, wananukia, ikanijia hamu, nikasema ngoja nile kuku, kumtazama vizuri yule mtru nikaona mwiko anaoopolea kuku umekaa kiajabu ajabu, kuutazamavizuri, nikaona umekaa kama mkono wa mtu uliokauka kabisa kwa moto. Nikataka ku panic, ikanijia sauti ya Arsis, ikanambia tulizana, kawaida tu hiyo. Nikanyamaza kimya, nikawa nashangaa shangaa, nikatazama kimgahawa kingine nikaona kuna mwanamke kakaa kama namfahamu hivi, nikasema ngoja nikamuone, kufika nikamuona ni yule mwanamke wa kijini nilijulishwa nae mapangoni kwa babu. Akacheka, akanambia kaa tuongee. Nikakaa.
Jini 1; Umeona mambo yale?
Mimi: Dah, nini kile?
Jin1: mkono wa mtu ule wa siku nyingi sana, umekaushwa ndio umegeuzwa mwiko wa chipsi.
Mimi; na zile chipsi kweli?
Jini 1; pale hakuna kisicho cha kweli isipokua huo mkono tu.
Mimi; Makubwa haya, na maziwa nimeshindwa kuyamalizia.
Jini 1; Maziwa mazuri yale, hayahusiani kabisa na yule mchawi anaechoma chipsi. Uchawi wa kijinga ule, hauna faida yoyote kwake, basi kuaminiushirikina tu. Mkono ule wa maiti, kabla haijaoza umekatwa umekaushwa, wanajua wenyewe wachawi wanavyoukausha. Wanawauzia hawa wanaopenda ushirikina, lakini hauna maana yoyote, wanajipigia pesa za bure tu.
Mimi; Sasa kwanini anautumia?
Jini 1; Wanasema unazidisha ladha ya chakula kikipikiwa na ukipakuliwa na ule mkono, basi mlaji huwezi kuisahau ladha yake, siku nyingine utarudi tu kula tena.
Mimi; Na inakua hivyo?
Jini 1; Ule una faida moja tu kwake, lakini haelewi, faida yake ni wale wanga na wachawi, wakija kununua chpsi wakiuona wanaelewa nini hicho, ndio wanakua wateja wakubwa, maana wao kula nyama za watu ni kawaida kabisa, lakini kwa mtu asie mwanga wala mchawi hauna lolote zaidi ya kiini macho tu, hauoni wala hajui kinachoendelea.
Mimi; Hatari hii.

Jini 1; utayaona mengi, mimi sikuja kwa ajili ya huo mkono, mimi nimekuja kukwambia usiende na hii gari, huyu dreva kaenda kufanya mambo ya kishirikina, hasafiri mpaka apite kwa huyo bibi yake aliekwenda, amtazamie safari itakuaje. Ni ushirikina tu, Nilikua nasubiri ushuke nikufahamishe hilo, wewe chukua mzigo wako uondoke. Mimi nilikua na nyinyi kwenye gari, sikutaka hata wewe unione, ungestuka.
Mimi; Ngoja nikachukue vitu vyangu safari imekua chungu hii.
Jini 1; Mwombe Mungu atakulinda, sisi ni msaada tu lakini mwenye kukulinda wewe na sisi ni Mwenyezi Mungu tu. Tazama kule upande wa pili wa barabara kwenye ile bar.

Nikatazama nikawa siamini ninachokiona.
Mimi; Masanamu yale?
Jini 1; watu wale, hakuna sanamu linaongea namna ile, nenda kawatazame vizuri, utawaona watakukaribisha, wenzako wanataka wateja wale.
Mimi; Wateja wa nini?
Jini 1; Wewe nenda ukajionee, usishtuke na jifanye hujui kitu. Mimi nipo nakungoja urudi nikusindikize upande gari.

Nikasogea, kuna bar pale, wasichana watatu wamekaa nusu uchi kabisa, lakini kwa kawaida unawaona wapo vizuri, kuwatazama kwa macho yaliofunguliwa, ndio nikaona, wana makucha marefu, wachafu sana, nywele zao zipo hovyo hovyo, kwa ufupi wanatisha.

Kufika, mmoja akaanza, "kaka karibu ukae hapa, kuna huduma zote hapa", nikamwambia mimi nilikua namtafuta mtu, kanambia atakua maeneo haya. Akasema "msubiri mpenzi, kaa na mimi hapa" kaa, nikununulie kinywaji gani, usijali mimi nataka mtu wa kuongea nae tu. Wale wengine wananitazama huku wananichekea, chekea, mara mmoja anioneshe maziwa yake, yamelala kabisa, mwengine ajipapase papase mapaja.

Nikatazama kule kwa kwa jini sikumuona lakini nikaona kuna watu wengine wamekaa pale. Nikawaambia ahsanteni niliokua namtafuta nimemuona. Yule mwanamke akanambia, kamuone uje nae basi. mimi sina haja ya pesa zako, nataka nikakufurahishe tu nafanya hata masaji, nitakunyoa, kama unasafiri nikutoe mchoko wote. Nikamwambia, poa wacha nimuone mwenzangu, nitafanya bidii nije nae. Nikaondoka, ile nakaribia pale kwenye kimgahawa naona tule jini anatokea barabara kubwa huku anacheka cheka.

Jini 1: bado upo? Nimeshakupatia mtu atakupakia kwenye gari ndogo. Nimetoka kukutafutia lifti.
Mimi; Wapi?
Jini 1; Pale barabara kubwa kwenye kona, hujaona wale polisi, mmoja wa kike mmoja wa kiume?
Mimi; Nakumbuka niliwaona tulivyokua tunaingia hapa.
Jini 1; Yule mwanamke ana jini la kiume la kichawi linamlinda, nimeongea nalo, majini wa kichawi mimi wananiogopa sana usinione hivi Akacheka. Taayari kasema anajua cha kufanya yule mwanamke akusimamishie gari uende, mimi nimeshaongea nae yule askari, anajua mimi binadam, tena dada yako, haya twende.


Nikaondoka nataka kuelekea kwenye gari nikaona yule msaidizi wa dereva anakuja na begi langu, jini akanambia nishamwambia akuletee begi lako, mwache alibebe mpaka barabarani, nikamwabia, hapana, ni jepesi halina uzito wowote.

Nikachukue begi langu nikamwabia ahsante, nikachukua simu nimpigie yule dereva, nikapiga simu ikawa haipatikani kabisa. Nikaanz akufatana na jini kuelekea barabara kubwa, kufika nakuta yule askari wa kike anaongea na gari iko pembeni, gari ndogo tu.
Askari: Haya mwabie aje, gari hii hapa, mdogo wako handsome, kwanini ulimficha huko?
Jini 21; Wacha utani bwana.
Askari; Sitanii, ataniwachia namna zake, ukiwa unarudi nipigie utakua mgeni wangu.
Mimi ; Nikacheka, unaitia aibu mbelke ya dada hapa.
Askari: usijali, mbo9na dadako yupo poa tu. Hya dereva huyu ndugu yangu, asije kunambia mmemtoza pesa, tena uhakikishe anakula vizuri njiani.
Dereva" Poa afande, leo mbona hujanipa bahasha ya kwenda kwenu?
Askari; Sikupi muhuni wewe, unataka kunichapa.haya nendeni bwana, nipo kazini.

Mimi: Ahsante afande.
Askatri, huondoki hapa nila muiniwachia namna nilizotaka. Nikamtajia namba zangu akapiga wakati huo huo nikawa nimeipata namba yake, Jini akasema mimi jamni mtanishusha Mlandizi hapo, akapanda nyuma. Tukaondoka.

Kufika Mlandizi yule dreva akasimama Jini 1 akashuka, aksema nipe dakika moja tu niongee na mdogo wamgu. Nikashuka.
Jini1; Haya niliingia kuhakikisha kuna usalama, ytuko poa, hehe mwenzzako huyo, safari njjema. Akaondoka huyo, nikaingia kwenye gari tukaanza safari. Nikawa anongea ongea na dereva, akanambia bro tutasimama kidogo Chalinze ninunue zawadi pale kama kuna mananasi na machungwa. Mie kwetu Dodoma, lakini napeleka hizi gari za transit Bujumbura. Sikai sana Chalinze,

Mimi; Poa, usijali tuko pamoja.

Itaendelea.
 
😂😂😂😂😂😂😂..... Haya mambo huwa yapo hvyo, ukisikia lazima uone ni kamba!!!

Siku nikiamka vizuri ntaleta kisa changu hapa.
(Maana mm nilikabidhiwa kwa mashetwan toka nikiwa mdogo, baadae wakasalitiwa nikanyang'anywa mikononi mwao ilikuwa n vita kali sana..... Wakamgeuka mzee wangu wakamuua kikatili, mzee akaona ni bora yeye afe kuliko mwanae awe mfalme wa mashetwan na wachawi🚶🚶

Siku moja nikiamka vizuri ntaisimamisha jf kwa muda😂

Maana ni visa vya mfululizo kwanzia miaka 4 mpk Sasa hivi nnavyoandika hii comment bado vita inaendelea 🏃
Tutafurahi kukusoma kisa chako. Hivi vitu vya viumbe visivyoonekana, ambao hawajakutana navyo hawawezi kuamini.
 
Inatokea post namba 179;


Kufika Chalinze nikamwambia dereva, twende upande ule kuna mama nafahamiana nae wa Kisomali, atatupatia vitu unavyotaka kwa bei poa.
Dereva; kwa Sofi msomali?
Mimi; Ndio hapo hapo.

Dereva; hapo ndipo napokwenda mimi, nachukua mirungi kwake, ananipa na mzigo wake unaoenda Morogoro na Dodoma, bro hizi kazi ukitegemea kusafirisha magari tu haya ya transit hazilipi. Tunajitahidi kama hivyo kama zipo order hapo, napakia.


Basi tukaingia kwa Sofia tukamkuta hayupo, yupo mwanamke mwengine wa Kisomali, na yeye ni wa Tanga, anaongea Kitanga. Nikasalimiana nae, nikamuuliza Anti Sofia hayupo?

Msomali; Anti yako Sofia siku nyingi kahamia Dar, mimi ndio nipo hapa siku hizi, mimi ndugu yake, watoto wa baba mkubwa na mdogo. Kwa hio upo na Anti Halima sasa. Hujapita hii njia siku nyingi? Sijawahi kukuona hapa.

Mimi; kweli, mimi sio mtu wa kupita sana njia hii, isipokua babangu anapita sana.
Halima; Anaitwa nani?
Mimi; Nikamtajia jina la mzee.
Halima; Usinambieeeee, ndio naona hizi sura nimeziona wapi? babako na mamako tumekua wote Tanga, tunajuana sana.
Mimi; Ndio wao wamenijulisha kwa Anti Sofia.
Halima; Wewe mtoto wa nyumbani kabisa, ngoja nimpigie mamako akwambie.

Halima akaanza kupiga simu akawa anaongea, namsikia anamwambia mama, ngoja nikupe surprise we malaya wa Kidigo.

Mimi: Haloo.
Mama; eeeh upo Chalinze? kweli hii surprise ya mwaka, mimi najua saa hizi labda ushafika Dodoma.
Mimi; Tulisimama kwa muda njiani, dereva alikua na kazi zake.
Mama; Nipe huyo Halima.

Sijui wakaongea nini pale, mwisho namsikia Halima anamwambia "huyu leo haendi popote, nimemkosa babake, yeye simkosi, nipo tayari hata kutuma vijana watie pancha gari lao". Nenda zako huko niwache kwa raha zangu, usinimalizie salio langu, kwaheri bwana, baadae. Akakata simu.

Halima; Umeamini sasa kama mamako ni rafiki yangu? Wewe mwanangu, kaa hapo unywe chai. Nikamwambia kahawa Anti. Akasema kahawa kama babako? Ngoja.

Akamwita mtu kwa ndani, akaleta chupa ya kahawa vikombe na visheti. Dah mtoto alieleta alikua wa Kisomali lakini bomba kweli, ingawa kavaa madiraa ya Kisomali, lakini anaonesha moto kweli.

Halima; Huyu mtoto wa dadangu, amepita tu hapa akaona abaki siku mbili anisaidie. Anakwenda Tanga, anaishi Dar huyu. Wewe si unaishi Dar? Mimi; ndio.

Halima; hamjuani?
Mimi; sijawahi kumuona.
Yule bintiu akasema, mimi namjua huyu, yeye kanisahau, wewe si kakake Nisha? Akamtaja jina wife wangu. Nikamwambia, huyo mke wangu.
Binti; Nilisikia, kumbe ni wewe mumewe, mimi namjua mamako pia, namjua na babako. Ma Shaa Allah Handsome kama babako,

Wewe tukija kwenu hatukukuti, miaka mingi mimi napajua kwenu, Ilala.
Halima; Si nimekwambia, wewe mtoto wa nyumbani, leo huondoki unabaki hapahapa.
Mimi; Leo siwezi nimetumwa kuna gari ya watu huko inaningoja mimi.
Halima; ukirudi basi usisahau kupita nikupe mzigo wa mamako.
Mimi; Poa anti.

Mara dereva akaja, akasema alienda kupiga rakaa msikitini.

Mimi; Ungenambia na mimi tungeenda wote,
Dereva; usijali utasali safar. Bi Halima, mzigo upo leo?
Halima; Upo wa Moro tu, ngoja niwaambie wautoe, sogeza gari basi.
Dereva; Usijali, nanunua mananasi na machungwa nakuja kupakia huo mzigo wako kwanza, juu yake naweka mananasi na machungwa.

Akaenda kwenye mananasi,nikamfata, kumuona muuza mananasi nikamkumbuka na yeye akawa ananitazama kama kaniona mahali hivi. Nikamwacha yule dereva ananunua mananasi, mimi nikajiambia sina wa kumpelekea zawadi nitachukua matatu ya kula mwenyewe. Ngoja nikanunue machungwa.

Nikaelekea kwenye machungwa, nikamkuta yule mzee rafiki yake baba, kuniona kanitazamaaa akanikumbuka. Aaah Simba umekuja tena?Ulituwachia bonge la kasheshe hapa, hebu twende kwanza tukaongee pale kwenye kahawa, maana babako anasema yeye haelewi chochote.

Machungwa yako yapo usijali, wewe staff hapa. Unataka na mananasi mangapi? Nikamwambia matatu tu sio makubwa sana, ya kula mimi tu njiani, akanambia, hayo umepata usijali. Twende tukanywe kahawa kwa Sofia, aah siku hizi yupo ndugu yake anaitwa Halima lakini sisi tumezowea kwa Sofi.

Tukaenda tukawa tunakunywa kahawa, kaanza. Basi siku ile bwana wale wanawake hawakutoka ndani, wakajaa wachawi usiku kucha wamefanya kila njia wameshindwa kutoka, mpaka asubuhi watu wakasema waitwe polisi. ,Maana watu wameshajazana na hawajui kwanini wanawake wameshindwa kutoka, ndani, kila mmoja na lake.

Basi akatokea mwanamke mmoja akasema niwacheni niongee ngee nao, akaingia ndani akaongea nao kama nusu saa, hajaulikana kapitia wapi, wale ndio wakatoka ndani, hawakuonekana tena mpka leo Chalinze hii, na hapa ndio imekua dawa, wanga qnapaogopa kama ukoma. Hebu nambie, umerithi mikoba ya babu yako? Nambie kweli bwana.
Mimi; Sijui, labda baba, mimi sikufanya kitu.
Machungwa; Ndio inavyokua hivyo una mavitu ya babu yako makubwa makubwa,babako mimi angenambia, asingenificha kitu, kakangu ndio anasimamia mashamba ya bibi yuako Muheza, umezindikwa wewe zindiko la simba la Kidigo, tutazamie kama kuna wengine wamejileta leta, uwakomeshe, sisi tunataka amani hapa.

Mimi nikawa nacheka tu. mara dereva akarudi na mananasi, nikamwabi huyu hapa ukitaka kununua machungwa atakupa best. Yule dereva akamwambia nataka pakacha ndogo tatu, usinipige tikitaka lakini.
Machungwa: Wewe upo na mwamba huyu nani akuchezee tikitaka? Naleta pakacha nne, lipia tatu zako tu, moja zawadi ya huyu mwamba, nawaambia na wenye mananasi wamletee mnanasi yake. Nikaagana nae, nikaona nimeletewa mananasi matano badala ya matatu na machungwa pakacha moja kubwa. Nikamwabia aliyeyaleta mwambie ahsante sana, Akasema namwambia, lakini mwenye mananasi anakuja mwenyewe, anasema amekuona lakini alikusahau.

Kidogpo akaja mwenye mananasi. Dah kijana, weewe muokozi wetu, pokea zawadi ya mananasi kutoka kwangu matatu na kutoka kwa jirani yangu mawili, tena ukichelewa kidogo utazungukwa na watu sasa hivi, Kile kisa kila mtu anakihadithia mpaka leo. Ule mkasa mzito

Halima; Kumbe ilikua ni wewe, alinambia Sofia, akaanza kucheka, Wadigo wa Tanga mna mambo nyinyi. Hayasemeki. Lakini tumeambiwa umefanya la maanna sana, watu wanachezeana sana hapa.

Drerva kaamka akasogeza gari kwa reverse, ukatiwa mzigo wa Halima halafu yakajazwa mananasi na mapakacha ya machungwa nyuma, tukaanza tena safari.

Inatokea post namba 181:

Tulivyofika mdaula, dereva akanambia mshikaji, kama unataka kusali, msikiti mzuri ule pale. Mimi nataka nile kidogo, ukisha sali njoo tule. Nikamwambia poa, twende nikaone kuna nini, mimi nimekula visheti vingi kwa Sofia.
Dereva: Kula mshikaji, mwili wako wa mazoezi huo unataka ule vizuri. Hapa kuna nyama nzuri sana, huyu Mwarabu anajua kutengeneza mbuzi, mie huwa napiga supu ya mbuzi hapa kila nikipita.

Tukaingia hoteli, ilikua imejaa watu, jamaa anaonesha ana chakula kizuri ingawa hoteli ni ya kizamani zamani. Nikaenda counter, jamaa yangu yeye kaagiza supu ya mbuzi na chapati, nikawauliza wana supu aina nyingine, wakanambia, ipo ya ng'ombe, nikamwambia mimi nitilie hiyo lakini naipiga kavu. Sitaki chapati. Akanambia kakae, nakuchagullia mwenyewe mnofu. Alikua mtu mzima hivi Mwarabu.

Tukawa tunakunywa supu pale, mara nikapigiwa simu, alikua yule dereva niliemuacha pale mbele ya kongowe. Akanambia nimeambiwa umetangulia bwana, bora bwana, ningekuchelewesha, mimi bado nipo, leo naona siondiki, si unajua waifu ytena, kanizuwia mpaka kesho. Ukifika nijulishe basi. Uko wapi sasa? Nikamwambia mimi ndio kwanza nipo Mdaula, tumekaa sana Chalinze. Sawa poa. Tutawasiliana zaidi.

Dereva; Mshikaji hebu nipe kisa, maana leo Chalinze nimeuziwa machungwa na mananasi kama bure. Kumbe unafahamiana sana na Sofi?

Mimi; Sio mimi, Sofi anafahamiana na wazazi wangu, mimi simjui sana.
Dereva: Yule ndio tajiri yangu, ana roho nzuri sana yule mama, hizi biashara mimi alinipa yeye, kuniona vile mtu wa mkeka, hata huyu tajiri nnaempelekea magari yake Burundi kaniunganisha nae yeye pia. Jana nilienda kumsalimia kwake na kumuuliza kama ana salamu zozote, akaniombea dua nifike salama. Mama poa sana yule, ndio maana Mungu anamfungulia. Yule mama nusu ya Chalinze alikua anaisaidia. Yule hata Kikwete anamjua, akipita hapa lazima anywe kahawa kwake. Mtu wake sana yule mama. Sofia maarufu sana, halafu yule mimi nakwambia sio Msomali yule. Yule hata sijui ana roho ya wapi, yeye kila mtu anacheka na kufurahi nae. Akija utafikiri kaja malkia. Watu wanavyojazana.


Dereva; Lakini mshikaji, kisa nilichokisikia juu juu pale kwenye mananasi, hebu nipe mshikaji wangu.

Tukamaliza kula ile tunaondoka tu, nambie ilikuaje mshikaji?

Mimi; Hata sikjui lakini kuna wanawake kumbe walikua mmoja anauza chakula uchi nje hapa, mmoja alikua na kiduka kidogo nae hivyo hivyo. Sasa siku hiyo bahati mbaya wakaumbuka na mimi nilikuwepo na mzee.

Ikawa huyu wa nje kaingia mule ndani dukani, ikawa anashindwa kutoka, sisi tumeondoka, ndio leo nimesikia walikaa mpaka siku ya pili asubuhi akaja mwanamke mwengine kuwatoa.
Drereva: Hilo litakua kubwa lao hilo, lina maujuzi kweli kweli. lakini mshikaji watu wote wanaamini wewe ndio ulifanya mambo, wanasema wale wanga wenyewe walikua wanalia wanaomba urudishwe uje kuwafungua.

Nambie mwanangu manake kwetu huko wanga na wachawi wengi sana. Mimi kinachonisaidia ibada mwanagu.
Mimi: Hakuna zaidi ya ibada.
Dereva; mwanagu mimi siachi kusali na kila siku lazima nisome Qur'an, Nashukuru wazazi wangu walitusisitiza tusome madrasa. Sisi nyumbani bwana amabae hajasoma sana ni mimi, lakini msahafu haunipi shida kabisa kuusoma Kiarabu, sema wenzangu wale wamefika mbali, maana madrasa ipo hapo hapo kwetu. Pale pale ulipopanda, kuna kijiji ka ndani kidogo, sio mbali na barabara, ndio kwetu, ukipita siku yoyote pita uwaone wazee, uone na tunavyoishi, ndio kujuana kwenyewe hivyo.


Mimi; Nakuahidi nitapita hata kama wewe haupo mradi kuna madrasa, nitakwenda nipate dua za watoto, dua za watoto nzuri sana, wanakua wanaomba kwa nia kabisa.

Dereva; Poa mshikaji, Pita tu wakati wowote, halafu si naliona lile afande lanajigonga gonga kwako, Nuksi kweli yule, anajiona sana kwa lile kalio lake. Nasikia mali ya mkubwa wa TRA pale checkpoint ndio piga ua handishwi pale ulipomkya, wenzake wote wanaondoshwa yeye yupo, mpaka katujua sura zetu wote. Usinwache yule, anahela kama nini, yule kila gari ikipita pale lazima imwachie kitu,, na ukijifanya mbishi anakucheki unaelekea wapi, anapiga simu bele huko, utakoma ubishi, hapingwi na mtu yule. Lkini mshikaji leo kakukubali yule mpaka kajifanya mshikaji wangu, si amekupigia unayo namba yake?
Mimi; Ndiyo.

Dereva; Ujiko huo, usimwache kabisa yule.
Mimi; Mimi mshikaji nina mke wangu halafu yule sio sampuli yangu kabisa.
Dereva; Yule kishakudondokea, lina hela lile, wewe lile unalichuna tu. Yule usimuone vile, ana daladala zake zinapiga Mbezi Mlandizi. Mshikaji ana hela yule halafu anaogopewa hata na maaskari wenzake. Mie nakwambia usimwache yule.

Mimi; Sasa mshikaji wewe mtu wa ibada unanifundisha usheatani?
Dereva; Wewe hujui anavyotupa tabu yule.
Mimi; Nitaongea nae usijali, chukulia hasumbui tena.
Dereva; Nakuaminia mwanangu. Halafu yule dada anaonesha mshikaji wake sana, yule tumemshusha mlandizi, Sijui na yule askari mwenzake?
Mimi; Yule kanambia anajuana nae tu, aliniombea lifti tu. Kuna dereva wa lori kaniwacha pale, Isingekua yule dada ningehangaika sana.

Dereva; Wewe ukiona mambo yanakunyookea hivyo inatakiwa usali kwa kumshukuru Mungu, wewe ni mtu mwema mwanangu, si unaona Chalinze mwenyeji kuliko mimi ninaepita siku zote pale. Muombe Mungu sana akuzidishie kua mwema.

Ya yule mwanamke nilikua naongea kwa hasitra tu, usinisikilize mshikaji, usifanye kuzini, wewe una mke bwana.
Mimi; Poa poa, naona hasira zimekwisha.
Dereva; Hivi nikiwafikiria wanavyotuhangaisha, wewe utaona, mpaka tufike tutasimamishwa zaidi ya mara mia, na leo bahati yetu wale wa mdaula naona wametuona tunatoka kula wametuwacha tu.
Mimi: Au yule afande kawapigia simu?
Dereva; Yule ujanja wake unaishia Mlandizi. mungu katusaidia.


Itaendelea.
 
Inagtokea post namba 174.

Maisha yakaendelea, koo za ki simba na mambo na nidhami, zake ambazo sitaki kuzihusisha sana na hiki kisa cha viumbe wasioonekana.

Kitu kimoja kingine muhimu kilinitokea safarini, nilikua nasafiri na gari kubwa, nimepewa lift na mteja wetu mmoja tunaemtengezea gari zake, alikua anaelekea Mwanza na mimi naelekea Shinyanga kwa kazi nilotumwa na mzee, kazi zetu za ufundi.

Tumeondoka Dar vizuri Alfajiri sana, dereva akanmbia ana mke mdogo hapo mbele kidogo ya Kongowe , Kibaha.ka hiyo atasimama hapo kwa muda awasalimie, mimi kama ninaharaka sana atanitafutia lifti hapo check point ya TRA ndipo alipo paki gari, alisema hapo kuna usalama zaidi kwa gari. Nikamwabia, wewe nenda tu, nikiondoka nitakupigia simu. Akachukua boda boda akamwacha kwenye gari utingoi wake na mimi nikashuka, kuna vijimgahawa vingi vingi tu, pako na heka heka nyingi za hapa na pale.

Nikaingia kwenye kimgahawa kimoja, nikaagiza maziwa ya moto Nikaletewa, kulikua na mtu mje hapo anakaanga chips kuku wanaukia, ikanijia hamu, nikasema ngoja nile kuku, kumtazama vizuri yule mtru nikaona mwiko anaoopolea kuku umekaa kiajabu ajabu, kuutazama umekaa kama mikono ya mtu iliokauka kaboisa kwa moto. Nikataka ku panic, ikanijia sauti ya Arsis, ikanambia tulizana, kawaida tu hiyo. Nikanyamaza, nikatazama kimgahawa kingine nikaona kuna mwanamke kakaa kama namfahamu hivi, nikasema ngoja nikamuone, kufika nikamuona ni yule mwanamke wa kijini nilijulishwa nae mapangoni kwa babu. Akacheka, akanambia kaaa tuongee. Nikakaa.
Jini 1; Umeoina maboi yale?
Mimi: Dah, nini kile?
Jin1: mkono wa mtu ule wa siku nyingi sana umekaushwa ndio umegeuzwa mwiko wa chipsi.
Mimi; na zile chipsi kweli?
Jini 1; pale hakuna kisicho cha kweli isipokua huo mkono tu.
Mimi: Makubwa haya, na maziwa nimeshjindwa kuyamalizia.
Jini 1; Maziwa mazuri yale, maziwa mazuri yale, hayahusiani kabisa na yule mchawi anaechoma chipsi. Uchawi wa kijinga hauna faida yoyote kwake, basi kuamini tu, mkono ule wa maiti, kabla haijaoza, umekaushwa, wanajua wenyewe wachawi wanavyoukausha. Wanawauzia hawa wanaopenda ushirikina, lakini hauna maana yoyote.
Mimi; Sasa kwanini anautumia?
Jini 1; Wanasema unazidisha ladha ya chakula kiki[pikiwa na ukipakuliwa na ule mkono basi mlaji huwezi kuisahau ladha yake, siku nyingine utarudi tu kula tena.
Mimi; Na inakua hivyo?
Jini 1; Ule una faida moja tu kwake, lakini haelewi, faida yake ni wale wanga na wachawi, wakija kununua chpsi wakiuona wanaelewa ndio wanakua wateja wakubwa, maana wao kula nyama za watu ni kawaida kabisa, lakini kwa mtua siye mwanga wala mchawi hauna lolote zaidi ya kiini macho tu, hauoni wala hajui.
Mimi; Hatari hii.
Jini 1; utayaona mengi, mimi sikuja kwa ajili ya huo mkono, mimi nimekuja kukwambia usiende na hii gari, huyu dreva kaenda kufanya mamboi ya kishirikina, asafiri mpaka apite kwa huyo bibi yake aliekwenda amtzamie safari itakuwaje. Ni ushirikina tu, Nilikua nasubiri ushuke nikufahamishe hilo, wewe chukua mzigo wako uondoke. Mimi nilikua na nyinyi kwenye gari, sikutaka hata wewe unione, ungestuka.
Mimi; Ngoja nikachukue vutu vyangu safari imekua chungu hii.
Jini 1; Mwombe Mungu atakjulinda, sisi ni msaada tu lakini mwenye kukulinda wewe na sisi ni Mwenyezi Mungu tu. Tazama kule upande wa pili wa barabara kwenye ile bar.

Nikatazama snikawa siamini ninachokiona.
Mimi; Masanamu yale?
Jini 1; wati wale, kuna sanamu linaongea namna ile, nenda kawatazame vizuri, utawaona watakukaribisha, wenzako wanataka wateja wale.
Mimi; Wateja wa nini?
Jini 1; Wewe nenda ukajionee, usishtuke na jifanye hujui kitu. Mimi nipo nakungoja urudi nikusindikize upande gari.

Niaksogea, kuna bar pale, wasicha watatu wamekaa nusu uchi kabisa, lakini kwa kawaida unawaona wapo vizuri, kuatazama kwa macho yaliofunguliwa, ndio nikaona, wana makucha marefu, wachafu sana, nywele zao zipo hovyo hovyo, kwa ufupi wanatisha. Kufika, mmoja akaanza, "kaka karibu ukae hapa, kuna huduma zote hapa", nikamwabia mimi nilikua namtafuta mtu, kanambia atakua maeneo haya. Akasema "msubiri mpenzi, kaa na mimi hapa" kaa nikununulie kinyaji gani, usijali mimi nataka mtu wa kuongea nae tu. Wale wengine wananitazama huku wananishekea, chekea, mara mmoja anioneshe maziwa yake, yamelala kabisa, mwengie ajipapase papase mapaja.

Nikatazama kule kwa kwa jini sikumuona lakini nikaona kuna watu wengine wamekaa pale. Nikawaambia ahsanteni niliokua namtafuta nimemuona. Yule mwanamke akanambia, kamuone uje nae basi. mimi sina haja ya poesa zako, nataka nikakufurahishe tum nafanya hata masaji, nitakunyoa, kama unasafiri nikutoe mchoko wote. Nikamwabia pao, wacha nimuone mwenzangu, nitafanya bidii nijae nae. Nikaondoka, ile nakaribia pale kwenye imgahawa naona tule jini anatokea barabata kubwa huku anacheka anacheka.

Jini 1: bado upo? Nimeshkupati mtu atakupakia kwenye gari ndogo. Nimetoka kukutafutia lifti.
Mimi; Wapi?
Jini 1; Pale barabara kubwa kwenye kona, hujaona wale polisi, mmoja wa kikwe mmoja wa kiume?
Mimi; Nakumbuka niliwaona tulivyokua tunaingia hapa.
Jini 1; Yule mwanamke ana jini la kiume la kichawi linamlinda, nimeongea nalo, majini wa kichawi mimi wananiogopa sana usinione hivi Akacheka. Taayari kasema anajua cha kufanya yule mwanamke akusimamishie gari uende, mimi nimeshaongea nae yule askari, anajua mimi binadam, tena dada yako, haya twende.


Nikaondoka nataka kuelekea kwenye gari nikaona yule msaidizi wa dereva anakuja na begi langu, jini akanambia nishamwambia akuletee begi lako, mwache alibebe mpaka barabarani, nikamwabia, hapana, ni jepesi halina uzito wowote.

Nikachukue begi langu nikamwabia ahsante, nikachukua simu nimpigie yule dereva, nikapiga simu ikawa haipatikani kabisa. Nikaanz akufatana na jini kuelekea barabara kubwa, kufika nakuta yule askari wa kike anaongea na gari iko pembeni, gari ndogo tu.
Askari: Haya mwabie aje, gari hii hapa, mdogo wako handsome, kwanini ulimficha huko?
Jini 21; Wacha utani bwana.
Askari; Sitanii, ataniwachia namna zake, ukiwa unarudi nipigie utakua mgeni wangu.
Mimi ; Nikacheka, unaitia aibu mbelke ya dada hapa.
Askari: usijali, mbo9na dadako yupo poa tu. Hya dereva huyu ndugu yangu, asije kunambia mmemtoza pesa, tena uhakikishe anakula vizuri njiani.
Dereva" Poa afande, leo mbona hujanipa bahasha ya kwenda kwenu?
Askari; Sikupi muhuni wewe, unataka kunichapa.haya nendeni bwana, nipo kazini.

Mimi: Ahsante afande.
Askatri, huondoki hapa nila muiniwachia namna nilizotaka. Nikamtajia namba zangu akapiga wakati huo huo nikawa nimeipata namba yake, Jini akasema mimi jamni mtanishusha Mlandizi hapo, akapanda nyuma. Tukaondoka.

Kufika Mlandizi yule dreva akasimama Jini 1 akashuka, aksema nipe dakika moja tu niongee na mdogo wamgu. Nikashuka.
Jini1; Haya niliingia kuhakikisha kuna usalama, ytuko poa, hehe mwenzzako huyo, safari njjema. Akaondoka huyo, nikaingia kwenye gari tukaanza safari. Nikawa anongea ongea na dereva, akanambia bro tutasimama kidogo Chalinze ninunue zawadi pale kama kuna mananasi na machungwa. Mie kwetu Dodoma, lakini napeleka hizi garu za transit Bujumbura. Sikai sana Chalinze,

Mimi; Poa, usijali tuko pamoja.

Itaendelea.
Daah shukran sana ndo namaliza kusoma hapa ulipoishia alfajir hii, napata funzo kubwa sana kuhusu ulimwengu usioonekana. Naamini kabisa hasa kulingana na uzoefu wa nloyapitia mpaka Sasa. Nakusubir
 
Back
Top Bottom