Etugrul Bey
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 6,514
- 15,247
Staring kakimbiaNaona huu uzi umejifia kifo cha mende
Arsis yupo, majukumu ni mengi sana.Staring kakimbia
Upo hai, ni mimi majukumu yameizidi kimo sipati muda wa kuingia hapa, nipo sana tiktok.Naona huu uzi umejifia kifo cha mende
Ni kweli kabisa, majini ni wengi kuliko binadam. Walikuwepo kabla ya binadam na wanaishi miaka mingi zaidi ya binadam.Uzi umejaa majini tupu
Huyo "mkinda wa buguruni" simfahamu. Unataka ushahidi kwenye lipi?"Hatufuati maneno ya majini hata Kama wanadai kuwa waislamu" haya ni maneno yako naomba nikuulize swali wewe una mamlaka gani katika dini hii ya uislamu kufikia hatua ya kusema hayo? Ikiwa Allah amekubali kuwa majini kuwa waislamu Mimi Nani nipinge? Alafu si kila jini ni shetani hata binadamu anaweza kuwa shetani (ushetani ni matendo maovu yanayomchukiza Allah). Allah anasema sikuumba majini na wanaadamu Ila waniabudu, je majini wanamuabudu Allah kwa Imani ipi? Kitabu kipi? Wanafuata mtume yupi kwa uma huu? Qurani hiyo ambayo wewe unasisitiza tuifuate ndio imetupa habari na hadithi za majini mfano kisa cha Nabii Suleimani,majini wapo na walitumiwa na Suleimani. Si kila jini ni muongo au shetani,Qurani ndio kila kitu hata majini waislamu wanafuata Qurani na Sunnah za mtume au umesahau kuwa Mtume ni rehema kwa viumbe vyote?
Alafu suala la Arsis kuzungumzia Nabii Isa na Bikra ya Mariam ulitakiwa utoe ushahidi wa kimaandiko na sio kuongelea pembeni Kama mkinda wa buguruni!
Upo sahihi kwa kiwango fulani.Allah (Subhaanahu Wa Ta'ala) ndio kawazungumzia, kawanukuu. Na Allah ni Mkweli na Yeye ana habari zote, Yeye Allah ni Mjuzi wa kila kitu. Wale majini waliamini walipoisikia Qur'an na Allah akamfunulia hilo Mtume wake katika Qur'an na kumpa habari hiyo na Allah akatuambia waliyoyasema. Ni Allah ndio ametupa habari ile.
Tunaifuata Qur'an na Sunnah iliyothibiti kwa ufahamu wa wema waliotangulia (Maswahaba na walioifuata njia yao katika vizazi vitatu bora vya kwanza).
Hatufuati manenomaneno ya majini hata kama watadai kuwa ni Waislam.
Sisi tumeshatoshelezwa, tunayo Qur'an, aliletwa Mtume Muhammad (Swala na Salamu ziwe juu yake) aliyeteremshiwa hiyo Qur'an akaifikisha na kuifundisha hiyo Qur'an na akatufikishia Dini ya Allah kama alivyofunuliwa na Mola wake.
Mtume akatuamrisha yale yote yatakayotuweka karibu na Pepo na kutuweka mbali na Moto, na akatukataza kila litakalotuweka karibu na Moto na kutuweka mbali na Pepo.
Na walikuwepo Maswahaba zake (Allah awaridhie wote) ambao walizichukua Qur'an na Sunnah, wakafundishwa na Mtume na wakazifahamu na Maswahaba wote wanajulikana. Na tukatakiwa kufuata njia yao na ufahamu wao. Na wao ndio wakazifundisha Qur'an na Sunnah kama walivyomsikia Mtume na kumuona Mtume. Walikuwa kama hawakuelewa jambo wanamfuata Mtume kumuuliza na Mtume anawafafanulia na haya yamepokelewa na kuhifadhiwa.
Ametuacha Mtume Muhammad (Swala na Salamu ziwe juu yake) katika njia nyeupe kabisa.
Wala hatuwafuati majini kuchukua Elimu kwao. Huwezi ukasema naenda kusoma Dini kwa jini. Na wala haifai kuwatumia majini.
Hivi unajua kuwa haipokelewi riwaya ya jini (mapokezi kutoka kwa jini)? Hakuna hadith ya Mtume iliyopokelewa kutoka kwa jini.
Kuna misingi ya kupokea habari tumepewa. Waislam tuna misingi ya kupokea khabari na riwaya.
Na jini haichukuliwi riwaya kutoka kwake. Kwanza utamchunguzaje jini ili ujue hali yake? Utajuaje kama ni thiqah ama la? Ni mkweli ama muongo? (na wengi ni waongo waki take advantage ya maumbile yao).
Sikuambii anayesema uongo wa wazi wazi kama huyu anayejiita Arsis. Mtu anakuambia kabisa eti kaambiwa na shaytwaan wake kuwa Bibi Maryam hakuwa bikra kabla ya kumzaa Nabii Issa (Amani iwe juu yake) na kwamba Nabii Issa (Amani iwe juu yake) sio mtoto wake wa kwanza, haya ni maneno yaliokuwa kinyume kabisa na wahyi (Qur'an na Sunnah).
Ndio maana kuna watu wanakuja na mambo ya ajabu ajabu unajiuliza wanayatoa wapi haya mambo ambayo yako mbali kabisa na Uislam! Kumbe wanadanganywa na mashetani wa kijini. Wengine wanaoteshwa na mashetani halafu wanakuja na mambo ya uzushi anakuambia kaota ndotoni.
Tubaki katika Qur'an na Sunnah iliyothibiti juu ya ufahamu wa Salafu Swaalih.
Tumche Allah ndugu zangu.
Mimi nimefikisha. Naondoka humu.
Unajua kuna siku moja kuna group moja la dini niliona tiktok nikaona jina lako,kumbe ni weweUpo hai, ni mimi majukumu yameizidi kimo sipati muda wa kuingia hapa, nipo sana tiktok.
Unaharibu uzi wa watu kwa kuweka mabandiko marefu yasioeleweka, fungua uzi wako unaohusiana na makanisa, hapa tunasoma habari za majinni.Sasa Nachotaka Ufute mawazo yote uliyowahi Kuambiwa na Dini Kuhusu Haya makanisa..
Kila Siku huwa Namwambia hata Mchungaji wa Jf Rabboni Kuwa biblia Imesukwa na Kuandikwa Kwa Codes nyingi sana..
Nitaanza Kanisa Moja Moja Mpaka Mwisho..
Tuanze na Kanisa La Efeso UFUNUO 2:1:-
Cha Kwanza Kabisa Ujumbe Huu wengi wanaamini kabisa Uliandikwa Kwa Malaika Wa makanisa fulani kama Efeso na Mengineyo..
Lakini hebu Tuangalie Maana Ya maneno Yaliyotumika..
Kwakuwa Mwandishi wa Ufunuo Kiasili aliandika kwa Lugha ya Kiyunani(kigiriki) tutaanza kwa Kucheza Humo Ili Tulainishe maana Kabla ya Kuanza Kuichambua Vizuri..
Ufunuo 2:1..
Τῷ ἀγγέλῳ τῆς ἐκκλησίας ἐν Ἐφέσῳ γράψον· Τάδε λέγει ὁ κρατῶν τοὺς ἑπτὰ ἀστέρας ἐν τῇ δεξιᾷ αὐτοῦ, ὁ περιπατῶν ἐν μέσῳ τῶν ἑπτὰ λυχνιῶν τῶν χρυσῶν·
WAnaitamka Hivi...
Tō angélōs tēs ekklēsí en Ephesō grápson: Tade légei ho kratōn tous heptá astéras en tē dexiá autou, ho peripatōn en mésō tōn heptá lychniōn tōn chrysōn.
Tafsiri yake kwa Lugha ya Malkia (lugha ya mayai):
"To the angel of the church in Ephesus write: 'These are the words of Him who holds the seven stars in His right hand and walks among the seven golden lampstands
Neno ἀγγέλῳ (Angelos) kwa Kigiriki lilitafasiriwa Kama Mjumbe Mpaka ilipofika karne ya 4 Baada ya Kuenea Kwa Ukristo walipoamua Kuwa Litafasiriwe kama malaika kwa sababu nao ni Wajumbe wa Mungu..
Ila Neno Hilo Asili yake ni Mjumbe So Badilisha Hiyo neno Malaika Weka Neno Mjumbe au Mpeleka Taarifa..
Neno ἐκκλησίας (ekklēsías) ambalo limetafasiriwa kama Kanisa ni neno la Kigiriki ambalo Linamaanisha Mkusanyo au Mkusanyiko au Mjumuisho au Kutaniko.. na Wala si lazima Liwe katika Muktadha wa Dini...
(Unaweza Ukayahakiki maneno kwa Sehemu Yoyote Ukitaka.)
Sasa Tufanye Mabadilko Kwenye Neno Kanisa Tuweke Mjumuiko au Mkutano au Kutaniko na kwenye Malaika tuweke Mjumbe..
Ufunuo wa Yohana 2:1
"Kwa mjumbe (Mtoa taarifa) wa Kutaniko (Jumuiko) la Efeso andika; Haya ndiyo anenayo yeye azishikaye hizo nyota saba katika mkono wake wa kuume, yeye aendaye katikati ya vile vinara saba vya dhahabu."
Na hiyo Ndiyo Ilipaswa Kusomeka Hivyo kwa Kiswahili..
Kufika Hapo Nadhani Umenielewa Sasa Twende kwe ye Nyota saba na Vinara saba..
Unafahamu Chochote Kuhusu Menorah?
Iliyokuwa Inakaa Kwenye Hekalu la Mungu Yerusalem na Kwenye Tabernacle ?
Ilikuwaje?
Hii Hapa Chini..
View attachment 3169285
Sasa Biblia inapozungumzia Vinara vya dhahabu inamaanisha Menorah nadhani umeshawahi kuiona Sana hii..
Chimbuko Lake..
Kutoka 25:37-38
"Nawe zifanye taa zake saba; nao wataziwasha hizo taa zake, zitoe nuru mbele yake.
Na makoleo yake, na visahani vyake, vyote vitakuwa vya dhahabu safi."
Kwenye Quran Pia Unaweza Ukasoma Kwenye
Surah An-Naba aya 12
وَبَنَيْنَا فَوْقَكُمْ سَبْعًۭا شِدَادًۭا
وَجَعَلْنَا سِرَاجًۭا وَهَّاجًۭا
Inatamkwa Hivi..
Wabanayna fawqakum sabAAan shidadan
WajaAAalna sirajan wahhajan
Maana Yake..
Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?
Na tukajalia kati yake Mianga
Umeona hata kwenye Quran?
Kwahyo Kumbe Kwenye Hivyo vinara Vilivyojengwa Kuna Mianga 7...
Sasa Lets see What is These 7 lamp au Menorah?
Unafahamu Chochote Kuhusu Chakrah 7 za Mwili wa Binadamu kiroho?
Ziko Chakra 7 Ambazo ndo Muongozo wa Ukuaji Kiroho kuanzia Chakra ya Chini kabisa Root chakra mpaka Chakra ya Juu Crown chakra..
Crown chakra Au Chakra ya Taji ni chakra ambayo humuunganisha Moja kwa Moja Muhusika na Nguvu ya Juu sana ya Kiroho unaweza Ukaita Mungu au Vyovyote utakavyoita..
Hujawahi Kusikia Watu wakiimba..
🎶Tukimaliza Kazi tutavalishwa Taji🎵
Wengi Huwa wanaimba wakifikiri kuna Siku watakuja Kuvalishwa Taji kama Ya Kifalme..
Hiyo inamaanisha Ukivumilia Katika Kiroho mpaka Mwisho utafika Kwenye Crown Chakra..
Sasa twendelee..
View attachment 3169340
Sasa Upi Uhusiano Huu na Fungu la Ufunuo 2 mpaka 3..
Au Makanisa hayo..
Tuanze na Tabia za Mtu aliyefungua Chakra ya kwanza au root chakra..
Tuanze na maana Yake kama Ilivyoandikwa Hapo "I AM"
Moja..
Sasa Mara Nyingi Mtu anapofungua ama Kuanza kupata Uelewa Kuhusu Mambo ya Kiroho na akaanza Kupractise..
Hufungua kwanza Root chakra (mlango wa Elimu na Maarifa)..
Na baadhi Huishia Kwenye Imbalance Power of The Chakrah..
Wanajikuta Chakra haijabalance..
Na Imbalance Root chakra husababisha..
Insecurity feelings, anxiety, fear, lack of trust. Trouble concentrating and deciding, being isolated from one's self as well as others..
sasa Hii ndo sababu Ikaja Maelezo ya Kuhusu Makutano au Majumuiko yote ya Watu wa Root chakra Yaani mtoa taatifa kuwaeleza Kitakachowakuta na maelezo yao..
turejee Maana Yetu sasa ya Kutoka kwenye Ufunuo tulivyoiweka Vizuri..
Ufunuo wa Yohana 2:1
"Kwa mjumbe (Mtoa taarifa) wa Kutaniko (Jumuiko) la Efeso andika; Haya ndiyo anenayo yeye azishikaye hizo nyota saba katika mkono wake wa kuume, yeye aendaye katikati ya vile vinara saba vya dhahabu."
sasa Naona baada ya Kukuelezea Hapo Umeweza Kuona utofauti wa fungu Hilo kabla ya Kueleza Na baada ya Kueleza..
View attachment 3169358
Sasa Twende Ndani..
Mpaka Ufike Kufungua Root chakra huwa Ni strugle na uvumilivu wa Kutosha na Ukiifungua Utapata elimu na Maarifa na Unaweza Kupewa Gift ya Utambuzi..
Na ndo maana Ya verse ya Pili na kama Umeona Hiyo ndo Imbalance ya Toot chakra kama Nilivyokuelezea Kabla..
Sasa onyo umeliona?
"Umeuacha Upendo wako wa Kwanza"
Unajua maana Yake ni Kila mtu anayefungua Root chakra Ugundua kuwa Mafundisho ya Kidini yanafundishwa Tofauti na jinsi anavyoyachambua Yeye na Hugundua Uongo mwingi wa Wachungaji na hao wanaojiita Watu wa Mungu.
Shida Inakuja wanaofungua Wao Kujiona ni bora Kuliko wote na ndo maana Ya rootchakra Umeona Imeandikwa "I AM"..
Kwahyo Baada ya Kujua Ukweli na Kuingia Ulimwengu wa Kiroho Hujiona Ni bora na Huanza Kuwasema Vbaya wale wasioweza Kuwa ndani ya Ukweli alionao..
Na Huanza kujenga Chuki Kwa watu ambao Zamani aliwaheshimu na Kuwajali kama wachungaji na Masheikh Na hata wafia Dini wengine..
Na ndo maana Ukienda Fungu la Tano la Sura hiyo hiyo Anaamrishwa Kurudia matendo ya kwanza..
Ufunuo wa Yohana 2:5..
"Basi, kumbuka ni wapi ulikoanguka; ukatubu, ukayafanye matendo ya kwanza. Lakini, usipofanya hivyo, naja kwako, nami nitakiondoa kinara chako katika mahali pake, usipotubu."
maana Yake Yale matendo yake anayofanya Hayafai anatakuwa abalance Kuujua Ukweli sio chanzo cha kuwaona wasio Jua hawana maana..Na ndo maana Anasema naja kwako na Nitakiondoa Kinara chako..
Na watu wasiotii kurudi kwenye Upendo wa Awali kuwaona walio Katika Imani zingine hawako sawa na wao na Kuendeleza Umimi Au ego!
Hunyang'anywa Uwezo w Kiroho na Maarifa hivyo huelekea Katika Kutokuwa na Imani kabisa..
Na hao ndo Huwa Wanakuwa wapinga Mungu (Atheists)
Kwa sababu ya Kungolewa Vinara vyao...
Sasa sijui kama Umenielewa?
Kama Una swali Kuhusu Kanisa La.kwanza Uliza
Karibu Arsis pole na majukumu, Darsa za kumalizia ni nyingi sana nakukumbusha tu.Tutarudi tena hivi karibuni na somo la namna ya kuita na kukamata majinni.
Tahadharini sana, kuita kukamata majini haomaanishi kuwakamata na kuwafuga. Ni kuwakamata kuteketeza mambo yao ya uchawi na kuwaonesha nia njema, wanaposalimu amri wanakuwa huru. Wanapokaidi kuna mawili tu, au wanauliwa muda huohuo au wanapelekewa jela za majini.
Tutakapoanza asjaribu kuita mtu jini mpaka amalize somo lote kamili, ambalo lina sura (chapters zaidi ya 13.
Tutaleta sura moja moja ili kila mmoja aelewe kwa kina na kama kuna maswali tutajibu kila sura kivyake.
Ni hatari sana kujifanya umeshaelewa ya kufanya kabla hujamaliza somo zima. Ni hatari kubwa sana, nasisitiza.
Kumbe ni Mjinga kiasi hiki.Mtoa mada unaonekana unayajua majini vizuri.
Hebu nitaftie Jini Moja Jema linalo shika dini vizuri kwa ajiri ya kuniletea pesa mimi ili zinisaidie kutatua changamoto mbalimbali za maisha.
Nadhani kwa utaalamu wako utanifanikishia hili.
Habari Dada faiza FaizaFoxyUnaharibu uzi wa watu kwa kuweka mabandiko marefu yasioeleweka, fungua uzi wako unaohusiana na makanisa, hapa tunasoma habari za majinni.
Mkuu .. What's wrong ukiendelea na hiyo mada kama mwenye uzi kakuruhusu?Habari Dada faiza FaizaFoxy
Samahani Sana Kwa kukukwaza kwa Bandiko Langu ambalo wewe Umeona Halina Maana..
Ufafanuzi:
Kama Ukiangalia Vizuri Bandiko hilo Limeandikwa Tarehe 05 December 2024 Obviously Lina Miezi Miwili Tangu liandikwe..
Na kama Umenotice Ni kwamba Baada ya Bandiko Hilo Sikuwasilisha Bandiko jingine tena kwenye Uzi huu..
Nini Kilitokea!
Watu waliomba Niongelee hiyo Mada na Nilikataa (Maana kwa Kawaida Huwa Sianzishi Mada Kwenye Mada ya Mtu mwingine unless Inahusiana na Jambo husika..
Ikabidi nimtafute Mwenye Uzi wake na Kumuuliza Kuhusu Maoni ya Watu kuongelea Kuhusu Muktadha Wa makanisa saba kama Ilivyoongelewa kwenye Ufunuo Na Ku Decipher the massage Behind nikapata Baraka Zote za Mtoa mada Kuwa ninaweza Kuliongelea..
Nilipoliongelea Baada ya Wiki moja Nikapokea Maoni Tofauti kutoka kwa Watu tofauti wengine ni watu ninaowaheshimu Sana kuniambia Nisitishe jambo hilo na Nilikubaliana nao na Nikasitisha Kuongelea Swala Hilo kwa muktadha wowote huku Wasomaji Nikiwaadaa Kuwa Nitawaletea Somo hilo nikipata Muda (Siri nyuma ya Kuahirisha Kila siku Kuleta somo hilo)..
Samahani Sana Kwa Kukereka lakini Kwa bahati mbaya Ni kwamba Kero yako Imechelewa Kufika kwa sababu Kero zote ziliwasilishwa ndani ya Wiki Moja huenda Ningeijibu kwa Muda..
Asante sana
Mjinga kivipi ?Kumbe ni Mjinga kiasi hiki.
In shaa Alah tutaliaza wiki hii, hili ndio kwa kiwango kikubwa lilinifanya nisitishe mada ya Comorro, kwani huko ndio nilipoanza kuliona mubashara. Ni very interesting, tutagusia kidogo nimalizie kipande cha Comorro japo kwa summary ili nikinza hili nidumu nalo nilimalize haraka, watu wasiende wakajidai mafundi wakajiumiza wao na wengine. Ni somo refu kiasi.Karibu Arsis pole na majukumu, Darsa za kumalizia ni nyingi sana nakukumbusha tu.
Hili somo la kuwakamata majini ni la muhimu sana lini utaanza kulitoa?
SawasawaIn shaa Alah tutaliaza wiki hii, hili ndio kwa kiwango kikubwa lilinifanya nisitishe mada ya Comorro, kwani huko ndio nilipoanza kuliona mubashara. Ni very interesting, ntagusia kidogo nomalizie kipande cha Comorro japo kwa summary ili nikinzq hili nidumu nalo nilimalize haraka, watu wasiende wakajidai mafundi wakajiumiza wao na wengine. Ni omo refu kiasi.
Hayo mambo yapo, ni ushirikina mjubwa sana ambao utakufikisha uanza kutoa kafara za damu za watu.Mjinga kivipi ?
Kama Sulemani aliyatumia Majini mema katika kumsaidia kufanyia kazi mbali mbali, kwanini mimi nisiichukue hiyo fulsa ili kujiongezea kipato?
Tambua kua kiumbe chochote duniani kinaweza kutumika katika shughuri za kuinua uchumi.
Punda anatumika kubeba mizigo, Ng'ombe anatumika katika shughuri za Kilimo.
Kwanini wewe umekasirika sana niliposema mtoa mada anisaidie kunipa majini kazi kama anauzoefu kwa upande huo?
Je ni kwanini wewe hupendi mimi kupata msaada toka kwa majini wema ?
Kumbuka ni Juzi Dr. Sule alitamka kuwa;
"Kuwatumia Majini wema kujiongezea kipato sio dhambi"
Ni kwanini wewe hutaki mimi kutumia hiyo fulsa?
Naam ni mambo mazito sana, kinga ya kwanza ni salat na kulinda udhu wetu. Tusiziache wala kuzidharau sala zetu tano kwa siku, na kila tuwezapo kusali za ziada tuzisali. Ni kinga kubwa sana. Hii dunia ina mengi sana mabaya tusiyoyaona.Sawasawa
Naona umeweka tahadhari sana watu wasijaribu mpka somo liishe, Mwenye masikio na asikie.
Nakushauri ulifungulie uzi wako kama alivoshauri dada yetu.Habari Dada faiza FaizaFoxy
Samahani Sana Kwa kukukwaza kwa Bandiko Langu ambalo wewe Umeona Halina Maana..
Ufafanuzi:
Kama Ukiangalia Vizuri Bandiko hilo Limeandikwa Tarehe 05 December 2024 Obviously Lina Miezi Miwili Tangu liandikwe..
Na kama Umenotice Ni kwamba Baada ya Bandiko Hilo Sikuwasilisha Bandiko jingine tena kwenye Uzi huu..
Nini Kilitokea!
Watu waliomba Niongelee hiyo Mada na Nilikataa (Maana kwa Kawaida Huwa Sianzishi Mada Kwenye Mada ya Mtu mwingine unless Inahusiana na Jambo husika..
Ikabidi nimtafute Mwenye Uzi wake na Kumuuliza Kuhusu Maoni ya Watu kuongelea Kuhusu Muktadha Wa makanisa saba kama Ilivyoongelewa kwenye Ufunuo Na Ku Decipher the massage Behind nikapata Baraka Zote za Mtoa mada Kuwa ninaweza Kuliongelea..
Nilipoliongelea Baada ya Wiki moja Nikapokea Maoni Tofauti kutoka kwa Watu tofauti wengine ni watu ninaowaheshimu Sana kuniambia Nisitishe jambo hilo na Nilikubaliana nao na Nikasitisha Kuongelea Swala Hilo kwa muktadha wowote huku Wasomaji Nikiwaadaa Kuwa Nitawaletea Somo hilo nikipata Muda (Siri nyuma ya Kuahirisha Kila siku Kuleta somo hilo)..
Samahani Sana Kwa Kukereka lakini Kwa bahati mbaya Ni kwamba Kero yako Imechelewa Kufika kwa sababu Kero zote ziliwasilishwa ndani ya Wiki Moja huenda Ningeijibu kwa Muda..
Asante sana