Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Usikwepe swali mkuu,humo kuna uchawi na kuna kuswali
Naona wewe ndio umekwepa swali.

Naona umeingiza dini, uchawi, kuswali yote katika andiko lako fupi kabisa. Vyote hivyo vinahusiana nini na hii mada?

Umeielewa mada lakini?

Nakushauri, tulia usome mada, ni elimu kubwa sana hii. Uliza kwa unayoyasoma hapa, sio ya kubuni kichwani mwako tu, hutoelewa kitu.
 
Inatokea post namba 98.

Haukupita muda nikaingia pangoni kulala. Cha ajabu ni kua, lile pango lilikua kubwa sana, lakini sikuhisi uoga hata kidpogo kulala mule.

Haikupita muda nikapitiwa na usingizi. Kstika kulala kwangu nikaota ndoto ya wazi kabisa. Nikawa kwenye ndoto naisikia ile sauti ya mwenye pete. Ikiniambia wazi ?mimi naitwa Arsis", kuniita si lazima upige kelele kama ulivyofanya leo. Unawe kuniita hata kwa kufikiria gtu, mimi nitafika, kuongea na mimi pia kukiwa na watu sio lazima useme kwa sauti, ukifikiria tu unachotaka kuongea na mimi, nitakujibu. Hii ndio nilikwambia mapema inaitwa "telepathy".

Sijui nii-ite ndoto au mawasiliano ya upande mmoja yakaendela; Kuanzia sasa wewe nitakua nakupa ujuzi wa vitu mbali mbali, utavoweza kufundisha wengine uwafundishe, vile ambavyo huvielewi niulize. Usifiundishe mtu kitu usichokielewa. Kitu kikubwa sana cha kuwafundisha atu ni namna ya kutatua matatizo yao na tiba zao. Kuna tiba utazielewa na kila utayoielewa upo huru na ni lazima ufundishe wengine. Si umeona afanyavyo babu yako? Babu yako hamnyimi mtu dawa na mengi hayafichi. Ukiona hujasikia kitu kutoka kwake elewa kua hicho hana ujuzi nacho, huwa anasaidiwa na wengine bila nyinyi kuona au kuelewa. Sasa yote ya babu yako utayapata wewe na zaidi sana. Saidia sana binadam wenzako matizo yao. Usibagie tajiri na masikini, wogte ni kitu kimoja. Tatizo la tajiri na tagtizo la masikini halina tofauti. Hakuna utajiri mkubwa zaidi ya afya.

Basi hayo ndio niliweza kuyashika clear kabisa kwa siku hiyo na sitasahau. Haujapita muda baada ya hio ndoto, nikaamshwa usingizini. Nikaamshwa na wanawake wawili, wakaniamsha kwa upole kabisa. Wakajitambulisha majina yao, huku mimi nikiwa nimekaa pale nilipolala, mmoja akasema sisi ni majini wazuri au wengine wanatuita maruhani. Hatupo hapa kudhuru mtu, tupo hapa kwa ajili wewe umechaguliwa kutatua matatzio ya watu, sisi wote tunafanya kazi chini ya mwenye hio pete ulioivaa lakini hatuna mamlaka nayo, na sisi tumepewa pete zetu utatuona sana tukiwa kama binadam, utatujua kwa kuziona pete zetu, pete zetu zinafanana na zina kito chekundu lakini kito chake hakijakooza kama chako na ni vito vya duara, tu. Zitazame. Wakanionesha vidole vyao. Nikawauliza "mbona siwaoni sura zenu". Mmoja kajibu sisi huwezi kutuona sura zetu za asili, utatuona kwa sura za kibinadam tutakapoonana mitaani huko. Tutakuja kwa sura tofauti za umri tofauti, usitegemee kutuona kwa sura au umbo utakalo lizowea, tunabadilika badilika, ndio kawaida yetu. Lakini pete hazibadiliki, hata tukija na mapambo mengine pete hizi tulizokuonesha zinakuepo na zinabaki hivi hivi kwenye vidole hivi hivi vya pete. Tumekuja kujitambulisha. Njoo kidogo tukutenbeze kwenye pango.

Nikaamka nilipokaa, mmoja, aliekua haongei, akatangulia mbele, yule mwengine akawa ubavuni kwangu. Sikuwa na uoga kabisa wla sikuhisi hofu yoyote. Yule akaendelea kunambia. Huyu ni mamangu mzazi, yeye haongei sana. Nikamuuliza, sijamsikia kuongea. Yule ambae haongei, akasema, mimi ni mtu mzima sana naitwa... Akanitajia jina lake, akanambia sisi kazi zetu atakueleza mwanangu, yeye ndie utamuona mara kwa mara, mimi nimekuja kujitambulisha tu, nikija utajua nimekuja, Huna haja ya kuniita kuuliza kitu, muite huyo tu. Isipokua napenda kukuelewesha kua kuanzia sasa tupo pamoja na wewe. Mwenye hizi pete ndio mfalme wetu kwenye ulimwengu usioonekana na kwa ulimwengu wenu wa kibinadam wewe ndio mfalme wetu na enzi yako ni hio pete yako. Sisi hatuwezi kukuita kwa jina tutakuita "bwana mkubwa" kuanzia sasa. Babu yako kaanza kukuita bwana mkubwa kunzia mchnga. Babu yako ni mtu anaeheshimika sana katika ulimwengu wetu, kwa ajili ya ukoo wake, ukoo wake usioonekana ni ukoo wa simba, ni wakali sana na wanaogopewa sana. Hakuna simba ambae hana damu ya kifalme kwenye dunia yetu.

Tukafka kwenye kama njia panda hivi ya pango, yule mama akanyamaza, akaingia uoande wa kulia, akaanza kuongea mwanae. Huku sasa unakwenda njia ya kwenda kwetu, huku haruhusiwi mtu kuingia bila kukaribishwa. Wewe peke yako unaruhusiwa kuja, ukija na mgeni hawezi kufika huku, ataishia pae njia panda. Hatua chache mbele tukakuta kama ukumbi mkubwa umepambwa vizuri sana, wakanambia, karibu ukae, kuna kama makochi lakini ya mito mitupu, mizuri, yule mtoto akakaa kwanza na mimi nikakaa tunatazamana, mama yake akaaga akasema yeye ndio anaondoka, ana mambo mengi ya kufanya. Nikamwabia "kwaheri" akanijibu "kwaheri" akapiga hatu mbili tatu kuelekea ndani akapotea sikumuona tena pangoni.

Yule aliebaki akanambia mimi hutohitaji kuniita kwa sasa, wewe utamuita mwenye pete tu akiamua yeye nije utajua uwepo wangu, ikibidi na mama aje basi utajua uweoo wake. Nimekuleta upajue kwetu, hapa ni mbali sana na unapolala lakini mfalme kaifupisha sana safari. Kwa leo usiulize chochote, tulikuja kujitambulisha tu kwako, kama una swali lolote utamuuliza mfalme. Nikamwambia "sawa, nimeelewa". Akanamia haya twende nikurudishe, karibu sana wakati wowote ukija hapa chukulia kua umeshakaribishwa, Ukihitaji kuja usisite, tutakuepo. Tukaondoka mpaka pale njia panda akanambia si unajua njia ya kurudia, mimi naishia hapa. Nikamwambia ndio naijua. Tukaagana akaondoka na mimi nikaondoka kurudi.

Ie narudi nasikia sauti kwa nje ya pango, watu wanaongea na yule kijana wa babu ninae lala nae nikasikia anaongea nje, na sauti ya babu. NIkatoka nje.

Itaendelea.
 
inatokea post namba 107.

Kutoka nje ya pango nikaona hakuna mtu pale nje, na niisikia sauti nilipokua kwa ndani ya pango, nilipotazama nikaona kuna moto kwa sehemu ile tuliokua tunachoma kamba. Nikasika "bwana mkuba. yupo hapa tunachoma kamba". Nikaelekea huko, nikamkuta babu n vijana wake wawili na mtu mzima mmoja mwaname lakini anaonesha huyu ni mgeni. Walikua wamekaa wote wanachoma kamba, kama tulivyofanya sisi.

Babu; Karibu bwana mkiubwa, huyu ni rafiki yangu anaishi Tanga mjini, tunafahamiana miaka mingi sana, yeye mwenyeji huku, sio mara yake ya kwanza kuja, Amekuja na wageni, wameeda kuoshwa baharini wana matatio yao, tukaona sisi tule kamba hapa. Huytu akisikia msimu wa kamba lazima aje na wageni huku.

Nikasalimiana na yule mgeni, sura zake zilikua sio ngeni kwangu lakini sikuweza kukumbuka nimemuona wapi, ingawa kulikua kuna mwei mkali na kweupe kabisa. Akanambia hunikumbiki bwana? Mimi mbona nakukumbika sana? Ile sauti sasa yake ndio ikanikumbusha nikamwabia, nimekuku,mbuka, wewe baba yake Tunda? Akasema ningeshangaa usingenikumbuka, Tunda yuko huko iwa bibi yako, tumekuja nae, yeye kalala mapema kama kawaida yake. Babu akasema aah, Tunfa hata angekua macho usinge,lta huku bila bibi gtake, maana akimuona bibi yake hataki kubanduka, sijui wana siri gani? Baba yake Tunda akajibu mambo yta wanawake huyajui bwana, siri yao ni kutusema sisi tu, hawana zaidi". Tukacheka, nikaambiwa kula kamba nwana., tumekuja na kahawa vile vile, tupo muda mrefu hapa, tukaona tusikuamshe.

Tukakaa pale wenzangu wanakula kamba, mimi nilikua nimeshiba sana, nikawa nakunywa kahawa na nasikiliza story zo za zamani. Hujapita muda sana, nikaona watu watano wanakuja kuelekea tulipokaa wanatokea mtoni, nikasikia "hodi, hodi" sauti a yule kijana wake mwengine babu, babu akasema karibuni mle kamba. Wakaja mpaka pale lakini mwanamke mmoja alikua nao yeye akaondoka kuelekea pangoni peke take, nikamkumbuka ni katika wale walionifata, alikua ni yule mama, lakini nikaona ajabu, haagani wala hamsemeshi mtu, Ikanijia sauti ya Arsis, Arsis ni yule alienipa pete. Sauti ikanambia, ule hamuoni mwengine isipokua wewe tu na babu yako, kamaliza kazi yake anarudi kule kwao. Hawa wengine wote hawamuoni hata akiongea hawamsikii, hata aliokua nao huko baharini na mtini hawajamuona wala kumsikia. Nikabaki nashangaa.

Babu akawakaribusha wale wageni, walikua wanawake wawili na wanaume wawili, wawili walikua vijana kabisa, wawili walikua makamo kidohgo lakini sio wazee. Nikatambulishwa nao, pale babu akawajulisha, huyu mjukuu wangu ankaa Dar., nyie mnaokaa dar labda mnajuana. kaeni mle kamba, hamuwapati namna hii jini huko. Tukakaa pale ikawa kama ni picnic tu, watu wanapiga story, vicheko furaha huku tunakula kamba.

Nikafahamu kua, mwynye matatizo alikua ni yile mwanamke mdogo, na yule kijana mwingine ni umewe, wanaishi Dar na ni marafiki zake Tunda, wale wawili ni wazazi wa yule binti, waliposikia ana matatizo analetwa kutibiwa huku kwa babu na wao wakaema wamsindikiza, ndio ujio wao pale.

Babu akawaambiam haya vihjana, maana eote walikua ni wadogoi kwake, matatizo ya huyu binti yamekwisha kabisa, na hivi kishaogeshwa ndio kamaliza mchezo kabisa. Mmama yeke akasem ahata mimi nimeshangaa, sasa hivi anacheka na kuongea, na anaweza kula namna hii. Babu akasema na mjukuu atatuletea haraka sana.

Kumbe yule binti alikua na tatzio la mashetani kabla hata hajaolewa, nikaelewa kua alikua na linalojiita jini mahaba, kwanza likyua hataki aoelewe, halafu likamfunga kizazi mwaka wa tano sasa, na binti akaanza kujmwa, hana furaha, hali, hashirikiani na wenzake, na ugomvi na mumewe nyumbani hauuishi, mpaka walipjuana na Tunda akawaambia twebdeni kwetu Tanga mkajaribu kumtibia, ndio akaongea na baba yake, baba yake akamwambi ngoja nitakuulizia wataalamu, ndio wakapanda siku waje leo kwa babu, kumbe aliwepo huko kuanzia asubuhi. Babu akawaambia kishafika hapa kishapona huyi, Hawakuamini, akawaambia tukishamkohesha baharini myajionea, ndio akawaketa wa muogeshe usiku huu. Kisa chao kwa ufupi ndio hicho.

Tukakakaa pale, mwisho wakaniaga wakaenda zao, yule kija akauliza mbona hawa wanabaki huku? Babu akawaambia hawa wanbapenda kamaba na adventure na wewe kijana mwenzao ukitaka baki nao. Yule kijana ilikua tayari abaki, baba yake Tunda akasema twende bwana, twende ukampe kampani keo, saa hizi Tunda haamkii hata umpigie ngoma atakua mnyoinge akibaki na wazee pekeetu. Ndio wakaondoka.

Mimi na kijana wabau tukabaki, akanambia, leo umelala sana, nimetoka umelala hata huna habari. Mimi Nikashangaa kimoyomoyo, huyu mimi nimetoka na wale wanawake nimeacha kalala, nimerudi hayupo, nikajisema haelewi kama nilitoka, anajua nimelala kumbe nimeenda kutembezwa mapangoni huko.

Tukakaa kidogo, nikamwabia nakwenda nikalale, kutaingia akfajiri sasa hivi. Akanambi, si usubiri alfajiri tu, ukilala sasa hivi utaamka kweli? Nikamwabia nitaamka, wacha nilale japo kidogo, nikamuacha nikaingia zangu kulala.


Itaendelea.
 
Kuna watu wamenitumia pm kuniuliza kama hiki kisa cha kweli. Napenda kuwafahamisha kua hiki kisa ni cha kweli kwa asilimia 98, labda kuna vionjo vya hapa na pale katika kuandika na fahamu zetu haziwezi kua na kumbukumbu ya mia kwa mia wakati wote, pia kiuhadithia moia kwa mia ni kazi ngumu sa, Kwa hio maelezo ya muhimu yoe ni ya kweli. Kuonana na vumbe visivyoonekana ki kawaida ni kweli, kua babu yangu yuko huko ninapohadithia ni kweli.

Nawahakikishia hakuna ninachozidisha wala kupunguyza isipokua vionjo vichache sana. Pia ieleweke mimi sio mwndishi wa hadithi na jaribu kukifanya hiki kisa kama cha kaiwada lakini naamini si kawaida kwa wengi wenu.

Pia naamini kuna wengine wana visa vya ukweli vingi na vya kusisimua sana lakini hawawezi kuvieleza kwa sababu moja au nyingine. Hata mimi kuyaeleza haya na mengine ya maisha yangu ninafanya juhudi kubwa sana.

Sio wepesi kama nilivyodhani na kuna nguvu kubwa sana inanizuwia, sema nipo namtaalamu, Arsis, siuna shaka wala wasi wasi kabisa.

Kwanza sikuelewa kama Arsis anaongia kunisoma JF, akanambia chochote ninachokifanya yeye anaelewa, kwa sababu yupo kariubu sana na mimi kuliko ninavyofikiria, akanitahadharisha, kama hataki niandike nisingeweza kuandika habari zake.

Sema Arsis, ni muelewa sana, amenikumbusha kua maandiko yangu yawe kwa njia ya kusaidia wengine kuelewa asioyaelewa. Wakiwa wana maswali wajibu kwa kadiri ujuavyo kwa faida yao, sio yako.

Wana JF mnaonisoma hayo ni kwa uchache sana, mengine, nakariisha sana maswali wakati wowote, nipo kwa ajili ya jamii.

Haya ninayoyaandika hapa hayahusiani kabisa na ushirikina. Mimi ni "braza men kwedli kweli" tena yule wa kujirisha sana, Tanzania na duniani, sema majukumu mengine yamenipiga breki kali sana. Na utu uzima umenijia naona niyaeleze niyajuayo labda itakua faiada japo kwa mooja wetu mwengine.

Karibuni muulize mnapokua na swali au maswali, lolote lile, linalohusiana na hiki kisa au lisilohusiana.
 
Inatokea post namba 108.

Kufika tu nikalala, sikuchelewa wala sikujua nimelala saa ngapi, nastuka natazama alipolala kijana wa babu naona hayupo. Kutazama upande wa kuingilia pangoni,, naona kunaanza kua kweupe kwa mbali, nikajua alfajiri tayari, nikaamka, nilipoondoka nikaona niibebe bakora yangu maana alfajiri kuingoia mtoni nako unaweza kukutana na nyoka, Nikaibeba nikailaza fimbo chini niingie mtoni nikaona imeamk yenyewe, nikaiwacha hivyo hivyo imesimama, nikaingia mtoni nikajitosa, nikaoga oga nikatawaza vizuri nikatoka, nikaelekea tulipozowea kusali, kweli nikamkuta kijana wa babu kisha sali, anasoma soma nyiradi zake. Nikasali nikamaliza, bakora yangu safari hii hii sikuilaza, nikaisimamisha, ukasimama yenyewe. Kumbe kijana wa babu akawa ananitazama yote yale.

Nilipomaliza kusali, nikasalimiana na kijana wa babu, akaniambia hii bakora yako kama ya babu? Zinasimama zenyewe? Sijui babu yako anazitengenezaje hizi bakora. Hata yake ile akiisimamisha inasimama, nikimuuliza anatengenezaje anacheka tu. Nikamwambia na mimi nitamuuliza, maana nimeona niliilaza chini inasimama yenyewe, aknambiaa "aah haiwezekani, sijawahi kumuona babu akiilaza chini. Na mimi nikacheka, yaishe. Nikamwabia narudi kulala pangoni bado usingizi haujaniishia. Akasema saa hizi utapata usingizi kweli, ngoja mimi niende nyumbani nikatazame kama kuna uji tayari bilete tunywe. Nikamwabia wewe kunya tu huko, na mimi ukija utakuja nichukua turudi wote nyumbani. Siku zangu tatu za kulala pangoni zimeeisha. Akacheka, akanambia kama uliambiwa ukae siku tatu mpka babu aje kukuchukua la sivyo huondoki huku bila yeye. Nikacheka, nikamwabia hao labda waginjwa zake anaowatibu, mimi nina kifaa hiki hawezi kunizuwia. Nikamuonesha fimbo, akanambia twebde uone kama kweli. Nikamwabia ukija tutakwenda acha nilale kidogo, jua bado halijapanda na ndani pale pazuri hata jua likipipanda panakua pamepoa tu. Akaniaga akaongoka mimi nikarudi kulala pagoni.


Nikalala sana, mpaka saa nne hivi nikastuka, nasikia sauti zinaongea nje ya pango, nikatoka pale ili nikajitupe baharinni niogelee. Kutoka nje namuona babu kaja na yule kijana mwenye mkewe alietibiwa jana, na kijana wa babu mmoja. Sio yule ninaelala nae pangoni.

Babu; "bwana mkubwa unalala sana, hufai kuishi shamba wewe. Nikamwambia babu jana mmeniweka mpaka karibu ya alfajiri, na mnanilisha kamba namna ile, si lazima nilale sana. Wakachela wote. Yule kijana akasema, sijawahi kula kamba kama niliokula huku, mnafaidi sana huku. Nikamwabia, kamba wa msimu hao, huwapati tena mpaka msimu mwingine, babu ndio anaijua misimu yake. Mwambie babu akupigie kabla ya msimu uwawahi. Kijana akasema leo babu kanambia nije kuwavuna mwenyewe nipeleke zawadi mjini. Nikamwambia, utashindwa mwenyewe pa kuwabeba.

Babu; Na wewe bwana mkubwa hutaki kuchukua zawadi ya mjini? Babako na mamako wamekuja leo asubuhi kukufata, siku zako zimekwisha huku. Ndio tumekuja kukufata.

Nikamwambia, aah babu nimepazowea huku pangoni. Babu akacheka, akasema basi wewe baki usiende mjini. Nikamwabia ngoja nikakusanye vitu vyangu, Babu akasema viwache tu watakuja vijana kuchukua, nyie mngojeni tule mwingine aje na uji, mnywe mkachumchukulie mwenzenu kamba apeleke zawadi. Babako kasema anakuja mwenyewe kuvuna kamba leo. Hivi muda huu huu nikienda mimi atakuja. Nikamuuliza yule kijana, umekuja na kitu cha kuwabebea kamba wako, akasema amekuja na kikapu kijana wa babu. Nikamwambia poa.

Babu akaniaga, akasema, haya bwana, mradi tumeonana ruksa kuondoka, mngojeni mwenzu mkambebee kamba, huyu na yeye avune mwenyewe, ainje raha na chungu yake. Mkewe bado kalala, yule alikua hajalala siku nyingi, hii wiki mazonge zonge yamemtoka atalala sana. Kishapoana yule.

Babu akaondoka, hatujakaa sana yule kijana akawa amefika.

Kijana wa babu; Haya twendeni kwenye kamba, kuna wahuni wa babu wanakuja wasianzishe fujo huko, maana wakija wale hata kamba wanapata shida. Wanakuja kuchukua mizigo yako. Nikamwambia poa. Tukaelekea kwenye kamba na mgeni wetu. Mgeni akashangazwa sana, hajawahi kuona kabla. Kutia mguu wake kwenye dimbwi akatoka nje mbio, akasema wanachoma choma miguuni, kama miba, nikamwambia kawaida yao hio kwa kua wapo wengi, tukampa nyavu akaanza kuhangaika, kidogo mwenyewe akaizowea akawa anaona raha. Akachota mpaka kapu likajaa, akasema nimekuja na kapu dogo sana. nikamwambia hayo makapu ndio saizi ya babu hiyo, hakupi kubwa wala hakuruhusu kuchukua kubwa zaidi ya hapo. Mwenyewe anasema mradi wake huu kajaaliwa na Mwenyezi Mungu. Kijana akasema, huu mradi mkubwa sana. Tukaanza kuondoka.

Kabla hatujafika nyumbani, tukakutana na kikundi cha vijana wadogo wadogo wa kiume, kama sita hivi, yule kijana wa babu akawaambia mchukue vitu vyote msiache kitu chochote pangoni, na vyangu nileteeni. Wakaondoka kuelekea pangoni na sisi tukaelekea nyumbani kwa kupitia baharini, maji yalikua madogo ya miguuni tu.

Itaendelea.
 
Inatokea post namba 111.

Tulipofika nyumbani nikaona babu na watu wengine kama sita saba hivi wamekaa pembeni ya nyumba kwa mbele, anapopenda kukaa babu kwenye kiti chake, vimewekwa na viti vingine vya plastiki. Nikaenda kuwasalimia, babu akanijulisha nao, akmwabia yule kijana wake chukau kamba hao wapeleke kwa bibi yako wamtilie barafu wasiharibike. Au wakukaangie bwana, uende nao kwa usalama zaidi, kamba wakizidi barafu wanaharibika pia, wana kipimo chake maalum. Mimi nashauri watengenezwe kabisa, ndio watakua salama zaidi, hata wakikaa mwezi watakua hawaharibiki, ukitaka kuwala wewe unaweza kuwakaanga tena au kuwapika. Utavyopenda. Wanakaushwa hao bila kutiwa chochote zaidi ya chumvi tu. Ufundi mtawafanyia wenyewe.

Baba yake Tunda alikuwepo, aksema hata mimi nakushauri wacha utengezewe, mimi ndivyo ninawachukua mika yote. Bibi yenu n9i mtaaalamu wa mapishi. Anawajua kamba vizuri kuliko mpishi ypyote yule.

Babu akasema si yupo kiwandani jamani. Watu wacheka., yule kijana akachukua lile kapu akaenda nalo uani.

Tukakaa kidogo na babu pale aknambi baba yako yupo ndani amaekuja, wote wapo ndani huko wanakusubiri kwa hamu. Mimi nakwenda kilingeni kidogo kama nusu saa tu ntakua nimerudi, nakwenda na wageni wangu hawa. Tiutaonana nikirudi. akaondoka na wageni wake na mimi nikaingia ndani, kuingia tu, dada yangfu akani surprise akanirukia akanikumbatia, sikujua kama na yeye wamekuja nae, alikiuwe[po mama, Tunfa na mkewe tule kijana na bibi, wanaongea ongea.

Bibi; Bwqana wewe yoka umekuja sikuoni au umeoa kimya kimya huku? Nikacheka tu. Dada yangu akasema haoi huyu mpaka niolewe mimi kwanza. Bibi akasema Mtajuana wenyewe, mradi kabla ya kuoa nimpe ruhusa yangu tu.Anipe kitoka unyumba changu.

Ikawa hakuna la maana zaidi nikaingia chumbani kwangu, nikakuta kumbe vijana walishaleta vitu vyangu, kilikua kibegi tu cha mgongoni kidogo, nikakifungua kutazama mkebe wangu wa pete kama upo. Nikauona upo na ile mizizi alionipa banu ipo, nikakuta na kifurushi kingine cha miti imekauka, nikainusa inatoa harufu nzuri ile miti. Sikujua kaweka nani, nikasema nitajua tu, nani kaweka, Nikaiengemeza fimbo yangu ukutani. nikaingia bafu nikakoga, nilipotoka nikabasili nguo, nikavaa t shirt yangu na jeans la blue, kama nipo mjini vile. Nikatoka nje.

Tunda; Bwna mkubwa huna hata hamu ya kuongea na mimi hatujaonana miaka? Nikamwambia ndio nilikua najitayarisha hivi nikukumbushe mambo yako ya zamani uliyokua mtundu. Akacheka. Tunda tulionana mara ya mwisho nikiwa na umri wa miaka 12, na yeye alikua kidogo mkubwa kwangu, sema alikua mtundu sana. mpaka anakera. Nakumbuka alikua kishajaa maziwa kifuani lakini anapenda sana kuwa na mimi muda wote nikiwa Tanga kwa babu. Nikatoka nje, mzee na yeye alikua ndani nilipoingia nikaambiwa kaenda kuvuna kamba chimbo lake, analijua mwenyewe hilo hamwambii mtu.

Nilipokaa nje pale, haikyupita muda babu akarusi, akasema haya jamani, tunashukutu Mungu kazi zimeisha salama, sasa rukhsa kuondoka, kamba wenu mtawaletewa kila mtu kikapu chake kwenye magari yenu. Qale wageni wakaaga, yule kijana na mkewe wakaondoka, Tunda nae na babake na wale wageni wengine wakaondoka. Baba nae akarusi akasema hatukai tena, bibi yako tumemwabia hata asipike, tumealikwa chakula Tanga, Tutakwenda kula Tanga, haya kaage tuondoke akaingia ndani tukkabaki mimi na babu.

Babuakanambia twebde kilingeni tukaagane babu, baba yako anaharaka ya kuwahi mabibi zake wa Tanga. huku anacheka. Tulipofika kilinegeni babu kakaanza.

Ba; Mjukuu wangu mzigo ulioubeba ni mkubwa sana kuliko unavyofikiria lakini pia ni mwepesi sana kuliko unavyofikiria. Tena wewe kwako utakua mwepesi zaidi kwa ajili ya hio pete yako, Hio pete mwenyewe ni mkubwa sana ki umri ki elimu ki maarifa na iuwezo. Hata mimi sijabahatika kupewa pete hiyo. Mimi sina haja ya kukueleza mengi isipokua wenyewe wenye pete na ile bakora watakueleza zaidi. Mimi ninashukuru nimetimiza yangu kab;la sijapondoka duniani. Mradi babu uwasikilie sana wenye matatizo yao. Usidharau yeyote. Sawa? Nikamjibu sawa babu nimeuelewa, akasema haya, mimi na wewe tutaongea kwa simu mara kwa mara sasaa, najua kuna vitu utahitaji kwangu, niulize wakati wowote lakini nagfahamu kwa sasa hautokumbana na mambo makubwa usioyaweza.

Sema bwana mkubwa, kumbuka, utaanza kuona wanga, wachawi, na mambo mengine hayasemeki, lakini wewe usiwasemeshe hata wakisemesha, kaa kimya endelea na yako kama huwaoni, watajitahidi sana kukutisha usiwaogope wala usiwajali, kuna viumbe watawashughulikia wenyewe wataanza kujiweka mbali na wewe na watakuogopa sana. Pia ukimuona mtu anaumizwa au kuteswa mbele yako anakuomba msamaha na msaada, usimsemeshe,mwache kama alivyo, huyo aliytaka kukudhuru vibaya sana, anachezea kichapo. Wrngiune akumwa hivyo akifika kwake haponi anaondoka, siku ya pili utasikia kuna maziko kama ni jirani yako. Ni ahyoi tru mjukuu wangu na ukiwa na chochotem narudia usifanye bila maelekezo, niulize kama hao wenye pete na bakora watakua wamecheleewa kukujibu, mimi simu yangu ipo wazi wakati wote. Haya twende zetu.

Tikaondoka kufika nyumbani nikakuta watu wameshaingiza vitu kwenye gari nagojewa mimi tu na babu waagane nae. Tukaagana, tiukapanda garri tukaelekea Tanga.

Tanga huwa tunakaa nyumba ya mama yangu ipo jirani kabisa na nyumba ya mama'ke lakini hakai mtu, huwa wanaingia kuisafisha kila siku, mpaka awepo mwenyewe au wageni wake wanaokuja Tanga wana upande wao wanafunguliwa. upande wa mama hauguswi mka tuje wenyewe.

Tumegika salama, nikaenda nyumba ya poili nilipopazowea kumuona bibi yangu na babu ma))zaa mama. kuniona wakafurahai sana. Bibi akasema nimewasikia mlivyinhgia nikasema huyu mume wangu hana hata hamu na mimi, mke wa Duga kishmlemaza.Nikacheka. nikaongea ongea na ndugu na jamaa wengine pale, wakaja mama na dada yangu, mzee yeye aliondoka hakukaa sana. Mama akasema kumwambia mamake, jamani tusimngoije yule bwana leteni chakula tule, maana hata mimi nataka kutoka nikawasalimie rafiki zangu wa Tanga.

Tukala pale, mama nae akaondoka na bdada yangfu na mimi hikaondoka nikaenda kwa washikaji zangu wa Tanga, mpaka baada ya kusali usiku nikarudi, nikakuta nyumbani hawajarudi, nikatoka tena nje nikaenda barazani kwa bibi nikakuta kuna vjana tunafahamiana tiukaanza stoery zapale mpaka kama saa nne hivi nikaona mama na mwanae wamerudi, wakaingia nyumbani moja kwa moja, nikawafata dada yanfu akasema huko isingekua mimi tusingerudi leo, hawataki kumwavhia huyu bibi aondoke. Mama na wewe nae si ungerudi, umenirudisha ma ,i,i kufanya nini, kwani watotrowadogo mnataka kunyonya nyinyi? Akanyanyka akasema anenda kwa mama yake huko, atalala huko huko. Dada yangu akawa anacheka, akamwanbia hasira hujamkuta umeo tu, usitutolee sisi mngije mwenyewe akija. Mama hakumjibu akatoka zake.

Dada yangu akanambia mumewe akirudi utamuona karudi mbio mbioo, gtena ngoja nikamtengezee kahwa ytalem hachelwi mzee, kabla ya saa tano kamili lazima awe karudi. Na kwli saa tanoi kabla ya dakika kama tano zee karudi, ile kuingia haija[pita dakika tanoi na mama karudi, mimi nikawaambia jamani kwaherini nakwenda kulala. Mama aksema bora, maana tunaondoka Alfajiri hapa, wahini kulala nwahii kuamka, mkichelewa tunawaacha mrudi na basi. Dada yangu akasema, hamuwezi kuondoka bila mimi hapa. hata funguo z gari hamjui ziko wapi. mama aksema baba yako hakosi funguo nyingine, wewe lala tu, usiamke mapema.

Tukaingia kila mmoja kulala, siku ya pili alfajiri tukaondoka kurudi Dar.


Kwa ufupi tulipofika Dar ndio nikaanza kuyaona macho yalivyofunguka.

Itaendelea.
 
Inatoka post namba 112.

Kabla ya kufika Dar nilichoanza kukiona Chalinze kilinitisha lakini nikavumilia kwa kujiamini.

Tumefika Chalinze mapema sana, kama saa mbili na nusu asubuhi. Mama akasema Chalinze tununue mananasi. Mzee hakufanya hiyana akaenda mpaka kwenye mananasi akapaki gari kwa pembeni kidogo ya wanapouza mananasi. Dada yangu akasema ngoija nishuke na kahawa ya mzee nilimtengenezea asubuhi, nikutilie na wewe? Nikamwabia nitilie. Tukatoka nje ya gari, wite, mimi na mzee tukaenda kuna kimkahawa kina viti, tukakaa na kahawa yetu, kumbe kile mkahawa, mwenyewe mwanamke mmoja wa Kisomali kamzowea mzee anamjuwa na mama. Akatusalimia, akamuuliza leo body guard yuko wapi? mzee akamwabia yule kule ananunua mananasi, mimi nikacheka, akasema huyu mdogo wako mbona mmefanana, Mzee akamwabia Sofia huachi zako? Unajifanya humjui huyu leo? Sofia akacheka akasema nilikua nataka nikuone, namjua sana, labda yeye ndio kanisahau, huyu aliekua analilia machungwa akipewa anayatupa nisimjue mimi? Nikacheka nikamwabia Abti Sofi nakujua sana, umesahau wiki iliopita nilikuja peke yangu hapa kukusalimia? Akasema nakumbiuka sana "ukaanza kunitongoza kama baba'ko", mrtoto wa nyoka ni nyoka tu. Mzee akamwanboia "mtoto ea simba huyu" Sofia aaha nilisahau simba mwenzangu. Sasa umeshamfundisha usimba mwanao. Baba aksema huyu mpaka akioa. Kwa ssa bado. Sofua "ada za simba wa kwenu kama za kwetu tu, hakuna mchezo mpaka mtu aoe au aolewe. Na yule malaya wako anaejishaua yuko wapi? Baba akacheka, yule kule na mamake wananunua mananasi. Sofia akanambia mimi "bwna mkubwa, nenda kwa yule mzee pale kwenye mananasi alievaa kofia, mwabie mimi namuita, mwambie na mamako aje, mimi namuigta akichelewa atamtafuta mumewe mpaka akome". Mimi nnikaenda nikafikisha ujumbe kama nilivyopewa kwa wote wawili.


Nikarudi nimeongozana na Dada yangu, kabla hatujafika akanambia ngja nimkere Anti Sofia, nikimkalia baba mapajani anaudhika kweli. Mimi kusikia hivyo nikamwabia siendi, mimi nakwenda pale kwenye machungwa, basi sister kufika kwa mzee kamkalaiza mapajani, Sofia: we malaya, ngoja uolewwee kwanza kisa cha kujishindilia nao, unamuumiza tu babako. Dah sikungpja kusikia, nikanyanyuka nikaondoka na mama na yule mzee wakawa washafika.

Sada hapo kwenye machungwa kabla sijafika, nikakuta wanawake wawili wanauza genge, mmoja ytupo uchi kabisa wa mnyama, yani hana nguo hata moja, kakaa kwenye kigoda na miguu kaichanua, mwenzake ndio anaongea na wateja. Yule mwanamke aknitazama sana, nikaona kanitazama mikonoi kuiona ile pete kama akastuka hivi, akanyanyuka akaingia kwenye mabanda yalikua karibu pale. Mimi nikaenda kwenye machungwa kufika kwenye machungwa, Nikamwabia mwenye machungwa nataka uniletee machungwa pale kwa Anti Sofia. Akanambia pale kwa Sofia simba msomali? Nikawa sijamuelewa akacheka, aksema yule simba mwenzako, hata wewe umenisahau? Babako machungwa huwa anachukua wapi akipita hapa. Nikamkumbuka ni rafiki sana ya mzee. Nikamwabia yeye yupo pale kwa Sofia. Mzee yule akasema machungwa anawalete huyu kijana wangu saa hivi. wewe simba usiwe na wasiwasi, machungwa mengine hapa yantoka shamba la bibi yako. Huku anacheka.

Nikamwabia poa. nikaondoka kurudi, yule mwanamke aliekua uchi nikamuona kavaa nguo lakini hajarudi pale, kasima kule banadani anaongea nini sijui huku ananitazama halafu anatazama chini na mwanamke mwingine, ni vijana tu. Ile narudi kwa mzee, nikasikia sauti ya Arsis masikioni, yule ulimtazama mara tatu, akaelewa umemuona kua ni mwanga. mjinga tu yule, hivi anakuogopa na yule anaeongea nae na yey alikua uchi dukani, ndio wanashauriana wakufanye nini lakini walichokiona hata banada wanaliona baya kukaa, wanataka kuondoka waende kwa wakubwa zao, wamezuiliwa kutoka. Ngoka nikuoneshe kitu kitu ujifunze dunia hgii Bwna Mkubwa.

Mie nikaka kwa mzee pale kwa sofia Dada yangu akasema kahawa yako imeshapoa. Sofia aksema ngoja nimepe kahawa yangu, wewe unajauje kutengeza kahawa? Akaja na chupa ya kahawa na vikombe vya kahawa. Mzee akasema aah, nilisahau kahawa yako Sofia. Sofia akamwambia ulisahau au unajizuzua tu upo na boy guard? Hujamwambia kua kila ukipita hapa lazima nikupikie kahawa uondoke nayo? Mama aksema anambie wakati nayajua sana, siku zigine mpaka kahawa ya nyumbani haitaki, anasema ntakunywa kwa sofia akiwa anakuja njia hii.

Sofia: kumbe unayajua eeh?
Mama; hanifichi kitu mimi.
Sofia; madawa yenu ya kidigo ymemwivia mwilini mwake. lakini humuwezi wewe huyu ukoo kubwa, dawa zako zinadunda hapo.

Wakati wanaongea wanatiana pale, Sofia kaleta kahawa na visheti, mama akamwabia hivi visheti hujatia limbata ya Kisomali?
Sofia: Wasomali sio wachawi sisi, sisi ni machezo tu.

Mara akaja yule mzee wa machungwa na na apu zima la machungwa.

Mzee wa machungwa: Simba isingekua bwana mkubwa kunambia uko hapa nisingejuakama umekuja.

Baba: Nisingethubutu kuondoka bila kuja machungwa yangu mnayiniibia shambani.

Wakacheka wote.
Sofia; Kumbe machungwa yako, mimi ananiuzia kama myeja wa kawaida, hata wakipita wageni zangu ndio anawapiga kweli.
Mzee wa machungwa: Wasomali wana pesa, utawafananisha na sisi wadigo.
Sofia: Nilikua sijui kama machungwa yanatoka shmani kwa simba.
Baba: Tena simba, ukichukua machungwa shambani hakikisha unamletea sofia kapu lake.
Mzee: Ngoja nianze kuletea sasa hivim haya yametoka kwenu, tena shmaba la bibi yajomkabisa. Mwaka huu bibi yule atatajirika, hizo Fuso za Wakenya zilizokua zinaingia kuvuna machungwa, Mashaallah. Sasa simba njoo huku wakati namletea machumgwa Sofia, wewe njoo tunong'one kidogo.

Mze akaamka akaenda nae kwenye machungwa.
Sofia: Babako Chalinze nzima wanamjua.
Mama: Hapa si wamejaa watu wa Tanga na muheza, lazima wamjue. Si kama wewe, wanagu huyu Sofia tumekua Tanga, msimuone hivi huyu, malkia huyu wa Tanga huyu.
Sofia; wasinione hivi nini "once a malkia always a malkia". Kama unabisha muulize mumeo. Una bahati upo na makinda wako hapa, ningemiuingiza ndani mumeo na wewe unayaona.
Mama ; Yule mzee wako wa Kisomali aliekuja kukuchakaza Chalize hapa yuko wapi?
Sofia: Huna habari ndugu yangu, kafariki zaidi ya miaka sasa. Nipo singo. Hivi unavyoniona nahamia Dar karibuni, namngoja huyu mtu nimemuuzia nyumba na hii shehemu hapa aje nondoke anakuja siku yoyote kuanzia sasa. Utanikoma nikija Dar.
Mama: Simu zangu si unazo, ukija nijulishe ulipo nije kukuonesha jiji.
Sofia: Mbona mumeo anapajua mpoaka kwangu, mimi siku nyingi nna nyumba yangu Dar, toka mume wangu yupo hai hatujakaa nyumba ya kupanfga sisi.
Mama: Eeeh nimekumbuka, uliolewa Dar, ytena nilija mpaka kwako pale Upanga,
Sofia: Sasa ulifikiri nyumba ya msajili ile, ile nyumba yangu na hivi nimeshawahamisha wapangaji, nangoja nije kuikarabati nihamie. Mwanagu mmoja yupo Dar ni Pilot wa Aur Tanzania, yule wa kike aliolea na Msomali wa QWatar huko, ana watoto watatu sasa. Yule mwengine wa kume anafanya kazi za baba'ke za malorry, hivi kila siku njiani, namwabia awachane nazo hataki. Anapita hapa kila siku mbili tatu, yeye ndio anakaa hapa sasa hivi na mkewe, wanawe wapo Dar wanasoma, wanakaa kwa yule mdgo wangu wa kiume unamkubuka?

Mama " Nisimkumbuke muhuni yule? Yule hatoki nyumbani hata hawa wanamujua, MImi nikauliza Anko Abdi? mama aksema ndio yeye hiyo, huyu dada yake mama mmoja baba mmoja.
Dada: Yule anaonesha alikua bonge la handsome alivyokua mdogo.
Sofia: Muulize mamako.


Mara mzee akarudi akaniita pembeni, kumbe na yule mzee wa machungwa yupo. Mzee.

Baba; Mwambie mwenyewe kilichotokea.
Machungwa: Mwanangu, kwanza pole sana. Haya mamboi si madogo mpaka yamefika kwangu, nimemueleza babako, yule mwanamke kumbe ni mwanga, mwenyewe kakiri, mimi wamekuja wakubwa zake kunieleza nije kukwambia umasamhe. Mimi nikajifanya kushangaa, kama sijui kitu kabisa.
Mimi; Kwani kuna nini?
Machungwa; Tule mwanamke anasema ulimuona akiwa hana nyuo, akaenda kumjulisha mwenzake ndani na yeye akawa hana nguo, wakataka waje kukukomesha sasa wameganda mule ndani hawawezi kutoka ingawa sasa hivi wamevaa nguo lakini hawawezi kutoka wakawaiata wenzao ndio wakawasiliana wakubwa zao, wakubwa zao wakataka kukufata hapa wakutie adabu, wakaishia njiani wakja kwangu walivyoona mimi naonge na ongea na wewe ndio wamebifata nije niwaombee msamaha. Uwawachie waendelee na mambo yao, wapo tayari kulipa fidia ypoyote.
Baba: Umefanya nini simba. Sijafanya lolte baba hata sijui nini kinaendelea.

Kidogo wakati bado baba namzu)ee wa machungwa wanaongea ikanijia sauti ya Arsis,

Arsis: wewe waambie hujui kitu, tena wasikufate tena kuletea mambo ya kipuuzi, sisi tutawatia dabu hawaji tena kufanya vbiasha )ra uchi. Umenielewa.
Mzee: Sasa tufanye nini jamani, mimi mjumbe tu? mjumbe hauawi. Mimi mwenyewe nashangaaa ujanja wangu wote sikuyajua haya. Wapumbavu wale wanakuja kutulisha uchafu wao hapa, ndio mimi sili kwa hawa mama ntilie nisiowajua. Sasa niwaambie nini wale jamaa zao?
Mimi; Waambie mimi sijui kitu na wasimisumbue, sijanywa hata kawahawa yangu. Sijui kinacheoendelea.
Baba; Haya bwana ahsate kwa kuniita, umesikia mwenyewe, ansema hajui nini kinaemdelea anajiponea ajabu. Waambie kama wana maneno zaidi wanifate mimi Dar. Lakini waje wamejitayarisha.
Mzee: Wacha utani bwana, alilosema huyu simab, ndio neno, wasimsumbue yeye na wasimsumbue mtu. Na mi nipeni ryuksa niondoke, nitajua cha kuzungumza nao. Samahani sana ,wajinga wale sasa watakoma wasikiri kila mtu wakucheewa. Aaondoka ake. Akasema na yale machungwa ni ya bibi yako zawadi ytangu kwako.

Tukaridi na mzuu tukanywa kahawa yetu na visheyi, akipakia machungwa kwenye gari, yule mzee wa mananasi nae alikua amyaleta kibao, Sofia akachagua, akasema mpeni elfu ishorini kwa ajili yangu. Mama akatoa akampa. Tukaondoka zetu., Nilikuja kujua siku ya pili nini kiliendelea na wale wachawi.

Itaendelea.
 
Tukaondoka salama pale, Dada yangu akamwambia anti Sofia ukija Dar uje kunifundisha kufanya visheti na kahawa yako, nimevipenda. Anti Sofia akaingia ndani akamtolea kopo zima la visheti, yale makopo ya biskuti makubwa. Akamwabia hii ndio biashara yangu kubwa hapa, navitengeneza kwa wingi wanaojua wananipa order, navipeleka sehemu nyingi sana, wewe ulikua hujui hii zawadi yako. Nakupa kwa sababu asingeolewa mamako unagekua mwanangu, kidogo babako anioe, huyo mdigo sijui akampa nini. Tukacheka tukaondoka.

Tulipoondoka kwenye gari nikajua dada yangu anamchokoza mama.
Dada; Anti Sofia anasema baba ilikua amuoe yeye wewe ukamt)roga kidogo akakuoa wewe, eti kweli? Ananesha alikua mzuri kweli?
Mama; Sofia anawatania, tu, amuoe miubwa kweli kwetu yule, kaolewa sisi bado tunasoma msimuone vile ana mwili mzuri. Lakini alikua mzuri mkweli, mpaka sasa mzuri .

Baba Sofia kajiweka pale kibiashara tu, pale anauza visheti Tanzania nzima, halafu hakuna Msomali anapita Chalinze bila kununua mirungi kwake, siku hizi haweki pale, anaweka kule uoande wa pili, kuna watu wake wanamuuzia, zinatembea simu tu, usimuone vile anapesa nyingi sana, yule muewe kamwachia Scania zaidi ya kumi, urithi wa wanawe. Huyomwanae mdogo wa kiume ndio anafanya kazi za kuzitrazama hizo. Hata wewe bwana mkubwa unazijua garizake, huwa zinakuja garage matra moja moja, zile anazokuja nazo Anko Abdi. Zile zote za Sofia na wanawe. Nikasema aaah, nimezijua na huto mwanae nimeshamjua, siku hizi wanzo benz moya mpya wamewachana na Scania kabisa.
Baba: ndio hizo hizo.
Mimi: Kweli ana pedsa, kwanini anakaa huku sasa?
Baba' Atahamia mjini hgivoi karibuni ana nyumba nyingi tu Dar. Hapa anatengeneza pesa nyingi sana, yule Waarabu wote wa Morogoro wanachukua kirungi kwake, magaru ya Wasomali na mengine mengi tu yanayopita hapa yanachukua miringi kwake. Yule kwa siku anafanya ya miilioni wo mpaka ishirini, usimuone vile.
Mama: Wasomali ni hodari sana kwa biashara.

Tukaneda mwndi mzuri tum hatukuchelewa sana tukawa tumeingia Dar, Vimbwanga vikaanzi mtaa wa Msimbazi, maana tulizunguka kupitia Kariakoo, kuna kitu mama alitaka kabla ya kwenda nyumbani. Ikabidi tupite Msimbazi.

Itaendelea.
 
Tukaondoka salama pale, Dada yangu akamwabia anyti Dofia ukija Dar uje kunidfundisha kufanya vishetu na kahawa yako, nimeivipenda. Anti Sofia akaingia ndani akamtolea kopo zima la vishetiu, yale makopo ya biskuti Akamwabia hii ndio biashara yangu kubwa hapa, naviutengeneza kwa wingi wanaojua wananipa order, navipeleka sejemu nyingi sana, wewe ulikua hujui hii zawadi yako. Nakupa kwa sababu asingeolewa mamako unagekua mwanagu mimi, kidpog babako anioe, huyo mdigo sijui akampa nini. Tukacheka tukaondoka.

Tulipoondoka kwenye gari nikajua dada yangu anamchokoza mama.
Dada; Anti Sofia anasema baba ilikua amuoe yeye wewe ukamt)roga kidogo akakuoa wewe, eti kweli? Ananesha alikua mzuri kweli?
Mama; Sofia anawatania, tu, amuoe miubwa kweli kwetu yule, kaolewa sisi bado tunasoma msimuone vile ana mwili mzuri. Lakini alikua mzuri mkweli, mpaka sasa mzuri .

Baba Sofia kajiweka pale kibiashara tu, pale anauza visheti Tanzania nzima, halafu hakuna Msomali anapita Chalinze bila kununua mirungi kwake, siku hizi haweki pale, anaweka kule uoande wa pili, kuna watu wake wanamuuzia, zinatembea simu tu, usimuone vile anapesa nyingi sana, yule muewe kamwachia Scania zaidi ya kumi, urithi wa wanawe. Huyomwanae mdogo wa kiume ndio anafanya kazi za kuzitrazama hizo. Hata wewe bwana mkubwa unazijua garizake, huwa zinakuja garage matra moja moja, zile anazokuja nazo Anko Abdi. Zile zote za Sofia na wanawe. Nikasema aaah, nimezijua na huto mwanae nimeshamjua, siku hizi wanzo benz moya mpya wamewachana na Scania kabisa.
Baba: ndio hizo hizo.
Mimi: Kweli ana pedsa, kwanini anakaa huku sasa?
Baba' Atahamia mjini hgivoi karibuni ana nyumba nyingi tu Dar. Hapa anatengeneza pesa nyingi sana, yule Waarabu wote wa Morogoro wanachukua kirungi kwake, magaru ya Wasomali na mengine mengi tu yanayopita hapa yanachukua miringi kwake. Yule kwa siku anafanya ya miilioni wo mpaka ishirini, usimuone vile.
Mama: Wasomali ni hodari sana kwa biashara.

Tukaneda mwndi mzuri tum hatukuchelewa sana tukawa tumeingia Dar, Vimbwanga vikaanzi mtaa wa Msimbazi, maana tulizunguka kupitia Kariakoo, kuna kitu mama alitaka kabla ya kwenda nyumbani. Ikabidi tupite Msimbazi.

Itaendelea.
Unatupoteza wasomaji na wafuatiliaji wa thread yako.

Unashika hiki unaacha, cha kule unahamishia huku!

Hakuna mtiririko mzuri wa usimuliaji na mtu hawezi kuelewa unaongelea nini.
 
Unatupoteza wasomaji na wafuatiliaji wa thread yako.

Unashika hiki unaacha, cha kule unahamishia huku!

Hakuna mtiririko mzuri wa usimuliaji na mtu hawezi kuelewa unaongelea nini.
Usijali nitajitahidi kurekebisha, mimi sio mwandishi, najaribu kukumbuka mambo ya miaka mingi nyuma haya. Chukua zile dondoo muhimu, kama hukuzielewa niulize, nipo tayari kuziandika tena, ili uelewe.
 
Usijali nitajitahidi kurekebiusha, mimi sio mwandishi, najaribu kukumbuka mambo ya mika mingi nyuma haya. Chukua zile dondoo muhimu, kama hukuzielewa niulize, nipo tayari kuziandika tena, ili uelewe.
Kwenye mtiririko wa hadithi yako sehemu ya 3 uliishia kusimulia umepelekwa na babu kuogeshwa maji chumvi ya bahari, ukavushwa nchi kavu na kuachwa kwenye madimbwi ya kamba mtoni.

Sasa baada ya hapo ukarukia hii uloweka muda si mrefu wahusika wakiwa ni wapishi wa visheti!

Ndonikasema hauunganishi simuliza yako, wadau hawawezi kuelewa.
 
Hata kama una gari, mimi naweza kukusafirisha wewe na gari lako nikakupeleka popote Tanzania ndani ya dakika tatu au chini kabisa ya hapo.
Uzi ulikuwa unashuka vizuri ila hapa umezidisha

Kagera hadi Mtwara anakubeba pamoja na gari lako kwa dakika 3, 🤣🤣🤣,

hakuna haja ya kuweka mafuta kwenye gari,..

hii ngumu kumeza, inakataa kabisa..

nasoma uzi kama vile naangalia katuni

1723855502370.png
 
Uzi ulikuwa unashuka vizuri ila hapa umezidisha

Kagera hadi Mtwara anakubeba pamoja na gari lako kwa dakika 3, 🤣🤣🤣,

hakuna haja ya kuweka mafuta kwenye gari,..

hii ngumu kumeza, inakataa kabisa..

nasoma uzi kama vile naangalia katuni

View attachment 3072158
Braza inawezekana sana tu
 
Back
Top Bottom