Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

قُلْ هَاتُوا۟ بُرْهَـٰنَكُمْ إِن كُنتُمْ صَـٰدِقِينَ...
Q27:64
...
Leteni hoja zenu kama nyinyi ni wasema kweli. 64
Simba.
Nimemjibu huyo mtanashati fake, kwamba andiko lake ndio chai, yeye anapenda sana hiyo lugha ya chai.

Umeelewa?
 
Hiki kisa cha Adam ni kizuri lakini kimefukuza watu wengi humu..... Watu wanavutika zaidi na elim iliyo kweny mfumo wa story, ila hiki kisa cha Adam ni elim ngumu inayohitaji kushughulisha akili kitu ambacho wengi hawapendelei

Kwenye visa vya Arsis popote alipozungumziwa
Jinn 1, 2 pamoja na Bakora... Hapo elim bubashara ilitolewa!!(hongera kwao)

MAFANIKIO NILOYAPATA KUPITIA ELIM KTK HUU UZI
a) kuwajua majinn na viumbe wa kiroho katika uharisia wao
b) kuijua mode of communication ya hao viumbe
C) kuweza zungumza nao kwa kupitia nafsi (telepathy)
D) kumchukulia jinn n kiumbe wa kawaida tu...

Kiufupi faida humu ipo,,,,, pia mengi yanayozungumzwa humu n kweli
(Hasa ile story ya vibuki ile ni ukweli mtupu 🚶🚶

Pia nimeweza kumhudhurisha kiumbe kukusaidia kufanya shughul zako (Kama ambavyo Arsis anaweza jibu maswali hum kupitia kwa Simba yani mnakuwa two in one🤝🤝

Ilianza kama udadisi mwisho ikawezekana.. Yani unaweza ita kiumbe kikajaa nafsin hlf mkaanza kufanya Jambo jema kwa pamoja!!!

Yote haya Asante kwa mleta uzi, maana katoa elim ya mambo mengi kwa maelezo, story na vitendo
Hapo kwenye kumuhudhurisha kiumbe, Ulitumia njia gani?
 
Hapo kwenye kumuhudhurisha kiumbe, Ulitumia njia gani?
Mbona yote tayar yamo humu.... Simba kishaelekeza, vingine ufanye kucopy yeye alivyokuwa anafanya kuwaita jinn 1, 2 na Bakora (ile ndo njia rahisi zaidi)

Pia cha kutia akilini n kuwa, hii unafanya kwa majini ambao tayar unafahamiana nao Yan ambao upo nao karibu🤝🤝

Ili kuepusha side effect za viumbe wa kiroho
(Usisome uzi Kama story vipo vingi vya kujifunza🚶
 
Safi, basi weka kipind au uanzishe uzi mwingine ili usiingiliane na huu uwe unaelezea Dawa na inatibu nini, ili walau huyo kiumbe wa fimbo watu wa jF wafaidike nae,
unaeza elezea ugonjwa huu na huu Dawa yake ni hii hii, au ukichukua hiki na hiki ukafanya hivi kinatibu hivi hapo kwa week mpaka mwezi utakua umefanya kazi kubwa sana na ndipo tutaona ufanisi na hakika wa habari zako
Nakupa rukhsa anzisha wewe uzi mwengine, chogta yote kuhusu dawa ulioyaona humu na kama kuna mengine utaulizwa tutakuja kuyajibu yanayohusu dawa kama tunazijua.

hata kuhusu umeme wa magari kama unapenda anzisha tu.
Simba.
 
Kisa cha Adam 2.2

Kwanza tulitazame neno hili Q 2:26 إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَسْتَحْىِۦٓ (A) “yastahyiy

Neno hilo pia tunalikuta kwenye Q 28:4 إِنَّ فِرْعَوْنَ عَلَا فِى ٱلْأَرْضِ وَجَعَلَ أَهْلَهَا شِيَعًۭا يَسْتَضْعِفُ طَآئِفَةًۭ مِّنْهُمْ يُذَبِّحُ أَبْنَآءَهُمْ وَيَسْتَحْىِۦ نِسَآءَهُمْ ۚ إِنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلْمُفْسِدِينَ ٤

Kama mnavyojionea hapo kuna “skun” kwenye “ha” حْ. "Skun" au wengine wanaita "sakna”, pia kuna “kasra” chini ya Ya, hizo zinamaanisha kuna Ya (Y) nyingine baada ya "Ya" (Y) inayotamkwa. Na hivyo ndio jinsi inavyoonyeshwa na hivyo ndivyo inavyotamkwa “stahiyiy”. Kama kuna wataalamu wa tajweed wananisoma lazima waseme "ndio ukweli".

Hata sisi tunaweza kutafuta audio au video ya wataalamu wa tajweed kwenye YouTube au popote ukajisikilizia.

Sehemu ya kuvutia (interesting) ni kwamba tahajia (spelling) zipo sawa na inavyotamkwa ni sawa kwa aya hizo zote mbili, aya Q 2:26 na katika aya Q 28:4.

Tuzipitie tafsir tofauti hapa chini kwa ufupi, tujionee wenyewe;

Atabari alilitafsiri neno hilo “haogopi” kwenye Q2:26 na kwa upande wa Q28:4 akatafsiri “kuwaweka” (keeping)

...wanawake wao hai, hii ndio kama maana ya msingi iliyompa Zamakshari (hii ni tafsiri pia) alitumie neno sawa na “hayat” ambayo ni uhai au kuishi.

Nimeweka hayo kwa ufupi tu lakini ukipitia ukajisomea, utajionea karibia tafsiri zote zipo kwenye kuhitilafiana kwa maana ya hilo neno kutoka aya moja na nyingine.

In shaa Allah ikifikia wakati wa kuitafuta maana kamili ya 28.Surat Al-Qas'as' tutajionea maana kusudiwa ya aya hiyo/hizo.

Kwenye maana yetu sisi ya “la yastahyiy” tumesema; ... “hatafuti” ; Mwenyezi Mungu hatafuti kuleta ugumu katika Maisha...

Baada ya neno hilo, sasa tuendelee kupiga mbizi, vipi tumeipata maaana kamili ya hizo aya kwa kutumia mbinu za tafsil, kiota na ndimi “lisan” kwa maneno mengine;

Tutazame neno mbu ”baudha” بَعُوضَة(C), tutaona kabla ya neno hilo kuna neno “ma” مَّا. Neno “baudha”.

Neno “baudha” ili kulifanyia tafsil inabidi tuingie kwenye elimu ya lugha ya Kiarabu kidogo, tukilitamka peke yake kama lilivyo andikwa inabidi tulitamke “baudhatun” kwa kua mwishoni mwake lina herufi “Ta” iliofungwa (Ta marbuta) ة.

Kwenye lugha ya Kiarabu kuna elimu inayoitwa “elimu ya “Sarf”, Kingereza chake ni “morpheme”, katika elimu ya sarf tunajifunza kua kuna maneno “mzazi” (parent words” ambayo hayabadili maana ya neno yanapongezewa kionjo bali hubadili matumizi ya hilo neno. Mfano mdogo ni neno “faul”, nikisema “hamala” ambayo inamaanisha “kubeba” nikisema “Hamil” inakua ni mbebaji, sarf yake ni “fail”, mtendaji, yule anaebeba “hamil”. Nikisema “mahmoul” ambayo ni sarf ya “maf’ul” inamaanisha “amebebwa”,

Kwa ufupi ndio utamu wa vionjo (sarf) vya lugha ya Kiarabu.

Tukirudi kwenye neno letu “baudha” bila herufi ya "ta" iliofungwa, linakua ni “baudh”

...

Kisa cha Adam 2.3

Baada ya kupitia "sarf" za maneno mbali mbali tumefikia tamati kua neno hilo halimaanishi mbu kwenye aya ya 26 na maana yake ni kama tulivoiweka kwenye ufafanuzi wetu juu hapo. Pia hakuna methali yoyote ya mbu au nyingine inayoongelewa hapo.

Pia naweza kusema hakuna hata mfano hapo bali kuna taarifa ya mbinu za ki qur’an zinazotumika Qur’an nzima. Ni tamko jema kutoka kwa Muumba wetu ambalo lipo mwanzo mwanzo wa Qur’an ili kutuongoza.

Neno "ma" liliopo kabla ya neno "baudh" ni la kukanusha, mfano mzuri na mwepesi kwa Kiarabu ni pale tunaposema nenpo "Fi" , maana hyake ipo. Na tukiiongezea "ma" kavbla ya "fi" inakua 'mafii" yaani 'hakuna.".

Cha kushangaza, sifahamu kwanini watafsiri walio wengi, kama si wote, hawakulitumia neno hilo katika tafsiri zao na mpaka wengine wamefikia kusema hilo ni neno la ziada. Hili tunaweza kulitolea ufafanuzi zaidi likiulizwa kipekee, kwani pia kuna baadhi ya watafsiri wamelipa maana nyingine.

Mimi naamini Qur’an haina neno au herufi ya ziada. Naamini kua kila neno au herufi iliotumika ndani ya Qur’an ina maana yake na sababu zake kamili kuwepo, labda iwe bado tu hatujajaaliwa kulijua. AlhamduliLlah sisi tumejaaliwa kuliona na kulitumia neno hilo na kufikia ufanunuzi tulioutoa wa aya hio.

Tukirudi juu hapo kwenye aya ya 27 inaweka wai kabisa kua hicho ni kikundi kimojawapo miongoni mwa vikundi vya Bani Israel, tafadhali rejea juu kidogo hapo tulipoweka ufafanuzi wa aya ya 27.

Natamani wasomaji waniulize kuhusu ahadi iliotajwa katika aya ya 27.

Kuna vitu muhimu sana vya kuvizungatia kabla hatujaendelea. Navyo ni kujionea wenyewe jinsi aya ya 26 na 27 zilivyoungana, yote yaliopo kwenye aya 26 ndio hayo hayo yanaendelea kuongelewa aya ya 27 na kuendelea. Qur’an tumesema ipo kama kiota, imeungana na kiushikana yote.

Tusifanye kosa la kama tunavyofanya wengi wetu, kufikia kutoa maamuzi ya aya fuani kuitengenisha na aya nyingine kabla hatujaielewa hata hio aya.

In shaa Allah tuendelee na aya ya 28 na tutajionea mambo yanaanza kua myepesi kila tunavyotumia mbinu ya kiota, kuunganisha ayat na sio kuziwachanisha.

...
 
Mbona yote tayar yamo humu.... Simba kishaelekeza, vingine ufanye kucopy yeye alivyokuwa anafanya kuwaita jinn 1, 2 na Bakora (ile ndo njia rahisi zaidi)

Pia cha kutia akilini n kuwa, hii unafanya kwa majini ambao tayar unafahamiana nao Yan ambao upo nao karibu🤝🤝

Ili kuepusha side effect za viumbe wa kiroho
(Usisome uzi Kama story vipo vingi vya kujifunza🚶
Point yangu ipo hapo uliposema ''kwa majini ambao tayari unafahamiana nao''.
najaribu ku- analyse maelezo yako na simba conclusion nayopata nikuwa:-
Njia ya kumita jini na akaja kwa kumtaja jina au kuita tu inafanya kazi kwa mtu ambaye tayari yupo connected na majini hao mfano simba anavyowaita jini 1 na 2 au wewe unavyowaita ulisema upo connected nao kwa sababu ya mzee wako kama sijakosea.
Sasa hapa nina swali vipi kwa mtu ambaye hayupo connected na majini anaweza tumia njia hiyo? kama hapana atumie njia gani akitaka kumuita jini tofauti na jinn catching na ouija board?
Swali la nyongeza hapohapo, Nilisikia kuwa mtu mwenye majini kuna vitu akila inaweza kuwa sababu ya jini kupanda au kuna udi akivuta harufu yake jini anapanada je kuna ukweli katika hili.
cc: Arsis
 
Point yangu ipo hapo uliposema ''kwa majini ambao tayari unafahamiana nao''.
najaribu ku- analyse maelezo yako na simba conclusion nayopata nikuwa:-
Njia ya kumita jini na akaja kwa kumtaja jina au kuita tu inafanya kazi kwa mtu ambaye tayari yupo connected na majini hao mfano simba anavyowaita jini 1 na 2 au wewe unavyowaita ulisema upo connected nao kwa sababu ya mzee wako kama sijakosea.
Sasa hapa nina swali vipi kwa mtu ambaye hayupo connected na majini anaweza tumia njia hiyo? kama hapana atumie njia gani akitaka kumuita jini tofauti na jinn catching na ouija board?
Swali la nyongeza hapohapo, Nilisikia kuwa mtu mwenye majini kuna vitu akila inaweza kuwa sababu ya jini kupanda au kuna udi akivuta harufu yake jini anapanada je kuna ukweli katika hili.
cc: Arsis
Nakumbuka nilikuelezea nyuma huko.

Nini ambacho hujakifahamu? Nikufafanulie zaidi.
Simba.
 
Arsis hongera kwa uzi huu, nimekuwa nikiufatilia kwa makini na nimejifunza mengi sana ambayo sikuwa nayafahamu.
Ila nina shida ya kigugumizi kikali sana, na kazi yangu mara nyingi ni ya kuongea hivyo napata ugumu sana kuitekeleza, Je kwa kumshirikisha bakora naweza kupata dawa ya kuondoa tatizo langu?
 
Nakumbuka nilikuelezea nyuma huko.

Nini ambacho hujakifahamu? Nikufafanulie zaidi.
Simba.
ulifafanua kuhusu njia za kuwaita ndio ila nimeona njia zile zinafanyakazi kwa mtu aliye connected tayari na majini, Ndio nauliza ukitoa njia ya jinn catching na oujia board je kuna njia nyingine mtu ambaye hayupo connected na majini anaweza ita jini?
na nimeongeza swali hapo kuwa nilipata sikia mtu mwenye shida ya majini kuna vyakula akila au harufu za udi akinusa vinasababisha jini kupanda, Je ni kweli?
 
Arsis ana wanafunzi wake na mim kamai kijana ninaomba niwe mwanafunzi wake nijionee ya dunia..nipate maarifa and of course arsis si mtaalamu wa lugha? Sio mbaya na mimi nikajifunza something like "sole mio" "Adios amigo"😁 and so on,

Mimi naamini ni genius ni vile tu kukosa maarifa na shida ya usikivu kunanifanya nionekana wa hovyo but believe me when I sauy "naomba niwe mwanafunzi wako, please notice me"... Nipo chini ya miguu yako
 
Back
Top Bottom