Habari zenu ndugu zangu?
Kwanza kabisa nitoe pongezi za dhati kwa mleta mada na wachangiaji wote kwa ujumla.
Kuna elimu kubwa iliyojificha wengi hatuifahamu vzr lakini kwa mapitio yanayowasilishwa tumejikuta mengi kati yao yanatuhusu kwa kiasi fulani,kama halijakugusa wewe basi kuna mtu unamfahamu anapitia haya hata kwa uchache.
Natanguliza samahani km nitakuwa nmetoka nje ya mada.
Mimi nina mke na tumefunga ndoa miezi 4 iliyopita, umri wetu ni 20's. Tangu tumeoana kumekuwa na changamoto ambazo nyingi kati ya hizo ni kwa mke wangu kupata maradhi ya mara kwa mara na ndoto za ajabu nyingine za vitisho nyingine za maelekezo(kama maono juu ya kitu fulani) kwa maelezo yake mke wangu anasema yeye ana walimu tangu alivyokuwa mdogo na alipofikisha umri fulani baba yake aliwafunga hao walimu kwa maana walikuwa wakimuonesha vitu ambavyo vipo juu ya umri wake(mfano kuona uchawi au kitu kibaya)
Natamani kumsaidia mke wng lakini ukweli mimi sifahamu chochote kuhusu hao walimu na sijui nianzie wapi maana nikimshauri mke wng twende kwa baba yake anakataa hataki hata kusikia.
Nahitaji msaada kwa yoyote atakaekuwa na uelewa wowote juu ya hili, mke wng ana asili ya tanga amechanganya kabila la msambaa na mgunya.
Samahani kama kutakuwa na uwasilishaji mbaya kwny uandishi mimi sio mzoefu wa kuchangia hoja hapa jamii forum.
Shukrani kwenu M/mungu awabaribiki nyinyi na vizazi vyenu.