Nimeacha kazi: Nianzie wapi kwenye biashara?

Nimeacha kazi: Nianzie wapi kwenye biashara?

Kama we sio muoga na afya yako ni nzuri,na unae passport kazi hiyo apo nchini Dubai

Pima afya yako I mean HIV, TB and hepatitis B and C

Visa 630000 for 3 month
Air ticket 610000

Try your luckyView attachment 1249814
Screenshot_20191031-124744.jpeg
 
milioni mbili hiyo nimeikusanya kwa mwaka mzima sio kwamba nimeipata kwa mara moja. Ni kweli nimeacha kazi nikiwa bado sina detailed plan ya nini cha kufanya. ila ndo nimeshaacha na nnaamini nitasavaiv, hapa nimekuja kuomba ushauri kwa watu wenye uzoefu. Kama wewe unahisi nimeleta habari ya uongo ni siwezi kukuaminisha tofauti ila kama unaweza kunisaidia kwa mwongozo, nitakushukuru sana.
rafiki sijasema habari ya uwongo hapana , uwe na amani. bali kawaida mtu akidunduliza na kuona ana wazo flani na na anona laweza timia ndio anaacha kazi, sasa wewe umefanya kinyuma umedunduliza mwaka mzima , je wakati unadunduliza ulikuwa wadunduliza kwa ajili gani? si unaona lazima ulikuwa na wazo. maana biashara nayo ni passion , kuna biashara nyingi lakini lazima uwe na passion ya biashara flani tuanzie hapo
 
Sijaona haja ya kumuuliza hili Swali
ni kweli ila niliona tuanzie hapo, maana lazima at back of his/her mind alikuwa anawaza kitu tukianzia hapo tunajenga hoja ya kusaidia, hata Dr ukienda huanza kukuliza historia then anajua aanzie wapi
 
Habari zenu wana jamvi,

Nimeacha ajira kwa hasira. Nimefanya maamuzi ya kipuuzi? sijui! Ngoja nianzie mbali kidogo kuwasimulia:

Nilihitimu Shahada yangu ya Uhandisi mwaka jana na baada ya kukaa mtaani kwa miezi mitatu tu nilifanikiwa kupata ajira. Nilipata ajira kama fundi mchundo (Technician) na sio Muhandisi kama nilivyotegemea. Kwa kweli nilivunjika moyo kwa hilo kwa kuwa wakati huo naingia kazini niliingia na jamaa mmoja naye akaajiriwa kama Technician ila yeye amesoma Veta Level 2.

Kilichoniuma mimi ni kwamba nina Stashahada Ya Uhandisi Pamoja na Shahada ya Uhandisi alafu bado nalipwa sawa sawa na mtu mwenye cheti cha Veta, tena kiuhalisia yeye analipwa kiasi kikubwa kwa kuwa yeye hana makato ya Bodi ya Mkopo ila mimi bodi wananinyoosha.

Wakati naanza kazi nilimuuliza bosi wangu kwa nini naajiriwa kama Technician na sio Engineer, akanijibu kwamba nitaweza kupandishwa huko mbeleni kulingana na utendaji. Basi mimi nikaanza kazi.

Kwa kweli kazi ilikuwa na changamoto kwa sababu nilikuwa na majukumu mengi. Nikiwa ofisini nilikuwa nikihusika katika usanifu na kuandaa mpango kazi na nikiienda site nilikuwa napigika zaidi maana nilikuwa nahusika kwenye kusimamia kazi, ununuzi wa materials, na pia nilikuwa nikihusika katika kazi za kufanya kwa mikono.

Yaani kwa ufupi nilikuwa nikifanya kazi za fundi mpaka za muhandisi mimi mwenyewe. Katika mradi wangu wa kwanza nikagundua hata dereva analipwa pesa nyingi kuliko mimi, nikazidi kuumia.

Sasa bwana mwezi uliopita, mwisho wa mkataba wangu ukafika, bosi akaniita akanikabidhi mkataba mpya, lakini baada ya kuupitia nikagundua mshahara ni ule ule na cheo ni kile kile. Basi mimi nikamuomba bosi anipe siku moja nikafikirie alafu nitakuja kusaini au la. Baada ya siku moja nilirudi na nikaamua kuweka dau la mshahara ninaloona mimi ni sahihi. Kwa kifupi bosi alikataa na mimi nilikataa na mimi nikaishia hapo kufanya kazi.

Sasa turudi kwenye kichwa cha uzi huu. Naomba mnishauri niazie wapi maisha ya biashara maana kazi nimeshaacha (na sijui kama lilikuwa wazo la busara), hapa nina 2 million ambayo nilifanikiwa kuikusanya kwa mwaka huo mmoja niliokuwa nikifanya kazi.

Sijawaambia wazazi wangu wala watu wangu wa karibu kwamba nimeacha kazi na ninafikiria kwenda mkoa ambao nitakuwa mbali nao nikaaendelee kujifunza maisha huko.

Nipo tayari kufanya biashara ya hali yoyote, nakaribisha ushauri.

Asanteni.
Biashara ya kuingiza nyanya mjini kutoka mkoa inalipa sana kwa maelezo zaidi sogea mabibo kwa madalali
 
Nipo Kigoma, Kasulu kwa sasa.
Kwangu Kwa hiyo million mbili ni nyingi Sana na nitakushauri ifuatavyo Ila kabla ya yote pesa tamu huja Kwa maumivu na kudhalilika. Kuna tuliomaliza hizo degree tukadharaurika nyumban mpaka kuondoka Kwa hasira pasipokujua na plan.
Kwa kigoma fursa nitakupa fursa mbili.
Ya Kwanza hiii inapendeza hasa kipindi kuanzia mwezi wa tano kuelekea wa tisa.
Utengenezaji wa tofali za kuchoma kibiashara tena za quality nzuri.
Kwa ujumla kama umefanya KAZI kwenye ishu za ujenz utakuwa unajua jinsi tofali zinavosumbua hasa kipindi cha ujenz Sana Sana kigoma mjini. Na challenge kubwa inatokana na uhaba wa miti ya kuchomea na wengi wanaoifanya hiyo KAZI hawana Ile munkari ya kupata pesa ya kufa mtu.
Mfano ukiwa kigoma mjini vile vitofali vidogo saiz ya tako vinaenda Kwa bei ya 100 mpaka hamsini. Lakini kuna wanaotengeza kubwa kidogo wanauza mpaka 250.
Kukodi lorry mfano toka kidahwe mpaka kigoma mjini la tofali1000 ni kama 80000.
SASA wewe unaweza amua tafuta site nzuri yenye upatikanaji wa maji na udongo wa mfinyanzi mzuri unatafuta vijana wako hata watano na ukapiga hesabu zako labda wafyatue hata tofali 100000 huku wewe ukiwa unahudumia chakula na malazi . Pia kuhangaikia kuni za kuja chomea.zaid ya hapo ukadili pia kutafuta wateja wa kuwauzia kusud utapoivisha tanuri lako uuze na kuwalipa wafanyakazi wako. Ukifanikiwa fyatua tofali hata 100000 nzuri zile kubwa kubwa unauza hata Kwa bei ya 200 huwez kosa pesa.
Mradi wa pili huu ni mgumu sana nao ni kuingia vijijin ukawa unatafuta Mise ya hasa vijijin vya mwambao MWA ziwa Tanganyika ukipata unabangulisha kabisa unasafirisha kuleta kigoma mjini. Ukifika unakamulisha na kuuza mafuta na mashudu
 
- Tafuta frem anzisha kampuni yako ya ujenzi hasa ukilenga wateja wa kawaida wenye kazi na mahitaji ya ujenzi
- Buni ramani za nyumba za gharama nafuu ambazo watu wengi hujenga kisha uza hizo ramani kwa bei nafuu ambayo hata mwenye ndoto ya kutaka kujenga miaka 10 ijayo anaweza kushawishika kujenga.
- Anza kutengeneza connection na wadau wengi kwenye tasnia hiyo ya Ufundi ili ikitokea fursa inayohitaji huduma ya taaluma yako wakupe fursa.
- Fungua social media accounts kwa ajili ya hiyo taaluma na ofisi yako (niliyokushauri ufungue) Kisha uwe unatoa ushauri mbalimbali kuhusu mambo ya ujenzi, pia kwa watakaotaka ushauri zaidi waambie wakuone ofisini kwako na uwape ushauri BURE, ili uweze kupata connection na wateja hasa wanapovutiwa na ushauri mzuri uliowapa.
- tembelea maeneo ambayo yana miradi mingi ya ujenzi kama Dodoma, Kigamboni nk kutafuta fursa (mkaa bure sio sawa na mtembea bure).
- Tafuta location nzuri fungua duka la Hardware hata kama una 50,000 Nunua mfuko mmoja wa cement na misumari uza, kadiri siku zinavyoenda bidhaa kwa ajili ya kuuza zitaongezeka.
- Nunua vifaa muhimu vya ujenzi ambavyo mara nyingi watu hupenda kukodisha ili uwe unakodisha.
- Kifupi Fanya biashara zinazoendana na taaluma uliyosomea kwani ina wigo mpana sana na ina fursa nyingi.
- Kama kweli umeweza kupata uchungu kwa malipo hafifu ya kuajiriwa, basi jua kuwa una roho ya biashara tena yule mfanyabiashara mwenye mafanikio. Jiandae kwa changamoto lakini usikate tamaa wala kurudi nyuma.
 
bado taarifa zimepinda. unafanya kazi, unapata million mbili huyo! unatimka na kuanza kuplan uifanyike kazi gani!! nilihani inaacha kazi una mikllion mbili tayari umepata fursa sasa unaona million mbili kwa mradi wako ukizifanyia zitakuwa a faia kuliko kazi hiyo.
hapo hajafunguka! unless hakuwa na kazi sasa kakwapua pahala anajikuta ana million mbili na hajui azifanyire nini!! Lakini wafabnya kazi , unalipwa unapata million mbili unaamua kupumzika kazi halafu unaleta jamvini hapo kwanza tuambie wewe una mawazo gani tuanzie hapo
Ngoja nicheke kwanza[emoji1787][emoji1787][emoji23]

Umeusoma Uzi wake vizuri mkuu?
 
Kwangu Kwa hiyo million mbili ni nyingi Sana na nitakushauri ifuatavyo Ila kabla ya yote pesa tamu huja Kwa maumivu na kudhalilika. Kuna tuliomaliza hizo degree tukadharaurika nyumban mpaka kuondoka Kwa hasira pasipokujua na plan.
Kwa kigoma fursa nitakupa fursa mbili.
Ya Kwanza hiii inapendeza hasa kipindi kuanzia mwezi wa tano kuelekea wa tisa.
Utengenezaji wa tofali za kuchoma kibiashara tena za quality nzuri.
Kwa ujumla kama umefanya KAZI kwenye ishu za ujenz utakuwa unajua jinsi tofali zinavosumbua hasa kipindi cha ujenz Sana Sana kigoma mjini. Na challenge kubwa inatokana na uhaba wa miti ya kuchomea na wengi wanaoifanya hiyo KAZI hawana Ile munkari ya kupata pesa ya kufa mtu.
Mfano ukiwa kigoma mjini vile vitofali vidogo saiz ya tako vinaenda Kwa bei ya 100 mpaka hamsini. Lakini kuna wanaotengeza kubwa kidogo wanauza mpaka 250.
Kukodi lorry mfano toka kidahwe mpaka kigoma mjini la tofali1000 ni kama 80000.
SASA wewe unaweza amua tafuta site nzuri yenye upatikanaji wa maji na udongo wa mfinyanzi mzuri unatafuta vijana wako hata watano na ukapiga hesabu zako labda wafyatue hata tofali 100000 huku wewe ukiwa unahudumia chakula na malazi . Pia kuhangaikia kuni za kuja chomea.zaid ya hapo ukadili pia kutafuta wateja wa kuwauzia kusud utapoivisha tanuri lako uuze na kuwalipa wafanyakazi wako. Ukifanikiwa fyatua tofali hata 100000 nzuri zile kubwa kubwa unauza hata Kwa bei ya 200 huwez kosa pesa.
Mradi wa pili huu ni mgumu sana nao ni kuingia vijijin ukawa unatafuta Mise ya hasa vijijin vya mwambao MWA ziwa Tanganyika ukipata unabangulisha kabisa unasafirisha kuleta kigoma mjini. Ukifika unakamulisha na kuuza mafuta na mashudu
Asante sana, je unafahamu zaidi kuhusu biashara ya mise? Je yenyewe ina msimu? Unaweza kuichanganua zaidi kama ulivyochanganua ishu ya tofali?
 
Witmak255,
Hapana ndugu mimi ni Civil Engineer. Karibu lakini uniambie hicho kitu.
Japo unahisi hukufanyiwa haki ila hiyo experience uliyoipata ni kubwa sana!! Mainjinia wengi wanajua theories tu lakini kazi za ufundi hawajui ila wewe tayri una theoury na una uzoefu full wa kazi za ufundi!!

Kitu cha muhimu zaidi ya yote ni kuhakikisha umesajiliwa na ERB either kama Gradute engineer au professional engineer!!

Then...

Wazo la kwanza, naamin unajua kutumia autocad na archcard/revit, anza kwa ku design simple houses then tumia mtandao wa kijamii kupost design zako... mtu akitaka una mchaji pesa plus akianza kujenga unaweza ongeza dau ili usimamie ujenzi na kuhakikisha jengo linajengwa kitaalamu!!

Wazo la pili, tafuta masela wako wawili watatu unao waamini then fungua kampuni ya ujenzi (hata class 6 si mbaya), hatua hii itaambatana na hatua ya kwanza, ukisha design jengo tumia kampuni yako kusimamia na kutekeleza ujenzi!!

Wazo la tatu...

Kama una ujuzi wa autocad na archcad tumia angalia fursa za freelancer... google "freelancer.com, upwork, fiverr" huko utakutana na freelancers wengine...go and compete, kama una ujuzi utapta tenda kwa kutumia ujuzi wako wa autocad/archcad!!

Wazo la mwisho!

Wazo lingine unaweza tafuta ajira kwenye kampuni ingine ya ujenzi, kwa ujuzi ulio nao unaweza pata dau zuri zaidi!!

Kila la heri mhandisi!
 
Back
Top Bottom