Mkuu naona maamuzi yako hayakuwa sahihi, kwasababu hata wewe hilo umeshalitambua. Milioni mbili nipesa nyingi endapo wakati unaacha kazi ungejua unaenda kufanya nini, vilevile nindogo sana sanaaaa tena sanaaaa kwasababu bado ujajua utaifanyia nini ili iongezeke huku nawewe ukila, ukivaa, nakulala.
Milioni mbili uliyoipata ndani yamwaka mmoja haikuwa ndogo kwasababu ndio ilikuwa kazi yako yakwanza toka umalize chuo. Vilevile umeweza kuweka akiba hiyo yamilion mbili hali yakuwa ulishakula, ukalipia room, ukavaa, umeonga, navitu vingine vidogovidogo umeshavifanya.
Hali yamaisha kwasasa ningumu sana na biashara ningumu sana mtu asikudanganye nasio kama nakukatisha tamaa ila ndio ukweli huo. Kwamazingira yaTZ mtu aliyetoka familia yahali yachini ukimkuta kajiajiri ujue kuna mawili hana elimu/vigezo vyakuajiriwa au kakosa ajira kabisa. Ila sikufichi ndoto zawengi nikuajiriwa nahuo ndio ukweli nayote hiyo nikutokana namazingira magumu yaupatikanaji mitaji namazingira magumu ya kibiashara.
Ndani yamwaka mmoja umeweza kumake milioni mbili inamaana ndani yamiaka mitano kazi hiyo hiyo ungeifanya vizuri bila kuongeza majukumu basi ungekuwa namilioni kumi!!! Miaka mitano unaweza kuiona mingi namilioni kumi unaweza kuiona ndogo kwakuipata ndani yamiaka hiyo mitano ila amini nakwambia miaka mitano inaweza kufika usiwe nahiyo milioni 10 ukawa hivyo hivyo ulivyo sana sana ukawa umenunua vitu vyandani tu ambavyo thamani yake isizidi milioni 1.5
Naamini kama umeacha kazi ukiwa namilioni mbili hiyo hiyo basi naamini tayari imeshapungua sio tena milioni mbili nakama ujaipunguza hiyo Milion mbili yako basi tayari umeshapunguza pocket money yako bila kuingiza kitu so namilioni mbili yako soon utaichokonoa2.
USHAURI: biashara ndio kama unaianza nakama ujawahi kufanya biashara naumetokea familia zetu hizi zakajamba nani, mara nyingi tunachoangalia katika hatua zamwanzo wabiashara ikuingizie faida yakula, kulipia room, na mengine mambo madogomadogo. Biashara ikishakuwezesha hayo hapo juu ndio utapata matamanio yakuiwezesha ili ikupatie pesa nyingi kwaajili ya maendeleo yako mwenyewe najamii nzima iliyokuzunguka yaani ndugu zako.
So angalia katika mazingira hayo uliyopo utafanya biashara gani unayoipenda nakuimudu kuifanya kwamoyo wako wote mpaka isimame ili iweze kukuletea maendeleo. Kisha wafate moja kwamoja wazoefu wahiyo biashara ili wakupe A-Z yahiyo biashara nawala usione aibu. Nahuo ndio ushauri wangu.
Poleni kwagazeti hili lanipashe.