CHASHA FARMING
JF-Expert Member
- Jun 4, 2011
- 7,872
- 9,263
Maisha sio kuajiriwa tu. labda riziki yake haiko huko kwenye kuajiriwa na Mungu alimpangia apewe mshahara mdogo ili aondoke huko make maisha yake hayako huko bali yako kwenye kuajiri.
Hivyo si kwamba kuajiriwa ndo kila kitu mkuu kwenye Dunia hii ya leo na pia hayo ni maamuzi yake binafisi sasa unapo anza kumpinga kwa maamuzi yake binafisi inakuwa sio kabisa
Hivyo si kwamba kuajiriwa ndo kila kitu mkuu kwenye Dunia hii ya leo na pia hayo ni maamuzi yake binafisi sasa unapo anza kumpinga kwa maamuzi yake binafisi inakuwa sio kabisa
Ungekuja kuomba ushauri kabla ya kuacha hiyo kazi, yaani kabla ya kumtunishia kifua huyo mwajiri wako; huenda ungepata mawazo mengi sana, yakiwemo hasi na chanya. Binafsi naona uliwahi sana kuacha hiyo kazi uliyokuwa ukiifanya. Ulitakiwa uvimilie miaka miwili au mitatu mbele kabla ya kuchukua uamuzi uliouchukua.
Siku zote wenzako tunaamini kwenye ile methali ya "mvumilivu hula mbivu" na pia ile ya "Haraka haraka haina mbaraka". Umeingiwa na wivu kumuona dereva analipwa mshahara mkubwa kuliko wewe! Unalipwa mshahara sawa na mtu wa level 2 huku ukiwa na stashahada na shahada juu!
Je, unafahamu amefanya kazi kwenye hiyo kampuni kwa muda gani? Unazifahamu changamoto alizopitia? Uvumilivu na uaminifu wake kwenye kampuni unaufahamu? Mahusiano yake na mwenye kampuni unayafahamu?
Mimi naona kiburi cha elimu kilikuponza na hivyo kuamua kuacha kazi eti ukajiajiri kwa kitu ambacho hata hukifahamu na kwa mtaji mdogo wa milioni 2 (Pesa hii ni nyingi kwa mjasiriamali aliyeanza na mtaji wa laki tano kushuka chini ila siyo kwa yule aliyekurupuka kama mtoa mada)
Ushauri wangu; Tafuta kazi nyingine ili urudi kwenye fani yako huku ukiendelea kujipanga kwa lengo la kuja kujiajiri siku za usoni.
Kwa sasa nadhani muda bado! Kama huamini, ingia kitaa halafu uone hiyo milioni mbili itakavyo pukutika ndani ya siku chache tu na kubakia huna kitu.