Nimeachwa na nimekubali, ingawa naumia moyoni

Nimeachwa na nimekubali, ingawa naumia moyoni

Scenario yako inafanana na yangu kidogo, mi nilimuacha mwanamke ninae mpenda nikiwa bado nampenda kwakua alifanya kosa moja tu ambalo nimejiwekea misingi sitamsamehe yoyote akifanya kosa hilo
Nikamwambia aniweke kwenye list ya watu wake waliokufa na hataniona tena,

kadri alivyokua anazidi kuniomba msamaha ndo jinsi nilivyokua nazidi kumchukia kila neno lake alilosema na yale aliyowahi kuyasema yote nilikua naona ni uongo sikumuamini tena na hata ningeishi nae nisingemuamini maisha yake yote

Alifikiri labda nilikua natania tu au ilikua ni hasira ila huo ndo msimamo wangu licha ya kuwa kweli nilimpenda lakin nimemuacha for my peace, dignity and survival

Mwanzo niliumia sana lakin nimejilazimisha hadi imefikia hatua sina hisia za upendo wowote kwake wala simchukii ila sitamani hata kumuona,

Kwa sasa sina hisia za kumpenda mwanamke yoyote nmekua kama chuma inayotembea.
 
Scenario yako inafanana na yangu kidogo, mi nilimuacha mwanamke ninae mpenda nikiwa bado nampenda kwakua alifanya kosa moja tu ambalo nimejiwekea misingi sitamsamehe yoyote akifanya kosa hilo
Nikamwambia aniweke kwenye list ya watu wake waliokufa na hataniona tena,

kadri alivyokua anazidi kuniomba msamaha ndo jinsi nilivyokua nazidi kumchukia kila neno lake alilosema na yale aliyowahi kuyasema yote nilikua naona ni uongo sikumuamini tena na hata ningeishi nae nisingemuamini maisha yake yote

Alifikiri labda nilikua natania tu au ilikua ni hasira ila huo ndo msimamo wangu licha ya kuwa kweli nilimpenda lakin nimemuacha for my peace, dignity and survival

Mwanzo niliumia sana lakin nimejilazimisha hadi imefikia hatua sina hisia za upendo wowote kwake wala simchukii ila sitamani hata kumuona,

Kwa sasa sina hisia za kumpenda mwanamke yoyote nmekua kama chuma inayotembea.
Aise
 
Umeberp akapiga🤣🤣🤣
Safi sana.

Pole mwaya.
 
Na pia nadhani ulijitoa sana kwake kwa kila kitu. Going forward be careful unapodeal na mwanadamu; na angalau uwe tayari kwa lo lote maana mwanadamu anaweza kubadilika wakati wo wote. Jitoe kwa upendo huku ukijua kuwa ni sadaka tu unatoa lakini siyo kwa kutegemea cho chote maana kusema kweli loyalty ya mtu huwezi kuinunua ama kwa material things wala upendo wako wa kweli. Mwanadamu anaweza kuwa kiumbe katili sana akiamua!

Lakini pia kama malengo yako yalikuwa safi kwa huyu binti (if your intentions were pure) basi ondoka na dhamira safi huku ukijua kuwa hukumpotezea muda wake...and the Universe will reward you handsomely. Mwache aende na mtakie mema ila usije ukashangaa huko mbele ya safari kama atataka kurudi tena.

Kwa sasa hakuna njia ya mkato. Kuumia ni lazima utaumia lakini utavuka. Kwa kadri muda unavyokwenda maumivu nayo polepole yatapungua; na nati hizo zinazokaza kwenye moyo zitaanza kuachia na furaha yako itarudi.

Na ni lazima uchukue tahadhari. Usije ukaishia kuchukia wanawake wote. Huyu hakuwa wako na imeonyesha hivyo. Hata kama ungelazimisha basi huko mbele ya safari ungeumia zaidi ya unavyoumia sasa. Angalia tu usije ukaenda huko ukilalama na kuita kila mwanamke ni laghai, mbwa na malaya. Hutakuwa sahihi. Na siku moja utakuja kumpata aliye wako ambaye atakuonyesha mwanamke mwema na waifu matirio yukoje. Endelea kumtafuta mwanamke huyo kwa roho njema, moyo safi na dhamira isiyo na mawaa na siku moja utampata tu.

Sasa umekua! 👏🏼👏🏼👏🏼💪💪
NAKAZIA 📌
 
Maisha ni lazima yaendelee.

Nakiri kwamba nilikuwa malaya sana zamani lakini nikaamua kubadilika baada ya kugundua kwamba mahusiano mengi kwa wakati mmoja yanapoteza muda, rasilimali fedha, yanadhoofisha mwili, akili n.k.

Nimekuwa kwenye mahusiano serious kwa takribani mwaka na nusu na Mwl mmoja wa Shule ya msingi. Mpole, msikivu, mcha Mungu, mnyenyekevu, sio mbinafsi, mshauri mzuri na zaidi ya yote amekuwa mfano bora wa mama wa familia. Nikaamua kumpenda kwa dhati. Nikawaambia hadi ma-x wangu. Nikawa najiachia nae, nikamtambulisha kwa baadhi ya wana.

Nikakaa kitako na Baba nipeleke barua ya posa, binti akaridhia. Barua ikaandikwa, mwanangu mmoja ambaye ameshaoa akakubali kuwa mshenga. Barua ilikuwa ipelekwe tangu j5 ya wiki iliyopita ila nikapata dharura tukaahirisha. Ilikuwa baada ya kupeleka posa ndio nikamtambulishe home.

J'mosi ya juzi akaanza kubadilika kuanzia kwenye mawasiliano na kila kitu. Jana nampigia simu aniambie barua tupeleke lini, akashtuka kama hajui kinachoendelea! Akajibu nisubiri kwanza, mara anaomba tupeane muda kuna mambo ajiridhishe!

Nikajiongeza, nikamwambia muda siwezi kumpa kwasababu tulishalizungumza hili. Aseme tu kama anadhani hatuwezi kuwa pamoja tena nitamuelewa. Akasisitiza nimpe muda! Nikamjaribu kwa kumwambia tuachane ili tusipotezeane muda (kumbuka hapa nilikuwa namjaribu); ili nione anawaza nini.

Lahaulaa, akasema 'SAWA'. Nikaishiwa nguvu. Nilikuwa barabarani nikasimama kwanza kwasababu nilipatwa na wenge nikahisi naweza kusababisha ajali.

Ina maana ile kupenana muda ilikuwa ni gia tu, alishaamua tuachane. Sikumtafuta tena tangu jana na yeye kakaa kimya mpaka muda huu!

Huyu ni msichana aliyeniaminisha kwamba hawezi kuniacha. Kwamba hata nikijaribu kumuacha atafanya jambo baya (ni kama alikuwa anatishia kujiua).

LAWAMA ZANGU ZOTE NAZIELEKEZA KWA RAFIKI YAKE MWENYE JINA LINALOANZA NA HERUFI 'J', ANAYEISHI MKOA UNAOANZA NA HERUFI 'M'. Mpenzi wangu alikuwa anamsikiliza sana, na mara nyingi wamekuwa wakiniongelea, nina kila sababu ya kuamini kwamba ushauri wake umechangia kumfanya mwanamke wangu afikie uamuzi huu. Huyu dada yeye kaolewa, leo kaamua kumfanyia figisu rafiki yake! We dada wewee....

Biblia imesema tushukuru kwa kila jambo. Pengine kuna jambo Mungu ameniepusha nalo. Naumia ila najikaza.
Pole sana mkuu,mshukuru Mungu pia kwa kuwa hamkuwa mmefika mbali sana,
 
Pole Mkuu Amicus Curiae huwa naelewa sana falsafa zifuatazo katika mahusiano.

1. Ni makosa makubwa mwanamke kufahamu kuwa bila yeye mambo yako yatakwqma, hakika mwanamke akilijua hilo lazima akusumbue tu.

2. Hii inabebana na iyo ya kwanza, kamwe mwanaume haupaswi kujishusha mbele ya mwanamke hasa mwanamke uliye naye kwenye mahusiano. Huna sababu ya kujieleza kwa jambo lolote kwake. Ila muhimu wewe muheshimu tu na mipaka izingatiwe.

3. Usimuombe mwanamke kumuoa wewe fanya mambo yako hadi siku yeye atakapoomba wewe umuoe na kamwe usikubali akuendeshe au kukulazimisha kumuoa

Sasa Mkuu huyu mwanamke alijua bila yeye mambo yako hayataenda, huyo usihangaike naye kabisa funga ukurasa focus kwenye mambo mengine.

Pole sana Mkuu Amicus Curiae
Safi sana
 
Back
Top Bottom