Nimeambukizwa virusi vya UKIMWI (H.I.V)

Nimeambukizwa virusi vya UKIMWI (H.I.V)

Mdogo Angu soma hapa ni muhimu USIACHE Nitaandika maelezo marefu kwa sababu inahitaji kuongea zaidi ili uweze kuelewa plz nitajaribu kufupisha kadri navyoweza !

Polee Sana!

Matatizo tumeumbiwa binadamu,Kikubwa ni kuamini kwamba kila linalotukuta lina sababu Japo si Rahisi kuijua sababu kwa mara moja!

Kwanza kabisa Unaonekana bado upo kwenye denial na bado huamini kama Kweli unaweza kuwa na maambukizi, tuliza akili Mdogo wangu huu wakati ulionao ni wakati ambao akili yako bado haiamini kila kitu na inaamini sana kuwa bado muda unao na unaweza kupona na kuondoa Virusi hivyo mwilini..

Huu ni wakati ambao akili yako inaamini kuwa HIV ni kifo na kumbe swala hilo si la kweli!

Kwenye wakati huu wengi sana hupotea na tunapoteza Wengi kwa kukosa washauri wenye uelewa mzuri wa maswala ya maambukizi na wengi huamini kila kitu wanachoambiwa na kuona mitandaoni, Na huku wengine wakitapeliwa Pesa nyingi sana huku tatizo lao likibaki pale pale..

Huu ni wakati ambao unapaswa kutulia na kufata ushauri wa Daktari na washauri wengine mahali ambapo umeanza huduma ya Tiba na matunzo nafikiri kuliko wakati wowote ule....

Mpaka Sasa Si WHO, CDC,CRO, Medspace wala NIMR waliotangaza Dawa ambayo huenda ni mbadala wa ART..
Japo bado baadhi ya reseaech na procedure zinaendelea....

Kwahiyo ukitoa pesa ili kupata suluhisho la hilo tatizo lako utakuwa unaibiwa....

Na mdogo wangu naomba nikushauri katu asije mtu yoyote kukudanganya kuhusu Kuacha kutumia Dawa za ART kwa kigezo utumie Dawa zake...

Kwa sasa katika mwili wako kuna High production ya Virus wanamultiply sana na ndo maana ni wakati mbaya sana kuacha kunywa dawa!
HIV virus Si kirusi kinacho attack nutrients za mwili kwamba utakunywa dawa yenye protein ili kuzidisha protein na kufanya Waondoke mwilini...

NGOJA NIKUPE SOMO KUHUSU HIV NA DAWA ZA ART ZINAVYOFANYA KAZI ILI UPATE UELEWA KUWA ART NI BORA KULIKO HIZO MITISHAMBA

HIV Ni ina kirusi cha RNA na kinafahamika kama Retrovirus kwa kuwa kina tabia ya kujibadili na kuwa DNA kwa Kujichanganya Na vinasaba vya Mwili wa binadamu na hapo ndo huweza kubadili baadhi ya commands kwenye mwili na ku alter information za kawaida za mwili na kuamrisha mwili kutengeneza Wadudu ama virusi wengi kadri iwezavyo...

Utengenezwaji huu na upangwaji wa Virusi (Virion)
Hufanyika kwa haraka sana ndani na nucleas na nje ya nucleas ya Cells za binadamu katika hali hiyo cells nyingi hushindwa kuhimili Hali hiyo na nyingi huwa weak na kuharibika...sana sana hizi Tcells aina ya CD4 Kwakuwa ndiyo attachment yake na receptor au kufuli l funguo yake ndipo lilipo...

Kuna hatua kadhaa hufanyika ili kirusi kiweze kutengenezwa na kuharibu cells hatua hizo ni...
  • Kufungamana au kujishikiza kwenye cells ambayo ni cells ya CD4 (CD4 receptors- CCR5) kwa lugha nyingine huitwa Binding au Attachements
  • Kuungana au Fusion kirusi huingia ndani ya cells na kutoa vitu vyake vilivyo ndani..
  • Kujibadilisha kwa lugha nyingine huitwa Reverse transcription--kwakuwa RNA ni vigumu kuweza kufanya transcription (Kutoa order katika miili yetu kumbuka order hutoka kwa DNA na hutumwa kwa mfumo wa mRNA) virusi hufanya reverse transcriPtion yaani hujibadili kutoka HIV-RNA na kuwa HIV DNA na hapa ndo shida huanza..
  • Hatua inayofuata ni kujizalisha kwa wingi inavyowezekana ili kupata virusi wengi hatua hii huitwa Replication..
  • Kwa kuwa Ndani ya cells katika replication ni utengezaji wa material tu hatua hii hufanyika Kupanga material zote zilizotengenezwa huitwa assembly
  • Hatua ya mwisho ni budding ni kutoka kwa ile ile virus zilizotengenzwa ili zikomae na kwenda kufanya hatua hizo kwenye cells nyingine....
Nafikir umeelewa kuhusu hizo hatua zote...
Hakuna dawa yoyote ya mitishamba itakayozuia hatua yoyote kufNyika....
Sasa ART ina kazi moja wapo ya kuzuia hatua hizo kufanyika ili kuzuia uharibifu wa cells zaid na kuongeza kinga kwa kufanya hivyo...

Kuna dawa za ART Zinazuia kufanyika kwa...
binding/attachments tunaziita CCR5 antagonist pia zipo Post attachment inhibitors
Pia zipo zinazuia hatua ya Fusion (Fusion inhibitors)
Hatua hizi za mwanzoni huwa ni ART za sindano na kwa Tanzania bado hatujawahi kuwa nazo kwa sababu ni ghali...
Na hatua zinazofuata zote huwa na inhibitors zake..
Lengo la kuzuia HIV kufanya hivyo vyote ni ili ishindwe kuzaliana na Mwili utashughulika na HIV zilizokuwa weak na hazieleweki through engalf system ya macrophages..

Sasa kwanini nimekuambia yote haya kwa sababu ya kukujengea Kujiamni mwenyewe kuwa bado Una nguvu na wala Usiwaze kuhusu hicho unachowaza uko sawa na kutumia dawa kutakuweka katika afya nzuri sana..

Ukiacha kutumia dawa kwa hali yoyote ile utasababisha usugu wa Dawa (Drugs Resistance) ambayo inaweza kupeleka kufail kwa matibabu ya ART (ART drugs Failure) na ukifika huku inakuwa ni hatari sana...kwa sababu ART tena haitaweza kufanya chochote kwwnye mwili wako..

Kwahiyo jitahidi unywe dawa kwa wakati na baada ya miezi sita Angalia hali ya virusi kama unatumia dawa na lishe bora unaweza kujikuta upo kundi la watu walio na kiasi kidogo sana cha HIV (TND for HIV in HVL- Target Not Detected for HIV in HIV VIRAL LOAD)..

Najua ni Safari ndefu lakini ni fupi kama utajiamini na kuondoa hofu yoyote..
Asante kwa muda wako..
Na kama una swali unaweza kuuliza

NB: hakuna mtu aliyepima HIV positive baada ya muda akawa negative unless kafanya Bone Marrow transplant na yenyewe huwa ina 5% ya curetage...
Kaka wakishacheki viral load wakiona ipo chini na CD4 zimebalance vizuri unaweza ukasimama kumeza dawa au bado zoezi la dawa litaendelea kama kawaida..
 
Kaka huu ugonjwa nimeupata mwaka huu mwez wa saba, nimegundua mwez wa kumi baada ya kujipima, nimeanza ARV's wiki moja nyuma. Kwanin mnabeza
Wewe!

Ulianza kutumia ARV za nini kama tayari afya yako sio mgogoro!?

Yaani ungeishi kawaida hata usingeugua kabisa!!!
Aliekuambia upime kwa ajili ya Nini!?
 
Nyie walokole mna tabu sana,

Huu ushauri wako ndio utamponya muhusika? Haya nenda kwenye Mahospitali ukawaombee wagonjwa wote ili wapone na warudi majumbani mwao.
Sijatoa ushauri wa kuponywa,
Yeye amtafute Mungu kwa bidii
Kuna utofauti wa kutafuta uponyaji na kumtafuta Mungu .
Watu wengi wanakimbilia uponyaji badala ya kumtufata Mungu
 
Huu ni utaalamu wa wataalamu, sio rahisi mim na jamii inayonizunguka kulifahamu ili
Ndio uchunguze. Muda unao maana ni maisha yote so we kuwa mdadisi tu.

Hata kama sio kupona fanya tu kama uchunguzi maana udadisi ndo akili
 
Wewe!

Ulianza kutumia ARV za nini kama tayari afya yako sio mgogoro!?

Yaani ungeishi kawaida hata usingeugua kabisa!!!
Aliekuambia upime kwa ajili ya Nini!?
Nilivyofika hospital walivyonipima na wao pia wakagundua ilo tatizo wakanipa matumaini then wakaniambia inabid niwahi kuanza dawa ivyo kesho kutu uje tukuanzishie dawa ndio nikaanza dawa,

walinihasa sana kwamba ni vyema nianze dawa mapema kabla ya virusi havijazaliana kwa wingi mwilini
 
Kaka wakishacheki viral load wakiona ipo chini na CD4 zimebalance vizuri unaweza ukasimama kumeza dawa au bado zoezi la dawa litaendelea kama kawaida..
Zoezi la kumeza dawa ni zoezi endelevu kwa maisha yako yote kwa sasa..kwani..
Mpaka sasa bado hakuna dawa ya kutibu moja kwa moja kama zitapatikana huenda itakuwa heri zaidi....

Hata kama HVL itaonyesha kiasi kidgo Sana cha HIV kwenye Damu au kiasi cha chini sana ambacho ni undetectable (TND) Huruhusiwi kuacha dawa kwani iliyofanya mpaka kuonekana na kupata majibu hayo ni hiyo hiyo dawa..
Ukiacha dawa utasababisha kuibuka kwa Mutant viral Species ambazo ni Hatari sana kwa Afya yako kwani zinaweza kusababisha hata usugu wa dawa na mwisho kushindwa kwa matibabu..na mwisho wa siku unaweza kupata AIDS
 
Kama umeanza dawa ni vizuri uendelee usikatishwe na walimwengu maana maisha ni yako mwenyewe na wategemezi wako. Kuna jamaa kadhaa tuliwapoteza baada ya kukataa hizo dawa. Ikifikia umepata fangasi kwenye ubongo aisee ni ngumu sana tena sana kuinuka tena
 
Mkuu unapona kabisa na ata nikipima baada ya mwaka au miaka haisomi kitu. Kuna yeyote unayemfahamu aliyepona kwa muda mref still ni Negative
Najaribu kuitafuta namba yake hapa halafu nitaku PM
 
Wewe!

Ulianza kutumia ARV za nini kama tayari afya yako sio mgogoro!?

Yaani ungeishi kawaida hata usingeugua kabisa!!!
Aliekuambia upime kwa ajili ya Nini!?
Acha kupotosha umma mkuu!
Neno dogo unaweza kulisema likaleta athari kubwa sana ambayo Matokeo yake huwa ni Irreversible..

Na ndo maana Sera ya Sasa Tanzania ni TEST and TREAT na imesaidia sana kupunguza kiwango cha maambukizi nchini kwa asilimia kubwa sana tumetoka kwenye Prevalence ya 9%. Kwa mwaka jana tuna Prevalence ya 5.0% Hii njia imesaidia sana kupunguza maambukizi mapya ....kupitia 95 95 95 ambayo zamani ilikuwa 90 90 90
 
Najaribu kuitafuta namba yake hapa halafu nitaku PM
Nitashukuru mkuu, Nitajaribu njia za dawa mbadala lakin ARV's sitoacha kumeza adi nihakikishiwe na madaktari kuwa ni Negative again but bila ivyo nitaendelea na mfumo[emoji17]
 
Habari wanaJF, mim ni kijana niliyekuwa ninajichunga na kuijari sana afya yangu kiasi cha kuwa na mabox ya vipimo vya H.I.V rapid test ghetto, ikiwa kama nimejichanganya bas nawahi dawa za PrEP,

Dawa za PrEP nimemeza round mbili yaani 2017, 2020 baada ya kucheza rough.

nilikuwa napima maambukizi na mwenza wangu mara kwa mara, Ivi sasa mwenza wangu anamalizia masomo ili mwakani July tuanze kuishi pamoja. sasa mwez Agosti mwaka huu nimekutana na mwanamke ambae tunameet na kusekx na uwa tunacheki afya sasa mwez huo nikapuuza kwakuwa tulicheki afya mwez May nikamla then maisha yakaendelea,

Mwez Octoba juzi tu nikajaribu kupima peke yangu ghetto nikakutana na mistari miwili CONTROL na 1, nilipima zaid ya mara tano apo apo gheto inasoma mistari miwili. Dah pressure ikawa kubwa.

Nikaenda Hospital napo inaonesha nipo POSITIVE, wakanianzishia dawa za ARV's adi sasa ninamaliza wiki tangu nianze dozi za ARV's. next wiki wananianzishia na dozi ya miezi sita ya Anti-T.B...

Juzi nipo YouTube nakuta kuna shuhuda nyingi sana kwamba kuna Mtaalamu anaponesha ili janga from POSITIVE to NEGATIVE anaitwa TR. MSIGWA, jaman waungwana kuna yeyote mwenye hakika na ili jambo ata ndugu yake alipata kupona kwa uyu docta maana kichwa kinawaka saiz sielewi, nikapata mawasiliano yake akaniambia dozi ni shilling 280k ya siku 45 inaitwa (4A9).

Wajameni ivi ili suala linaukweli dawa iyo ya Asili inasaidia kwa yeyote aliyawahi pata experience hii ata kwa ndugu yake kuhusu uyu mtaalamu TR. MSIGWA na dawa yake ya 4A9 maana ninawiki tu tangu nianze kumeza ARV's lakin naihis hali ya kuzichoka tayar. .

nawasilisha:

Kujichunga ni ku abstain, then ndo hayo ma box, pole.

"mabox ya vipimo vya H.I.V rapid test ghetto"
 
Zoezi la kumeza dawa ni zoezi endelevu kwa maisha yako yote kwa sasa..kwani..
Mpaka sasa bado hakuna dawa ya kutibu moja kwa moja kama zitapatikana huenda itakuwa heri zaidi....

Hata kama HVL itaonyesha kiasi kidgo Sana cha HIV kwenye Damu au kiasi cha chini sana ambacho ni undetectable (TND) Huruhusiwi kuacha dawa kwani iliyofanya mpaka kuonekana na kupata majibu hayo ni hiyo hiyo dawa..
Ukiacha dawa utasababisha kuibuka kwa Mutant viral Species ambazo ni Hatari sana kwa Afya yako kwani zinaweza kusababisha hata usugu wa dawa na mwisho kushindwa kwa matibabu..na mwisho wa siku unaweza kupata AIDS
mkuu inakuaje dozi ya PrEP iweze kuangamiza virusi vilivyoingia mwilini na wamesema havina dawa, au apo nimeshindwa kuelewa sawasawa
 
Nitashukuru mkuu, Nitajaribu njia za dawa mbadala lakin ARV's sitoacha kumeza adi nihakikishiwe na madaktari kuwa ni Negative again but bila ivyo nitaendelea na mfumo[emoji17]
Huyo Jamaa hataki hata kujitangaza hadharani lakini nikiipata namba ya ndugu yake nitakutumia.
 
Kujichunga ni ku abstain, then ndo hayo ma box, pole.

"mabox ya vipimo vya H.I.V rapid test ghetto"
ni ktk harakati ya kukikinga kitu ambacho saiz tayar kimeingia ndani ya mwili wangu tena kirahis kabisa
 
Habari wanaJF, mim ni kijana niliyekuwa ninajichunga na kuijari sana afya yangu kiasi cha kuwa na mabox ya vipimo vya H.I.V rapid test ghetto, ikiwa kama nimejichanganya bas nawahi dawa za PrEP,

Dawa za PrEP nimemeza round mbili yaani 2017, 2020 baada ya kucheza rough.

nilikuwa napima maambukizi na mwenza wangu mara kwa mara, Ivi sasa mwenza wangu anamalizia masomo ili mwakani July tuanze kuishi pamoja. sasa mwez Agosti mwaka huu nimekutana na mwanamke ambae tunameet na kusekx na uwa tunacheki afya sasa mwez huo nikapuuza kwakuwa tulicheki afya mwez May nikamla then maisha yakaendelea,

Mwez Octoba juzi tu nikajaribu kupima peke yangu ghetto nikakutana na mistari miwili CONTROL na 1, nilipima zaid ya mara tano apo apo gheto inasoma mistari miwili. Dah pressure ikawa kubwa.

Nikaenda Hospital napo inaonesha nipo POSITIVE, wakanianzishia dawa za ARV's adi sasa ninamaliza wiki tangu nianze dozi za ARV's. next wiki wananianzishia na dozi ya miezi sita ya Anti-T.B...

Juzi nipo YouTube nakuta kuna shuhuda nyingi sana kwamba kuna Mtaalamu anaponesha ili janga from POSITIVE to NEGATIVE anaitwa TR. MSIGWA, jaman waungwana kuna yeyote mwenye hakika na ili jambo ata ndugu yake alipata kupona kwa uyu docta maana kichwa kinawaka saiz sielewi, nikapata mawasiliano yake akaniambia dozi ni shilling 280k ya siku 45 inaitwa (4A9).

Wajameni ivi ili suala linaukweli dawa iyo ya Asili inasaidia kwa yeyote aliyawahi pata experience hii ata kwa ndugu yake kuhusu uyu mtaalamu TR. MSIGWA na dawa yake ya 4A9 maana ninawiki tu tangu nianze kumeza ARV's lakin naihis hali ya kuzichoka tayar. .

nawasilisha:
Imekaa kitapeli tapeli☹
 
Aliekuambia upime kwa ajili ya Nini!?
sasa shehe usipopima utajuaje hali ya afya yako?

ukipima ukajua hali yako ndo unaweza kujilinda we binafsi na kuwalinda wengine unaoshirikiana nao

nje ya hapo unaweza kuwa unaeneza hii shida kwa wengine bila kujua au unaleta mtoto duniani lakn ana maambukizi tayari sasa uo ni uchoyo na binafsi mkubwa hata mungu hapendi

linda kizazi hiki na cha baadae, acha kuishi gizani kapime ujue hali yako
 
Habari wanaJF, mim ni kijana niliyekuwa ninajichunga na kuijari sana afya yangu kiasi cha kuwa na mabox ya vipimo vya H.I.V rapid test ghetto, ikiwa kama nimejichanganya bas nawahi dawa za PrEP,

Dawa za PrEP nimemeza round mbili yaani 2017, 2020 baada ya kucheza rough.

nilikuwa napima maambukizi na mwenza wangu mara kwa mara, Ivi sasa mwenza wangu anamalizia masomo ili mwakani July tuanze kuishi pamoja. sasa mwez Agosti mwaka huu nimekutana na mwanamke ambae tunameet na kusekx na uwa tunacheki afya sasa mwez huo nikapuuza kwakuwa tulicheki afya mwez May nikamla then maisha yakaendelea,

Mwez Octoba juzi tu nikajaribu kupima peke yangu ghetto nikakutana na mistari miwili CONTROL na 1, nilipima zaid ya mara tano apo apo gheto inasoma mistari miwili. Dah pressure ikawa kubwa.

Nikaenda Hospital napo inaonesha nipo POSITIVE, wakanianzishia dawa za ARV's adi sasa ninamaliza wiki tangu nianze dozi za ARV's. next wiki wananianzishia na dozi ya miezi sita ya Anti-T.B...

Juzi nipo YouTube nakuta kuna shuhuda nyingi sana kwamba kuna Mtaalamu anaponesha ili janga from POSITIVE to NEGATIVE anaitwa TR. MSIGWA, jaman waungwana kuna yeyote mwenye hakika na ili jambo ata ndugu yake alipata kupona kwa uyu docta maana kichwa kinawaka saiz sielewi, nikapata mawasiliano yake akaniambia dozi ni shilling 280k ya siku 45 inaitwa (4A9).

Wajameni ivi ili suala linaukweli dawa iyo ya Asili inasaidia kwa yeyote aliyawahi pata experience hii ata kwa ndugu yake kuhusu uyu mtaalamu TR. MSIGWA na dawa yake ya 4A9 maana ninawiki tu tangu nianze kumeza ARV's lakin naihis hali ya kuzichoka tayar. .

nawasilisha:

Mkuu utaliwa hela zako?

Swali la kujiuliza kama kweli anaponya kwanini asiende CTC wapone watu.

Hizo Dawa zake zingekua zinaponya ungekua ushaona watu wanatoa ushuhuda! subir dawa walioifanyia utafiti huko ulaya
 
Back
Top Bottom