Nimeamini Kinachopiganiwa Gaza Ni Mafuta Na Gas

Sasa kama uzi sijausoma Insu ya mafuta nimeijuaje?.
Sema Uzi nimeusoma ila Nilichokiandika kipo nje na natamanio yako, hiyo ndiyo shida.
Kutaja Gaza Maline hakufanyi andiko lako liwe relivant.
Unauliza Gasi na Mafuta yatafikaje Ulaya wakati huo huo Ulaya ina mpango na mafuta toka Africa baada ya Putin kakazaa na Rubo yake.
By the way maandiko kama yanawatukanisha Hamas kuwa ni wapumbavu, wameanzisha vita ili Mafuta yao yachukuliwa na Wazayuni.
 
Ikiwa akili ama hekima kubwa ni KUAMINI Gaza kuna mafuta yanayowatoa udenda Waisrael basi hiyo akili mimi sihitaji.
Ni bora ni baki mjinga.
HINT: Ujinga wako haupo kwenye kukataa kuwa mafuta ndio yanayowatoa udenda Israel hapo Gaza.

Rudia kusoma tena ulichokiandika taratibu, utaona ujinga wako ulipo.
 
Sasa unadhani kwa madini aloandika mwamba hapa anaweza akawa team za hovyo kama zako?
 
HINT: Ujinga wako haupo kwenye kukataa kuwa mafuta ndio yanayowatoa udenda Israel hapo Gaza.

Rudia kusoma tena ulichokiandika taratibu, utaona ujinga wako ulipo.
Kuna hitaji akili ya uendawazimu kuamini kuwa Hamas walitumwa na IDF ili waue raia wao ili wachukue mafuta.
Mimi ngoja nichague kubaki Mjinga
 
Uzi mrefu nilikua nataka kuishia kati ila kila nikishuka nakuta nondo juu ya nondo nikaumaliza
Ila nahisi umenizidi elimu huu uzi ingawaje kwa uchache wa akili zangu sioni kama DT atamaliza madhila ya wapalestine hasa dhidi ya Israel bora ingekua dhidi ya Misri ama Syria angeweza kumaliza ingawaje DT kajipambanua sio mtu wakutabirika kabisaaaa
Pia Israel analengo mama ndio hilo lakuwahamisha wapalestine ila kama anashirikiana na Misri kwanini Misri asifungue kivuko cha Rafah
Maana uhakika Rafah ikifunguliwa malaki kama sio mamilioni kama sio wapalestine wote wataihama ghaza kwenda Misri
Pia Israel inajua kabisa kama haiwezi kupigana na hamas nandio maana mashambulio yake yooote anakua analenga raia moja kwa moja yaani ili waihame gaza
Ila sioni israel ikiifanikiwa kwenye hilo labda(ra) kama kivuko cha rafah kitafunguliwa
Waarabu wabaya sana hasa jordan na misri linapokuja suala la wapalestina ndio maana Mohammad Morsi hawakumuacha salama
Kama suala lipo hivyo Russia anafanyaje kama kaweza kwa Syria atawezaje kwa Israel maana nna imani hili atakua analijua
Ingawaje wazungu wote awe nani awe nani linapokuja suala la Israel hua lao moja usiwaamini na wala hawaaminiki
 
Kama ni kweli basi hii vita haitokaa iishe hadi mwisho wa hii dunia.

Hakuna mmoja anayeweza kuja kumwamini mwenzake wakati wowote ule.

Israel hataweza kukubali Palestine wapate maendeleo yoyote yale ya maana kwa hiyari.

Hawataki hata Taifa la Palestine liundwe.

So this cycle of violence will never end. Maana Israel wanaamini Palestine wakipata maendeleo, wanaweza kutaka kulifuta Taifa la Israel.
 
Kila kiongozi ana mazuri yake na mabaya yake. Obama ndiye raisi amepigana vita zaidi ya Clinton. Ameua sana akifatiwa na Bush Jr kwa miaka ya karibuni. Ameipa Iran nafsi ya kujipanga kwa nuclear. Ametetea ushoga kwa herufi kubwa duniani.
Trump ametukana sana watu weusi. Lakini yeye amejali nchi yake zaidi. Yaani amedili na kuongea uchumi kwa njia za kibiashara zaidi. Ameitambua Israel that is okay. Amepunguza gharama za vita kwa nchi kwa kurudisha majeshi nyumbani. Na anasema akiingia vita ya Ukraine itaisha. Kuisha kwa vita ya Ukraine kunaweza kutuliza vita ya hapo Gaza. Hata hivyo Trump ni pro Israel hili ni debatable.
Point yangu ni kila mtu ana kariba yake ya uongozi. Huwa namuona Trump anaongoza usa kifikra za kibiashara zaidi. Na siyo kiprotali za kijeshi na kuwaachia majenerals sijui majaji wamuingoze. Ndiyo maana upinzani kwake ni mkali zaidi.
 
leo hii mmesahau kuwa walipewa ofa ya kuachia mateka ili idf wasivamie Gaza ? unajuwa mmekuwa kama wehu , jambo lipo wazi ila mnang'ang'ania ujinga ili kujifurahisha , hao HAMAS ni wapumbav , hata Nyerere alipigania Uhuru lakin hakuhatarisha maisha ya raia wanyonge kwa kuchukua hatua zisizo na matumanini ya kufanikiwa bali ni kupelekea vifo vya raia tu
 
Wapalestina waende Jordan, simple
 
nyiny watu mna matatizo ya akili , oct 2023 mlikuwa mnashangilia upuuz wa Hamas , leo mnakuja na stori za Mafuta na Gas , lini mtaanza zitumia akili zenu ?
 
Huyu akili zake kama za bundi sasa Israel atoke westbank aje east afrca kweli??Umefikiria wakati unaandika huu ujinga wako??
kwahiyo Idf waliamka na kuanza shambulia Gaza ? kwann wasubilie mpk 2023 ? oct 2023 mlikuwa mnashangilia upuuz wa Hamas leo hii unasema mafuta sijui gesi , nyiny watu kichwani ni buree , tuliwaambia msishangilie mtawaponza wana Gaza HAMKUELEWA
 
Hakika wewe ni mjinga , usiyejua chochote , hao unaowatukuza wanatoa maeneo salama na bado wanayalipua.

Na hapo unajiona umeandika vya maana , kumbe umeandika pumba tupu.
 
Wewe hakuna unachofahamu hapo na inaonekana huna shughuli yoyote ya kufanya ndio maana unapoteza muda kuandika habari ndefu isiyo na maana.

Hivi hapo kwenye kijiwe chenu hamjui kwamba kwa sasa Marekani ndio nchi ya kwanza duniani kwa uzalishaji wa mafuta au bado mnafikiri ni Saudi Arabia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…