Nimeamini safari ya kuitafuta na kuishika ml 100 as cash ni ngumu mno. Najitaidi lakini yataka moyo!

amshapopo

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2014
Posts
1,834
Reaction score
4,161
Habari wakuu,

Kiukweli kwenye haya maisha sio lazima ufundishwe kila kitu. Kuna wakati unafika unajaribu kupambana na kulifanya jambo fulani ndipo unakuja kujua mtu mwenye mafanikio ni wa kumheshimu sana. Ml 100 kwa kuzitamka zinaweza kuonekana ni pesa kidogo sana but in reality kuna baadhi ya wafanyakazi wanastaafu na hawajawahi fikisha kiwango hichi cha pesa.

Nimepambana kuinvest kwa upande wangu nimeamini kuwa na kiwango hicho cha pesa yataka moyo. Now mimi nimefikisha 56ml as cash na nimeinvest UTT.

Je, wenzangu mliofikisha kiwango hicho cha pesa mlifanyeje, na kwa muda gani? Tupeane uzoefu
 
Ni 0.1% ya watanzania wenye kuwahi kumiliki 100m kwa cash ni 5% ya watanzania wana miliki assets ambazo zinaweza kuwapa 100m.......95% ya watanzania ni hand to mouth economy. Hi mada hapa sio mahara pake.
 
broo ukipata biashara iliyochangamka hiyo pesa utaona ndogo na humu humu kuna watu wanasonya kuhusu hiyo pesa uliyosema.... kila mtu anaweza pata hiyo pesa shida ni moja umeandaa mfereji upi kwa ajiri ya kukinga hiyo fedha kaka....
 
Baada ya miaka 10, 2034 utakuwa tayari na 100M. Ukiziacha huko huko UTT

Kwa sasa hivi endelea na harakati nyingine. Hiyo 56M, achana nayo wala hutakiwi kuifikiria.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…