Mkuu ni PM nikupeleke Tanga wilaya ya handeni lakini upande inao pakana na korogwe just KM 35 kutoka barabara kuu ya Tanga Dar.
Asante sana mkuu, ninatuma pm
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu ni PM nikupeleke Tanga wilaya ya handeni lakini upande inao pakana na korogwe just KM 35 kutoka barabara kuu ya Tanga Dar.
Elnino ;
naweza kupata kibarua cha kuwalimia watu kwa trakta huko uliko ; gharama ya kulima kwa ekari ni kiasi gani nifanye mahesabu.
Kwa mnaotaka kulima mahindi karibuni wilayani Mpwapwa ama Kongwa.................ulimaji wake ni nafuu na hautajutia.
JF
Hali ya uchumi ni ngumu sana kwa watu wote hasa tunategemea mwisho wa mwezi. Weekend nilijaribu kupiga hesabu za mishahara yangu in next 10 years....ooooooooooops hazikufika hata 500millions Tshs.
Kwa maneno mengine kama sintantafuta kitu mbadala mbali na mshahara wangu cha kufanya basi nishakufa maskini na sintakuwa na chochote cha kuwaachia wanangu.
Maisha ni magumu sana kadri siku zinavyoenda mbele, sasa nimeamua kuanza kilimo kwa mara ya pili, awamu hii natumia mshahara wangu kama mtaji, nimewaambia kwa mara ya pili sababu kilimo cha kwanza nilifanya pamoja na wazazi wangu hadi nilipomaliza form four miaka hiyo, hicho hakikuwa na manufaa yeyote sababu ya mtaji na ufahamu.
Kwa sasa nimeanza na heka 50 ( 70m by 70m), nipo morogoro - pale Tuliani. Heka zote zimeshalimwa sasa tunapanda - nita expand my project up to 1,000 in next 3 - 5 years.
Makadirioni kwamba kila hekari average ni gunia 30, nitategemea kupata gunia 1500 za mahindi kutokana na hekari zangu za sasa 50. Kila gunia average selling price ni Tshs 60,000. kwa hiyo nitapata average Tshs 90m by July this year.
Running cost itakuwa approx 5m, so super profit ni 85m by July 2010.
Sasa 85m kwa mtu anayepokea sh 1million kwa mwezi ni mshahara wake wa miaka 7 na ushee-- teh teh teh teh
By next year nitaexpand to 200 hektas, nitalipima shamba langu na nijaribu kutafuta mikopo katika mabenki - or mbia toka SA au Zimbabwe. by 2015 wakati Dr Slaa anakuwa Rais wa nchi nitakuwa millionea. sasa ole wenu mseme nimefanya ufisadi.
This is a challenge to you JF- hasa mnaopata less than 5m per month - think twice and join me.
Kumbuka shairi la darasa la nne - Kama mkitaka mali mtayapata shambani - huu ni wosia.
By Elnino
Wana JF,
Wengi sana wanataka kujua jee kwa miaka hii miwili (Misimu miwili ya kilimo) sasa tunaingia wa tatu je mafanikio yangu ni yapi, Challenges ni zipi? na najipangaje kwa msimu huu. Nitawaletea updates zote wiki hii.
In short kilimo lazima mtu ujipange vizuri si kuvamia - siwakatishi tamaa lakini nitawaambia kila kitu, wapi nilienda vizuri na wapi nilikosea, kwa nini na nilichukua hatua zipi na je kilimo bado ni njia pekee ya kumkomboa mtanzania maskini?
By Elnino
UPDATE KWA WANA JAMII
Msimu wa kilimo 2010
Kwanza kheri za xmas. Niliamua kulima heka 50 za kuanza ambapo nilinunua heka moja kwa Tshs. 50,000 kufanya jumla yote kuwa Tshs. 2.5m. Kilimo kilianza msimu wa kilimo 2010 ambapo heka zote zililimwa kwa Trekta kwa Tshs 30,000/- Kila hekari. Tulipanda mvua za mwanzo kwa mikoa ya morogoro ambapo ni Mid January.
Mahindi hayakuota kwa uhakika hivyo ilibidi turudie tena kupanda wakati wa kupalilia. Baada ya marudio tathmini ilionyesha Mahindi yameota vizuri sana hivyo ikanipa moyo wa kupata mafanikio.
Uangalizi ulikuwa mzuri kwani tuliweka kambi kule kule shambani, mimi pamoja na majukumu mengine ya kiofisi (muajiriwa) nilipata nafasi mara moja kwa mwezi atleast kutembelea na kuona jinsi kazi inavyokwenda.
Wakati wa mahindi kubeba watoto Mvua huko Tuliani ilipotea kwa muda, hapo tukawa na wasiwasi sana, ilivyorudi mahindi yakawa yamedhoofu, hata hivyo jambo hili halikunifanya niwe na mawazo mengi kwani bado wakulima wenyeji walinipatia moyo kwamba mavuno yatakuwa mazuri.
Kipindi cha mavuno nilikuwa shambani, kazi ilianza vizuri, tulivuna na kupigapiga mahindi yetu na kupaki kwenye magunia, hapa sasa ndiyo ilikuwa kuona matokeo ya kazi yetu yote tuliyoifanya tangu kununua shamba, kulima, kupalilia, kuvuna na parking.
Ndgu zangu kwa ufupi hali ilikuwa mbaya sana, malengo yangu hayakutimia hata nusu yake, tulipata magunia 60 tu kwa hekari zote 50. niliishiwa nguvu na niliamua mahindi hayo yabakie huko huko shambani kwa muda wakati natafakari wapi tumekwama na je option B ni ipi.
Labda niwape tu gharama kwa ufupi:
Ununuzi wa shamba 2.5m; Kulima kwa heka ni Tsh. 30,000; kupalilia kwa heka 15;000 hii ni pamoja na kurudia kurudia kupanda sehemu ambazo hazikuota; kuvuna tuliingiza nguvu kazi wenyewe plus additional ya Tshs. 50,000.
Jumla ya gharama zote bila Man Power yangu ya ndugu yangu ambaye ni Project Manager inakuwa Tshs. 4.8m. mapato tukapata gunia 60 @56,000 = 3,360,000/=
Msimu wa kilimo 2011:
Kumbukeni nilianza na magunia yangu 60 niliyopata hasara toka msimu uliopita (sikuyauza); baada ya kufanya tathmini kwa kina nikaona ni vigumu sana kutoka kwa kutumia hiki kilimo cha kizamani hasa ukizingatia sina mtaji wa kutosha, hivyo nikaamua kubadilisha plan nzima. Kwa sasa tukaamua msimu huu hatutafanya kilimo badala yake tutanunua mazao toka kwa wenzetu na kuuza wakati yatakapopanda bei, ingawa bado kwa wakati huo nilifikiria sana kufanya food processing yaani uchumi wa kilimo. (agro -economics)
Mwezi wa tatu mwaka huu, tulianza kuwapa advance wakulima wenzetu - Mahindi na pesa ili mavuno yakifika basi warudishe mkopo kwa mahindi. hapa ni hesabu zilifanyika sababu ukipata gunia moja basi utarudisha mawili na ukipata Tshs mia basi utarudisha mia mbili.
Hatukuwa na wasiwasi sababu hawa tuliowakopesha ni wakulima wenzetu na majirani - wakuu mwezi wa tano tulianza kupokea mafao, tulikusanya mahindi gunia mia 300. Gunia hizi hatukuziweka tu, nilianza muda huo huo mwezi wa tano kusafirisha dar kwa ajiri ya processing.
Animals food processing:
Moja kwa moja nilijiingiza kwenye processing ya vyakula vya mifugo kazi ambayo naifanya mpaka sasa, na bado tunanunua mahindi kwani hayo gunia 300 hayatoshi ya yaliisha mapema tu. Nimeshafungua kampuni ya inafanya kazi mpaka sasa ingawa mwanzo huwa mgumu ila tunafanya vizuri kwani sasa kampuni ina miezi sita na mapato yanaonekana.
Je nitaendelea na Kilimo au nitanunua mazao na kufanya food processing tu?
Wakuu kilimo si lelemama, lazima mtu ujipange kweli kweli, kwa sasa nasitisha kilimo kwa muda lakini nitaendelea na kufanya processing ya vyakula vya mifugo; ila bado nitakuwa vijijini kwani nahitaji haya mazao kwa kazi yangu hii.
Bado nina muda kama nilivyowaahidi kwamba kufikia 2015 basi niwe nimetokana na huu umaskini - kwa sasa mungu akibariki nitakuwa naachana na ajira mwezi tarehe kama ya leo mwakani kwani kazi za kampuni yangu zimeanza kuzidi na zinahitaji uwepo wangu.
Kwa wale mnaotaka kulima siwakatishi tamaa ila muwe waangalifu sana kwani katika kilimo unaweza kuingiza Tshs 10m then ukapata 2m tu, mimi nimebadilisha upepo kwa muda, nikirudi kwenye kilimo basi nitarudi kivingine si hivi.
Mwisho Xmas njema na Kheri ya mwaka mpya.
K
Mimi nitabakia mjini hapa hapo kukimbizana kimbizana tu na mgambo wa jiji mpaka kitaeleweka. mashambani siendi.
Mmh running cost ya 5m tu......I doubt very much
Maskini jeuri mzima kaka,
Hujajibu ombi langu la mbegu za mapapai mbegu fupi.
ndoto ka ya alinacha alipokuwa kabeba mayai akaishia kupasua. Anyway kilimo kinatoa ila jiandae kucmama wewe kama wewe c unaijua sirikali yetu inatuongopea tangu tunapata uhuru mpk leo kuwa kilimo n uti wa mgongo na hakijawah hata siku moja kuboresha mazngra. M n mkulima mzuri tu npo dabaga mufind iringa na songea magagura nalima mahindi karibu.
UPDATE KWA WANA JAMII
Msimu wa kilimo 2010
Wakati wa mahindi kubeba watoto Mvua huko Tuliani ilipotea kwa muda, hapo tukawa na wasiwasi sana, ilivyorudi mahindi yakawa yamedhoofu, hata hivyo jambo hili halikunifanya niwe na mawazo mengi kwani bado wakulima wenyeji walinipatia moyo kwamba mavuno yatakuwa mazuri.
Msimu wa kilimo 2011:
Kwa sasa tukaamua msimu huu hatutafanya kilimo badala yake tutanunua mazao toka kwa wenzetu na kuuza wakati yatakapopanda bei, ingawa bado kwa wakati huo nilifikiria sana kufanya food processing yaani uchumi wa kilimo. (agro -economics).
Animals food processing:
Moja kwa moja nilijiingiza kwenye processing ya vyakula vya mifugo kazi ambayo naifanya mpaka sasa, na bado tunanunua mahindi kwani hayo gunia 300 hayatoshi ya yaliisha mapema tu. Nimeshafungua kampuni ya inafanya kazi mpaka sasa ingawa mwanzo huwa mgumu ila tunafanya vizuri kwani sasa kampuni ina miezi sita na mapato yanaonekana.
Je nitaendelea na Kilimo au nitanunua mazao na kufanya food processing tu?
Wakuu kilimo si lelemama, lazima mtu ujipange kweli kweli, kwa sasa nasitisha kilimo kwa muda lakini nitaendelea na kufanya processing ya vyakula vya mifugo; ila bado nitakuwa vijijini kwani nahitaji haya mazao kwa kazi yangu hii.
Bado nina muda kama nilivyowaahidi kwamba kufikia 2015 basi niwe nimetokana na huu umaskini - kwa sasa mungu akibariki nitakuwa naachana na ajira mwezi tarehe kama ya leo mwakani kwani kazi za kampuni yangu zimeanza kuzidi na zinahitaji uwepo wangu.
Kwa wale mnaotaka kulima siwakatishi tamaa ila muwe waangalifu sana kwani katika kilimo unaweza kuingiza Tshs 10m then ukapata 2m tu, mimi nimebadilisha upepo kwa muda, nikirudi kwenye kilimo basi nitarudi kivingine si hivi.
Mwisho Xmas njema na Kheri ya mwaka mpya.
Elnin0:
Mkuu Elnino, asante kwa update hakika kuna mengi ya kujifunza. Nimefuatilia huu uzi tangu mwanzo na nafurahishwa na wazo la Agroprocessing. Pamoja na hasara uliyoipata kwenye msimu wa kwanza, mie nadhani ukipata suluhisho la tatizo la kwanza; ukosefu wa mvua!
Fani yangu mimi ni Rasilimali Maji, na huku ninapopiga boxi wakulima wengi wanahakikisha kuna maji endapo mvua hazikufanya vizuri; tena hawatumii gharama kubwa sana. Tukapata suluhisho la kupata maji kunyweshea mnazao kila mvua zinapochelewa basi inaweza kututoa.
Vipi ukafikiria combination ya kulima na Agroprocessing? kununua kutoka kwa wakulima wengine iwe nyongeza lakini sehemu kubwa itoke shambani kwako?
Fani yangu mimi ni Rasilimali Maji, na huku ninapopiga boxi wakulima wengi wanahakikisha kuna maji endapo mvua hazikufanya vizuri; tena hawatumii gharama kubwa sana. Tukapata suluhisho la kupata maji kunyweshea mnazao kila mvua zinapochelewa basi inaweza kututoa.
kwako?