Nimeamua Kulima kwa mara ya Pili kilimo cha mahindi

Nimeamua Kulima kwa mara ya Pili kilimo cha mahindi

Wakati mwingine kwenye mipango yako weka na assumptions, mahesabu huwa hayaendi hivyo. huu ni ushauri wangu kwako.

Nafikiri ameweka consideration hapo aliposema kisio la chini kabisa kimsingi ekari moja yawea kupa hadi gunia 30!
 
Ni wazo zuri mkubwa lakini kwa hii TZ ni kazi kwelikweli labda kwa Morogoro si unajua mvua hazieleweki watabiri wa hali ya hewa hawatendi kazi ipasavyo utafukia chini milioni zako tano unakuja kuvuna mabua au vijunia 20 sijui utakuwa umefanya nini!

Nakushauri kuandaa shamba mapema lima na panda mbegu kwa wakati pia panda zao ambalo litahimili kiasi cha mvua kitakachokwepo mwaka huo, ni sawa miaka ya nyuma ekari moja ulikuwa unaweza kupata gunia 40 za mahindi lakini siyo sasa kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa.

Usikurupuke itakula kwako.
 
Nzokanhyilu...............ulipata response kwenye hii? can I offer to share the cost? I too need this
Nina uwezo wa kuwatengenezea biz-plan katika wiki 2-3 at an affordable price kama bado ni wahitaji tafadhari ni-pm
 
Nzokanhyilu...............ulipata response kwenye hii? can I offer to share the cost? I too need this
Sikupata jibu kitu ambacho kilinishangaza kutokana na "mshikamano" niliokuwa nikiona hapa. Ila kupitia private network nilipata mtu na ninashughulikia. Ikiwa tayari, nikaikubali nitakushitua.

Otherwise msikilize Mbogela. Kuandika biz-plan mtu yeyote anaweza, hata mimi naweza nikiwa na facts /figures /numbers. Nakushauri ongea na mtu yeyote anayetoa huduma hiyo umsome majibu yake kabla hujaingia makubaliano.

Anayenishughulikia yeye ana specialize kwenye kilimo.
Katika mizunguko, quote za biz-plan nimepewa offer kati ya $300 hadi $1200 (!!).
 
hongera mzee kwa uamuzi mzuri,pia rasimilisha biashara ili usikumbwe na sunctions za kuuuza nje ya nchi mahindi yako
 
Hii sred kila nikiifuatilia sion kama mkuu ELNINO alifanikiwa au laa... aliandika vizuri sana lakini naona lasy edited ni march 2010...


anyway, naomba kama kuna mtu keshapata uzoefu wa kilimo kwa mwaka huu alivyovuna ilikuwa kiasi gani kwa ekari 1, na je mauzo yalikuwaje mwaka huu kwa gunia?

NOTE: from point of ur experience plz sio kusikia..

SENKS
 
kusema ukweli kilimo ni kizuri na watu wanatajirika kwa kilimo sema uvivu wetu na kutaka utajiri kirahisi ndio unatuponza ila ukitia nguvu kwenye kilimo hakika mshahara utausahau kabisa, ila kilimo ni bora ulime sehemu ambapo unaweza ukavuta maji na kumwagilia mvua zikigoma pia kilimo kinakatisha tamaa sana kwenye masoko, kilimo kinahitaji mtaji wa kutosha, mvua zikigoma unalima tena lkn kama mtaji mdogo mvua zikigoma msimu huo hulimi tena.

Soko la mazao kuna kipindi mavuno yanakuwa mengi kila mkulima anabarikiwa mazao yanakua mengi utauza kwa hasara, pia sera ya serikali kuzuia kuuza mazao nje nalo ni tatizo,wakati unalima huku ukihangaika na vibarua wapo kimya hawakusaidii chochote ukisha vuna tu wanakupangia bei na mahali pa kuuza, angalia wakulima wa kahawa wanalima kwa gharama kubwa wakisha vuna tu wanaambiwa wauze kwenye vyama vya ushirika kwa bei watakayo wao ushirika na tena ni kwa mkopo hata kama bei itapanda kwenye soko la dunia bado mkulima watamlipa ile ile aliyouzia.

Wanafaidi wafanyakazi wa ushirika, serikali inatakiwa uwaruhusu wakulima wauze kokote watakako pata soko, pia serikali itulinde wakulima ipige marufuku juice toka dubai wakati matunda yanaoza mashambani tanga, juice zitengenezwe hapa hapa, ipige marufuku nyanya toka nje kuokoa za wakulima wa iringa zinazo oza kwa kukosa soko, ipige marufuku apples toka africa kusini ili zile zinazozalishwa njombe kule uwemba zipate soko.

Ipige marufuku shahiri ya kutengenezea pombe ili wanaolima wapate soko, kama wakullima wazalisha kwa kiwango cha chini hao wanunuzi watoe mbegu na elimu kwa wakulima ila wazalishe wanavyo taka wao,wakati kiwanda cha ivory kinaanza kukamua mafuta ya alizeti walienda kwenye vijiji zinakolimwa alizeti kwa wingi na kutoa mbegu ya alizeti wanazotaka wao,wakulima wakalima na wao wakaja kununa kwa wingi hayo ndio yanatakiwa kufanyika hapa nchini kwetu na sisi vijana tutahamasika kulima maana soko litakuwepo,hv kule manyara shahiri na ngano si inakubari kule?kwann serikali haiwalizimisha hawa watengeneza bia kulima hapa hapa nchini?

kama wanavyo fanya viwanda vya sukari?miwa imekuwa mkombozi kwenye baadhi ya maeneo,wakulima wanalima kwakua soko lipo,nenda wilaya missenyi mkoan kagera ukaone watu walivyo hamasika na kilimo cha mua.
Hongera sana EL kwa uamuzi wa busara. Ila nadhani hapo kwenye bold kwangu mm ni pazuri mno kuwa kweli (too good to be true) please please naomba upadefend.
 
Leo inakaribia miaka miwili tangu El uanze kilimo. Mbona hujatupa feedback au labda mimi nilipitwa ulitoa?
 
Msuruhishi acha uchokonozi. inawezekana kuna mawili, alipata hasara au kilimo kilimotoa kisawasawa na yupo busy anavuna (may be mara ya tatu au ya nne)
 
Wakuu inawezekana mambo yake bomba hana muda wakuja hapa siunajua kilimo kinavyo toaga. kama mwadui vile
 
Hii sred kila nikiifuatilia sion kama mkuu ELNINO alifanikiwa au laa... aliandika vizuri sana lakini naona lasy edited ni march 2010...


anyway, naomba kama kuna mtu keshapata uzoefu wa kilimo kwa mwaka huu alivyovuna ilikuwa kiasi gani kwa ekari 1, na je mauzo yalikuwaje mwaka huu kwa gunia?

NOTE: from point of ur experience plz sio kusikia..

SENKS

Mradi wakilimo kama unaufanya serious hapa nchini unalipa! Issue kubwa ya msingi kuzongatia ni kujitoa katika kutegemea mgawo wa maji toka kwa Mwenyezi MUNGU-kuwa na chanzo chako hakika ni zaidi ya 50% ya mafanikio ya uwekezaji huo...

Mie pia najaribu. Nashukuru wana JF-majadiliano ya jamii yamesaidia kunipa "near correct modus operanda"! Kujifunza kwa malengo vs mafanikio na matatizo walipota wenzetu!

Nina ahidi ku-share matokeo! Keep it up guus kwani hii ni njia mbadala ya kuwa WEVI (kama una cha kuiba)
 
Wana JF,

Wengi sana wanataka kujua jee kwa miaka hii miwili (Misimu miwili ya kilimo) sasa tunaingia wa tatu je mafanikio yangu ni yapi, Challenges ni zipi? na najipangaje kwa msimu huu. Nitawaletea updates zote wiki hii.

In short kilimo lazima mtu ujipange vizuri si kuvamia - siwakatishi tamaa lakini nitawaambia kila kitu, wapi nilienda vizuri na wapi nilikosea, kwa nini na nilichukua hatua zipi na je kilimo bado ni njia pekee ya kumkomboa mtanzania maskini?
 
Heshima kwako ELNINO.


Uliyosema ni kweli mkuu wangu kilimo si lelemama lazima ukubali kuna kupata na kukosa Mkuu nasubiri nondo zako.


Wana JF,

Wengi sana wanataka kujua jee kwa miaka hii miwili (Misimu miwili ya kilimo) sasa tunaingia wa tatu je mafanikio yangu ni yapi, Challenges ni zipi? na najipangaje kwa msimu huu. Nitawaletea updates zote wiki hii.

In short kilimo lazima mtu ujipange vizuri si kuvamia - siwakatishi tamaa lakini nitawaambia kila kitu, wapi nilienda vizuri na wapi nilikosea, kwa nini na nilichukua hatua zipi na je kilimo bado ni njia pekee ya kumkomboa mtanzania maskini?
 
Wana JF,
Wengi sana wanataka kujua jee kwa miaka hii miwili (Misimu miwili ya kilimo) sasa tunaingia wa tatu je mafanikio yangu ni yapi, Challenges ni zipi? na najipangaje kwa msimu huu. Nitawaletea updates zote wiki hii.
In short kilimo lazima mtu ujipange vizuri si kuvamia - siwakatishi tamaa lakini nitawaambia kila kitu, wapi nilienda vizuri na wapi nilikosea, kwa nini na nilichukua hatua zipi na je kilimo bado ni njia pekee ya kumkomboa mtanzania maskini?
nilipatwa na wasiwasi sana juu ya uwepo wako, lakini nimefarijika kwa kuwa upo bado.

Kabla hujaleta nondo zako, nilijaribu kwenda kufanya utafiti mdogo wa kilimo cha mahindi wilayani chunya.
Nilichoka baada ya kufahamu kuwa kwa hekari uzalishaji ni wastani wajuu gunia 9 kwa hekari.

Gharama zote ukijumuisha unapata profit ya at most 50,000 kwa ekari. Ilinifanya nifikiri upaya dhamira yangu ya kilimo, na sasa nataka kilimo cha vitunguu maji.
 
Back
Top Bottom