Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
naomba report ya kazi yako kama kuna mafanikio katika kile ambacho ulipanga?
nataka kufanya kazi kama hiyo pia, ila uoga ndio unanikaba..
ni kweli lakini mazingira yanafanya hata nionekane nawasaidia, mtu ana heka 4 shambani lakini mwanae anahitaji kwenda shule, uniform pamoja na matumizi mengine, hakuna benki wala kitu cha kuweka rehani shamba lake apate pesa.Kilimo kweli kigumu, lakini to be fair unapowalangua wakulima nako nikuwatia umaskini na kuondoa uezekano wa wao kuondokana na umaskini.
Mkuu Malila.Mkuu EL asante,
Nikupongeze kwa ujasiri wa kusema ukweli wa hali halisi iliyokutokea.Nikupe shukrani pia kwa kutoacha kilimo na kuingia ktk usindikaji wa mazao ya kilimo. Hii ndio picha halisi ya kilimo cha kutegemea mvua.
Je hilo shamba unalifanyia nini kwa sasa? Je una mpango wa kuliuza? 2013 mimi nitaingia ktk kilimo cha mahindi rasmi huko Iringa,hopeful nitakuwa mteja wako ktk kiwanda chako.
Malila, kweli sijajua nitalifanya nini hilo shamba, kwani kuna kibanda kidogo na mifugo kiasi - kuna mtu anaishi pale.Mkuu EL asante,
Nikupongeze kwa ujasiri wa kusema ukweli wa hali halisi iliyokutokea.Nikupe shukrani pia kwa kutoacha kilimo na kuingia ktk usindikaji wa mazao ya kilimo. Hii ndio picha halisi ya kilimo cha kutegemea mvua.
Je hilo shamba unalifanyia nini kwa sasa? Je una mpango wa kuliuza? 2013 mimi nitaingia ktk kilimo cha mahindi rasmi huko Iringa,hopeful nitakuwa mteja wako ktk kiwanda chako.
Esther, Kwa ufupi hii biashara inahitaji pesa nyingi kiasi - ni vigumu kukupa mchanganuo lakini utahitaji machine ya processing complete approx 30m.Ni experience nzuri uliyoipata na ninaamini imewasaidia wengi. Nimekuwa encouraged sana na flexibility yako na hasa pale ulipoamua hata kutouza mazao ili kupata muda wa kufikiri nini kifanyike! Hongera!
Naomba kama utaweza tusaidie mchanganuo wa hii ya food processing ... gharama tangu mwanzo mpaka umeziingiza sokoni. Je kuna mashine unapaswa kununua? Ni tsh ngapi? Soko lako liko wapi? (I mean wateja wako wakubwa) na je soko hilo ni reliable?
Natanguliza shukurani!
mkuu upo? yes kilimo ni kizuri na kinaweza kumlipa mtu, lakini bila kuwa makini ni hatari, unaweza kujikuta unapoteza mtaji wote.Elnino, asante kwa habari na kutupa hali halisi ya huko.
Ntakutafuta siku moja nikiwa mitaa ya Morogoro/Dar kwani kuna mambo itakuwa vema kuongea moja kwa moja.
Habari kama hizi kwa kweli ni nzuri sana kwa watu kuja na kusoma ili wajue waanzie wapi na wategemee nini.
safi mkuu, kwa mfano mimi kijijini ambapo kuna shamba langu nawakilishwa na nakuwa napata updates zote (active member) za mipango ya kijiji chetu- na mapato yetu tunalipa kodi kadri tunavyopangiana wenyewe kwa maendeleo ya kijiji chetu.Brother El Nino nimekuelewa. Siamini serikali yaweza kufanya chochote manake vituko vilivyopo huko kwa wakuu wenyewe unaweza kujua nini cha ku-expect. Nothing!!. Rai yangu tu kwamba tujitahidi hata kwenye huo unyonyaji tujaribu kurejesha japo kidogo kwenye hiyo community tuliovuna ili walau ianze kujikongoja.
Mkuu Malila.
Wakati unaendelea nakujiandaa na kilimo cha mahindi 2013 inabidi niwe karibu nawewe maana namimi nampango huo huo maana kwa miaka mitatu nimekuwa nalima mpunga ifakara bila mafanikio yakuridhisha ivo nataka niugawe mtaji wangu mara mbili ktk mahindi na mpunga maana nimeshafanikiwa kupata nyenzo kidogo za kulimia.
JF
Hali ya uchumi ni ngumu sana kwa watu wote hasa tunategemea mwisho wa mwezi. Weekend nilijaribu kupiga hesabu za mishahara yangu in next 10 years....ooooooooooops hazikufika hata 500millions Tshs.
Kwa maneno mengine kama sintantafuta kitu mbadala mbali na mshahara wangu cha kufanya basi nishakufa maskini na sintakuwa na chochote cha kuwaachia wanangu.
Maisha ni magumu sana kadri siku zinavyoenda mbele, sasa nimeamua kuanza kilimo kwa mara ya pili, awamu hii natumia mshahara wangu kama mtaji, nimewaambia kwa mara ya pili sababu kilimo cha kwanza nilifanya pamoja na wazazi wangu hadi nilipomaliza form four miaka hiyo, hicho hakikuwa na manufaa yeyote sababu ya mtaji na ufahamu.
Kwa sasa nimeanza na heka 50 ( 70m by 70m), nipo morogoro - pale Tuliani. Heka zote zimeshalimwa sasa tunapanda - nita expand my project up to 1,000 in next 3 - 5 years.
Makadirioni kwamba kila hekari average ni gunia 30, nitategemea kupata gunia 1500 za mahindi kutokana na hekari zangu za sasa 50. Kila gunia average selling price ni Tshs 60,000. kwa hiyo nitapata average Tshs 90m by July this year.
Running cost itakuwa approx 5m, so super profit ni 85m by July 2010.
Sasa 85m kwa mtu anayepokea sh 1million kwa mwezi ni mshahara wake wa miaka 7 na ushee-- teh teh teh teh
By next year nitaexpand to 200 hektas, nitalipima shamba langu na nijaribu kutafuta mikopo katika mabenki - or mbia toka SA au Zimbabwe. by 2015 wakati Dr Slaa anakuwa Rais wa nchi nitakuwa millionea. sasa ole wenu mseme nimefanya ufisadi.
This is a challenge to you JF- hasa mnaopata less than 5m per month - think twice and join me.
Kumbuka shairi la darasa la nne - Kama mkitaka mali mtayapata shambani - huu ni wosia.
Natafuta mashamba mazuri ktk maeneo ambayo mvua si tatizo, pia maeneo ambayo naweza kulima soya/maharage. Nitakupa feedback kila nikipata fursa nzuri ktk kilimo cha mahindi.