Nimeamua 'kusilimu' je, kisheria na kiimani nitaruhusiwa kuongeza wake nikihitaji?

Nimeamua 'kusilimu' je, kisheria na kiimani nitaruhusiwa kuongeza wake nikihitaji?

Kufunga ndoa na mwanamke Myahudi au Mkristo inaruhusiwa kutokana na rai ya Maulamaa wengi.

Ibn Qudaamah (Allaah Amrehemu) alisema katika [Al-Mughni 7/99]: "Hakuna tofauti ya rai za maulamaa kuhusu kuruhusiwa kuwaoa wanawake wa Kitabu. Na miongoni mwa walio na rai hii ambayo ilisimuliwa kutoka kwao ni 'Umar, 'Uthmaan, Talhah, Hudhayfah, Salmaan, Jaabir na wengineo".



Ibn Al-Mundhir kasema: "Hakuna usimulizi ulio sahihi kutoka kizazi cha mwanzo kusema kwamba hivyo ni haraam. Al-Khallaal amesimulia katika Isnaad yake kwamba Hudhayfah, Talhah, Al-Jaaruud ibn Al-Mu'alla na Udhaynah Al-'Abdi wote walioa wanawake wa Ahlul-Kitaab. Hii pia ilikuwa ni rai ya maulamaa wengine wote"

.

Ushahidi mkuu kuhusu masuala haya ni aya ambayo Allaah سبحانه وتعالى Anasema (Na imefasiriwa kuwa na maana):



((الْيَوْمَ أُحِلَّ لَكُمُ الطَّيِّبَاتُ وَطَعَامُ الَّذِينَ أُوتُواْ الْكِتَابَ حِلٌّ لَّكُمْ وَطَعَامُكُمْ حِلُّ لَّهُمْ وَالْمُحْصَنَاتُ مِنَ الْمُؤْمِنَاتِ وَالْمُحْصَنَاتُ مِنَ الَّذِينَ أُوتُواْ الْكِتَابَ مِن قَبْلِكُمْ إِذَا آتَيْتُمُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ مُحْصِنِينَ غَيْرَ مُسَافِحِينَ وَلاَ مُتَّخِذِي أَخْدَانٍ وَمَن يَكْفُرْ بِالإِيمَانِ فَقَدْ حَبِطَ عَمَلُهُ وَهُوَ فِي الآخِرَةِ مِنَ الْخَاسِرِينَ))





((Leo mmehalalishiwa kila vilivyo vizuri. (vitu vyote vilivyo halaal, katika chakula Allaah Alichokifanya halaal kama nyama iliyochinjwa, maziwa, mafuta, mboga, matunda) Na chakula (Wanyama waliochinjwa na wengine wanolika) cha walio pewa Kitabu (Mayahudi na Manaswara) ni halali kwenu, na chakula chenu ni halali kwao. Na pia wanawake wema miongoni mwa Waumini, na wanawake wema miongoni mwa waliopewa Kitabu (Mayahudi na Manaswara) kabla yenu, mtakapowapa mahari yao, mkafunga nao ndoa, bila ya kufanya uhasharati wala kuwaweka kinyumba. Na anayekataa kuamini (Tawhiyd ya Allaah na nguzo zote za Imani yaani kuamini Allaah, Malaika Wake, Vitabu Vyake, Mitume Yake, Siku ya kufufuliwa, na Qadhaa na Qadar) bila shaka amali yake imepotea, naye katika Akhera atakuwa miongoni mwa wenye khasara)) [Al-Maaidah:5:5]



Maana ya Muhswanaat (wanawake wema) ni wale ambao walio huru na walio katika stara. (Yaani katika heshima na aliye bikra, asiye mhuni) Ibn Kathiyr (Allaah Amrehemu) amesema katika Tafsiyr yake:

"Hii ni rai ya maulamaa wengi wao na hii ndivyo inavyoelekea kuwa hali yenyewe. Asije kuwa dhimiyah (mwanamke asiye Muislam aliye katika hifadhi ya Kiislam) lakini pia asiyekuwa katika stara (heshima, bikra). Ikiwa atakuwa katika hali hii atakuwa amepotoka na mwenye ufisadi, na mumewe atamalizikia kuwa kama inavyoeleza katika methali: "Amenunua tende mbaya na amekhiniwa katika uzito na mizani pia" .



Maana iliyo dhahiri katika aya ni vile ilivyomaanisha "al-Muhsnah"(mwanamke mwenye stara, (aliyekuwa bikra, asiyekuwa mhuni) naye ni mwanamke aliyejiepusha na zinaa kama Allaah سبحانه وتعالى anavyosema katika Aya nyingine:



((مُحْصَنَاتٍ غَيْرَ مُسَافِحَاتٍ وَلاَ مُتَّخِذَاتِ أَخْدَانٍ))



((….wawe wanawake wema, si makahaba wala si mahawara)) An-Nisaa: 4:21





Wakristo na Mayahudi ni Makafiri na washirikina, kutokana na Qur'aan, lakini wametolewa katika kuharamishwa kuolewa wanawake wao kwa sababu Allaah سبحانه وتعالىAnasema katika aya yenye maana:





((وَلاَ تَنكِحُواْ الْمُشْرِكَاتِ حَتَّى يُؤْمِنَّ وَلأَمَةٌ مُّؤْمِنَةٌ خَيْرٌ مِّن مُّشْرِكَةٍ وَلَوْ أَعْجَبَتْكُمْ وَلاَ تُنكِحُواْ الْمُشِرِكِينَ حَتَّى يُؤْمِنُواْ وَلَعَبْدٌ مُّؤْمِنٌ خَيْرٌ مِّن مُّشْرِكٍ وَلَوْ أَعْجَبَكُمْ أُوْلَئِكَ يَدْعُونَ إِلَى النَّارِ وَاللّهُ يَدْعُوَ إِلَى الْجَنَّةِ وَالْمَغْفِرَةِ بِإِذْنِهِ وَيُبَيِّنُ آيَاتِهِ لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ))



((Wala msiwaoe wanawake washirikina mpaka waamini. Na mjakazi Muumini ni bora kuliko mshirikina hata akikupendezeni. Wala msiwaoze (binti zenu) wanaume washirikina mpaka waamini. Na mtumwa mwanamume Muumini ni bora kuliko mshirikina hata akikupendezeni. Hao wanaitia kwenye Moto, na Allaah Anaitia kwenye Pepo na maghafira kwa idhini Yake. Naye Huzibainisha Aya zake kwa watu ili wapate kukumbuka)) [Al-Baqarah: 2:221]





Hii ni njia ya dhahiri kabisa ya kuwafikiana baina ya aya mbili.





Allaah سبحانه وتعالى Amewaelezea kuwa ni washirikina kama Anavyosema:





((اتَّخَذُواْ أَحْبَارَهُمْ وَرُهْبَانَهُمْ أَرْبَابًا مِّن دُونِ اللّهِ وَالْمَسِيحَ ابْنَ مَرْيَمَ وَمَا أُمِرُواْ إِلاَّ لِيَعْبُدُواْ إِلَهًا وَاحِدًا لاَّ إِلَهَ إِلاَّ هُوَ سُبْحَانَهُ عَمَّا يُشْرِكُونَ))





((Wamewafanya makuhani wao na wamonaki wao kuwa ni marabi badala ya Allaah, na pia Masihi bin Maryamu. Na wala hawakuamrishwa isipo kuwa wamuabudu Mungu Mmoja, hapana mungu ila Yeye. Subhanahu, Ametakasika na hayo wanayomshirikisha nayo)) [At-Tawbah: 9:31]



Kwa hiyo 'Watu wa Vitabu' ni makafiri na washirikina, lakini Allaah سبحانه وتعالى Ameturuhusu kula nyama zao na kuwaoa wanawake wao ikiwa watakuwa wenye stara (wenye heshima sio wahuni). Hii imeruhusiwa kutokana na maana ya aya iliyo katika Suratul-Baqarah 2:221 (tulioitaja hapo juu).





Lakini ifahamike kwamba ni bora na usalama kabisa kutokuoa wanawake wa Kitabu khaswa kwa siku hizi.



Ibn Qudaamah (Allaah سبحانه وتعالىAmerehemu) alisema: Kwa vile hali ni hii, ni bora kutokuoa mwanamke wa Kitabu kwa sababu 'Umar aliwaambia wale waliowaoa wanawake wa Kitabu "Waacheni (Wapeni talaka)" kwa hiyo wakawapa talaka isipokuwa Hudhayfah. 'Umar akamuambia: "Mpe talaka". (Hudhayfah) akasema: "Je, Unashuhudia kuwa yeye ni haraam?" Akasema: "Yeye ni mkaa wa moto wenye kuwaka mpe talaka". Akasema: "Je, Unashuhudia kuwa yeye ni haraam?" Akasema: "Yeye ni mkaa wa moto wenye kuwaka". Akasema: "Najua kuwa yeye ni mkaa wa moto wenye kuwaka lakini yeye ni halali kwangu". Baada ya muda akampa talaka na akaulizwa "Kwa nini hukumpa talaka alipokuamrisha 'Umar?" Akasema: "Sikutaka watu wafikiri kuwa nimefanya kosa (kwa kumuoa)".

Labda alikuwa akimpenda au labda kwa sababu walipata mtoto pamoja kwa hiyo alimpenda". [Al-Mughni 7/99]

Vile vile Hadiyth hii ifuatayo Sahiyh inasema:



Ibn 'Umar alipokuwa akiulizwa kuhusu kumuoa mwanamke Mkristo au Myahudi, alikuwa akisema: "Allaah Ameifanya kuwa ni Haraam kwa Muumini kuoa wanawake wanaomshrikisha Allaah katika ibada, na sijui lililo kubwa zaidi kuliko kumshirikisha Allaah katika ibada na kadhalika kama mwanamke kusema 'Iysa ni Mungu ingawa yeye ni mja tu wa Allaah" [Al-Bukhaariy]





Shaykh Ibn Baaz (Allaah Amrehemu) alisema: "Ikiwa mwanamke wa Kitabu anajulikana kuwa ni mwenye stara (sio muhuni) na kujiepusha na njia ambazo zinampeleka mtu katika uasharati, inaruhusiwa kwa sababu Allaah سبحانه وتعالى Ameruhusu hivyo na Ameturuhusu kuwaoa wanawake wao na kula nyama zao.



Lakini siku hizi kuna khofu kwamba wale wanaooa huenda wakakutana na uovu zaidi. Wanaweza kuwaita katika dini yao na wanaweza kuwalea watoto wao katika Ukristo. Kwa hiyo hatari ipo hakika na ni kubwa. Ili kuwa katika amani, Muumini ni bora asiwaoe. Na katika hali nyingi hakuna uhakika kama mwanamke hatofanya vitendo vya uasharati au hatowaleta watoto waliotoka katika uhusiano wa mwanzo. Lakini mwanamume akitaka kufanya hivyo basi hana dhambi kwake ili ajiweke katika stara na ainamishe macho yake kwa kumuoa. Ajitahidi kumuita katika Uislamu na awe na hadhari na uovu wake na hadhari ya kumruhusu asimvute yeye au watoto wake katika ukafiri". [Fataawa Islaamiyyah, 3/172]

Na Allaah Anajua zaidi
 
c373258a29f05d6881248963d1d741c4.jpg
soma aya ya 5
 
Kwani mke hatambuliki wakati uislamu unaruhusu mwanaume kuoa mwanamke ambae ni ahlul kitab, ijapokuwa ni bora zaidi ukimsilimisha?
Hakuna ndoa kama hiyo mbele ya Uislamu, shari waamini kwanza(wasilimu)
 
Hakuna ndoa kama hiyo mbele ya Uislamu
Kasome surat al maida aya ya 5, usije na porojo zako, kisha nambie aya inasemaje {makafiri ndio imeharamishwa na sio ahlul kitab} kama huijui quran kaa kimya
 
Ila angekuwa alishakufuata mpoo iman moja ungemtaka ridhaa yake ya kuongeza MKE na akikukatLia hauruhcw kuoa
Si kwali kwamba uombe ridhaa kwa mke ndiyo hapana mwanamke anajulishwa tu na si kuombwa ruhusa.
Unapobadili dini unapaswa kufunga ndoa upya na mkeo uliomuoa kwa dini ya kikristu anapaswa kusilimu.
Hakuna ndoa ya mkristu na muislaam.
 
Chukulia katika mazingira ambayo ninauhuru (wa kikatiba) kuchagua dini yyte ile ninayoitaka. Na uhuru huu ninayo haki ya kuutekeleza wakati wowote ule. Sifungwi kubaki kwenye dini fulani.

Katika mazingira ya kuwa nimeoa mke kwa ndoa ya kikristo ambayo inaruhusu mke mmoja tu kwa mume mmoja na inatambulika hivyo kisheria. Nikiwa kwenye ndoa hiyo, kesho nikaamua kubadili dini na kuwa muislam na huko ninaruhusiwa kuwa na wake hadi wanne.

MASWALI:
1. Kwakua nitakua nimekana dini yangu ya awali, Je sheria itaendelea kumtambua huyu mke wa ndoa ya kikristo?

2. Hata kama tumeamua kuishi pamoja kama wanandoa (yeye abaki kuwa mkristo), je nitakua na uhuru kisheria kuongeza wake?

3. Hata kama tumeamua kuishi pamoja (na mke wangu naye abadili dini na kuwa muislam), je tutakuwa tumefunga ndoa au tutahitaji kuoana upya?

Nielewesheni kisheria na kwa imani ya kiislam pia.
Ukishabadili dini ndoa imekufa, inabakia kuwa huna ndoa yoyote hivyo ni wewe kuanza kazi upya ya kufunga aina ya ndoa upendayo
 
Namba 2 bado ina utata mkuu, unaizungumziaje aya ya Quran inayosema ".....mmeruhusiwa kuwaoa waliopewa kitabu...."??. Kumbuka nyakati za maswahaba wapo waliokuwa wanaishi na wanawake wa kiyahudi licha ya kuwa wanawake hao hawakuwa wamesilimu na mtume hakuwambia kuwa ndoa zao ni batili.
Maswali haya kwa sehemu kubwa ni ya kisharia yanatakiwa kujibiwa na wanazuoni. Kwa nilivopata elimu kidogo ni kuwa wote wakibadili dini ndoa inabaki ile ile ya awali. Ila mmoja akibadili kwakweli sifahamu.
Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amependekeza Muislamu aoe wanawake Waislamu walioshika dini. Kwa hiyo kwanza ni kufanya jitihada ya kuwaoa wanawake Waislamu walioshika dini kisha tena kama haikuwezekana ndio aelekee kwa Ahlul-Kitaab.

Na ifahamike kuwa ni bora na usalama kabisa kutokuoa wanawake wa Kitabu khaswa kwa siku hizi ila ikiwa atakubali kusilimu kisha atazamwe tabia yake na kama ataendeleza dini yake sawa sawa.



Ibn Qudaamah (Allaah Amerehemu) alisema: Kwa vile hali ni hii, ni bora kutokuoa mwanamke wa Kitabu kwa sababu 'Umar aliwaambia wale waliowaoa wanawake wa Kitabu "Waacheni (Wapeni talaka)" kwa hiyo wakawapa talaka isipokuwa Hudhayfah. 'Umar akamuambia: "Mpe talaka". (Hudhayfah) akasema: "Je, Unashuhudia kuwa yeye ni haraam?" Akasema: "Yeye ni mkaa wa moto wenye kuwaka, mpe talaka". Akasema: "Je, Unashuhudia kuwa yeye ni haraam?" Akasema: "Yeye ni mkaa wa moto wenye kuwaka". Akasema: "Najua kuwa yeye ni mkaa wa moto wenye kuwaka lakini yeye ni halali kwangu". Baada ya muda akampa talaka na akaulizwa "Kwa nini hukumpa talaka alipokuamrisha 'Umar?" Akasema: "Sikutaka watu wafikiri kuwa nimefanya kosa (kwa kumuoa)".

Labda alikuwa akimpenda au labda kwa sababu walipata mtoto pamoja kwa hiyo alimpenda". [Al-Mughniy 7/99]



Vile vile Hadiyth hii ifuatayo Sahiyh inasema:

((Ibn 'Umar alipokuwa akiulizwa kuhusu kumuoa mwanamke Mkiristo au Myahudi, alikuwa akisema: "Allaah Ameifanya kuwa ni Haraam kwa Muumini kuoa wanawake wanaomshirikisha Allaah katika ibada, na sijui lililo kubwa zaidi kuliko kumshirikisha Allaah katika ibada na kadhalika kama mwanamke kusema 'Iysaa ni Mungu ingawa yeye ni mja tu wa Allaah")) [Al-Bukhaariy]



Shaykh Ibn Baaz (Allaah Amrehemu) alisema: "Ikiwa mwanamke wa Kitabu anajulikana kuwa ni mwenye stara (sio muhuni) na kujiepusha na njia ambazo zinampeleka mtu katika uasherati, inaruhusiwa kwa sababu Allaah سبحانه وتعالى Ameruhusu hivyo na Ameturuhusu kuwaoa wanawake wao na kula nyama zao.



Lakini siku hizi kuna khofu kwamba wale wanaooa huenda wakakutana na uovu zaidi. Wanaweza kuwaita katika dini yao na wanaweza kuwalea watoto wao katika Ukristo. Kwa hiyo hatari ipo hakika na ni kubwa. Ili kuwa katika amani, Muumini ni bora asiwaoe. Na katika hali nyingi hakuna uhakika kama mwanamke hatofanya vitendo vya uasherati au hatowaleta watoto waliotoka katika uhusiano wa mwanzo. Lakini mwanamume akitaka kufanya hivyo basi hana dhambi kwake ili ajiweke katika stara na ainamishe macho yake kwa kumuoa. Ajitahidi kumuita katika Uislamu na awe na hadhari na uovu wake na hadhari ya kumruhusu asimvute yeye au watoto wake katika ukafiri". [Fataawa Islaamiyyah, 3/172]





Hivi Sasa Je, Tunao Ahlul-Kitaab?



Hivi sasa tunao Ahlul-Kitaab nao ni Wakristo na Mayahudi. Lakini wao wamekufuru na kumshirikisha Allah. Kwa hiyo ni makafiri na washirikina, kutokana na Qur-aan.



((اتَّخَذُواْ أَحْبَارَهُمْ وَرُهْبَانَهُمْ أَرْبَابًا مِّن دُونِ اللّهِ وَالْمَسِيحَ ابْنَ مَرْيَمَ وَمَا أُمِرُواْ إِلاَّ لِيَعْبُدُواْ إِلَهًا وَاحِدًا لاَّ إِلَهَ إِلاَّ هُوَ سُبْحَانَهُ عَمَّا يُشْرِكُونَ))

((Wamewafanya makuhani wao na wamonaki wao kuwa ni marabi badala ya Allaah, na pia Masiyh bin Maryam. Na wala hawakuamrishwa isipokuwa wamuabudu Mungu Mmoja, hapana mungu ila Yeye. Subhanahu, Ametakasika na hayo wanayomshirikisha nayo)) [At-Tawbah: 9:31]



Lakini wametolewa katika kuharamishwa kuolewawanawake wao kwa sababu Allaah سبحانه وتعالىAnasema katika aayah yenye maana:

((وَلاَ تَنكِحُواْ الْمُشْرِكَاتِ حَتَّى يُؤْمِنَّ وَلأَمَةٌ مُّؤْمِنَةٌ خَيْرٌ مِّن مُّشْرِكَةٍ وَلَوْ أَعْجَبَتْكُمْ وَلاَ تُنكِحُواْ الْمُشِرِكِينَ حَتَّى يُؤْمِنُواْ وَلَعَبْدٌ مُّؤْمِنٌ خَيْرٌ مِّن مُّشْرِكٍ وَلَوْ أَعْجَبَكُمْ أُوْلَئِكَ يَدْعُونَ إِلَى النَّارِ وَاللّهُ يَدْعُوَ إِلَى الْجَنَّةِ وَالْمَغْفِرَةِ بِإِذْنِهِ وَيُبَيِّنُ آيَاتِهِ لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ))

((Wala msiwaoe wanawake washirikina mpaka waamini. Na mjakazi Muumini ni bora kuliko mshirikina hata akikupendezeni. Wala msiwaoze (binti zenu) wanaume washirikina mpaka waamini. Na mtumwa mwanamume Muumini ni bora kuliko mshirikina hata akikupendezeni. Hao wanawaitia kwenye Moto, na Allaah Anawaitia kwenye Pepo na maghafira kwa idhini Yake. Naye Huzibainisha Aayah zake kwa watu ili wapate kukumbuka)) [Al-Baqarah: 2:221]



Washirikina waliotajwa katika Aayah hii ni wale walio nje ya Ahlul-Kitaab mfano Baniani, Majusi, Mabudha na kadhalika.



Kwa hiyo 'Watu wa Vitabu' ni makafiri na washirikina, lakini Allaah سبحانه وتعالىAmeturuhusu kula nyama zao na kuwaoa wanawake wao ikiwa watakuwa wenye stara (wenye heshima sio wahuni). Hii imeruhusiwa kutokana na maana ya Aayah iliyo katika Suratul-Baqarah 2:221 (tulioitaja hapo juu).



Na Allaah Anajua Zaidi
 
Chukulia katika mazingira ambayo ninauhuru (wa kikatiba) kuchagua dini yyte ile ninayoitaka. Na uhuru huu ninayo haki ya kuutekeleza wakati wowote ule. Sifungwi kubaki kwenye dini fulani.

Katika mazingira ya kuwa nimeoa mke kwa ndoa ya kikristo ambayo inaruhusu mke mmoja tu kwa mume mmoja na inatambulika hivyo kisheria. Nikiwa kwenye ndoa hiyo, kesho nikaamua kubadili dini na kuwa muislam na huko ninaruhusiwa kuwa na wake hadi wanne.

MASWALI:
1. Kwakua nitakua nimekana dini yangu ya awali, Je sheria itaendelea kumtambua huyu mke wa ndoa ya kikristo?

2. Hata kama tumeamua kuishi pamoja kama wanandoa (yeye abaki kuwa mkristo), je nitakua na uhuru kisheria kuongeza wake?

3. Hata kama tumeamua kuishi pamoja (na mke wangu naye abadili dini na kuwa muislam), je tutakuwa tumefunga ndoa au tutahitaji kuoana upya?

Nielewesheni kisheria na kwa imani ya kiislam pia.
1. Sheria ya nchi Itaendelea kumtambua mke wako wa ndoa.

2.kama mkeo Wa awali ukitaka kuishi naye kwakuwa umebadili dini ( kidini) itakupasa ufunge NAYE ndoa ya kiislam , na yeye akibaki na imani yake Kwani uislamu haiitambui ndoa ya awali Mkibaki na ndoa ya kikristu Utakuwa unazini naye. Pia utaruhusiwa kuongeza mke Kwani hata serikali inatambua ndoa ya wake wengi na imani ya dini Yako inaruhusu kuoa mpaka wake wanne na wote wana haki

3. Kama mwanamke naye akiamua kubadili dini, ndoa yenu ya awali itatambulika Kisheria ya nchi, kidini mnapaswa mfunge ndoa ya kiislam .
 
Masharti ya kuwaoa Ahlul-Kitaab



Sharti La Kwanza:



Lakini kuna sharti ya kuwaoa hao kama ilivyo katika Aayah kuwa: (wanawake wema miongoni mwa waliopewa Kitabu)



Abu Ja'afar Muhammad ibn Jariyr At-Twabariy ametoa maana ya 'muhswana' (mwema) katika Jaami' Al-Bayaan Ta-wiyl Aayatil-Qur-aan 8/165. "Muhswana ina maana kwamba ni mwanamke ambaye mwema aliyesitirika na msafi (kutokana na machafu ya zinaa) ambaye anajihifadhi sehemu zake za siri kutokana na kitendo cha Zinaa kama Aayah inavyosema:

((وَمَرْيَمَ ابْنَتَ عِمْرَانَ الَّتِي أَحْصَنَتْ فَرْجَهَا))

(Na Maryam binti wa 'Imraan, aliyelinda ubikira wake)) [At-Tahriym: 12]

Kwa maana kwamba amejilinda na kila kitendo chenye shaka na amejihifadhi na mwenendo wa uasherati.



Vile vile maana ya Muhswanaat (wanawake wema) ni wale ambao walio huru na walio katika stara. (Yaani katika heshima na aliye bikra, asiye mhuni) Ibn Kathiyr (Allaah Amrehemu) amesema katika Tafsiyr yake:

"Hii ni rai ya Maulamaa wengi wao na hii ndivyo inavyoelekea kuwa hali yenyewe. Asije kuwa dhimiyah (mwanamke asiye Muislam aliye katika hifadhi ya Kiislam) lakini pia asiyekuwa katika stara (heshima, bikra). Ikiwa atakuwa katika hali hii atakuwa amepotoka na mwenye ufisadi, na mumewe atamalizikia kuwa kama inavyoeleza katika methali: "Amenunua tende mbaya na amekhiniwa katika uzito na mizani pia".



Maana iliyo dhahiri katika aayah ni vile ilivyomaanisha "al-Muhswanah" (mwanamke mwenye stara, (aliyekuwa bikra, asiyekuwa mhuni) naye ni mwanamke aliyejiepusha na zinaa kama Allaah سبحانه وتعالى Anavyosema katika Aayah nyingine:

((مُحْصَنَاتٍ غَيْرَ مُسَافِحَاتٍ وَلاَ مُتَّخِذَاتِ أَخْدَانٍ))

((….wawe wanawake wema, si makahaba wala si mahawara)) [An-Nisaa: 4:21]



Lakini tunasisitiza kuwa ni mwanamume pekee anayeweza kufunga ndoa na Ahlul-Kitaab, ama mwanamke wa Kiislamu haruhusiwi kuolewa na mwanamume wa Ahlul-Kitaab



Sharti Ya Pili:



Ni kwamba mwanamume awe ndiye mwenye mas-uliyah na nyumba na watoto, kwani kwa Hikma ya Allaah سبحانه وتعالى Amemfanya mume awe kiongozi wa nyumba kwa sababu itakuwa ni wepesi kwake kumuongoza mkewe. Na inabidi Muislamu anapooa Ahlul-Kitaab ajitahidi awezavyo kumuongoza katika dini ya Uislamu.



Sharti Ya Tatu:



Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amependekeza Muislamu aoe wanawake Waislamu walioshika dini. Kwa hiyo kwanza ni kufanya jitihada ya kuwaoa wanawake Waislamu walioshika dini kisha tena kama haikuwezekana ndio aelekee kwa Ahlul-Kitaab.

Na ifahamike kuwa ni bora na usalama kabisa kutokuoa wanawake wa Kitabu khaswa kwa siku hizi ila ikiwa atakubali kusilimu kisha atazamwe tabia yake na kama ataendeleza dini yake sawa sawa.



Ibn Qudaamah (Allaah Amerehemu) alisema: Kwa vile hali ni hii, ni bora kutokuoa mwanamke wa Kitabu kwa sababu 'Umar aliwaambia wale waliowaoa wanawake wa Kitabu "Waacheni (Wapeni talaka)" kwa hiyo wakawapa talaka isipokuwa Hudhayfah. 'Umar akamuambia: "Mpe talaka". (Hudhayfah) akasema: "Je, Unashuhudia kuwa yeye ni haraam?" Akasema: "Yeye ni mkaa wa moto wenye kuwaka, mpe talaka". Akasema: "Je, Unashuhudia kuwa yeye ni haraam?" Akasema: "Yeye ni mkaa wa moto wenye kuwaka". Akasema: "Najua kuwa yeye ni mkaa wa moto wenye kuwaka lakini yeye ni halali kwangu". Baada ya muda akampa talaka na akaulizwa "Kwa nini hukumpa talaka alipokuamrisha 'Umar?" Akasema: "Sikutaka watu wafikiri kuwa nimefanya kosa (kwa kumuoa)".

Labda alikuwa akimpenda au labda kwa sababu walipata mtoto pamoja kwa hiyo alimpenda". [Al-Mughniy 7/99]



Vile vile Hadiyth hii ifuatayo Sahiyh inasema:

((Ibn 'Umar alipokuwa akiulizwa kuhusu kumuoa mwanamke Mkiristo au Myahudi, alikuwa akisema: "Allaah Ameifanya kuwa ni Haraam kwa Muumini kuoa wanawake wanaomshirikisha Allaah katika ibada, na sijui lililo kubwa zaidi kuliko kumshirikisha Allaah katika ibada na kadhalika kama mwanamke kusema 'Iysaa ni Mungu ingawa yeye ni mja tu wa Allaah")) [Al-Bukhaariy]



Shaykh Ibn Baaz (Allaah Amrehemu) alisema: "Ikiwa mwanamke wa Kitabu anajulikana kuwa ni mwenye stara (sio muhuni) na kujiepusha na njia ambazo zinampeleka mtu katika uasherati, inaruhusiwa kwa sababu Allaah سبحانه وتعالى Ameruhusu hivyo na Ameturuhusu kuwaoa wanawake wao na kula nyama zao.



Lakini siku hizi kuna khofu kwamba wale wanaooa huenda wakakutana na uovu zaidi. Wanaweza kuwaita katika dini yao na wanaweza kuwalea watoto wao katika Ukristo. Kwa hiyo hatari ipo hakika na ni kubwa. Ili kuwa katika amani, Muumini ni bora asiwaoe. Na katika hali nyingi hakuna uhakika kama mwanamke hatofanya vitendo vya uasherati au hatowaleta watoto waliotoka katika uhusiano wa mwanzo. Lakini mwanamume akitaka kufanya hivyo basi hana dhambi kwake ili ajiweke katika stara na ainamishe macho yake kwa kumuoa. Ajitahidi kumuita katika Uislamu na awe na hadhari na uovu wake na hadhari ya kumruhusu asimvute yeye au watoto wake katika ukafiri". [Fataawa Islaamiyyah, 3/172]
 
Hivi Sasa Je, Tunao Ahlul-Kitaab?



Hivi sasa tunao Ahlul-Kitaab nao ni Wakristo na Mayahudi. Lakini wao wamekufuru na kumshirikisha Allah. Kwa hiyo ni makafiri na washirikina, kutokana na Qur-aan.



((اتَّخَذُواْ أَحْبَارَهُمْ وَرُهْبَانَهُمْ أَرْبَابًا مِّن دُونِ اللّهِ وَالْمَسِيحَ ابْنَ مَرْيَمَ وَمَا أُمِرُواْ إِلاَّ لِيَعْبُدُواْ إِلَهًا وَاحِدًا لاَّ إِلَهَ إِلاَّ هُوَ سُبْحَانَهُ عَمَّا يُشْرِكُونَ))

((Wamewafanya makuhani wao na wamonaki wao kuwa ni marabi badala ya Allaah, na pia Masiyh bin Maryam. Na wala hawakuamrishwa isipokuwa wamuabudu Mungu Mmoja, hapana mungu ila Yeye. Subhanahu, Ametakasika na hayo wanayomshirikisha nayo)) [At-Tawbah: 9:31]



Lakini wametolewa katika kuharamishwa kuolewawanawake wao kwa sababu Allaah سبحانه وتعالىAnasema katika aayah yenye maana:

((وَلاَ تَنكِحُواْ الْمُشْرِكَاتِ حَتَّى يُؤْمِنَّ وَلأَمَةٌ مُّؤْمِنَةٌ خَيْرٌ مِّن مُّشْرِكَةٍ وَلَوْ أَعْجَبَتْكُمْ وَلاَ تُنكِحُواْ الْمُشِرِكِينَ حَتَّى يُؤْمِنُواْ وَلَعَبْدٌ مُّؤْمِنٌ خَيْرٌ مِّن مُّشْرِكٍ وَلَوْ أَعْجَبَكُمْ أُوْلَئِكَ يَدْعُونَ إِلَى النَّارِ وَاللّهُ يَدْعُوَ إِلَى الْجَنَّةِ وَالْمَغْفِرَةِ بِإِذْنِهِ وَيُبَيِّنُ آيَاتِهِ لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ))

((Wala msiwaoe wanawake washirikina mpaka waamini. Na mjakazi Muumini ni bora kuliko mshirikina hata akikupendezeni. Wala msiwaoze (binti zenu) wanaume washirikina mpaka waamini. Na mtumwa mwanamume Muumini ni bora kuliko mshirikina hata akikupendezeni. Hao wanawaitia kwenye Moto, na Allaah Anawaitia kwenye Pepo na maghafira kwa idhini Yake. Naye Huzibainisha Aayah zake kwa watu ili wapate kukumbuka)) [Al-Baqarah: 2:221]



Washirikina waliotajwa katika Aayah hii ni wale walio nje ya Ahlul-Kitaab mfano Baniani, Majusi, Mabudha na kadhalika.



Kwa hiyo 'Watu wa Vitabu' ni makafiri na washirikina, lakini Allaah سبحانه وتعالىAmeturuhusu kula nyama zao na kuwaoa wanawake wao ikiwa watakuwa wenye stara (wenye heshima sio wahuni). Hii imeruhusiwa kutokana na maana ya Aayah iliyo katika Suratul-Baqarah 2:221 (tulioitaja hapo juu).



Na Allaah Anajua Zaidi
 
Uhuru wa kuabudu unakujaje sasa. Coz kuongeza wake ni suna na tena ni ibada (kwa imani ya kiislam, nadhani) kama utaamua kuoa mjane. Sasa iweje pawe na mkataba unaokupunguzia uhuru wako wa kuabudu coz mke/mume anaweza asiridhie kuvunja mkataba
Katika mchakato wa kujaza fomu ya usajili wa ndoa ambayo ni hati rasmi ya serikali wanandoa watarajiwa hujaza kipengere kinachoainisha muundo wa ndoa itakayofungwa yaani MONOGAMY au POLYGAMY, kipengere hiki ni mkataba baina ya wanandoa mbele ya msajili wa ndoa tarajiwa baada ya hapo wote watatu yaani (Mume, Mke na kasisi, Imam au DC) watasaini makubaliano hayo, sasa ukiachilia mbali huu mtindo wa kufanya mambo kienyeji unaoedelea ktk jamii, kimsingi huwezi kuanzisha mkataba juu ya mwingine bila kwanza kutanzua ule wa awali kisheria, hivyo endapo Mume atabadili dini na kutaka kuingia ktk mfumo wa imani ya ndoa za polygamy ni lazima ajaze fomu ya makubaliano mengine sambamba na Imani yake mpya.
 
Majibu!
1.Sheria ya kiislam itamtambua mkeo ikiwa na yeye amesilimu(amekuwa muislam)
2.Kama yeye akibaki kuwa mkristo ww utakuwa unazini (utapata dhambi) kwa mujibu wa sheria za kiislam kwa kuwa uislam haukubali ndoa ya muislam na asiye muislam(lazima mke &mume wawe wote waislam)
3.Wote mukibadili dini (mukiwa waislam)hamtatakiwa kufunga ndoa mpya ila ndoa yenu ile ile muliofunga mkiwa wakristo inatosha,Ispokuwa kama wakati mulipokuwa wakristo hamkufunga ndoa basi hapo ndio itawalazimu kufunga ndoa.
Namba 2 si kweli
 
Majibu!
1.Sheria ya kiislam itamtambua mkeo ikiwa na yeye amesilimu(amekuwa muislam)
2.Kama yeye akibaki kuwa mkristo ww utakuwa unazini (utapata dhambi) kwa mujibu wa sheria za kiislam kwa kuwa uislam haukubali ndoa ya muislam na asiye muislam(lazima mke &mume wawe wote waislam)
3.Wote mukibadili dini (mukiwa waislam)hamtatakiwa kufunga ndoa mpya ila ndoa yenu ile ile muliofunga mkiwa wakristo inatosha,Ispokuwa kama wakati mulipokuwa wakristo hamkufunga ndoa basi hapo ndio itawalazimu kufunga ndoa.
Maelezo yamejitosheleza kabisa hakuna la kuongeza.



#naenda_zimbabwe
 
1. Ndio sheria itaendelea kumtambua mke wa kikristo kwani mwanaume muislam anaweza kuwa na ndoa na mtu ambae ni ahlul kitab.
2. Ndio
3. Hakuna haja ya kufunga ndoa upya kwani Uislamu inatambua ndoa ilimradi iwe imefata taratibu za kidini.
Uislamu unatambua ndoa yoyote ilimradi iwe imefata taratibu za kidini, muislam mwanaume ameruhusiwa kuoa mwanamke asiekuwa muislam, pia kama akimsilimisha ni vizuri zaidi, lakini kama mlioana kwa dini nyongine baadae mkasilimu basi hakuna haja ya kuoana upya, na kama mwanamke akiamua kubaki kule kule kwenye dini yake basi haibatilishi ndoa. Na bado huyo mwanamke atatambulika kama mke wako.
Asante sana kwa ufafanuzi maridhawa.
 
Swali jepesi tu ahlul kitab wapo, waliomaanishwa tunao dunia ya sasa!?
Mwenyezi MUNGU asingewataja kwenye Quran kama hawapo. Kumbuka hata waislam wamebadilika sana, zama za mtume hakukuwa na madhehebu ktk uislam but siku hizi yapo. Kuna shia, sunni, suffi, ahmadiyya n.k. Ukiulizwa waislam wa zama za mtume wapo? Utajibu nn ikiwa zama za mtume hakukuwa na madhehebu?. Maswala haya hata wanazuoni huwa wanaamua kujiepusha kutoa hukumu ya moja kwa moja. Kwa maana hiyo watu wa kitabu wapo isipokuwa nao wamegawanyika kama ilivotokea kwa waislam.
 
Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amependekeza Muislamu aoe wanawake Waislamu walioshika dini. Kwa hiyo kwanza ni kufanya jitihada ya kuwaoa wanawake Waislamu walioshika dini kisha tena kama haikuwezekana ndio aelekee kwa Ahlul-Kitaab.

Na ifahamike kuwa ni bora na usalama kabisa kutokuoa wanawake wa Kitabu khaswa kwa siku hizi ila ikiwa atakubali kusilimu kisha atazamwe tabia yake na kama ataendeleza dini yake sawa sawa.



Ibn Qudaamah (Allaah Amerehemu) alisema: Kwa vile hali ni hii, ni bora kutokuoa mwanamke wa Kitabu kwa sababu 'Umar aliwaambia wale waliowaoa wanawake wa Kitabu "Waacheni (Wapeni talaka)" kwa hiyo wakawapa talaka isipokuwa Hudhayfah. 'Umar akamuambia: "Mpe talaka". (Hudhayfah) akasema: "Je, Unashuhudia kuwa yeye ni haraam?" Akasema: "Yeye ni mkaa wa moto wenye kuwaka, mpe talaka". Akasema: "Je, Unashuhudia kuwa yeye ni haraam?" Akasema: "Yeye ni mkaa wa moto wenye kuwaka". Akasema: "Najua kuwa yeye ni mkaa wa moto wenye kuwaka lakini yeye ni halali kwangu". Baada ya muda akampa talaka na akaulizwa "Kwa nini hukumpa talaka alipokuamrisha 'Umar?" Akasema: "Sikutaka watu wafikiri kuwa nimefanya kosa (kwa kumuoa)".

Labda alikuwa akimpenda au labda kwa sababu walipata mtoto pamoja kwa hiyo alimpenda". [Al-Mughniy 7/99]



Vile vile Hadiyth hii ifuatayo Sahiyh inasema:

((Ibn 'Umar alipokuwa akiulizwa kuhusu kumuoa mwanamke Mkiristo au Myahudi, alikuwa akisema: "Allaah Ameifanya kuwa ni Haraam kwa Muumini kuoa wanawake wanaomshirikisha Allaah katika ibada, na sijui lililo kubwa zaidi kuliko kumshirikisha Allaah katika ibada na kadhalika kama mwanamke kusema 'Iysaa ni Mungu ingawa yeye ni mja tu wa Allaah")) [Al-Bukhaariy]



Shaykh Ibn Baaz (Allaah Amrehemu) alisema: "Ikiwa mwanamke wa Kitabu anajulikana kuwa ni mwenye stara (sio muhuni) na kujiepusha na njia ambazo zinampeleka mtu katika uasherati, inaruhusiwa kwa sababu Allaah سبحانه وتعالى Ameruhusu hivyo na Ameturuhusu kuwaoa wanawake wao na kula nyama zao.



Lakini siku hizi kuna khofu kwamba wale wanaooa huenda wakakutana na uovu zaidi. Wanaweza kuwaita katika dini yao na wanaweza kuwalea watoto wao katika Ukristo. Kwa hiyo hatari ipo hakika na ni kubwa. Ili kuwa katika amani, Muumini ni bora asiwaoe. Na katika hali nyingi hakuna uhakika kama mwanamke hatofanya vitendo vya uasherati au hatowaleta watoto waliotoka katika uhusiano wa mwanzo. Lakini mwanamume akitaka kufanya hivyo basi hana dhambi kwake ili ajiweke katika stara na ainamishe macho yake kwa kumuoa. Ajitahidi kumuita katika Uislamu na awe na hadhari na uovu wake na hadhari ya kumruhusu asimvute yeye au watoto wake katika ukafiri". [Fataawa Islaamiyyah, 3/172]





Hivi Sasa Je, Tunao Ahlul-Kitaab?



Hivi sasa tunao Ahlul-Kitaab nao ni Wakristo na Mayahudi. Lakini wao wamekufuru na kumshirikisha Allah. Kwa hiyo ni makafiri na washirikina, kutokana na Qur-aan.



((اتَّخَذُواْ أَحْبَارَهُمْ وَرُهْبَانَهُمْ أَرْبَابًا مِّن دُونِ اللّهِ وَالْمَسِيحَ ابْنَ مَرْيَمَ وَمَا أُمِرُواْ إِلاَّ لِيَعْبُدُواْ إِلَهًا وَاحِدًا لاَّ إِلَهَ إِلاَّ هُوَ سُبْحَانَهُ عَمَّا يُشْرِكُونَ))

((Wamewafanya makuhani wao na wamonaki wao kuwa ni marabi badala ya Allaah, na pia Masiyh bin Maryam. Na wala hawakuamrishwa isipokuwa wamuabudu Mungu Mmoja, hapana mungu ila Yeye. Subhanahu, Ametakasika na hayo wanayomshirikisha nayo)) [At-Tawbah: 9:31]



Lakini wametolewa katika kuharamishwa kuolewawanawake wao kwa sababu Allaah سبحانه وتعالىAnasema katika aayah yenye maana:

((وَلاَ تَنكِحُواْ الْمُشْرِكَاتِ حَتَّى يُؤْمِنَّ وَلأَمَةٌ مُّؤْمِنَةٌ خَيْرٌ مِّن مُّشْرِكَةٍ وَلَوْ أَعْجَبَتْكُمْ وَلاَ تُنكِحُواْ الْمُشِرِكِينَ حَتَّى يُؤْمِنُواْ وَلَعَبْدٌ مُّؤْمِنٌ خَيْرٌ مِّن مُّشْرِكٍ وَلَوْ أَعْجَبَكُمْ أُوْلَئِكَ يَدْعُونَ إِلَى النَّارِ وَاللّهُ يَدْعُوَ إِلَى الْجَنَّةِ وَالْمَغْفِرَةِ بِإِذْنِهِ وَيُبَيِّنُ آيَاتِهِ لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ))

((Wala msiwaoe wanawake washirikina mpaka waamini. Na mjakazi Muumini ni bora kuliko mshirikina hata akikupendezeni. Wala msiwaoze (binti zenu) wanaume washirikina mpaka waamini. Na mtumwa mwanamume Muumini ni bora kuliko mshirikina hata akikupendezeni. Hao wanawaitia kwenye Moto, na Allaah Anawaitia kwenye Pepo na magha**** kwa idhini Yake. Naye Huzibainisha Aayah zake kwa watu ili wapate kukumbuka)) [Al-Baqarah: 2:221]



Washirikina waliotajwa katika Aayah hii ni wale walio nje ya Ahlul-Kitaab mfano Baniani, Majusi, Mabudha na kadhalika.



Kwa hiyo 'Watu wa Vitabu' ni makafiri na washirikina, lakini Allaah سبحانه وتعالىAmeturuhusu kula nyama zao na kuwaoa wanawake wao ikiwa watakuwa wenye stara (wenye heshima sio wahuni). Hii imeruhusiwa kutokana na maana ya Aayah iliyo katika Suratul-Baqarah 2:221 (tulioitaja hapo juu).



Na Allaah Anajua Zaidi

Weka sawa hapo pana utata
 
Swali jepesi tu ahlul kitab wapo, waliomaanishwa tunao dunia ya sasa!?
Kutokana na mabadiliko ya kimapokeo hadi kufika sasa na kuendelea, katika ulimwengu huu watu wa kitabu hakuna, kwani kila utakayemgusa tayari ni mshirikina [thalithu thalatha]
 
Majibu!
1.Sheria ya kiislam itamtambua mkeo ikiwa na yeye amesilimu(amekuwa muislam)
2.Kama yeye akibaki kuwa mkristo ww utakuwa unazini (utapata dhambi) kwa mujibu wa sheria za kiislam kwa kuwa uislam haukubali ndoa ya muislam na asiye muislam(lazima mke &mume wawe wote waislam)
3.Wote mukibadili dini (mukiwa waislam)hamtatakiwa kufunga ndoa mpya ila ndoa yenu ile ile muliofunga mkiwa wakristo inatosha,Ispokuwa kama wakati mulipokuwa wakristo hamkufunga ndoa basi hapo ndio itawalazimu kufunga ndoa.
Chukua hayo majibu uyafanyie kazi.
 
Back
Top Bottom