Nimeamua kusimamisha masomo ya PhD nje ya nchi ili nijitayarishe kwaajili ya kugombea ubunge 2025 katika jimbo la Mbozi Mashariki

I salute ur comment mkuu
 
Kwanini usifanye vyote viwili?
 
Labda kama una sababu nyingine ila naona umekosea sana kuacha PhD na full scholarship kwenda kugombea ubunge ambao ni miaka mitatu ijayo na huna uhakika utachaguliwa. Lazima kuna kitu kingine. Kama hujaacha tatadhali endelea na masomo!
 
Sema hiyo scholarship yako ya China haina Maslai nadhani ingekuwa ulaya nchi Kama UK sidhani Kama ungejiuliza mara mbili. Kugombea Ubunge Ni Hadi 2025 na mchakato unahitaji miez Kama mitatu tu ya kujiandaa so kuacha masomo yako yenye Maslai mapana kisa ubunge haupo sahihi maana huko unaenda kubeti.
 

..Nakushauri umalize PhD yako.

..Au tafuta namna ya kufanya yote mawili yaani PhD na harakati za ubunge.

..kuna watu wako kwenye ubunge / siasa na wameweza kusoma Masters au PhD.
 
Acha kukatisha tamaa wenye mawazo tofauti na wewe? Au nawe ni mbunge wa eneo hilo?
 
Honesty doesn’t take people very far in life. But then if I am deemed a fool from the opinion of others why bother to air it. With that insight I might as well dish the nasty.

Hivi mtu ambae una promote biashara isiyo na maadili ya kusaidia watu kufaulu degrees zao unethically kwa ku assess kazi zao ili wafaulu (shida zaidi sio wewe) Ila hiyo serikali iliyokuwa kimya kuacha wapuuzi kama nyie ku advertise ujinga wenu.

Binafsi na kuona ni mtu ambae very unethical.

Na kuhusu Oil and Gas industry, ufahamu wako ni mdogo sana. As Plato put it in his ship leadership analogue, popularity wins.

Huko kwenye environmental issues ndio mweupe kabisa, but then with the Tanzania audience you don’t need much to get ahead.

Hivi unawezaje ku apply Phd, upate nafasi ambayo very competitive and then abandon the mission.

Common sense says Phd takes roughly about 2 years minimum to complete from your acceptance date. Should you have chosen to do it by then you would have graduated to pursue ya political ambitions.

Vilaza kama nyie uwongo wenu kuaminika ni kwa sababu ya audience ya J.F.

Binafsi sikatai unaweza kuwa.na ajira katika sector ya nishati, ila kwa kukusoma uelewa wako wa hiyo industry ni mdogo sana.

Sometimes I have to tell what it is. Don’t mind me, just remember Plato ship analogue.
 
Umeona JF Watu Wanavyolalama Kuhusu Tanzania
Nchi Inavyobolewa Ukipata Nafasi Usiende Kufanya Ujinga
Ukiingia Kwenye Kamati Hizo Ndiyo Force Account Zenu



Jimbo Nitakushauri Huko Unakogombea Ndiyo Wazazi Wangu Wametokea
 
Hiyo itakuwa PhD fake ya miaka 2.

Andika kwa kiswahili tu tutaelewa
Kwani we unadhani Phd ni kitu special sana?

That’s just a five chapter thesis same as in

First degree 10000 words
Masters 10000- 25000 words
Doctorate 50000+ words

All you need is to pick is a topic of Interest and extrapolate it following the rules required in writing the five chapters thesis.

Binafsi najiamini naweza fyatua any degree ambayo aihitaji complex mathematics nor laboratory researches.

Sitanii na huyu dada uelewa wake wa oil and gas ni very limited. Kwa mie ambae nimezifyatua hizo.

Mengine ni kupongezana ujinga kama ilivyo hada yenu watanzania.
 

Kwahiyo mama kwenye uteuzi bado HAJAKUONA?

#YNWA
 
Hongera Mkuu kwa kusimama katika kile unachokiamini na kuifukuzia ndoto yako. Kwa kweli siasa za bongo ni ngumu na zinafigisu nyingi. Kujuana, rushwa, ushirikina n.k. Huenda ukawa vzr sana kwenye sera na mipango yako ya kuikomboa jamii lakini wapinzani wako wakawa vzr zaidi kwenye mipango ya nje ya uwanja ukajikuta unapata kura 6 kwa wajumbe halafu mwenzio kura 300. Ingawa kiuhalisia wewe unakuwa upo vizuri mno kuliko huyo mshindi.

Ushauri wangu kwako:
1. Kama ndio kwanza unakwenda kujihusisha na siasa actively and openly, nashauri hizo harakati uzianze mapema sana kujipitisha ujulikane. Ukichelewa sn kupita utaonekana ni msaka tonge tu. Pia lijue eneo lako kwa marefu na mapana. Vitongoji, kata na vijiji.

2. Pamoja na kutaka kujulikana, kuwa makini sana usijitangaze wazi kuwa unautaka ubunge ktk hatua hii. Watakula kichwa huko mbele kwa kujitangaza mapema na kukatisha ndoto yako. Ila Jitoe kama msamalia mwema kwenye mashule nunua hata madaftari ya bei poa peleka kama msaada, kwenye misiba jitokeze na sapoti unachoweza, michezo n.k

3. Wajue wajumbe wote wa chama chako wanaopiga kura za uteuzi wa wagombea na uwe nao karibu sn kwa namna unaweza. Jishushe sn. Sometimes siasa na unafki ni ndugu wa damu.
4. Fanya uchaguzi makini wa jimbo ambalo unaweza kummudu kiongozi aliyepo. Awe ni yule ambaye si waziri na hana jina wala mambo makubwa sn ameyafanya jimboni.

Alternatively:
Ni ngumu lakini inawezekana, kwa mtu anayejitokeza na kuingia kwenye siasa kwa mara ya kwanza tu na akapata ubunge. Hivyo, naweza pia kukushauri kutoacha shule hiyo kubwa huku ukizingatia umepata Full Scholarship na unalipiwa kila kitu; ada hadi kula na kulala.

Endapo ningelikuwa ni mimi, ningeendelee na masomo ila kipindi cha kuchukua fomu ama shortly before, ningeomba udhuru kdg chuoni na kuja japo kwa awamu hii kutest zari na kutanguliza jina kwa mipango ya mbele. Ukiipata fursa basi alhamdulillahi ila ukikosa fursa ya kupita basi, kule chuoni pia unakuwa hujapoteza unarudi na kuendelea. Uzuri haya majimbo na siasa zipo tu. Ukitanguliza jina na baadae ukapata hiyo PHD ktk chama tunaweza kukuangalia pia ktk eneo lingine. Wengi walio na elimu nzr na ambao wamejitokeza tu angalau hufikiliwa hata nafasi za Dc, Rc, Ded n.k

So, bro chakata bongo before muda wa hiyo fursa ya masomo haijakoma. Usije kosa kote. Nakutakia kila la Kheri.

Asante.

Nzwangendaba
 
Aliyekwambia tunachagua Wasomi waganga njaa ni nani?
 
Ahsante sana kwa ushauri mzuri. Ushauri huu nitaanza kuufanyia kazi kwa uharaka sana rafiki.
Hawa nadhani ndiyo diaspora wa CHADEMA wanaoenda kupigana vita Ukraine ili watupatie tumehuru, wakiuliwa ndiyo wanamkumbuka Mama Tanzania waliyemkana. Elimu ni kitu cha kwanza; Mtume aliwaasa Waislamu wote waende China na kila mahali kujiongezea elimu, yeye huyu anataka aache shule abaki kipofu atuongoze vipofu wapi na wapi. Please ignore him.
 
Huyu ni mwanaccm tafadhali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…