Nimeamua Kustaafu Rasmi JF, Utangazaji na Uandishi wa Habari Baada ya Kuhudumu Miaka 30. Niko Free Kujiunga Siasa, Nimejiunga CCM na Nitagombea Ubunge

Nimeamua Kustaafu Rasmi JF, Utangazaji na Uandishi wa Habari Baada ya Kuhudumu Miaka 30. Niko Free Kujiunga Siasa, Nimejiunga CCM na Nitagombea Ubunge

Wanabodi,
Mimi mwanabody mwenzenu, nilianza kazi ya media tarehe kama ya leo, miaka 30 iliyopita, hivyo ilipofika tarehe hii siku ya leo, ndio siku yangu rasmi ya kustaafu kazi hii ya media, hivyo sasa nimestaafu rasmi uandishi wa habari, utangazaji na pia nimestaafu rasmi jf.

Kustaafu uandishi wa habari na utangazaji ni kufuatia kuhudumu kwa muda mrefu wa kutosha katika tasnia ya habari, kuhudumu fani moja kwa miaka 30 sii haba.

Kufuatia media ethics za misingi mikuu ya fani ya uandishi wa habari, ni truthfulness, Objectivity, Impartiality na Balancing, mwandishi wa habari wa ukweli ili aweze ku practice objectivity na impartiality hapaswi kuwa mwanachama, mfuasi au mshabiki wa chama chochote cha siasa, huwezi kuwa mwanachama wa chama cha siasa halafu ukawa objective au impartial, hivyo mimi siku zote humu jf nilikuwa sina chama, lakini sasa kuanzia leo baada ya kustaafu rasmi, leo hii hii majira ya saa 10:00 asubuhi, nitaelekea pale ofisi ndogo ya CCM Lumumba kwa Polepole kujiunga rasmi CCM na kukabidhiwa kadi yangu ya uanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM.

Sababu ya kuamua kujiunga na chama cha Mapinduzi ni sababu kuu 7.
  1. CCM ndicho chama kilicholeta uhuru na ukombozi Tanzania kutoka katika makucha ya wakoloni, wakati huo kikitwa TANU. Hivyo CCM ndicho chama pekee mkombozi wa Watanzania, na ni kufuatia sifa hii, CCM kimepewa hatimiliki ya kuitawala Tanzania milele.
  2. Kufuatia kukubalika sana na kuaminika sana na Watanzania, CCM ndicho chama pekee nchini Tanzania chenye long experience ya uzoefu wa muda mrefu wa uongozi na kuitawala Tanzania, hivyo unajiunga na most experienced party yenye long experience ya uzoefu wa muda mrefu.
  3. CCM kimefanya mengi makubwa, mazuri nchini mwetu tangu tumepata uhuru kwa kuongoza vita dhidi ya maadui umasikini, ujinga, maradhi, rushwa, uzembe, ufisadi, ukoloni mambo leo, unyonyaji, ukupe, ukabaila, ubepari, hadi vita hizi za kisiasa za ubeberu, utandawazi na kuongoza mapambano ya kiuchumi kuipeleka Tanzania kuwa nchi ya viwanda, nchi ya uchumi wa kati kuelekea Tanzania kuwa donor country.
  4. Japo Tanzania ni nchi ya vyama vingi vya siasa, lakini kiukweli kabisa, tunapozungumzia chama haswa cha siasa kwa maana halisi ya chama cha siasa, kwa Tanzania, kiukweli kabisa tuna chama kimoja tuu cha siasa ambacho ni CCM ambacho pia ni chama dola, vyama vingine vyote ni kama vyama vijivyama au vikundi tuu vya watu wanaofanya tuu siasa, vingine ni vyama watu, vingine ni saccos na vingine ni vyama vibaraka tuu na vingine ni vya jina tuu au vyama makaratasi tuu, kule ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, hivyo in reality Tanzania hatuna any serious opposition party ya kushindana na CCM, hivyo kama kuna mtu yoyote anayeamua sasa kujiunga siasa, chama pekee cha kujiunga nacho ni CCM.
  5. Sababu ya 5 na ya mwisho ni lisemwalo, lipo kama halipo linakuja. Japo mimi ni Msukuma, na jina langu la ubini ni Mayalla, siku zote nimekuwa nikielezwa na Wasukuma wa Ukweli maana ya jina Mayalla kwa Kisukuma ni ukame, drought unaosababisha famine, baa la njaa, lakini siku hizi kuna Wasukuma wa aina nyingi nyingi wengine ni wakuja tuu hivyo hata maana ya jina la Mayalla linabadilika badilika kutegemeana na Msukuma wa wapi. Toka siku ile nilipouliza lile swali Ikulu nikajibiwa kuwa Mayalla kwa Kisukuma ni Njaa, kiukweli kauli nyingine huumba, tangu nilipoitwa Njaa, kauli ile ikaniumbia njaa ya ukweli, hadi jina langu humu na mitaani ninaitwa Pasco Manjaa!. Baada tuu ya swali lile, contracts zangu zote za kampuni yangu ya PPR za serikalini zilisitishwa hivyo njaa ikaanza kunitembelea, tenda za maonyesho ya Saba Saba zikafutwa, tenda za kuandaa kipindi vya elimu kwa umma zikafutwa, ile ofisi yangu jengo la NHC pale Mtaa Mkepu niliokuwa nalipia pango sawa mshahara wa DC nikafunga, nilikuwa na wafanyakazi 20, nikawapunguza 15, tukabaki 5 na kuhamia kwenye kaji chumba jengo la Posta House. Kwa kwa vile mimi ni mwandishi wa habari, baada ya kufungiwa huko kote nikaamua kurejea newsroom kuandika makala za magazeti nako ndio vile tena nikaitwa Dodoma kuhojiwa na Kamati ya Bunge. Kila ninachogusa hakiendi. Sasa limeingia hili janga la Corona, hakuna kazi kabisa, ofisi nimefunga niko home sina hili wala lile ndipo likanijia hili wazo la kujiunga CCM na kugombea ubunge ili sasa nikawatumikie watu. Mtaji wa ubunge nimeamua kuuza kila kitu changu, kuanzia nyumba, na kila kitu kilichomo, magari, na container lililosheni mali za thamani kubwa.
  6. Kwa vile aliyenisababishia njaa hii ni Rais Magufuli kuniita njaa, kauli yake imeumba njaa, hivyo sasa najiunga CCM na kugombea ubunge jimbo fulani lililokuwa linashikiliwa na upinzani, kwasababu madhila haya amenisababishia rais Magufuli ambaye sio tuu ni home boy wangu, bali ndiye Mwenyekiti wa CCM, japo kwenye kura za maoni CCM, mimi sitaongoza, lakini siamini kama ataweza kunipita hivi hivi homeboy wake aliyemuita Njaa na kumsababishia njaa, hivyo nitateuliwa kupeperusha bendera ya CCM uchaguzi wa 2020.
  7. Kufuatia Kukubalika sana kwa CCM nchi nzima kulikosababishwa na kasi ya Awamu ya 5, ukiishateuliwa kupeperusha bendera ya CCM, wewe unakuwa tayari ndio Mbunge mtarajiwa unaesubiri kuapishwa tuu na ili kuokoa gharama za kufanya kampeni, kama kawaida ya CCM, uchaguzi Mkuu tutautumia ule wembe wa uchaguzi wa serikali za mitaa. Hivyo nitamsaidia sana rais Magufuli katika eneo la sekta ya habari.
  8. Kufuatia CCM kuwa ni watu wasiopendwa sana humu jf, nimenote wana CCM ambao ni wana jf, akiwemo Paul Makonda, Nape Mnauye, Juliana Shonza, Kigwangala, Prof. Tibaijuka, Mwigulu na wengine, hawachangii tena mijadala humu jf, hivyo na mimi nikiishajiunga tuu na kupokekewa pale CCM Lumumba na Polepole from then nitakuwa sichangii tena mijadala yoyote humu jf kama makada wengine watangulizi wangu. Nitakuwa Facebook, Twitter, Instagram na Snapchat
  9. Hivyo kwa bandiko hili, kwanza nawashukuru sana wana jf kwa Ushirikiano wenu katika kipindi chote cha miaka zaidi ya 10 tuliokuwa wote humu jf, nawaaga kwaherini ya kuonana, japo nitakuwa sichangii ila jf nitaendelea kuitembelea na likes nitakuwa naendelea kuzimwaga ila kiukweli nitawa miss sana na kufuatia uraibu wangu na jf, pia mimi mwenyewe nitateseka sana.
  10. Nimalizie kwa kuwaomba Ushirikiano wenu, naombani support yenu kwa kuniunga mkono katika safari yangu hii ya kujiunga CCM, kugombea ubunge na kumsaidia rais Magufuli na kuisadia nchi yangu Tanzania.
NB. Kwavile kwa bandiko hili ndio nimeaga jf, nawaombeni msiniulize maswali au kitu kwasababu sita jibu kitu. Muwe na siku njema nambeni niwaachie zawadi hizo hapo chini kwa anayetaka kuniungisha, bei ni karibu na bure.
View attachment 1405534View attachment 1405535
Hizo items zote hapo nje, nazigawa bure ila utalazimika kunichangia kidogo pesa za maandalizi ya kampeni za ubunge
1. Gari Subaru Legacy ni twin turbo na sun roof
Thamani yake ni TZS 8,000,000
Lakini unachangia TZS 5,000,000 tuu
Linatembea

2. Toyota Estima pia ni turbo na Sunroof
Thamani yake ni TZS 6,000,000
Unachangia TZS 4,000,000 tuu
Linatembea

3. Suzuki Alto
Thamani yake ni TZS 4,000,000
Unachangia TZS 2,500,000 tuu.
Halitembei, linahitaji TZS 500,000 kuingia barabarani.

4. Empty Container
Thamani yake ni TZS 6,000,000
Unachangia kwa TZS. 4,000,000 tuu.

Vigezo na Masharti

1.Prices ni fixed hakuna majadiliano yoyote ya aina yoyote.

2. Mali zote zitauzwa kama zilivyo

3. Unaruhusiwa kuja kukagua any time during office hours

4. Enquiries zinafanywa kwa SMS or WhatsApp only kupitia number yangu hii
0784 270403.
Please, please please, usipige simu, ni SMS and WhatsApp Only halafu mimi ndio nitakupigia.

Natanguliza shukrani,
JF kwaherini
Media Kwaherini
CCM nipokeeni
Wenu
Paskali
0784 270403 SMS na WhatsApp Only
Please usinipigie hata kunisalimia tuu,
Tuma SMS or WhatsApp mimi ndio nitakupigia.
April Fool in action
 
Huna jipya mkuu, siku nyingi wewe ni buku saba
Sasa sijui unatangaza nini au ndio kutokujielewa?

Bora utuachie JF yetu maana ninyi ndio mnaipotezea JF thamani kwa kujaza thread za kiccm zisizo na mantiki kwa Taifa

Nenda utarudi kapa, tangu umpige Jiwe lile swali hakuuamini tena na anakisasi hivyo huko utanyooshwa na kusomeshwa namba sana

Sent using Jamii Forums mobile app
Pascal ni somo, si kila mmoja atalifaulu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pascal atastaafu vyote ila sio JF,leo ni April foolish day,na gari gani hiyo ya 2.5M🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Kwani mtu hawazi kuwa Mbunge na kuendelea na taaluma yake?..au katiba ya Tz hairuhusu?
 
Pamoja kuwa leo ni tarehe Mosi, lakini kuna ukweli wa baadhi ya hoja zako mkuu.

Nafurahi kwa namna unavyoweza changamsha genge letu,kijiwe chetu hiki cha kahawa.

Napokea text eti Pascal Mayalla anahamia ccm,kajitoa JF..

ni kacheka tu heeee heee ni magu tune.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanabodi,
Mimi mwanabody mwenzenu, nilianza kazi ya media tarehe kama ya leo, miaka 30 iliyopita, hivyo ilipofika tarehe hii siku ya leo, ndio siku yangu rasmi ya kustaafu kazi hii ya media, hivyo sasa nimestaafu rasmi uandishi wa habari, utangazaji na pia nimestaafu rasmi jf.

Kustaafu uandishi wa habari na utangazaji ni kufuatia kuhudumu kwa muda mrefu wa kutosha katika tasnia ya habari, kuhudumu fani moja kwa miaka 30 sii haba.

Kufuatia media ethics za misingi mikuu ya fani ya uandishi wa habari, ni truthfulness, Objectivity, Impartiality na Balancing, mwandishi wa habari wa ukweli ili aweze ku practice objectivity na impartiality hapaswi kuwa mwanachama, mfuasi au mshabiki wa chama chochote cha siasa, huwezi kuwa mwanachama wa chama cha siasa halafu ukawa objective au impartial, hivyo mimi siku zote humu jf nilikuwa sina chama, lakini sasa kuanzia leo baada ya kustaafu rasmi, leo hii hii majira ya saa 10:00 asubuhi, nitaelekea pale ofisi ndogo ya CCM Lumumba kwa Polepole kujiunga rasmi CCM na kukabidhiwa kadi yangu ya uanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM.

Sababu ya kuamua kujiunga na chama cha Mapinduzi ni sababu kuu 7.
  1. CCM ndicho chama kilicholeta uhuru na ukombozi Tanzania kutoka katika makucha ya wakoloni, wakati huo kikitwa TANU. Hivyo CCM ndicho chama pekee mkombozi wa Watanzania, na ni kufuatia sifa hii, CCM kimepewa hatimiliki ya kuitawala Tanzania milele.
  2. Kufuatia kukubalika sana na kuaminika sana na Watanzania, CCM ndicho chama pekee nchini Tanzania chenye long experience ya uzoefu wa muda mrefu wa uongozi na kuitawala Tanzania, hivyo unajiunga na most experienced party yenye long experience ya uzoefu wa muda mrefu.
  3. CCM kimefanya mengi makubwa, mazuri nchini mwetu tangu tumepata uhuru kwa kuongoza vita dhidi ya maadui umasikini, ujinga, maradhi, rushwa, uzembe, ufisadi, ukoloni mambo leo, unyonyaji, ukupe, ukabaila, ubepari, hadi vita hizi za kisiasa za ubeberu, utandawazi na kuongoza mapambano ya kiuchumi kuipeleka Tanzania kuwa nchi ya viwanda, nchi ya uchumi wa kati kuelekea Tanzania kuwa donor country.
  4. Japo Tanzania ni nchi ya vyama vingi vya siasa, lakini kiukweli kabisa, tunapozungumzia chama haswa cha siasa kwa maana halisi ya chama cha siasa, kwa Tanzania, kiukweli kabisa tuna chama kimoja tuu cha siasa ambacho ni CCM ambacho pia ni chama dola, vyama vingine vyote ni kama vyama vijivyama au vikundi tuu vya watu wanaofanya tuu siasa, vingine ni vyama watu, vingine ni saccos na vingine ni vyama vibaraka tuu na vingine ni vya jina tuu au vyama makaratasi tuu, kule ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, hivyo in reality Tanzania hatuna any serious opposition party ya kushindana na CCM, hivyo kama kuna mtu yoyote anayeamua sasa kujiunga siasa, chama pekee cha kujiunga nacho ni CCM.
  5. Sababu ya 5 na ya mwisho ni lisemwalo, lipo kama halipo linakuja. Japo mimi ni Msukuma, na jina langu la ubini ni Mayalla, siku zote nimekuwa nikielezwa na Wasukuma wa Ukweli maana ya jina Mayalla kwa Kisukuma ni ukame, drought unaosababisha famine, baa la njaa, lakini siku hizi kuna Wasukuma wa aina nyingi nyingi wengine ni wakuja tuu hivyo hata maana ya jina la Mayalla linabadilika badilika kutegemeana na Msukuma wa wapi. Toka siku ile nilipouliza lile swali Ikulu nikajibiwa kuwa Mayalla kwa Kisukuma ni Njaa, kiukweli kauli nyingine huumba, tangu nilipoitwa Njaa, kauli ile ikaniumbia njaa ya ukweli, hadi jina langu humu na mitaani ninaitwa Pasco Manjaa!. Baada tuu ya swali lile, contracts zangu zote za kampuni yangu ya PPR za serikalini zilisitishwa hivyo njaa ikaanza kunitembelea, tenda za maonyesho ya Saba Saba zikafutwa, tenda za kuandaa kipindi vya elimu kwa umma zikafutwa, ile ofisi yangu jengo la NHC pale Mtaa Mkepu niliokuwa nalipia pango sawa mshahara wa DC nikafunga, nilikuwa na wafanyakazi 20, nikawapunguza 15, tukabaki 5 na kuhamia kwenye kaji chumba jengo la Posta House. Kwa kwa vile mimi ni mwandishi wa habari, baada ya kufungiwa huko kote nikaamua kurejea newsroom kuandika makala za magazeti nako ndio vile tena nikaitwa Dodoma kuhojiwa na Kamati ya Bunge. Kila ninachogusa hakiendi. Sasa limeingia hili janga la Corona, hakuna kazi kabisa, ofisi nimefunga niko home sina hili wala lile ndipo likanijia hili wazo la kujiunga CCM na kugombea ubunge ili sasa nikawatumikie watu. Mtaji wa ubunge nimeamua kuuza kila kitu changu, kuanzia nyumba, na kila kitu kilichomo, magari, na container lililosheni mali za thamani kubwa.
  6. Kwa vile aliyenisababishia njaa hii ni Rais Magufuli kuniita njaa, kauli yake imeumba njaa, hivyo sasa najiunga CCM na kugombea ubunge jimbo fulani lililokuwa linashikiliwa na upinzani, kwasababu madhila haya amenisababishia rais Magufuli ambaye sio tuu ni home boy wangu, bali ndiye Mwenyekiti wa CCM, japo kwenye kura za maoni CCM, mimi sitaongoza, lakini siamini kama ataweza kunipita hivi hivi homeboy wake aliyemuita Njaa na kumsababishia njaa, hivyo nitateuliwa kupeperusha bendera ya CCM uchaguzi wa 2020.
  7. Kufuatia Kukubalika sana kwa CCM nchi nzima kulikosababishwa na kasi ya Awamu ya 5, ukiishateuliwa kupeperusha bendera ya CCM, wewe unakuwa tayari ndio Mbunge mtarajiwa unaesubiri kuapishwa tuu na ili kuokoa gharama za kufanya kampeni, kama kawaida ya CCM, uchaguzi Mkuu tutautumia ule wembe wa uchaguzi wa serikali za mitaa. Hivyo nitamsaidia sana rais Magufuli katika eneo la sekta ya habari.
  8. Kufuatia CCM kuwa ni watu wasiopendwa sana humu jf, nimenote wana CCM ambao ni wana jf, akiwemo Paul Makonda, Nape Mnauye, Juliana Shonza, Kigwangala, Prof. Tibaijuka, Mwigulu na wengine, hawachangii tena mijadala humu jf, hivyo na mimi nikiishajiunga tuu na kupokekewa pale CCM Lumumba na Polepole from then nitakuwa sichangii tena mijadala yoyote humu jf kama makada wengine watangulizi wangu. Nitakuwa Facebook, Twitter, Instagram na Snapchat
  9. Hivyo kwa bandiko hili, kwanza nawashukuru sana wana jf kwa Ushirikiano wenu katika kipindi chote cha miaka zaidi ya 10 tuliokuwa wote humu jf, nawaaga kwaherini ya kuonana, japo nitakuwa sichangii ila jf nitaendelea kuitembelea na likes nitakuwa naendelea kuzimwaga ila kiukweli nitawa miss sana na kufuatia uraibu wangu na jf, pia mimi mwenyewe nitateseka sana.
Nimalizie kwa kuwaomba Ushirikiano wenu, naombani support yenu kwa kuniunga mkono katika safari yangu hii ya kujiunga CCM, kugombea ubunge na kumsaidia rais Magufuli na kuisadia nchi yangu Tanzania.
AprilFool[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Mayalla kwetu inamaanisha njaa, tokea mkuu akuchane kwenye ile press na ulivyoitwa kuhojiwa bungeni uligeuka kuwa nyoka asiye na sumu, kila la heri huko uendako ni haki yako ya kikatiba tunasubiri kukuona majukwaani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom