Nimeanza Biashara ya Kukopesha, naomba ushauri

Nimeanza Biashara ya Kukopesha, naomba ushauri

Nafanya biashara ya pesa mkuu. Kama zilivyo benki zote za biashara

riba zangu ni kwa siku 7 unaleta elfu 2 kwa kila elfu 10 unayochukua.

kuna wengine wanachukua kwa siku 3, 4 mpaka 5 lakini interest iko palepale.

View attachment 2160027
nakusanya hio hela kutoka kwa wakopaji wadogo wale wa teni teni every day.

Nashukuru Mungu mtaji umekua kwa kasi sana kutoka 100,000 mpaka sasa inagonga laki 6.

nakopesha wale ninaowajua kiundani.

nisiowajua wanaweka vitu bondi.

CHANGAMOTO
mpaka sasa changamoto yangu ni mtaji umepungua wakopaji wamekuwa wengi, tena wale LEGIT wanaoletwa na wateja WAKONGWE.

imagine kama jana kuna mmama kaletwa anataka laki 1, arudishe 120k leo.

nilishangaa sana lakn nilipouliza kiundani waliniambia wanaenda ku top up mkopo wao kwenye kikundi na huwa wanafanya hivyo ili WAPATE MIKOPO MARA 2.

Hii biashara inalipa ila inahitaji uwe mtu makini sana.

SIO KILA MTU NI WA KUKOPESHA
CHUNGUZA KABLA HUJAKOPESHA.
ULIZA ULIZA KWA WANAOMJUA

kokudo note something
Poa.
 
This week earning chat ndio hio.
watu wanakopa hadi kwa masaa tu wanarudisha hela ya wiki🙏🙏🙏

IMG_20220323_191528_391.jpg
 
Mimi wanakimbia nikiwaambia 20% riba kwa siku 14 hii ipoje kwako
Kwangu sikimbiwi mkuu sana sana mimi inafikia hatua naishiwa hela kabisa ya kukopesha.

Jana tu mtu kachukua elfu 90 anadai ni emergence anairudisha leo saa 3 (ni mmama tunaivana sana) anairudisha kwa riba Tsh elfu 8.

asubuhi napokea sms kama hii. Riba ni ile ile ishaeleweka na watu hawaipingi
Screenshot_20220324-073643.png

cha msingi uweke msimamo wako.

mi kuvumilia wiki 2 siwezi aisee
 
Sidhan kma utaweza kuiendesha long term na kwa ukubwa kwa hiyo strategy
Mkuu kwangu imefikia hatua sasa natafutwa, na wanajipangia riba wenyewe.

Screenshot_20220324-142441.png


huyu alichukua jana 90,000
akarudisha 98,000 leo tarehe 24.3.2022

Aliniomba laki 1 nikawa sina ndo nikampa 90.

kairudisha hio kisha ananitumia sms anataka 30k.

riba wamejiwekea 3,000 kesho saa tano naifuata.

mambo ya long term or short term tumuachie Mungu mkuu.

Nipo kwenye gem toka mwaka jana na mpaka sasa nalisongesha tu cha muhimu kwa watu nisiowaamini huwa nabeba vitu naweka bondi.
 
Nimejaribu kuweka Tangazo mtaa wa pili kwamba nakopesha.

duh nimepigiwaa simu hizo mpaka nimechoka!

Msimamo wangu uko pale pale, sitoi hela bila kitu kuwekwa bondi.

baada ya hapo ndio tunaandikishana.
Hahaha duh
 
Sidhan kma utaweza kuiendesha long term na kwa ukubwa kwa hiyo strategy
Kwa Taarifa Yako,
Hii Biashara nimeiwekea Malengo Ya mwaka huu 2022, ilete pesa sio chini ya milioni 1 na nusu net profit (riba)

nitaendelea nayo sana hata kama nikihama huu mtaa ninaoishi.

nishajua chocho za kuwapatia hawa wanaokopa sana.

𝒎𝒂𝒍𝒆𝒏𝒈𝒐 𝒎𝒂𝒌𝒖𝒖 𝒉𝒂𝒔𝒂:
mpaka ije ifike December 2022 nimepanga kununua kiwanja cha laki 7 na kuanza ujenzi wa chumba na sebule Haraka.

na inawezekana kwa sababu,

napata faida ya Tsh 40,000 mpaka 65,000 kwa wiki.

ikiendelea hivyo baada ya miezi 8 ntakua na NP of 1,280,000 kwa average ya 40,000 kila wiki.

pembeni nako nafanya udalali sana.

huu mwaka lazima nitimize malengo.
 
Back
Top Bottom