Nimechoshwa na Huu umungu mtu unaooneshwa na serikali! Mpaka Sasa Mshahara haujatoka? Mnatuchukuliaje?

Nimechoshwa na Huu umungu mtu unaooneshwa na serikali! Mpaka Sasa Mshahara haujatoka? Mnatuchukuliaje?

Logically nikikulipa kabla ya deadline si kosa, kwa sababu sijakucheleweshea mshahara, nikikulipa baada ya deadline ni kosa kwa sababu nimekucheleweshea mshahara.

Huelewi nini hapo?
Hivi ukimlipa mtu kila baada ya tarehe 23 ya mwezi na mwingine akawa analipwa kila baada ya tarehe 30 ya mwezi unadhani hawa watu wawili wana tofauti?,Hapo hakuna tofauti wote wamefanya kazi kwa siku 30 ndipo wakapokea mafao yao
 
Unazunguka sana, nimeshakwambia serikali yenyewe haifuati hiyo standing order waliyojiwekea, kwanini wao walipe mshahara kabla ya mwisho wa mwezi?

Najua utarudi kulekule kuwatetea kwasababu ya mahesabu yao, nikikuuliza tena kwanini mahesabu yao wasiyafanye mapema? utaanza kuzunguka tuanze mwanzo.

Naona tuishie hapa, kila mmoja abaki na lake, japo sijapendezwa na namna unavyoitetea serikali hata ikivunja sheria iliyojiwekea.
Serikali haija violate standing order mpaka itakapolipa mshahara baada ya mwisho wa mwezi.

Kwa kutotaka ku violate standing order, serikali inaanza kulipa mishahara mapema kabla ya mwisho wa mwezi. Ndiyo maana mshahara wa May unaweza kuliowa May 23. Hapo wamekuwahishieni mshahara, hiyo si violation ya standing order. Violation ni kupitukiza mwisho wa mwezi bila kulipa mshahara, kulipa kabla ya mwisho wa nwezi si violation, kwa sababu mshahara kuwahishwa si tatizo, tatizo ni mshahara kucheleweshwa.

Mpaka sasa mwisho wa mwezi June haujafika, wewe unadai mshahara wa mwezi gani? May?

Kwa sababu kama unadai mshahara wa June, mwezi haujaisha bado. Subiri mwezi uishe halafu kama serikali haijalipa mshahara njoo hapa July 2 ulalamike hujalipws amshahara wa June, nitakuunga mkono.

Wewe huna savings unaishi paycheck to paycheck?

Ukikosa kazi kwa mwaka unaweza ku survive kwa savings zako?
 
Hivi ukimlipa mtu kila baada ya tarehe 23 ya mwezi na mwingine akawa analipwa kila baada ya tarehe 30 ya mwezi unadhani hawa watu wawili wana tofauti?,Hapo hakuna tofauti wote wamefanya kazi kwa siku 30 ndipo wakapokea mafao yao
Sasa kama hamna tofauti watu wanalalamika nini?

Si serikali inaweza kuwalipa tarehe 30 June? Kwani tarehe 30 June imefika tayari?

Kama kuwalipa tarehe 23 na tarehe 30 hakuna tofauti, kelele zote hizi za nini? Mbona tarehe 30 haijafika bado?

Huelewi tatizo.

Watu hawana hela, wanategemea mshahara kufanya kila kitu, mshahara mdogo vitu bei ghali, watu wanategemewa na famikia kubwa sana, wafanyakazi wachache, watu tegemezi wengi.

Ukiwalipa mshahara wa May tarehe 23 May, ikifika tarehe 23 June mshahara umekwisha, ndiyo maana wanalazimisha walipwe mshahara wa June tarehe hiyo hiyo 23.

Tatizo watu wanaishi paycheck to paycheck. Tatizo mshahara mdogo.

Hayo ndiyo matatizo.

Watu wangekuwa na savings za kujikimu kwa miezi sita mpaka mwaka, usingesikia kelele kwa sababu serikali haijalipa mshahara tarehe 23 June.
 
Serikali haija violate standing order mpaka itakapolipa mshahara baada ya mwisho wa mwezi.

Kwa kutotaka ku violate standing order, serikali inaanza kulipa mishahara mapema kabla ya mwisho wa mwezi. Ndiyo maana mshahara wa May unaweza kuliowa May 23. Hapo wamekuwahishieni mshahara, hiyo si violation ya standing order. Violation ni kupitukiza mwisho wa mwezi bila kulipa mshahara, kulipa kabla ya mwisho wa nwezi si violation, kwa sababu mshahara kuwahishwa si tatizo, tatizo ni mshahara kucheleweshwa.

Mpaka sasa mwisho wa mwezi June haujafika, wewe unadai mshahara wa mwezi gani? May?

Kwa sababu kama unadai mshahara wa June, mwezi haujaisha bado. Subiri mwezi uishe halafu kama serikali haijalipa mshahara njoo hapa July 2 ulalamike hujalipws amshahara wa June, nitakuunga mkono.

Wewe huna savings unaishi paycheck to paycheck?

Ukikosa kazi kwa mwaka unaweza ku survive kwa savings zako?
Umeshaniweka kwenye kundi la watumishi wa umma, sijui nimeajiriwa ofisi gani ya serikali!.

Kuvunja sheria maana yake ni kutoifuata, hivyo unaweza kuivunja kwa kuwahi tarehe au kupitiliza tarehe, kufuata sheria maana yake ufanye vile sheria inavyotaka/agiza, naona umeanza kuleta majibu ya kisiasa, pumzika.
 
Naona Uzi ushaanza kuwa kimya,, Itakuwa mama kashamwaga hela huko.
 
Umeshaniweka kwenye kundi la watumishi wa umma, sijui nimeajiriwa ofisi gani ya serikali!.

Kuvunja sheria maana yake ni kutoifuata, hivyo unaweza kuivunja kwa kuwahi tarehe au kupitiliza tarehe, kufuata sheria maana yake ufanye vile sheria inavyotaka/agiza, naona umeanza kuleta majibu ya kisiasa, pumzika.
Basi wewe ni mtu mjingamjinga tu unayependa kuzozana kwa mambo bila mantiki, kuliko nilivyofikiri.

Bora hata ungekuwa mtumishi wa serikali ningesema kwamba ujinga wako si wa asili, umeletwa na njaa.

Ujinga wako unaonekana kuwa ni wa asili. Hupendi facts tu.

What's next, utataka mshahara ulipwe exactly midnight tarehe ya mwisho wa mwezi, ukiwahishwa sekunde moja tu umevunja standing order ya serikali, na ukilipwa sekunde moja tu baada ya hapo pia umevunjwa standing order hiyo?
 
Basi wewe ni mtu mjingamjinga tu unayependa kuzozana kwa mambo bila mantiki, kuliko nilivyofikiri.

Bora hata ungekuwa mtumishi wa serikali ningesema kwamba ujinga wako si wa asili, umeletwa na njaa.

Ujinga wako unaonekana kuwa ni wa asili. Hupendi facts tu.

What's next, utataka mshahara ulipwe exactly midnight tarehe ya mwisho wa mwezi, ukiwahishwa sekunde moja tu umevunja standing order ya serikali, na ukilipwa sekunde moja tu baada ya hapo pia umevunjwa standing order hiyo?
Umesha panic, i'm a free minded person aisee, niko huru kujadili chochote akili yangu inaniruhusu, acha hasira kunywa maji utulie, hii ndio JF.

Sio lazima niwe na njaa ili nijadili, njaa sio ubongo, hauna hoja.

Hiyo what's next yako is nothing to me, naona umejigeuza mpiga ramli, pumzika au endelea na hao wengine kwangu umechoka!.
 
Hivi Kwanini waTanzania tunakuwa mazwazwa hivi kwenye haki zetu? Mpaka Leo jumatatu ya tarehe 24 Mshahara hamna na vivo hivyo hamna kauli yoyote ile kutoka kwa serikali hasa hasa Karibu mkuu utumishi yeye yupo Kimya tu! Hii haikubaliki kabisa

From now siwezi kuendelea kufanya kazi mpaka napewa stahiki yangu kwa maana Mshahara Nyie wengine watumishi ambao hamjielewi au hamjui haki zenu endeleeni na kazi zenu!

Bullshit!!!!!!!!!!

Note
Moderator msifute Huu Uzi naona siku hizi mmekuwa machawa na boss wenu mello
==========

Ufafanuzi kuhusu Mishahara ya Mwezi June
- Kuanzia mwezi huu, June 2024 mishahara ya watumishi wa umma itakuwa inalipwa Kati ya tarehe 28 - 30
Mbona tarehe ya mwisho wa mwezi bado haijagota? Usipolipwa hadi July 1, ndio ulalamike.
 
Umesha panic, i'm a free minded person aisee, niko huru kujadili chochote akili yangu inaniruhusu, acha hasira kunywa maji utulie, hii ndio JF.

Hiyo what's next yako is nothing to me, naona umejigeuza mpiga ramli, pumzika au endelea na hao wengine kwangu umechoka!.
Fact.

Serikali haijachelewa kulipa mshahara wa June kwa sababu mwezi wa June haujaisha bado.

Standing order ya serikali inasema mshahara unalipwa mwisho wa mwezi. That is the deadline.

Deadline ya serikali kulipa mshahara wa June haijafika bado.

Ukililia mshahara aa June kabla mwezi haujaisha, hiyo ni njaa yako tu.
 
Fact.

Serikali haijachelewa kulipa mshahara wa June kwa sababu mwezi wa June haujaisha bado.

Standing order ya serikali inasema mshahara unalipwa mwisho wa mwezi. That is the deadline.

Deadline ya serikali kulipa mshahara wa June haijafika bado.

Ukililia mshahara aa June kabla mwezi haujaisha, hiyo ni njaa yako tu.
Iko hivi; watumishi walilipwa mshahara wa mwezi uliopita tarehe 22/23 hivyo ilivyofika June 22/23 tayari ni siku 30/31 yaani mwezi.
Hivyo, wako sahihi acheni kuwatoa ufahamu kwa kutumia tarehe zenu.
 
Iko hivi; watumishi walilipwa mshahara wa mwezi uliopita tarehe 22/23 hivyo ilivyofika June 22/23 tayari ni siku 30/31 yaani mwezi.
Hivyo, wako sahihi acheni kuwatoa ufahamu kwa kutumia tarehe zenu.
Iko hivi.

Mshahara uliolipwa 22/23 May ulikuwa mshahara wa May. May yote, kuanzia May 1 mpaka May 31.

Mshahara huo si wa mpaka May 22/23.

Mshahara huo serikali ilikuwa na muda wa kuulipa mpaka mwisho wa mwezi wa May.

Ila serikali iliwahisha kulipa mshahara wa May kwa wiki moja ili kuhakikisha process zote za payroll zinakamilika kabla ya mwisho wa mwezi kufika, ili isi violate standing order ya kulipa mshahara by mwisho wa mwezi

Kwa hiyo, usianze kuhesabu siku 30 baada ya May 22/23 ili kulipwa mshahara wa June.

Serikali ina muda mpaka June 30 kulipa mshahara wa June.

Moja ya matatizo ninayoyaona ni kwamba watu wanahesabu siku 30 kutoka tarehe waliyolipwa mshahara wa May wakitegemea walipwe mshahara wa June katika siku hizo 30.

Standing order ya serikali kuhusu mishahara haijasema mshahara utalipwa ndani ya siku 30 baada ya mshahara wa mwisho kulipwa.

Standing order ya serikali imeweka mwisho wa mwezi kama deadline ya serikali kulipa mshahara.

Deadline hiyo kwa mwezi June haijafika bado, ndiyo kwanza tupo June 25. Serikali inaweza kulipa mshahara June 30 na bado ikawa haijavunja standing order hii.

Kwa kifupi, mshahara unatakiwa kulipwa mwisho wa mwezi, kama mwisho wa mwezi haujafika bado, wafanyakazi hawana haki ya kulalamika mshahara umecheleweshwa.

Angalia standing order ya serikali section ya kulipa mishahara imewekwa hapa post #290.
 
Watumishi wa umma hovyo sana. Sijui wanajikuta kina nani. Kazi zao nyingi ni planned already. Hakuna kuumiza kichwa sana. Kazi zenyewe mtu yoyote anafanya. Shukuru sana umejikuta hapo. Watu wenyewe mkifika kazini hamna multitask. Uje huku PS watu wanafanya kazi tanotano na bado mshahara unatoka tar 40. Tulia ndugu. Tulia
 
Watumishi wa umma hovyo sana. Sijui wanajikuta kina nani. Kazi zao nyingi ni planned already. Hakuna kuumiza kichwa sana. Kazi zenyewe mtu yoyote anafanya. Shukuru sana umejikuta hapo. Watu wenyewe mkifika kazini hamna multitask. Uje huku PS watu wanafanya kazi tanotano na bado mshahara unatoka tar 40. Tulia ndugu. Tulia
Hii thread inaonesha jinsi watumishi wa umma wengi wanavyoishi "paycheck to paycheck".

Ukichelewesha paycheck moja kwa wiki (kwa kuangalia tarehe ya paycheck ya mwisho, si kwa kuangakia standingborder ya serikali) tu watu wanalalamika.

Wakati kwa standard mtu anatakiwa kuwa na savings za kujikimu kwa miezi 6 mpaka mwaka mmoja, aweze kuishi vizuri bila kutegemea mshahara.

Watunishi wa umma Tanzania wanashindwa kuvumilia mshahara kulipwa mwisho wa mwezi kabla hata standing order haijawa violated.
 
Fact.

Serikali haijachelewa kulipa mshahara wa June kwa sababu mwezi wa June haujaisha bado.

Standing order ya serikali inasema mshahara unalipwa mwisho wa mwezi. That is the deadline.

Deadline ya serikali kulipa mshahara wa June haijafika bado.

Ukililia mshahara aa June kabla mwezi haujaisha, hiyo ni njaa yako tu.
Ajabu sana, huoni kama serikali ikilipa mshahara wa mwezi June, tarehe 30, itakuwa imewanyonya watumishi karibia wiki nzima tangu walipowalipa mshahara mwezi wa May, tarehe 23?

Hiyo standing orders waliiweka ili waifuate, kama wanajiwekea sheria wasizoweza kuzifuata wao wenyewe ni wazembe, usitetee huu uzembe wao kwa kulazimisha tarehe 30 iwe deadline hata kama inapitiliza.

Na wao kwa kujua hili, ndio maana wamekuwa na consistency ya kulipa mishahara tarehe 23 ya kila mwezi, ili wasizidishe muda kama unavyowaruhusu na hiyo standing orders yako.
 
Ajabu sana, huoni kama serikali ikilipa mshahara wa mwezi June, tarehe 30, itakuwa imewanyonya watumishi karibia wiki nzima tangu walipowalipa mshahara mwezi wa May, tarehe 23?

Hiyo standing orders waliiweka ili waifuate, kama wanajiwekea sheria wasizoweza kuzifuata wao wenyewe ni wazembe, usitetee huu uzembe wao kwa kulazimisha tarehe 30 iwe deadline hata kama inapitiliza.

Na wao kwa kujua hili, ndio maana wamekuwa na consistency ya kulipa mishahara tarehe 23 ya kila mwezi, ili wasizidishe muda kama unavyowaruhusu na hiyo standing orders yako.
Serikali ikilipa mshahara wa June June 30, haitawanyonya watumishi mshahara wa wiki moja.

In fact Tanzania kila mwezi serikali inapowalipa mshahara watumishi tarehe 22/23 ndiyo watumishi wanainyonya serikali kwa kulipwa mshahara wiki moja kabla ya mwisho wa mwezi.

Kwa sababu, mshahara uliolipwa May 22/23 haukuwa mshahara wa kazi iliyofanywa mpaka May 22/23. Ulikuwa mshahara wa mwezi wote wa May kuanzia May 1 mpaka May 31.

Usione mshahara umelipwa May 22/23 ukafikiri mshahara huo ni wa kazi iliyofanywa mpaka May 22/23.

Mshahara huo ni wa mwezi wote wa May, umelipwa kwa kazi ya May 1 mpaka May 31.

Kwa nini huelewi hili?
 
Serikali ikilipa mshahara wa June June 30, haitawanyonya watumishi mshahara wa wiki moja.

In fact nyie kila mwezi serikali inapowalipa mshahara tarehe 22/23 ndiyo mnainyonya serikali kwa kulipwa mshahara wiki moja kabla ya mwisho wa mwezi.

Kwa sababu, mshahara uliolipwa May 22/23 haukuwa mshahara wa kazi iliyofanywa mpaka May 22/23. Ulikuwa mshahara wa mwezi wote wa May kuanzia May 1 mpaka May 31.

Usione mshahara umelipwa May 22/23 ukafikiri mshahara huo ni wa kazi iliyofanywa mpaka May 22/23.

Mshahara huo ni wa mwezi woye wa May, umelipwa kwa kazi ya May 1 mpaka 31.

Kwa nini huelewi hili?
mazoea. Umejitahidi kufafanua lakini wapi! Alafu hao ndo watumishi wa serikali
 
mazoea. Umejitahidi kufafanua lakini wapi! Alafu hao ndo watumishi wa serikali
Hawa watu kwa hoja zao hizi napata shaka sana kuhusu ufanisi wao kazini.

Yani watu wanafikiri mshahara ukilipwa tarehe 23 huo ni mshahara wa kazi iliyofanywa mpaka tarehe 23 tu!

Hawaelewi huo ni mshahara wa mwezi mzima, umelipwa tarehe 23 tu.
 
Hawa watu kwa hoja zao hizi napata shaka sana kuhusu ufanisi wao kazini.

Yani watu wanafikiri mshahara ukilipwa tarehe 23 huo ni mshahara wa kazi iliyofanywa mpaka tarehe 23 tu!

Hawaelewi huo ni mshahara wa mwezi mzima, umelipwa tarehe 23 tu.
hili nalo ni tatizo, watu wa aina hiyo hawana shukrani, ni sawa na mtu aliezoea kupewa zawadi mara kwa mara, siku ukikosa kumletea/kumpa zawadi inakuwa kesi ya madai, tena serious kabisa! [emoji23]
Ukishaliona hilo ni hakuna kutoa ofa tena!
 
Mshahara unalipwa kwa standing order ya Katibu Mkuu utumisho.

Imewekwa hapa post number #290.

Serikali inatakiwa kulipa mshahata mwisho wa mwezi. Ikiwahisha sawa, lakini haitakiwi kupitiliza mwisho wa mwezi bila kulipa mshahara.

Sasa huu mshahara wanaodai watu ni wa mwezi gani? Mwezi May?

Kwa sababu kama ni wa mwezi June, mwezi haujaisha bado.
Nimeona mkuu asante sana.
 
Back
Top Bottom