Nimechukizwa na wananchi kushangilia vifo vya wanachama sita wa CCM kwenye ajali Njombe. Taifa limegawanyika, tusipuuze

Mmi nimefurahi sana tena naomba sana hii ajali ingewapata wale 4 ngazi za juu kabisa ...... nimewachoka kuliko kuchoka kwenyewe .... hapo kuwa sote tuta kufa ...... haiweekqni una apa kwa kutumia kitabu cha dini tena mbele za watu huku una nyanyasa wanachi unatumia cheo chako kuwa nyima hakizao ...... kila nikisoma ripoti ya CAG ....... nashikwa na hasira sana [emoji22]
 
uimara wa magari yanayobeba wanaccm uchunguzwe

View attachment 2781656
Nilipoona picha hii kwa mara ya kwanza, niliamini ni miwani/mawani ndiyo yananidanganya kuwa hii ni "mifugo" inapandishwa kwenye lori tayari kupelekwa mmadani!
Ni mpaka pale nilipoona video yake hawa "binadamu" wakilalamika kuwa wapewe hela yao waliyohaidiwa kwanza kabla ya kupanda hilo lori, ndipo nilipoamini kuwa utumwa bado upo na kuwa "miwani" yangu haina shida.
 
Ni punguani tu asiyeweza kufungamanisha uhusika wa CCM na matatizo tuliyonayo.
 
😆😆😆
 
Naamini wanasiasa wetu hasa kutoka CCM wanatudharau sana wananchi, na wanatoa kauli zisizo na utu hata kidogo. Haya ndiyo matokeo ya uongozi usiojali na wenye kujaa jeuri.
Ila hatupaswi kufikia hatua ya kufurahia vifo vya watanzania wenzetu kwa sababu ya itikadi zetu. Ni ukosefu wa utu uliopitiliza, ni dalili za kukata tamaa, ni hatari kweli kweli, ni bomu linalosubiri kuondolewa safety pin tu lilete madhara yasiyo na kikomo.
 
Mbona CCM waloshangalia Lissu alipopigwa risasi. Tena wengine walikebehi kuwa kwanini hakufa, wakalaumu wapiga risasi. Ungeanza na hao kwanza. Tusiwe wanafiki Bali wakweli.
Hilo haliwezi kuhalalisha watu kufurahia vifo vya watanzania wenzao. Viongozi wanaliingiza taifa hilo kwenye dimbwi lililojaa tope.
 
"Kuna mahali watawala wanatakiwa kuweka sawa mambo, tulipofikia ni pabaya sana"

Mkuu 'Idimi', ninakubaliana nawe moja kwa moja kuhusu hili uliloeleza katika mstari huo; lakini kweli unamwona kiongozi yeyote sasa hivi mwenye uwezo wa kufanya haya unayoeleza wewe?

Mimi naona kama viongozi tulionao sasa, kila mmoja wao ni maslahi mbele kwanza kabla ya kingine chochote. Hali hiyo ndiyo inayozidisha chuki baina ya wananchi.

Kiuhalisia hatuna viongozi, bali tuna watawala.
 
Bora hayo madhara take tu, kwani madhara ya Sasa ya kuwa na chawa Kila Kona huyaoni?
 
Ninakubaliana nawe katika yote uliyoeleza hapa. "Utu/ubinaadam" unapotea miongoni mwetu.

Lakini ukitafakari kwa kina, haya yote ni matokeo ya matendo ya hao hao wasiojali utu/ubinaadam wa raia wanaowatawala. Hawa ndio wanapopata majanga kama haya, raia wanakuwa kama wamepata fursa ya kuwakumbusha kukosa utu/ubinaadam katika matendo yao juu ya raia wanaowatawala.

Na kwa bahati mbaya sana, hakuna viongozi wanaostuka, mambo kama haya yanapojitokeza bayana kiasi hiki na kuanza kujihoji kati yao hali inavyozidi kuharibika.
Ni kama viziwi na vipofu kwa wakati mmoja. Wao wanachojua ni kunogewa tu matokeo ya matendo yao haya mabaya.
 
Ukiona hivyo ujue Ccm yenyewe ndo chanzo cha hiyo chuki

Ubaya waliuanzisha wao ccm kwa nini wachukiwe hata kwenye ajali?

Watende haki uone kama watachukiwa!


Huko walikokuwa wanaenda hamna wanachama hadi marehem watoke walipotoka?


Kwa nini ni ccm tu ndo isombe watu kwenda kujaza uwanja na si vyama vingine?

Naamini kabisa vyama vingine vikisomba watu trafick hawataruhusu hilo jambo

HAKI HUINUA TAIFA
 
Duniani hapa kila mtu yuko na anachokipendelea hivyo isikupe shida sana
 
Mkianza kujadiri WANAWACHEKA MAREHEM bila kujua WHY MAREHEM WANACHEKWA sitoshangaa MAREHEM WAKICHEKWA ZAID
 

Dini ni upuuzi,imeharibu uwezo na akili za mwanadamu. I wish dini zisiwepo ulimwenguni.
 
Dini ni upuuzi,imeharibu uwezo na akili za mwanadamu. I wish dini zisiwepo ulimwenguni.
Dini zilikuja kwa nia njema kabisa, lakini baadaye zikaingiliwa na wale wenye nia ovu za kupata madaraka kwa njia yeyote ile !!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…