Nimefanya Maamuzi Sahihi na Makini Niliyoahidi Takribani Saa 72 zilizopita, Naelekea ....

sawa Ben ila kumbuka kuna michujo wa ndani ya vyama dhidi ya watia nia ndani ya chama pindi ukiachwa usikate tamaaa bali mbinu na uwezo wako ujumuike na mgombea kwenye kampeni ilimpate ushindi.naushindi huo utakua ni furaha kwako...
 
Ruttashobolwa

Jiongoze kaka uzi umefika page ya sita mkuu wewe umebaki na hoja moja tu "Kwahiyo Ben saanane siyo msaliti tena"..!! Huna hoja nyingine zaidi ya hiyo? Mbona wewe ni mtu mzima mwenye akili timamu, nini tatizo lililopo kwenye uelewa wako? Eti unachochea kuni..!! Ili ikusaidie nini ndugu yangu? Hivi utakula hizo kuni unazochochea hapa..?

Angalau Ritz mwenzio kamtakia heri Kamanda na kijana mwenzake kwenye malengo yake,wewe hata kufungua mdomo kukubali tu kile kilichocndikwa na Ben hapa umeshindwa..!! Umebaki kushabikia vitu visivyo na Msingi Vitakusaidia nini KJ...!!??

Anyway ngoja tumsubiri Ritz hapa amesema anaanza kushisha.matusi yaliyotukanwa na Bavicha kwa Ben Saanane, Ila mimi namuomba aonyeshe pia Namna Vijana wa Ccm,Act na wengineo wasikubaliana na Chadema jinsi walivyokhwa wakimsifu Ben kwamba ni kijana makini amabaye hajawahi kutokea Tanzania na Chadema yote..!! Hapa aanze na post zako zote ulizotoa kumuhusu Ben..

Alitukanwa Yesu alipokuwa ktk harakati za kuwaletea ukombozi itakuwa Ben ndani ya Cdm? Mume na Mke hugombana na kufukuzana itakuwa Ben na Makamanda wenzake tena wasiofahamiana kabisa? Lakini kubwa kuliko yote Wewe inakuwashia nini kwa kutukanwa kwa Ben? Unapungukiwa na nini hasa?

Watu wengine bwana..!!!

BACK TANGANYIKA
 
Last edited by a moderator:
kamanda mabere malando alisema, mshauri mkuu wa zzk ni huyu mmiliki wa jf so, huenda kunaukweli hapo, nyuzi za uongo wanazoleta ccm=act, hata kama ni za kuchafua mtu, hakuna ushahidi zitaachwa hata siku nzima, sasa leta maada yenye ushahidi inayohusu ccm=act, au zzk, ndani ya sekunde 5 imenyofolewa na ukicheza una kula ban, kwa kweli jf inaelekea kuwa kama mitandao minginze ya hovyo kabisa;
sasa act wanatoa wapi ujinga wanao andika. Mods mko wapi au tuamini mnaibeba act?? Taarifa nyingi zinazoletwa na hawa mamluki ni za uongo. Tumeona hata zitto akitoa taarifa za uongo na mnazipokea. Hata pale walengwa wanapokanusha mods mnakaa kimya
 
Yericko Nyerere, Asante sana komredi wangu

Ha ha ha ha umewaacha ACT wavizia mizoga midomo wazi,maana yake wamegeuka mafisi wavizia mizoga inayotupwa na wenzao.

Wakisikia mwanachama yeyote wa CHADEMA anataka kuchukua maamzi magumu,maamzi magumu wanaoyajua wao ni kwenda ACT,mwisho watameza na visivyo mezaka.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu kwahiyo ile sumu sasa ni direct kwa spika siyo zitto tena lakini mlangoni pale bungeni kunamashine sijui kama utaingia nayo ndani.

Bora wewe umejitambua na kuunga mkono nakwenda Bungeni Ben sanane! Hayo ya sumu ni uzushi tu.
 
Ben akigombea namfuata katika jimbo hilo nami nikagombee, najua madhaifu yake huyu mkaanga Sumu.

Jimboni wagombea wanaenda kujinadi namna watakavyoshirikiana na wananchi wa jimbo husika katika kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi wewe unaenda kunadi madhaifu ya watu?

BTW mbona umekomaa mno kutoa comments nyingi katika uzi huu, ni mahaba binafsi kwa huyu mtoa nia au wivu? Hueleweki kabisa!
 

Hahahaha ACT harakat zao kama za futuhi
 
MODS WANAENDEKEZA SANA UPUUZI WA HAWA CCM=ACT KWA KWELI, SIJUI WANAPEWA MLUNGULA AU VIPI?? SHUTUMA ZA UONGO KABISA ZINAACHWA HAPA, LAKINI JANA NIMEMSHAURI MAKENE AJITAHIDI KUWA SHARP, WATU WA CHAMA WANAPOKUWA ATTACKED BILA USHAHIDI AJE MARAMOJA KUTOLEA MAELEZO, OTHERWISE, HILI SUALA LA BEN NA LA SILINDE NA WENJE, NA DADA ROSE LIMESHANGAZA SANA WATU, NA KUNA WATU WAMEVUNJIKA SANA MIOYO, COZ YA KUTOPATA UKWELI WA TAARIFA; MODS HAWAKO FAIR AT ALL.....[QUOTE=Mzito Kabwela;12419399]Mkuu, nafurahishwa na viongozi wa Chadema kuendelea kunyamaza kimya.. kurugenzi ya habari, Mohamedi Mtoi na wadau muhimu wamenyamaza. Kurugenzi ya Usalama ya Chama itakuwa iko busy kuinvestigate huu mchezo wa kuigiza ulioanzishwa na ACT kwa kushirikiana na CCM. Huenda watu wetu wanashiriki...[/QUOTE]
 
Ben, Kwanza nikupe hongera kwa maamuzi yako, lakini ukweli tuuzungumze hapa mapema. hakuna mgombea uchaguzi atakayekuwa akiwakilisha Chadema isipokuwa UKAWA na lazima ukubalike na mfumo watakao uweka. Aidha mfumo huo tayari bado haujatangazwa ama bado UKAWA hawajafikia maridhiano juu ya Uwakilishi. Mkigawana Majimbo lazima uwe umepewa jimbo tayari kama mgombea na kupitishwa maana yaonyesha kuna kugawana hakuna uchaguzi mdogo halali muda huo uko wapi?

Kwa nini sisi wengine tunakuwa na hasira na Chadema? ni kwa sababu hizi, sababu ambazo chama kimevutwa ktk ushirika ambao chama kimeshindwa kutangaza sera zake, maono yake juu ya mabadiliko wanayokusudia kuwapelekea wananchi isipokuwa lengo limebadilika kuwa ubishani bungeni. Wewe hapa umeeleza vizuri sana nia yako ya kugombea Ubunge lakini haya ni maono yako leo yapo JF lakini wananchi vijijini hawafahamu hilo wamepumbazwa na katiba Mpya. Na ni maono yako sio sera za UKAWA hivyo mbunge hawezi badilisha maisha ya wananchi ikiwa sio lengo la UKAWA. Na unapogombea kujaza Bunge huwezi waahidi wananchi mabadiliko maana hutaongoza nchi ila mnaahdi kubishana juu ya maamuzi ya CCM.

Tumezisikia hadithi hizi miaka mingi toka wabunge wa CCM wakiahidi wananchi kwa uchungu kabisa wakielewa nini matatizo ama mahitaji yao lakini hakuna lilofanyika. Ahadi za Wabunge na mipango ya chama hutofautiana kwa mbali kabisa, hivyo maadam UKAWA hawana sera ya pamoja isipokuwa ahadi za Katiba ya Wananchi, UKAWA hawana mpango maalum juu ya mambo muhimu yanayowakwaza wananchi isipokuwa kupitia mapungufy ya CCM inanipa shida sana kukupongeza kwa sababu hii ni ahadi tu kama ahadi nyinginezo. Kwa bahati mbaya sana tupo wengine tunaojua serikali hufanya vipi kazi zake, na tumeona wabunge wa Upinzani wakibakia kulaumu tu CCM juu ya ukosekanaji wa maji, barabara au huduma bora katika majimbo yao maana wao hawana jukumu wala meno ya kupeleka maendeleo hayo majimboni ila lugha za udanganyifu tu wapewe kura.

Tunakutakia kheri kwa maamuzi yako lakini fikra zako zitabakia hapa JF kwa sababu sio fikra za pamoja zinazounda umoja wa UKAWA. Na kibaya zaidi ni kwamba mpango wa kugawana majimbo ili UKAWA iwe na viti vingi Bungeni ni mpango wa kusadikika haswa ukizingatia kwamba bado tunatumia katiba ya zamani. NEC ipo chini ya CCM, TISS sio chombo huru, Polisi sio chombo huru, mahakama na jaji mkuu sio mtu huru. Hawa wote watalazimka kukitumikia chama. Na iwapo CCM watataka kuhakikisha UKAWA hawapati asilimia 50 bungeni UKAWA hawatapata, na bakora mtacharazwa! Kama leo mmeshindwa kwenye katiba Mpya mkainua mikono na kubakia kulaumu, mtaweza vipi kufanya tofauti ikitangazwa mmeshindwa Uchaguzi!
 
We mbeba sumu nani akupeleke bungeni, badala ya bungeni utaelekea Jela Magereza
 
Mi nilifikiri maamuzi magumu kweli kumbe upuuzi tu. Jimbo la Rombo lisahau wanarombo bado wanampenda Selasini
 
Ben na hicho kigugumizi chako utachangia hoja gani bungeni? we endelea kutumwa tumwa chips mayai na Mbowe hapo Ufipa
 
Sasa ACT wanatoa wapi ujinga wanao andika. Mods mko wapi au tuamini mnaibeba ACT?? Taarifa nyingi zinazoletwa na hawa mamluki ni za uongo. Tumeona hata Zitto akitoa taarifa za uongo na mnazipokea. Hata pale walengwa wanapokanusha mods mnakaa kimya

Mkuu, huu mchezo haufanywi kwa bahati mbaya.......Mods, watu wetu na hao wazushi wa ACT wote ni 'mazganyanza'
 
Alichokifanya Ben ni kitu kibaya sana japokuwa baadhi mnafurahia kwa Ben kukanusha na kutangaza nia. Kulikuwa na tatizo gani kwa Ben kuja kukanusha taarifa kabla ya watu kuanza kufunguka kwa kauli chafu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…