Nimefika Tabora, nawaambia wanipeleke mjini wanasema ndio hapa tulipo!

Nimefika Tabora, nawaambia wanipeleke mjini wanasema ndio hapa tulipo!

Nililetaga Uzi wangu kuhusu biashara ya spare nahisi mwaka jana,

nilienda kuongea na rafiki yangu akanishauri nifungue vitu vya urembo wa magari, Kwa kweli nilianza kwa ugumu sana nikiwa bado sielewi vitu vingi.

Mkoa wa Tabora ni mkoa mkubwa sana, changamoto Kwanini bado maendeleo ni machache ni sababu ya miundombinu ilikuwa mibovu, kwa sasa kidogo panaanza kufunguka.

Nilileta Uzi wa makontena ya kuhifadhia ndizi bado sikupata muitikio mzuri sana, japo kuna mtu nipo naongea nae kwa sasa ananielekeza baadhi ya mambo.

Ukifika Katavi, Kahama, Geita utaona kuna fursa nyingi sana.

Binafsi nililemaa sana kukaa kariakoo, lakini hivi sasa kila siku akili inapanuka kukutana na watu tofauti tofauti na fursa ni nyingi.

Karibu mkuu.
Huko unakosema kuna fursa kuna watu kibao wako huko na hawajatoboa na hizo fursa.

Usione watu ukadhini ni wajinga.

Ukisikia Kilo ya Mahindi Tanga au Mbarali Mbeya ni Tsh 500 tu.

Ukienda Dar kilo ya Sembe ni Tsh 2000.

Unaweza kujiuliza kwanini watu wa huko hawafanyi viashara ya Mahindi kupeleka Dar?
 
Nini kiliupata huu mkoa? Nimewahi kufika Nzega na Igunga nikajua Tabora mjini patakuwa bora zaidi ya kule nimeshangaa.

Yaani mjini center nyumba ni za kizamani, hakuna kabisa modern buildings. Katikati ya mji nyumba zina mabati yameoza.
Ndiyo ujue ccm imeshika hatamu.

Hujaona misururu ya wateja bank na magari used yenye no E njiani?
 
Huko unakosema kuna fursa kuna watu kibao wako huko na hawajatoboa na hizo fursa.
Mkuu Bush,
Nisome taratibu na kunielewa.

Hapana sehemu nimesema kuhusu kutoboa nimesema zipo fursa.

Geita kuna vijana wanapata pesa nyingi sana lakini wanaotoboa ni wachache, wengi zikiishia kwenye katikati ya mapaja na pombe.

Nimezungumzia kutoka nje ya kariakoo, nilikuwa na mentality ya kariakoo ni kila kitu na Nina ofisi mpaka sasa, lakini nilipotoka nimejifunza kuna fursa nyingi sana.

Soma unielewe nimezungumzia fursa sio kutoboa, ndio maana Unaweza ukawa na rafiki yako mmeajiriwa Polisi mwaka mmoja, mna cheo sawa kwa maana mlipata fursa Lakini akakushinda maendeleo.

Mapambano yaendelee mkuu.
 
Nini kiliupata huu mkoa? Nimewahi kufika Nzega na Igunga nikajua Tabora mjini patakuwa bora zaidi ya kule nimeshangaa.

Yaani mjini center nyumba ni za kizamani, hakuna kabisa modern buildings. Katikati ya mji nyumba zina mabati yameoza.
Halafu unakuta mtu anahangaika kuamini hawezi kumiliki kiwanja DSM halafu haonii fursa kama hii ya tabora
 
Nini kiliupata huu mkoa? Nimewahi kufika Nzega na Igunga nikajua Tabora mjini patakuwa bora zaidi ya kule nimeshangaa.

Yaani mjini center nyumba ni za kizamani, hakuna kabisa modern buildings. Katikati ya mji nyumba zina mabati yameoza.
Utakuwa hujatembea hii nchi au bado una umri mdogo sana.wat did u expect toka mkoa mdogo kama Tabora ulitaka uwe kama Arusha or Mwanza.
 
Nini kiliupata huu mkoa? Nimewahi kufika Nzega na Igunga nikajua Tabora mjini patakuwa bora zaidi ya kule nimeshangaa.

Yaani mjini center nyumba ni za kizamani, hakuna kabisa modern buildings. Katikati ya mji nyumba zina mabati yameoza.
Acha uongo mkuu.

Tabora mjini kuna ghorofa nyingi kuliko jiji la Mbeya, Tanga na Mwanza na mji ni mkubwa kuliko Dodoma, Morogoro, Tunduma na Moshi
 
Nini kiliupata huu mkoa? Nimewahi kufika Nzega na Igunga nikajua Tabora mjini patakuwa bora zaidi ya kule nimeshangaa.

Yaani mjini center nyumba ni za kizamani, hakuna kabisa modern buildings. Katikati ya mji nyumba zina mabati yameoza.
Ndio mana tuliona bora tuwe na serikali za majimbo kila mapato yetu yanakuja kuboresha jiji lenu kwa nini?Mapato ya tumbaku ,asali ,na mpunga pia mazao ya misitu yabaki kuijenga mboka manyema.
 
Back
Top Bottom