Nimefuatilia ziara ya waziri Gwajima mikoani, kiukweli madudu ni mengi. Yule Ummy alikuwa anapiga siasa tu!

Nimefuatilia ziara ya waziri Gwajima mikoani, kiukweli madudu ni mengi. Yule Ummy alikuwa anapiga siasa tu!

Kila eneo analopita waziri wa afya Dr Gwajima katika ziara zake mikoani ni vilio tu, wananchi wanalalamikia Huduma hafifu, uhaba wa dawa nk....nk

Kiukweli hii wizara ina madudu mengi sana na sielewi waziri aliyetangulia Da Ummy Mwalimu na wasaidizi wake walikuwa wanafanya kazi gani!?

Chapa kazi Dr Gwajima wananchi tuko nyuma yako.

Maendeleo hayana vyama!
Nafikiri huyu mama anajikita kwenye utaratibu was kitaaluma zaidi, na namna taaluma inavyotakiwa kuleta matokeo chanya katika eneo la kazi (Yaani utekelezaji wa majukumu) na sio mbwembwe za kupayuka hovyo.
 
Majina ya Gwajima ni shida sana.
Usije ukamuita mwanao Gwajima
 
Makubwa ya Ummy Mwalimu ni yepi bwashee!
Ukweli mchungu hausemwi, mbali ya madhaifu ya baadhi watumishi, kubwa ni bajeti pesa iliyotegwa haipelekwi kamilifu ukiacha pesa ya kujenga maboma, dawa , vifaa tiba mtihani, hata wanachokusanya hakirejeshwi. Deni msd limefikia ukomo, kuna wakati msd anaambaza dawa za wahisani pekee kwa baadhi wateja.
 
Huyo Gwajima unaemsifia alikuwa Mlurugenzi wa Tiba miaka mingi, baadae akaja kuteuliwa Naibu Katibu Mkuu Tamisemi upande wa Afya akiwa kama Mtendaji alipaswa kuwa kishashughulikia kwa kuwa ndio wajibu wake Mkuu

Inakuaje leo ndio aone matatizo hayo

Labda kwa kuwa Naibu Katibu Mkuu hana fursa ya kutembea na Vyombo vya habari!

Wizi wa Dawa hauwezi kumalizwa kwa Ziara za kustukiza

Kuna Wazalendo pale walipendekeza MSD (bohari kuu ya dawa) ikiagiza dawa nje zipigwe chapa kabisa ya (GOT) i.e Goverment of Tanzania ikimaanisha kama sabuni inawezekana kupigwa chapa ya mbuni au mshindi au protex kwny mche kwanini ishindikane kwa vidonge wakati huwa vinatenezwa kwa order kubwa viwandani, dawa za chupa nazo zipigwe nembo ya Serikali

Hii ingezuiwa wizi wa dawa kwa kuwa tungeikuta pharmacy au hospital binafsi tungeijua kuwa imetokea Serikalini, …waliotoa ba kutaka kuteleleza wazo hilo nadhan wangeweza kuhadithia fitna waliyopigwa baada ya wazo hilo

Miaka ya mwanzo ya 1990s niliwahi kuzuru Kiwanda cha Cement cha Twiga, vioo vilivyowekwa vyooni vyote viliandikwa 'Kioo hiki kimeibiwa Wazo hill'

yale Maandishi yalisaidia sana kuzuia wizi wa vioo vile!
 
Kweli ili uwe mwanaccm mzuri lazima uwe na Phd ya unafiki! Ummy aliyemwagiwa sifa lukuki kuwa kaishinda Corona kwa maombi ya kishindo hadi akaitwa mama wa corona leo anaonekana alikua mzugaji
 
Kila eneo analopita waziri wa afya Dr Gwajima katika ziara zake mikoani ni vilio tu, wananchi wanalalamikia Huduma hafifu, uhaba wa dawa nk....nk

Kiukweli hii wizara ina madudu mengi sana na sielewi waziri aliyetangulia Da Ummy Mwalimu na wasaidizi wake walikuwa wanafanya kazi gani!?

Chapa kazi Dr Gwajima wananchi tuko nyuma yako.

Maendeleo hayana vyama!
Hata JK mlikuwa mkimsifia kwenye utawala wake na alipo kuja 'huyu' mkaanza kusema nchi ilichezewa sana kipindi cha JK.

Kwa sisi tunao wafahamu tabia zenu hatushangai, ngoja aje 'Gwajima' mwingine mtamponda huyu wa sasa pia bwashee!!
 
Gwajima ni miongoni mwa waliokuwa wasaidizi wa Ummy.

Tumlaumu Gwajima kwa kutomsaidia na kumshauri Ummy ipasavyo
Kwa post hii johnthebaptist kila unapoleta post zake humu JF tumia senses zako zote. Ona sasa ulivyoachwa uchi. Kumbe waziri wa sasa wa afya ambaye alikuwa Naibu Katibu Mkuu ktk Wizara hiyo hiyo alikuwa anamhujumu kwa nguvu zake zote aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo kipindi hicho; Mhe. Ummy!
 
Hata kama ataongez miaka bado tu ataachia madaraka iwe kwa uzee au kifo na mambo yake yote yatakua uchi.
Hata Kikwette alipotoka tulisikia mengi yakiwamo kusaini mikataba ambayo hata mwenda wazimu asinge saini.

Tuombe Mungu CoviD atunusuru. Bila shaka tutasikia mengi kuhusu chattle na hata zile 1.5Tr baada ya jiwe.

Labda tu kama ana mpango wa kufuata nyayo za nduguye Mr. quarter pin.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Kweli ili uwe mwanaccm mzuri lazima uwe na Phd ya unafiki! Ummy aliyemwagiwa sifa lukuki kuwa kaishinda Corona kwa maombi ya kishindo hadi akaitwa mama wa corona leo anaonekana alikua mzugaji
Nafikiri vyama vya siasa kiujumla ni unafki mtupu,leo Mbowe anaulumu serikali kwa suala la Corona wakati kipindi cha kampeni wakati watu wanajazana kwenye mikutano ya kampeni za chadema hakuwahi hata kuwaambia wananchi kuchukua tahadhari wakati huo waliungana na Magufuli kwenye imani ya kwamba hakuna corona Tz ili tu la kwao lipite.
 
Kila eneo analopita waziri wa afya Dr Gwajima katika ziara zake mikoani ni vilio tu, wananchi wanalalamikia Huduma hafifu, uhaba wa dawa nk....nk

Kiukweli hii wizara ina madudu mengi sana na sielewi waziri aliyetangulia Da Ummy Mwalimu na wasaidizi wake walikuwa wanafanya kazi gani!?

Chapa kazi Dr Gwajima wananchi tuko nyuma yako.

Maendeleo hayana vyama!
Ummy Mwalimu alikuwa anashirikiana na Mkurugenzi wa MSD ambaye yuko Segerea kwa tuhuma za utakatishaji fedha. Waziri Ummy, Bwanakunu na mganyabiashara wa dawa Bahari Pharmacy ndiyo wameidhoofisha MSD kwa mikataba feki ya dawa, ku- supply delivery kits zilizo expire.

Waziri Gwajima asijisumbue kwenda mikoani kuwafokea madokta na mafamasia wasio na madawa, bali aende MSD akajionee UOZO. Kuna madawa yapatayo Sh 30 Bilioni ambayo yame expire.
 
Huo uhaba wa dawa una zaidi ya miaka sasa . Hivi wafahamu pamoja na Serikali kujinasibu kuongeza bajeti ya dawa lakini kiuhalisia hiyo bajeti haitoki? Hivi unafahamu kwa zaidi ya miaka 2 Serikali haikupeleka pesa ya kununua dawa kutoka Hazina kwenda kwenye Zahanati, Vituo vya Afya na Hospitali? Hizo dawa zingenunuliwa kwa pesa ipi?

Hivi wafahamu pesa za Mfuko wa Afya ( Health Sector Basket Fund) hazikupelekwa Halmashauri almost mwaka wote wa 2020? Wadhani uendeshaji wa Idara ya Afya katika mila Halmashauri ya Wilaya (CHMT) na Sekretatieti za Mikoa ( RHMT) ulikuwaje?

Serikali itimize wajibu wake wa Msingi wa kuhakikisha MSD Kuna dawa za kutosha na pesa kwenye Vituo ziwepo za kutosha Kama utaona hivyo vilio
Kwa taarifa yako Serikali ya Magufuli imepeleka Fedha nyingi MSD kuliko kipindi chohote toka nchi ipate UHURU mwaka 1961. Kati ya July 2016 Hadi Mei 2019 Hazina walipeleka Tsh 314 Bilioni sawa na Tsh 104 Bilioni kwa mwaka. Mwaka 2015/16 wakati Serikali ya JK inaondoka walipeleka Tsh 30 Bilioni.

Katika historia ya MSD kipindi cha UMMY Mwalimu tulijionea kwa mara ya kwanza Waziri akiwa na mahusiano ya karibu sana na Mkurugenzi wa MSD Laurean Bwanakunu. Walikuwa na mahusiano ya kingono na kugawana Fedha kwa kupitia kwa Katwaza wa Bahari Pharmacy ambaye walikuwa wanampa mikataba mingi ya ku-supply dawa hasa vile vifaa vya kits za kujifungulia akina mama.

Haya ninayoyasema siyo majungu yako kwenye Ripoti ya Katibu Mkuu Hazina kutokana na special audit ya October 2019- February 2020. Na matokeo ya Special Audit hiyo ndiyo Rais JPM aliweza kumtumbua Bwanakunu kutoka nafasi ya kuwa Mkurugenzi Mkuu wa MSD. Na hatimaye kufunguliwa mashtaka ya kuhujumu uchumi na TAKUKURU.

Mtaji wa MSD umekatika kabisa kwa vile kipindi cha Bwanakunu wamekuwa wananunua dawa zenye muda mfupi toka nje ya nchi hivyo basi kuna mrundikano wa madawa yapatayo Bilioni zaidi ya 30 ambayo yame EXPIRE.

Kwa mwaka 2019/20 kweli Serikali haikupeleka Fedha kwa kuwa ilikuwa inataka ijiridhishe kwa nini mtaji unaporomoka.

Lakini Bwanakunu hakupaswa kutumbuliwa peke yake bali hata Waziri UMMY Mwalimu alipaswa atumbuliwe pia. Nashangaa DOUBLE STANDARDS za JPM kumuacha na kumfanya Waziri wa Mazingira na Muungano.

Kama MSD imefeli na wamegundua tatizo Ni Mkurugenzi Mkuu basi na Waziri anahusika kwa vile alikuwa ANAMLINDA. Kama Tume ingekuwa imeundwa na UMMY Mwalimu na kugundua mauza uza ya Bwanakunu Basi Waziri angekuwa hana hatia. Lakini Tume iliundwa na Dotto James, Katibu Mkuu Hazina

Tumuache Dr Dorothy Gwajima afanye kazi, kamwe tusimfananishe na UMMY Mwalimu.
 
Kwa taarifa yako Serikali ya Magufuli imepeleka Fedha nyingi MSD kuliko kipindi chohote toka nchi ipate UHURU mwaka 1961. Kati ya July 2016 Hadi Mei 2019 Hazina walipeleka Tsh 314 Bilioni sawa na Tsh 104 Bilioni kwa mwaka. Mwaka 2015/16 wakati Serikali ya JK inaondoka walipeleka Tsh 30 Bilioni.

Katika historia ya MSD kipindi cha UMMY Mwalimu tulijionea kwa mara ya kwanza Waziri akiwa na mahusiano ya karibu sana na Mkurugenzi wa MSD Laurean Bwanakunu. Walikuwa na mahusiano ya kingono na kugawana Fedha kwa kupitia kwa Katwaza wa Bahari Pharmacy ambaye walikuwa wanampa mikataba mingi ya ku-supply dawa hasa vile vifaa vya kits za kujifungulia akina mama.

Haya ninayoyasema siyo majungu yako kwenye Ripoti ya Katibu Mkuu Hazina kutokana na special audit ya October 2019- February 2020. Na matokeo ya Special Audit hiyo ndiyo Rais JPM aliweza kumtumbua Bwanakunu kutoka nafasi ya kuwa Mkurugenzi Mkuu wa MSD. Na hatimaye kufunguliwa mashtaka ya kuhujumu uchumi na TAKUKURU.

Mtaji wa MSD umekatika kabisa kwa vile kipindi cha Bwanakunu wamekuwa wananunua dawa zenye muda mfupi toka nje ya nchi hivyo basi kuna mrundikano wa madawa yapatayo Bilioni zaidi ya 30 ambayo yame EXPIRE.

Kwa mwaka 2019/20 kweli Serikali haikupeleka Fedha kwa kuwa ilikuwa inataka ijiridhishe kwa nini mtaji unaporomoka.

Lakini Bwanakunu hakupaswa kutumbuliwa peke yake bali hata Waziri UMMY Mwalimu alipaswa atumbuliwe pia. Nashangaa DOUBLE STANDARDS za JPM kumuacha na kumfanya Waziri wa Mazingira na Muungano.

Kama MSD imefeli na wamegundua tatizo Ni Mkurugenzi Mkuu basi na Waziri anahusika kwa vile alikuwa ANAMLINDA. Kama Tume ingekuwa imeundwa na UMMY Mwalimu na kugundua mauza uza ya Bwanakunu Basi Waziri angekuwa hana hatia. Lakini Tume iliundwa na Dotto James, Katibu Mkuu Hazina

Tumuache Dr Dorothy Gwajima afanye kazi, kamwe tusimfananishe na UMMY Mwalimu.
Mama hana utulivyo hana hekima kwa watumishi
 
Kwa taarifa yako Serikali ya Magufuli imepeleka Fedha nyingi MSD kuliko kipindi chohote toka nchi ipate UHURU mwaka 1961. Kati ya July 2016 Hadi Mei 2019 Hazina walipeleka Tsh 314 Bilioni sawa na Tsh 104 Bilioni kwa mwaka. Mwaka 2015/16 wakati Serikali ya JK inaondoka walipeleka Tsh 30 Bilioni.

Katika historia ya MSD kipindi cha UMMY Mwalimu tulijionea kwa mara ya kwanza Waziri akiwa na mahusiano ya karibu sana na Mkurugenzi wa MSD Laurean Bwanakunu. Walikuwa na mahusiano ya kingono na kugawana Fedha kwa kupitia kwa Katwaza wa Bahari Pharmacy ambaye walikuwa wanampa mikataba mingi ya ku-supply dawa hasa vile vifaa vya kits za kujifungulia akina mama.

Haya ninayoyasema siyo majungu yako kwenye Ripoti ya Katibu Mkuu Hazina kutokana na special audit ya October 2019- February 2020. Na matokeo ya Special Audit hiyo ndiyo Rais JPM aliweza kumtumbua Bwanakunu kutoka nafasi ya kuwa Mkurugenzi Mkuu wa MSD. Na hatimaye kufunguliwa mashtaka ya kuhujumu uchumi na TAKUKURU.

Mtaji wa MSD umekatika kabisa kwa vile kipindi cha Bwanakunu wamekuwa wananunua dawa zenye muda mfupi toka nje ya nchi hivyo basi kuna mrundikano wa madawa yapatayo Bilioni zaidi ya 30 ambayo yame EXPIRE.

Kwa mwaka 2019/20 kweli Serikali haikupeleka Fedha kwa kuwa ilikuwa inataka ijiridhishe kwa nini mtaji unaporomoka.

Lakini Bwanakunu hakupaswa kutumbuliwa peke yake bali hata Waziri UMMY Mwalimu alipaswa atumbuliwe pia. Nashangaa DOUBLE STANDARDS za JPM kumuacha na kumfanya Waziri wa Mazingira na Muungano.

Kama MSD imefeli na wamegundua tatizo Ni Mkurugenzi Mkuu basi na Waziri anahusika kwa vile alikuwa ANAMLINDA. Kama Tume ingekuwa imeundwa na UMMY Mwalimu na kugundua mauza uza ya Bwanakunu Basi Waziri angekuwa hana hatia. Lakini Tume iliundwa na Dotto James, Katibu Mkuu Hazina

Tumuache Dr Dorothy Gwajima afanye kazi, kamwe tusimfananishe na UMMY Mwalimu.


This is madness!

Nilimuona Ummy kama mtendaji muadilifu sana!

Binaadamu kama Binaadamu!
 
Kila eneo analopita waziri wa afya Dr Gwajima katika ziara zake mikoani ni vilio tu, wananchi wanalalamikia Huduma hafifu, uhaba wa dawa nk.

Kiukweli hii wizara ina madudu mengi sana na sielewi waziri aliyetangulia Da Ummy Mwalimu na wasaidizi wake walikuwa wanafanya kazi gani!?

Chapa kazi Dr Gwajima wananchi tuko nyuma yako.

Maendeleo hayana vyama!
Si mlisema MAGUFULI amenyoosha nchi Nyie na kwamba nidhamu ya watumishi imerejea sasa siasa gani? Wadudu gani hayo?

Kama unaamini ummy alikuwa anapiga siasa twambie yyale maduka ya MSD yaliyofunguliwa na MAGUFULI yapo wapi na ni mangapi yana dawa za kutosha hata wasiende kununua dawa kwenye maduka binafsi!

Acha kupayuka kama mwenyekiti wewe
 
Back
Top Bottom