Kinoamiguu
JF-Expert Member
- Nov 29, 2018
- 11,936
- 15,196
Nadhani mpandisha uzi hajui hasa kazi na majukumu ya katibu mkuu. Yeye anakaa kwenye keyboard kusifia tuHuyo Gwajima unaemsifia alikuwa Mlurugenzi wa Tiba miaka mingi, baadae akaja kuteuliwa Naibu Katibu Mkuu Tamisemi upande wa Afya akiwa kama Mtendaji alipaswa kuwa kishashughulikia kwa kuwa ndio wajibu wake Mkuu
Inakuaje leo ndio aone matatizo hayo
Labda kwa kuwa Naibu Katibu Mkuu hana fursa ya kutembea na Vyombo vya habari!
Wizi wa Dawa hauwezi kumalizwa kwa Ziara za kustukiza
Kuna Wazalendo pale walipendekeza MSD (bohari kuu ya dawa) ikiagiza dawa nje zipigwe chapa kabisa ya (GOT) i.e Goverment of Tanzania ikimaanisha kama sabuni inawezekana kupigwa chapa ya mbuni au mshindi au protex kwny mche kwanini ishindikane kwa vidonge wakati huwa vinatenezwa kwa order kubwa viwandani, dawa za chupa nazo zipigwe nembo ya Serikali
Hii ingezuiwa wizi wa dawa kwa kuwa tungeikuta pharmacy au hospital binafsi tungeijua kuwa imetokea Serikalini, …waliotoa ba kutaka kuteleleza wazo hilo nadhan wangeweza kuhadithia fitna waliyopigwa baada ya wazo hilo
Miaka ya mwanzo ya 1990s niliwahi kuzuru Kiwanda cha Cement cha Twiga, vioo vilivyowekwa vyooni vyote viliandikwa 'Kioo hiki kimeibiwa Wazo hill'
yale Maandishi yalisaidia sana kuzuia wizi wa vioo vile!