muafi
JF-Expert Member
- Oct 6, 2015
- 2,557
- 6,128
Habari zenu
Katika hali isiyo ya kawaida siku ya leo nimepewa rasmi barua ya kuachishwa kazi kwa kosa la utovu wa nidhamu
Shughuli ilianzia Alhamisi iliyopita mida ya saa tatu bosi aliniita ofisini na kuniagiza vitumbua vya mia tisa
Kwakweli kulingana na nilivyokuwa mimi mtu mzima nimevaa nimependeza, nimechana nywele vizuri kama kazi inavyotaka
Nilikuwa nimevaa yale mashati ya kuwaka waka yale ya tetroni na nimechomekea na kuvaa suruali ya kitambaa, kitendo cha bosi kuniagiza vitumbua vya mia tisa kwangu niliona kama ni fedheha kubwa sana kwasababu sio majukumu yangu na ni kama dharau kwangu,
Yaani mimi nitoke ofisisni niende nje eti nimeagizwa vitumbua? Nilimwambia bosi kuwa sitaweza kwenda maana nina kazi na niko bize.
Mimi nina mke na watoto uniagize vitumbua?
Ijumaa nilisimamaishwa kazi na leo rasmi nimeachishwa kazi
Hivi hii ni sawa kweli? nakusudia kwenda kwenye vyombo vya sheria
Katika hali isiyo ya kawaida siku ya leo nimepewa rasmi barua ya kuachishwa kazi kwa kosa la utovu wa nidhamu
Shughuli ilianzia Alhamisi iliyopita mida ya saa tatu bosi aliniita ofisini na kuniagiza vitumbua vya mia tisa
Kwakweli kulingana na nilivyokuwa mimi mtu mzima nimevaa nimependeza, nimechana nywele vizuri kama kazi inavyotaka
Nilikuwa nimevaa yale mashati ya kuwaka waka yale ya tetroni na nimechomekea na kuvaa suruali ya kitambaa, kitendo cha bosi kuniagiza vitumbua vya mia tisa kwangu niliona kama ni fedheha kubwa sana kwasababu sio majukumu yangu na ni kama dharau kwangu,
Yaani mimi nitoke ofisisni niende nje eti nimeagizwa vitumbua? Nilimwambia bosi kuwa sitaweza kwenda maana nina kazi na niko bize.
Mimi nina mke na watoto uniagize vitumbua?
Ijumaa nilisimamaishwa kazi na leo rasmi nimeachishwa kazi
Hivi hii ni sawa kweli? nakusudia kwenda kwenye vyombo vya sheria