NIMEFUKUZWA TENA
BAADA ya kuweka video hii ya TBC nikatolewa kundini:
View: https://youtu.be/-bwoz3jI7RA?si=rJdx_0PlMIHxm4Wm
Nilikuwa kwenye group moja nikafukuzwa naamini wengi mlisoma makala ile.
Bahati nikawa nimebakia katika group kwa no. yangu nyingine ambayo siitumii sana na kwa sababu hiyo ikawa sijui kama bado niko kundini.
Nikajiambia mwanzo hapa nimetimuliwa kwa makala niandikazo na moja ya sababu nilielezwa sielezi vizuri historia ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.
Nikaamua kuanzia sasa hapa kundini nitaweka vipindi nilivyofanya na TBC, AZAM na stesheni nyingine na vikarushwa kwa wananchi wote wa Tanzania.
Niliamini kwa kufanya hivyo nitakuwa nimewadhihirishia viongozi wa group kuwa Mohamed Said anakubalika hadi na vyombo vikubwa ikiwemo TBC.
Nikaweka video kama tatu hivi nazungumza historia ya Baba wa Taifa.
Haikunisaidia kitu.
Nadhani nimedumu kundini kwa siku kama tatu hivi leo wamenifukuza.
Inaelekea historia ya Mwalimu Nyerere itakiwayo ni ile ya zamani yuko peke yake wasitajwe wenzake