Nimefukuzwa tena kundini

Nimefukuzwa tena kundini

Wewe mzee nakufikiria sana enzi zako ulikuwa mjanjamjanja sana.

Una mambo fulani hivi hutaki yakupite licha ya umri wako.

Kumb. Sisi wengine ni wajukuu zako kwahiyo kwenye uzi wako usishangae tukaleta utani utani wa mjukuu na babu.

Nakuja kukuibia mke mzee wangu
Bisma...
Kwa umri wenu nyie ni wanangu kwani mimi ni miaka 71 na mjukuu wangu wa kwanza ana miaka 10.
 
NIMEFUKUZWA TENA

BAADA ya kuweka video hii ya TBC nikatolewa kundini:


View: https://youtu.be/-bwoz3jI7RA?si=rJdx_0PlMIHxm4Wm

Nilikuwa kwenye group moja nikafukuzwa naamini wengi mlisoma makala ile.

Bahati nikawa nimebakia katika group kwa no. yangu nyingine ambayo siitumii sana na kwa sababu hiyo ikawa sijui kama bado niko kundini.

Nikajiambia mwanzo hapa nimetimuliwa kwa makala niandikazo na moja ya sababu nilielezwa sielezi vizuri historia ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.

Nikaamua kuanzia sasa hapa kundini nitaweka vipindi nilivyofanya na TBC, AZAM na stesheni nyingine na vikarushwa kwa wananchi wote wa Tanzania.

Niliamini kwa kufanya hivyo nitakuwa nimewadhihirishia viongozi wa group kuwa Mohamed Said anakubalika hadi na vyombo vikubwa ikiwemo TBC.

Nikaweka video kama tatu hivi nazungumza historia ya Baba wa Taifa.
Haikunisaidia kitu.

Nadhani nimedumu kundini kwa siku kama tatu hivi leo wamenifukuza.
Inaelekea historia ya Mwalimu Nyerere itakiwayo ni ile ya zamani yuko peke yake wasitajwe wenzake

Ndo ujue athari ya brainwash inayofanywa kwa wananchi.

Tuwekee hapa historia tutawaeleza wenetu ukweli ili tusiishi kwenye giza la uongo dhidi ya nchu yetu
 
1. Msikiti una uhusiano sana na DPW, kuna fununu kuwa watajenga msikiti mkubwa sana Mbeya, hii imekaaje?

2. Ni ajabu sana karibu waislam wote wameuelewa mkataba wa bandari kuliko wanasheria...hii imekaaje? (PAMOJA NA ELIMU YA MASHEIKH NI TIA MAJI TIA MAJI LKN MKATABA WAMEUELEWA KWA HARAKA SANAA)

3. Masheikhe wengi wametoa matamshi tata ya kuwakemea na kuwakejeli TEC waliochagua kulinda maslahi ya nchi...hii nayo imekaaje?

Kuna HARUFU YA UDINI ULIOJIFICHA CHINI YA DPW.

Nikwambie tu, moto huwezi kufunikwa na kipande cha khanga mzee Mohamed, tusubiri, tuombe uzima
Hili lina mantiki sana mkuu.

Lakini kuoanisha histotia ya uhuru na upumbavu uliowekwa kwenye huu mkataba ni sawa na kulazimisha tembo kulala kitandani.

Tuanzishie huu uzi tutiririke maana vifua vimejaa
 
Glenn,
Kwa nini unanilazimisha nikujibu?
Nina umuhimu upi kwako?

Huu ni uwanja huru sote tunajadiliana.
Hatutishani wala kupeana "ultimatum," hapa.

Mzee Mohamed Said
Ikiwa mwandiko wangu umeonyesha hata dalili au viashiria vya kukutisha, ninaomba RADHI SANA KWAKO.

Nia yangu sio kukutisha au kukulazimisha.

Nia yangu nilitaka kujua UTHABITI WA MAHAKAMA YAKO YA NDANI katika kutoa hukumu na haki.

Mwenye mahakama huru ndani yake hajui kupendelea kwa mrengo wake au kwa maslahi yake bali huhukumu sawa na kweli ilivyo.

Nitafurahi nikipata maoni yako huru kuhusu bandari.
Naheshimu mawazo yako

Asante sana
Mungu akubariki sana
Glenn
 
Bisma...
Kwa umri wenu nyie ni wanangu kwani mimi ni miaka 71 na mjukuu wangu wa kwanza ana miaka 10.
Umejitahidi, kwangu wewe ni baba mdogo.
Asante kwa kuwa hapa, kuna wakati unatoa elimu bora kabisa.
 
Mzee Mohamed heshima mbele.

Ningependa umjibu mdau aliyeweka maswali kweye post nambari 15.

Kuhusu historia kuchezewa haijaanza leo , hata enzi hizo mtu akipishana na mchonga alionja joto ya jiwe refer to Kambona na zile nyimbo alizotungiwa baada ya kutimkia UK.

Hadi kesho mimi hstoria nyingi za Tanzania siziamini , zina bias ya kutosha hata mapinduzi ya Zanzibar wanampinduzi halisi hawajapewa heshima stahiki.
 
Glenn,
Unadhani Maaskofu wameelewa?
Msikiti una uhusiano gani na DPW?

Masheikh ni tofauti na Maaskofu hawana uwezo wa kuikaripia serikali wala kumfukuza mtu msikitini wala kufuta dhambi zake.
Kumbe maaskofu wote ni zero kichwani?
Walikurupuka bila kuusoma mkataba?
Masheikh ndio waliuelewa zaidi?

Nyie watu dini imeharibu.
Tunajua fika mnachokitetea nyuma ya mlango wa DPW.

Katika hili tutaambiana bila woga.
Tutawanyooshea kidole bila woga.
Tutawakemea tena na tena.

Nasemaje?
Bwana huwalinda wasio na hila; Nalidhilika, akaniokoa.

Zaburi 116:6
 
Kumbe maaskofu wote ni zero kichwani?
Walikurupuka bila kuusoma mkataba?
Masheikh ndio waliuelewa zaidi?

Nyie watu dini imeharibu.
Tunajua fika mnachokitetea nyuma ya mlango wa DPW.

Katika hili tutaambiana bila woga.
Tutawanyooshea kidole bila woga.
Tutawakemea tena na tena.

Nasemaje?
Bwana huwalinda wasio na hila; Nalidhilika, akaniokoa.

Zaburi 116:6
Kumbe upo vitani huku na hujanishtua wakunyumba
 
Back
Top Bottom