Nimefukuzwa tena kundini

Nimefukuzwa tena kundini

Hata akiwa mimi ndiye adm na ukaleta upotoshaji nakupiga block.

Kuna wakati mnapandikiza uongo ili uwe kweli sababu mnaweza kuunda kutokana na kusikia kutoka kwa waliokuwepo na ambao hata wao kuna mengine wana_adjust au updates to new version of history.

Mada zako hizo ni kwa Mwl. Nyerere tu au hata issues nyingine za mapinduzi ya zanzibar unawaandikia huko groupuni?.
 
Hata akiwa mimi ndiye adm na ukaleta upotoshaji nakupiga block.

Kuna wakati mnapandikiza uongo ili uwe kweli sababu mnaweza kuunda kutokana na kusikia kutoka kwa waliokuwepo na ambao hata wao kuna mengine wana_adjust au updates to new version of history.

Mada zako hizo ni kwa Mwl. Nyerere tu au hata issues nyingine za mapinduzi ya zanzibar unawaandikia huko groupuni?.
Today...
Nimeshirikishwa katika miradi ya kuandika historia ya Afrika na Oxford University Press Nairobi (2007), mradi wa kuandika Dictionary of African Biography na Havard (2008), mradi wa kuandika maisha ya Julius Nyerere (2013) na mradi wa kuandika historia mpya ulioanzishwa na Rais Magufuli (2021).

Nilikuwa Research Assistant wa Dr. Harith Ghassany wakati anatafiti historia ya Zanzibar na kuandika kitabu: "Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru.'' (2010).

Nimeandika sana kwingi.

Unaweza kunisoma: mohamedsaidsalum.blogspot.com
 
Joa...
Nini maana ya kwiva?

Historia hii ni historia ya babu na baba zangu.

Sikusomeshwa kwenye shule au chuo chochote kile.

Ninayoeleza hapa ndivyo nilivyopokea kutoka kwao.
Mzee Mohamed,
Kwiva ni kivumishi Cha neno kuiva/iva/wiva/kwiva

Je wewe ni mjukuu/mtoto kutoka ukoo upi haswa kati ya mbili unazozielezea,Je ni wa Nyerere au ni wa Sykes?
 
Mzee Mohamed,
Kwiva ni kivumishi Cha neno kuiva/iva/wiva/kwiva

Je wewe ni mjukuu/mtoto kutoka ukoo upi haswa kati ya mbili unazozielezea,Je ni wa Nyerere au ni wa Sykes?
Joa...
Mimi ni mjukuu wa Salum Abdallah.

Babu yangu ni mmoja wa waasisi wa TANU Western Province 1954 na muasisi wa Tanganyika Railways African Union (TRAU) 1955 Kasanga Tumbo akiwa katibu.

Chini ya uongozi wao waliunganisha TRAU na TANU kupigania uhuru wa Tanganyika.

Hapa ndipo ulipokuwa uhusiano wa Babu yangu na Julius Nyerere.

Alikuwa mtumishi wa Tanganyika Railways akifanyakazi ya kufua chuma Loco Shed Dar es Salaam katika miaka ya 1920 Kleist Sykes akiwa Accounts Clerk.

Kleist na babu yangu walikuwa majirani nyumba zao zikitazamana Mtaa wa Kipata na New Street na watoto wao walisoma Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika Muslim School ambayo walijenga babu zetu kama juhudi za kukwepa watoto wao kusoma shule za wamishionari.

Babu yangu alihamishwa kwenda Tabora mwaka wa 1947 Loco Shed ilipoondolewa Dar es Salaam na kupelekwa Tabora.

Salum Abdallah aliongoza mgomo wa Railway wa mwaka 1947, 1949 na wa 1960 uliodumu siku 82.

Mwaka wa 1964 babu yangu alikamatwa pamoja na viongozi wengine wa wafanyakazi na kuwekwa kizuizini Jela ya Uyui Tabora.

Huu ukawa ndiyo mwisho wa maisha yake ya siasa.

Alifariki mwaka wa 1974 na alipata mazishi makubwa na TANU ilisoma rambirambi wakimsifia kwa mchango wake katika kupigania uhuru wa Tanganyika kwa hali na mali
 
Joa...
Mimi ni mjukuu wa Salum Abdallah.

Babu yangu ni mmoja wa waasisi TANU Western Province 1954 na muasisi wa Tanganyika Railways African Union (TRAU) 1955 Kasanga Tumbo akiwa katibu.

Chini ya uongozi wao waliunganisha TRAU na TANU kupigania uhuru wa Tanganyika.

Hapa ndipo ulipokuwa uhusiano wa Babu yangu na Julius Nyerere.

Alikuwa mtumishi wa Tanganyika Railways akifanyakazi ya kufua chuma Loco Shed Dar es Salaam katika miaka ya 1920 Kleist Sykes akiwa Accounts Clerk.

Kleist na babu yangu walikuwa majirani nyumba zao zikitazamana Mtaa wa Kipata na New Street na watoto wao walisoma Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika Muslim School ambayo walijenga babu zetu kama juhudi za kukwepa watoto wao kusoma shule za wamishionari.

Babu yangu alihamishwa kwenda Tabora mwaka wa 1947 Loco Shed ilipoondolewa Dar es Salaam na kupelekwa Tabora.

Salum Abdallah aliongoza mgomo wa Railway wa mwaka 1947, 1949 na wa 1960 uliodumu siku 82.

Mwaka wa 1964 babu yangu alikamatwa pamoja na viongozi wengine wa wafanyakazi na kuwekwa kizuizini Jela ya Uyui Tabora.

Huu ukawa ndiyo mwisho wa maisha yake ya siasa.

Alifariki mwaka wa 1974 na alipata mazishi makubwa na TANU ilisoma rambirambi wakimsifia kwa mchango wake katika kupigania uhuru wa Tanganyika kwa hali na mali
Hakika historia imekaa mahali pake kabisa ndio maana imenyooka.... Hongera Kwa babu kuwa mmoja wa waasisi wa kupigania uhuru wa nchi yetu
 
Nikajiambia mwanzo hapa nimetimuliwa kwa makala niandikazo na moja ya sababu nilielezwa sielezi vizuri historia ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.
Wanakutimua sio kwa kumsema vibaya nyerere bali kwa kuendekeza udini. Wasilisha jumbe zako bila udini mzee watakusikiliza
 
Ndugu yangu usijidanganye, hukubaliki hata na mtoto mdogo. Kwa vile wewe ni mdini
Mnachojidai kukikemea ndicho kinacho wasumbua, hiyo ndio historia ya kweli japokua hamuipendi, mmejaribu kuipotosha mmeshindwa. Nyinyi ndio wadini msiopenda ukweli ujulikane.

 
Kuna watu historia ya Nyerere wanavyoielewa kuwaambia mambo mengine ni sawa na wewe kuambiwa hiyo Dini Yako ni feki kamwe huwezi kukubali.

Taratibu wataelewa Mzee wangu. Kama Kuna haja tuanzishe group letu huko unashusha mizigo unavyoweza.
Huwezi kufananisha dini na mjivuni mmoja. Ni ujinga huo.
 
Wanakutimua sio kwa kumsema vibaya nyerere bali kwa kuendekeza udini. Wasilisha jumbe zako bila udini mzee watakusikiliza
Niqu...
Hili swali la dini nimelijibu mara nyingi sana.

Wananitimua kwa kuwa wao wangependa historia ya Mwalimu Nyerere ibaki kama ilivyoandikwa.

Mimi kuja na historia ya Abdul Sykes na wazalendo wengine hawakupenda.

Itazame video ya Earle Seaton iko hapa uone vipi mwaka wa 1950 hadi 1952 yeye na Abdul Sykes pamoja na TAA Political Subcommittee walivyoweka mikakati ya kufungua maongezi na UNO.

Wao wangependa haya yasiwepo wanaona inaharibu historia ya Julius Nyerere.

Lakini ukweli ni kuwa Nyerere hakuwapo.

Hapa dini iko wapi?

Au kwa kuwa Mufti Sheikh Hassan bin Ameir na Sheikh Said Chaurembo walikuwa wajumbe wa TAA Political Subcommittee?

Au kueleza historia hii ndiyo kumsema vibaya Mwalimu Nyerere?
 
Unatolewa kwenye makundi pengine kwa sababu stori yako ni moja tu ya Sykes

Huchangii mada nyingine, wewe ukiamka ni Sykes, ukishinda ni Sykes, Ukilala ni Sykes. Kiufupi pengine unateka makundi kwa mjadala mmoja.

Hebu jirekebishe uanze kuchangia mada nyingine za kijamii n.k
Unawachosha watu na mjadala "mono"
 
Kumbe maaskofu wote ni zero kichwani?
Walikurupuka bila kuusoma mkataba?
Masheikh ndio waliuelewa zaidi?

Nyie watu dini imeharibu.
Tunajua fika mnachokitetea nyuma ya mlango wa DPW.

Katika hili tutaambiana bila woga.
Tutawanyooshea kidole bila woga.
Tutawakemea tena na tena.

Nasemaje?
Bwana huwalinda wasio na hila; Nalidhilika, akaniokoa.

Zaburi 116:6
Tazama unavyobweka, kuhororoja na kubwabwaja bila mpango.

Umeulizwa swali jepesi sana, tulizana ulijibu:

"Unadhani Maaskofu wameelewa?"

Mandonga alipoulizwa kwanini anaitwa "Mandonga"? Alijibu "ndonga hata upepo wake ukikupitia unalewa".
 
Tazama unavyobweka, kuhororoja na kubwabwaja bila mpango.

Umeulizwa swali jepesi sana, tulizana ulijibu:

"Unadhani Maaskofu wameelewa?"

Mandonga alipoulizwa kwanini anaitwa "Mandonga"? Alijibu "ndonga hata upepo wake ukikupitia unalewa".
Hakuna sheikh ameelewa nkataba, akili zenyewe za kuelewa ziko wapi?

Akina Kipozeo?
Alhad yule?😂😂😂😂

Mnamtaka mkoloni wenu aliyewaletea dini tu
 
Unatolewa kwenye makundi pengine kwa sababu stori yako ni moja tu ya Sykes

Huchangii mada nyingine, wewe ukiamka ni Sykes, ukishinda ni Sykes, Ukilala ni Sykes. Kiufupi pengine unateka makundi kwa mjadala mmoja.

Hebu jirekebishe uanze kuchangia mada nyingine za kijamii n.k
Unawachosha watu na mjadala "mono"
Missile,
Historia ya Sykes ni ya ukoo mmoja lakini imebeba historia ya wazalendo wengi na mambo mengi sana.

Inakwenda nyuma miaka 100 na imethibitishwa na matukio ya kihistoria.

Inaanza na Shaka na kutoka kwake Afrika ya Kusini unakuja Mozambique Imhambane kijiji cha Kwa Likunyi hapa unamsoma Hermann von Wissmann.

Huyu ndiye aliyewaleta Sykes Pangani, Germany Ostafrika mwishoni mwa 1800 kama askari mamluki.

Hapa Sykes unawasoma pamoja na Abushiri bin Salim na Mtwa Abdallah Mkwawa katika vita.

Unakuja Vita Vya Kwanza Vya Dunia unakutana na Kleist Sykes na Von Lettow Vorbeck wanapigana na Waingereza Mwele Juu, Tanga.

Kleist anakutana na Dr. Kwegyir Aggrey mwaka wa 1924.

Naamini unaijua historia ya Dr. Aggrey.

Historia hii yote Kleist kaiandika.

Abdul Sykes anakutana na Jomo Kenyatta Nairobi 1950.

Abdul anakutana na Earle Seaton.

Unaujua mchango wa Earle Seaton katika uhuru wa Tanganyika?

Abdul Sykes anakutana na Julius Nyerere nyumbani kwake Dar es Salaam Mtaa wa Stanley baadae ukawa Mtaa wa Aggrey 1952.

Naamini unamjua Julius Nyerere katika historia ya uhuru wa Tanganyika na historia ya Afrika.

Hii si historia ndogo.

Nimeandika kitabu na yaliyo ndani ya kitabu hiki ndiyo haya tanayojadili hapa sasa zaidi ya miaka 10 na kila siku historia hii inawavutia wasomaji wapya.

Hakuna aliyechoshwa na historia hii mngechoshwa mngekuwa kimya.

Yule anaeisoma historia hii kwa mara ya kwanza hawi kimya lazima ataniandikia.

Hii ndiyo sababu ya mimi kurejea hapa tena na tena na historia ya Sykes.

Hii ndiyo sababu ya kitabu cha Sykes kuchapwa mara nne kwa Kiingereza na Kiswahili toka kichapwe London 1998.

Kitabu kimewagusa wengi.

Historia hii si ya kawaida hasa kwa kuwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ni sehemu ya historia ya Abdul Sykes.

Hii ndiyo sababu vyombo vingi vya habari kunifanyia mahojiano BBC, SABC, DW, Al Jazeera, TBC1, AZAM na stesheni nyingi za TV Online.


View: https://youtu.be/9wacS4y7IBY?si=WPDjgd-97bzHXa-n
 
Back
Top Bottom