Nimefukuzwa tena kundini

Nimefukuzwa tena kundini

Glenn,
Pole sana huna ujuzi wa historia ya elimu.

Hapana haja ya mimi kukujibu hilo ingia Google soma historia ya elimu utaelimika.

Ukiwa uko Dar-es-Salaam nenda Maktaba ya Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam soma paper ya Ishumi.

Hii ni paper maarufu kuhusu elimu Tanganyika.
Mkuu unaweza weka hiyo Pepa hapa?
 
Glenn,
Hilo la kuelemea mimi siwezi kukuingilia wewe ikiwa unaona hivyo sawa.

Hakika nilikuwa kijana lakini tayari makala zangu zikichapwa na majarida maarufu ya Afrika yaliyokuwa London kama New African na Africa Events.

Kwa nini Nyaraka za Sykes nilipewa mimi hili swali angelijibu marehemu Ally Sykes kama angekuwa hai.

Lakini naamini nyaraka hizi nilifunguliwa mimi kwa sababu kwanza aliniuliza kama naweza kuandika kitabu.

Nikamjibu naweza.

Akanifungulia safe ambayo ilikuwa haijafunguliwa kwa miaka 30.

Hili alilifanya naamini kwa yeye kuniamini mimi kama mwanae kutokana ule uhusiano na ihsani ilyokuwapo baina ya baba yangu na yeye toka udogo wao.

Labda nikueleze kitu.

Nina mswada wa kitabu cha maisha ya Ally Sykes: "Under the Shadow of British Colonialism: The Life of Ally Sykes. "

Hii ni Autobiography mimi na yeye tulikaa kitako akanihadithia maisha yake kuanzia kuzaliwa kwake 1926.

Tulipofika 1942 alipotoroka nyumbani kuijiunga na KAR aende Burma WWII akampigia simu Peter Colmore akamwambia, ,"Namleta Mohamed Said mwanangu nataka umweleze tulivyokutana Nairobi kwenye duka la Assanand Music mweleze urafiki wetu."

Peter Colmore, Peter Colmore, Peter Colmore mtu wa pekee.

Si akili ya kawaida.

Ally Sykes akanijulisha kwa mtu mwingine Jim Bailey kichwa hatari.

Hawa wote kama yeye walikuwa matajiri wakubwa.

Tusimame hapa.

Ukitaka kumsoma ni nani ingia: mohamedsaidsalum.blogspot.com.
Maadam uliwahi kunikaribisha ofisni kwako, nitajongea nikuhoji nikidhi kiu yangu, kuna kitu kinanikereketa kooni.

Nikiendelea kukuhoji kwa maandishi naweza nisi sound vyema, nanjijua sio mwandishi mzuri lakini ni mzungumzaji mzuri sana tu.
 
Nje ya mada naomba nikuulize hivi nini sababu ya kutokuwepo uraia pacha?.

1 Bibi yangu alikuwa na passport ya British na alipo zalipo zaliwa( kabla ya kuwa Tanzania)

2 Jee ni ulikuwa uoga wa Nyerere kwa Kambona na Abdul-rahman Babu?.

3 Uoga wa ccm kutokutaka challenge na wasomi wenye raia pacha watakao wafunua macho wananchi walio lala?.

4 Kuilinda Tanzania kutoka kwa raia wageni kutokumiliki rasilimali ya nchi?.(mbuga,madini na wawekezaji wa hisa wengi ni wageni kwa sasa)

5 Mtanzania aki nyanganywa uraia wa kupewa na kurudishwa kwao Tanzania jee atapokelewa kama nani?.
Killa...
Sina ujuzi wa hayo.
 
Maadam uliwahi kunikaribisha ofisni kwako, nitajongea nikuhoji nikidhi kiu yangu, kuna kitu kinanikereketa kooni.

Nikiendelea kukuhoji kwa maandishi naweza nisi sound vyema, nanjijua sio mwandishi mzuri lakini ni mzungumzaji mzuri sana tu.
Glenn,
Karibu sana ndugu yangu.
Ofidi yangu iko upenuni kwa sitting room yangu.

Pole sana najua umeshangazwa na haya ninayoweka hapa.
 
Hapana, siyo dunia nzima, rudi kafanye homework. Mfumo huo tuliletewa wajinga ndiyo waliwao. Hata waliotuletea hawaufati.

Sehemu ambayo haifwati western christian economic system ni masikini wa kutupwa kama chad, mali, maurtania, somalia au afghanistan na pakistan au sijui mynamar , lkn wote walioendelea wanafwata christian western economic system kuanzia China mpaka uae na Saudia wote wanafwata western christian civilization au unafikiri chimbuko la western justice system ni nini? Unapokwenda Mahakamani na kupata haki hiyo ni system ya wapi?
 
Glenn,
Karibu sana ndugu yangu.
Ofidi yangu iko upenuni kwa sitting room yangu.

Pole sana najua umeshangazwa na haya ninayoweka hapa.
Utajali nikikualika mgahani mzee wangu?
Upenuni sitakuwa huru kuzungumza, kiuhalisia nina ni nidhamu ya Kiafrika, nikiwa kwa mtu sipendi kuwa mzungumzaji
 
Mnachojidai kukikemea ndicho kinacho wasumbua, hiyo ndio historia ya kweli japokua hamuipendi, mmejaribu kuipotosha mmeshindwa. Nyinyi ndio wadini msiopenda ukweli ujulikane.

Aipo...
Wanajisikia vibaya kwa kuchelewa stesheni kupanda treni ya uhuru.

Wakajikuta hawana historia ya kuandika wala kuhadithia.

Wakaamua isiwepo na hii historia ya wazee wetu.
 
Glenn,
Sijui una maana gani na "uanaharakati."

Haya ninayokuandikia ni kutoka academic research nilizofanya na kuandika.
Pengine mwandiko wangu umekuwa mkali sana, na haikuwa lengo langu nieleweke vile lkn ninachokilenga ni huenda makala zako zinaegemea zaidi.
Naomba niishie hapa maadam Mungu akipenda tutazungumza zaidi
 
Utajali nikikualika mgahani mzee wangu?
Upenuni sitakuwa huru kuzungumza, kiuhalisia nina ni nidhamu ya Kiafrika, nikiwa kwa mtu sipendi kuwa mzungumzaji
Glenn,
Usiwe na hofu kuna faragha ya kutosha.

Nimefanya vipindi vingi hapa na TBC1, AZAM na wengineo.

Tutazungumza vizuri tu toa hofu.
Nataka uje kwangu uwe ndugu yangu.
 
Pengine mwandiko wangu umekuwa mkali sana, na haikuwa lengo langu nieleweke vile lkn ninachokilenga ni huenda makala zako zinaegemea zaidi.
Naomba niishie hapa maadam Mungu akipenda tutazungumza zaidi
Glenn,
Toa hofu tuko pamoja.
 
Nimeshirikishwa katika miradi ya kuandika historia ya Afrika na Oxford University Press Nairobi (2007), mradi wa kuandika Dictionary of African Biography na Havard (2008), mradi wa kuandika maisha ya Julius Nyerere (2013) na mradi wa kuandika historia mpya ulioanzishwa na Rais Magufuli (2021).

Nilikuwa Research Assistant wa Dr. Harith Ghassany wakati anatafiti historia ya Zanzibar na kuandika kitabu: "Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru.'' (2010).
Nimeandika sana kwingi.
So unataka marehemu mzee Nyerere tumfanye nini kutokana na researches zako, maana inaonekana a lot of your articles ni Nyerere, Nyerere na Nyerere tu?.
 
Glenn,
Nimefukuzwa sikupata kibano.
Kibano wamekipata wao.

Niliweka video za vipindi nilivyofanya na AZAM, TBC na vituo vingine namzungumza Mwalimu Nyerere.

Video ya mwisho namweleza Earle Seaton na Abdul Sykes 1950 na mikakati ya UNO.

Video hii ipo hapa.

Itazame halafu jiulize kweli watu hawa walikuwapo au ni hadithi anazotunga Mohamed Said?
Mohamed Said, ukiona umefukuzwa pahala ujue watu wamechoka na ujumbe wako ulioupeleka. Tangu nikufahamu ndani ya jf kila wakati unaandika negativity za Nyerere dhidi ya Waislam. Kifupi unapalilia udini!! Si kwamba watu wanakuchukia, hapana, wanachukia jumbe zako.
 
So unataka marehemu mzee Nyerere tumfanye nini kutokana na researches zako, maana inaonekana a lot of your articles ni Nyerere, Nyerere na Nyerere tu?.
Today,
Hapana unasoma tofauti utafiti wangu hauko kwa Mwalimu Nyerere.
Utafiti wangu ulianza na mchango wa wazee wangu katika historia ya uhuru wa Tanganyika.

Swali la kwanza nilijiuliza vipi historia ya TANU imeandikwa babu zangu hawamo?
Nimejiuli swali hili kwa kuwa naijua historia ya TANU.

Mtu asiyeijua yeye ataona sawa tu.

Sasa historia yangu chembelecho, ''a lot of your articles ni Nyerere, Nyerere na Nyerere tu.''

Hapana rejea kusoma vyema utaona nawataja wazee wangu Nyerere anaingia kama sehemu ya historia ya marehemu wazee wangu waliokuwa na yeye katika kupigania uhuru wa Tanganyika.
 
Today,
Hapana unasoma tofauti utafiti wangu hauko kwa Mwalimu Nyerere.
Utafiti wangu ulianza na mchango wa wazee wangu katika historia ya uhuru wa Tanganyika.

Swali la kwanza nilijiuliza vipi historia ya TANU imeandikwa babu zangu hawamo?
Nimejiuli swali hili kwa kuwa naijua historia ya TANU.

Mtu asiyeijua yeye ataona sawa tu.

Sasa historia yangu chembelecho, ''a lot of your articles ni Nyerere, Nyerere na Nyerere tu.''

Hapana rejea kusoma vyema utaona nawataja wazee wangu Nyerere anaingia kama sehemu ya historia ya marehemu wazee wangu waliokuwa na yeye katika kupigania uhuru wa Tanganyika.
Na ndipo hapa ninapokuuliza, historia ipi inawasahau hao unaoita babu zako? Ulishaandika mengi na kuweka hiyo historia, unatakeje tena? au unataka iweje ndio ujue historia imewakumbuka hao babu zako? Unataka wafanyweje hasa?
 
Mohamed Said, ukiona umefukuzwa pahala ujue watu wamechoka na ujumbe wako ulioupeleka. Tangu nikufahamu ndani ya jf kila wakati unaandika negativity za Nyerere dhidi ya Waislam. Kifupi unapalilia udini!! Si kwamba watu wanakuchukia, hapana, wanachukia jumbe zako.
Glenn...
Hapana huwezi kuchoka kusoma historia hii.
Si kama najisifu ''track record'' inaonyesha hivyo.

Niko full booked ''Nyerere Day.''
Ukipenda ingia You Tube angalia video za nyuma Nyerere Day nimezungumza stesheni ngapi?

Sioni hiyo ''negativity'' labda utuwekee hapa kila mtu ashuhudie.
Kusahihisha historia iliyofuta ni kupalilia udini?

Vipi kufuta historia ya Waislam hicho ni nini?
Mimi sijahisi hata siku moja kama nachukiwa.

Sijua wewe hili kuwa nachukiwa umelipata wapi?
Naandikiwa na watu wengi sana wakiomba kunitembelea.

Hapa JF nimekuwa Mwandishi Bora Jukwa la Historia mara mbili mfululizo mwaka wa 2021 na 2022.

Maktaba yangu ni kati ya Maktaba tatu bora zilizosheheni historia ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere: Maktaba ya Salim Ahmed Salim, Brig. General Hashim Mbita na yangu Mohamed Said.

Haya yameandikwa kwenye kitabu: ''Nyerere Biography'' (2020).
Je, hizi ni dalili za mtu anaechukiza?
 
Na ndipo hapa ninapokuuliza, historia ipi inawasahau hao unaoita babu zako? Ulishaandika mengi na kuweka hiyo historia, unatakeje tena? au unataka iweje ndio ujue historia imewakumbuka hao babu zako? Unataka wafanyweje hasa?
Mbussi,
Sina nitakacho.
 
Back
Top Bottom